< Ezekieli 46 >

1 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Lango la ukumbi wa ndani linaloelekea upande wa mashariki litakuwa linafungwa kwa siku sita za juma, ila siku ya Sabato na siku ya Mwezi Mwandamo litafunguliwa.
Ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: la porte du parvis intérieur, laquelle regarde l'Orient, sera fermée les six jours ouvriers, mais elle sera ouverte le jour du Sabbat, et pareillement elle sera ouverte le jour de la nouvelle lune.
2 Mkuu anayetawala ataingia kupitia baraza ya njia ya lango la ukumbi na kusimama karibu na nguzo ya lango. Makuhani watatoa sadaka za mkuu anayetawala za kuteketezwa na sadaka za amani. Mkuu anayetawala atasujudu kwenye kizingiti cha njia ya lango, kisha atatoka nje, lakini lango halitafungwa mpaka jioni.
Et le Prince y entrera par le chemin de l'allée de la porte [du parvis] extérieur, et se tiendra près de l'un des poteaux de [l'autre] porte, et les Sacrificateurs prépareront son holocauste et ses sacrifices de prospérité; puis il se prosternera sur le seuil de cette [autre] porte, et ensuite il sortira; mais cette [autre] porte ne sera point fermée jusques au soir.
3 Siku za Sabato na za Mwezi mwandamo watu wote wa nchi wataabudu mbele za Bwana penye lile ingilio la ile njia.
Tellement que le peuple du pays se prosternera devant l'Eternel à l'entrée de cette [autre] porte-ci, les jours de Sabbat et des nouvelles lunes.
4 Sadaka ya kuteketezwa aletazo mkuu anayetawala kwa Bwana siku ya Sabato itakuwa ni wana-kondoo sita na kondoo dume mmoja, wote wasiwe na dosari.
Or l'holocauste que le Prince offrira à l'Eternel le jour du Sabbat sera de six agneaux sans tare, et d'un bélier sans tare.
5 Sadaka ya nafaka inayotolewa pamoja na huyo kondoo dume itakuwa efa moja na sadaka ya nafaka inayotolewa na hao wana-kondoo itakuwa kiasi apendacho mtu pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
Et le gâteau pour le bélier [sera] d'un épha, et le gâteau pour chacun des agneaux sera selon ce qu'il pourra donner; mais il y aura un hin d'huile pour chaque épha.
6 Siku ya mwezi mwandamo atatoa fahali mchanga, wana-kondoo sita na kondoo dume, wote wasiwe na dosari.
Et au jour de la nouvelle Lune [son holocauste] sera d'un jeune veau, sans tare, et de six agneaux et d'un bélier, aussi sans tare.
7 Atatoa kuwa sadaka ya nafaka efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja na kondoo dume mmoja na pamoja na wana-kondoo kama atakavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
Et il offrira pour le gâteau du veau, un épha, et pour le gâteau du bélier, un [autre] épha, et pour chacun des agneaux selon ce qu'il pourra donner; mais [il y aura] un hin d'huile pour chaque épha.
8 Wakati mkuu anayetawala aingiapo, atapitia kwenye baraza ya njia ya lango, naye atatoka nje kwa njia hiyo hiyo.
Et comme le Prince sera entré [au Temple] par le chemin de l'allée de cette [même] porte [du parvis] extérieur, laquelle regarde l'Orient, aussi sortira-t-il par le même chemin.
9 “‘Wakati watu wa nchi wanapokuja mbele za Bwana katika sikukuu zilizoamriwa, yeyote aingiaye kwa lango la kaskazini kuabudu atatoka nje kwa lango la kusini na yeyote aingiaye kwa lango la kusini atatoka nje kwa lango la kaskazini. Hakuna mtu yeyote atakayerudi kwa kupitia lango lile aliloingilia, lakini kila mmoja atatoka nje kwa lango linalokabili lile aliloingilia.
Mais quand le peuple du pays [y] entrera pour se présenter devant l'Eternel, aux fêtes solennelles, celui qui y entrera par le chemin de la porte du Septentrion pour y adorer l'Eternel, sortira par le chemin de la porte du Midi; et celui qui y entrera par le chemin de la porte du Midi, sortira par le chemin de la porte qui regarde vers le Septentrion; tellement que personne ne retournera par le chemin de la porte par laquelle il sera entré, mais il sortira par celle qui est vis-à-vis.
10 Mkuu anayetawala atakuwa miongoni mwao, akiingia nao ndani wanapoingia, naye atatoka nao nje wanapotoka.
Alors le Prince entrera parmi eux, quand ils entreront; et quand ils sortiront, ils sortiront [ensemble].
11 “‘Kwenye sikukuu na kwenye sikukuu zilizoamriwa, sadaka ya nafaka itakuwa efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja pamoja na kondoo dume mmoja, pamoja na idadi ya wana-kondoo kama mtu apendavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
Or dans ces fêtes solennelles, et dans ces solennités, le gâteau d'un veau sera d'un épha, et [le gâteau] d'un bélier d'un [autre] épha, et le gâteau de chacun des agneaux sera selon que le Prince pourra donner, et il y aura un hin d'huile pour chaque épha.
12 Mkuu anayetawala anapotoa sadaka ya hiari kwa Bwana, ikiwa ni sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya amani, lango linaloelekea mashariki litafunguliwa kwa ajili yake. Atatoa sadaka yake ya kuteketezwa au sadaka yake ya amani kama afanyavyo katika siku ya Sabato. Kisha atatoka nje, naye akiisha kutoka nje, lango litafungwa.
Que si le Prince offre un sacrifice volontaire, quelque holocauste, soit quelques sacrifices de prospérités en offrande volontaire à l'Eternel, on lui ouvrira la porte qui regarde l'Orient, et il offrira son holocauste et ses sacrifices de prospérités comme il les offre le jour du Sabbat, puis il sortira, et après qu'il sera sorti, on fermera cette porte.
13 “‘Kila siku utamtoa mwana-kondoo wa mwaka mmoja asiyekuwa na dosari kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, utaitoa kila siku asubuhi.
Tu sacrifieras chaque jour en holocauste à l'Eternel un agneau d'un an sans tare, tu le sacrifieras tous les matins.
14 Pia kila siku asubuhi pamoja na hiyo sadaka utatoa sadaka ya nafaka, ikiwa na sehemu ya sita ya efa pamoja na theluthi moja ya hini ya mafuta ya kuchanganya na ule unga. Utoaji wa sadaka hii ya nafaka kwa Bwana ni amri ya daima.
Tu offriras aussi tous les matins avec lui un gâteau, fait de la sixième partie d'un épha, et de la troisième d'un hin d'huile pour en détremper la fine farine; c'est là le gâteau continuel qu'il faut offrir par ordonnances perpétuelles.
15 Kwa hiyo mwana-kondoo na sadaka ya nafaka na mafuta vitatolewa kila siku asubuhi kwa ajili ya sadaka ya daima ya kuteketezwa.
Ainsi on offrira tous les matins [en] holocauste continuel cet agneau et ce gâteau détrempé avec cette huile.
16 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ikiwa mkuu atawalaye atatoa zawadi kutoka kwenye urithi wake na kumpa mmoja wa wanawe, hiyo zawadi itakuwa pia kwa wazao wake, itakuwa mali yao kwa urithi.
Ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: quand le Prince aura fait un don [de quelque pièce] de son héritage à quelqu'un de ses fils, ce don appartiendra à ses fils; parce qu'ils ont droit de possession en l'héritage.
17 Hata hivyo, kama atatoa zawadi kutoka urithi wake na kumpa mmoja wa watumishi wake, mtumishi anaweza kuiweka mpaka mwaka wa uhuru, kisha itarudishwa kwa mkuu anayetawala. Urithi wake ni wa wanawe peke yao, ni mali yao.
Mais s'il fait un don [de quelque pièce] de son héritage à l'un de ses serviteurs, le don lui appartiendra bien, mais seulement jusques à l'an d'affranchissement, auquel il retournera au Prince; [car] quoi qu'il en soit, c'est son héritage qui appartient à ses fils, [c'est pourquoi] il leur demeurera.
18 Mkuu anayetawala hana ruhusa kuchukua urithi wowote wa watu na kuwaondoa kwenye mali zao. Mkuu atawalaye atawapa wanawe urithi wao, kutoka kwenye mali zake mwenyewe, ili kwamba pasiwe na mtu wangu yeyote atakayetengwa na urithi wake.’”
Et le Prince n'usurpera rien de l'héritage du peuple, les fraudant de la possession qui leur appartient, [seulement] il laissera en héritage à ses fils la possession qui lui appartient, afin qu'aucun de mon peuple ne soit chassé de sa possession.
19 Kisha mtu yule akanileta kwa kupitia kwenye ingilio lililokuwa kando ya lango mpaka kwenye vyumba vitakatifu vinavyoelekea kaskazini, ambavyo ni vya makuhani, naye akanionyesha mahali fulani upande wa mwisho wa magharibi.
Puis il me mena par l'entrée qui était vers le côté de la porte, aux chambres saintes qui appartenaient aux Sacrificateurs, lesquelles regardaient vers le Septentrion, et voilà, il y avait un certain lieu aux deux côtés du fond qui regardaient vers l'Occident.
20 Akaniambia, “Mahali hapa ndipo makuhani watakapotokosea sadaka ya hatia na sadaka ya dhambi na kuoka sadaka ya nafaka, kuepuka kuzileta katika ukumbi wa nje na kushirikisha utakatifu kwa watu.”
Et il me dit: c'est là le lieu auquel les Sacrificateurs bouilliront [le reste de la bête qu'on aura sacrifiée pour] le délit, et [le reste de la bête qu'on aura sacrifiée pour] le péché, et où ils cuiront les gâteaux; afin qu'ils ne les emportent point au parvis extérieur pour en sanctifier le peuple.
21 Baada ya hapo akanileta kwenye ukumbi wa nje na kunizungusha kwenye pembe zake nne, nami nikaona katika kila pembe ya huo ukumbi kulikuwa na ukumbi mwingine.
Puis il me fit sortir vers le parvis extérieur, et me fit traverser vers les quatre coins du parvis, et voici, il y avait un parvis à chaque coin du parvis.
22 Katika pembe nne za huo ukumbi wa nje kulikuwa na kumbi nyingine, zenye urefu wa dhiraa arobaini na upana wake dhiraa thelathini, ambapo hizo kumbi kwenye hizo pembe nne zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
Tellement qu'aux quatre coins de ce parvis il y avait d'autres parvis qui y étaient joints, et ils étaient longs de quarante [coudées], et larges de trente; [et] tous quatre avaient une même mesure, [et] avaient leurs [quatre] coins.
23 Mzunguko wa ndani wa hizo kumbi nne ulikuwa na ukingo wa jiwe, zikiwa na sehemu zilizojengwa kwa ajili ya moto kuzunguka chini ya huo ukingo.
Tous ces quatre parvis avaient une rangée de bâtiments élevés tout à l'entour, et ce qui était bâti au dessous de ces rangées de bâtiment élevé, tout [à] l'entour, c'étaient des lieux propres à cuire.
24 Akaniambia, “Hizi ndizo sehemu za kupikia ambazo wale wanaohudumu kwenye Hekalu watatokosea dhabihu za watu.”
Et il me dit: ce sont ici les cuisines, où ceux qui font le service de la maison cuiront les sacrifices du peuple.

< Ezekieli 46 >