< Ezekieli 46 >

1 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Lango la ukumbi wa ndani linaloelekea upande wa mashariki litakuwa linafungwa kwa siku sita za juma, ila siku ya Sabato na siku ya Mwezi Mwandamo litafunguliwa.
Voici ce que dit le Seigneur Dieu: La porte du parvis intérieur qui regarde l'orient sera fermée les six jours de travail; elle sera ouverte les jours du sabbat et à chaque nouvelle lune.
2 Mkuu anayetawala ataingia kupitia baraza ya njia ya lango la ukumbi na kusimama karibu na nguzo ya lango. Makuhani watatoa sadaka za mkuu anayetawala za kuteketezwa na sadaka za amani. Mkuu anayetawala atasujudu kwenye kizingiti cha njia ya lango, kisha atatoka nje, lakini lango halitafungwa mpaka jioni.
Et le prince entrera par le chemin du vestibule de la porte intérieure, et il s'arrêtera au seuil de la porte, et les prêtres prépareront ses holocaustes et ses hosties pacifiques. Et il adorera au seuil même de la porte, puis il sortira, et la porte ne sera pas fermée jusqu'au soir;
3 Siku za Sabato na za Mwezi mwandamo watu wote wa nchi wataabudu mbele za Bwana penye lile ingilio la ile njia.
Et le peuple de la terre adorera près de cette porte, et il se prosternera devant le Seigneur, les jours de sabbat et de nouvelle lune.
4 Sadaka ya kuteketezwa aletazo mkuu anayetawala kwa Bwana siku ya Sabato itakuwa ni wana-kondoo sita na kondoo dume mmoja, wote wasiwe na dosari.
Et le prince offrira les jours de sabbat, en holocauste au Seigneur, six agneaux sans tache et un bélier sans tache,
5 Sadaka ya nafaka inayotolewa pamoja na huyo kondoo dume itakuwa efa moja na sadaka ya nafaka inayotolewa na hao wana-kondoo itakuwa kiasi apendacho mtu pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
Et l'oblation d'un gâteau pour le bélier, et un don volontaire de sa main par agneau; et il y aura dans le gâteau un hin d'huile.
6 Siku ya mwezi mwandamo atatoa fahali mchanga, wana-kondoo sita na kondoo dume, wote wasiwe na dosari.
Et il offrira, le jour de la nouvelle lune, un veau sans tache, et six agneaux et un bélier sans tache.
7 Atatoa kuwa sadaka ya nafaka efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja na kondoo dume mmoja na pamoja na wana-kondoo kama atakavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
Et il y aura un gâteau pour le bélier; et le gâteau pour le veau, comme pour les agneaux, sera une oblation; il donnera par agneau selon le pouvoir de sa main, et il y aura un hin d'huile dans le gâteau.
8 Wakati mkuu anayetawala aingiapo, atapitia kwenye baraza ya njia ya lango, naye atatoka nje kwa njia hiyo hiyo.
Et lorsque le prince entrera dans le temple, il passera par le chemin du vestibule du parvis, et il sortira par le chemin de la porte.
9 “‘Wakati watu wa nchi wanapokuja mbele za Bwana katika sikukuu zilizoamriwa, yeyote aingiaye kwa lango la kaskazini kuabudu atatoka nje kwa lango la kusini na yeyote aingiaye kwa lango la kusini atatoka nje kwa lango la kaskazini. Hakuna mtu yeyote atakayerudi kwa kupitia lango lile aliloingilia, lakini kila mmoja atatoka nje kwa lango linalokabili lile aliloingilia.
Et lorsque le peuple de la terre viendra devant le Seigneur, celui qui arrivera les jours de fête pour adorer par le chemin de la porte qui regarde l'aquilon, sortira par la porte du midi; et celui qui arrivera par le chemin de la porte du midi sortira par la porte de l'aquilon; nul ne s'en ira par le chemin qu'il aura pris pour entrer, mais il marchera droit devant lui pour sortir.
10 Mkuu anayetawala atakuwa miongoni mwao, akiingia nao ndani wanapoingia, naye atatoka nao nje wanapotoka.
Et le prince au milieu d'eux entrera avec eux quand ils entreront, et il sortira quand ils sortiront.
11 “‘Kwenye sikukuu na kwenye sikukuu zilizoamriwa, sadaka ya nafaka itakuwa efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja pamoja na kondoo dume mmoja, pamoja na idadi ya wana-kondoo kama mtu apendavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
Et aux fêtes et aux solennités générales il y aura oblation d'un gâteau par veau et d'un gâteau par bélier; et le prince donnera par agneau selon le pouvoir de sa main, et il y aura un hin d'huile par gâteau.
12 Mkuu anayetawala anapotoa sadaka ya hiari kwa Bwana, ikiwa ni sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya amani, lango linaloelekea mashariki litafunguliwa kwa ajili yake. Atatoa sadaka yake ya kuteketezwa au sadaka yake ya amani kama afanyavyo katika siku ya Sabato. Kisha atatoka nje, naye akiisha kutoka nje, lango litafungwa.
Si le prince prépare en action de grâces un holocauste pacifique au Seigneur, il ouvrira pour lui seul la porte qui regarde l'orient, et il préparera l'holocauste et les hosties pacifiques, comme il fait le jour du sabbat; puis il sortira, et en sortant il fermera les portes.
13 “‘Kila siku utamtoa mwana-kondoo wa mwaka mmoja asiyekuwa na dosari kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, utaitoa kila siku asubuhi.
Et chaque jour, dès le matin, il offrira en holocauste au Seigneur un agneau d'un an sans tache.
14 Pia kila siku asubuhi pamoja na hiyo sadaka utatoa sadaka ya nafaka, ikiwa na sehemu ya sita ya efa pamoja na theluthi moja ya hini ya mafuta ya kuchanganya na ule unga. Utoaji wa sadaka hii ya nafaka kwa Bwana ni amri ya daima.
Et il fera dès le matin, pour cet agneau d'oblation d'un sixième d'éphi de fleur de farine et du tiers d'un hin d'huile pour y être mêlée; cette oblation au Seigneur sera de règle perpétuelle.
15 Kwa hiyo mwana-kondoo na sadaka ya nafaka na mafuta vitatolewa kila siku asubuhi kwa ajili ya sadaka ya daima ya kuteketezwa.
Vous sacrifierez l'agneau, et vous offrirez dès le matin l'huile et la farine; cet holocauste sera perpétuel.
16 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ikiwa mkuu atawalaye atatoa zawadi kutoka kwenye urithi wake na kumpa mmoja wa wanawe, hiyo zawadi itakuwa pia kwa wazao wake, itakuwa mali yao kwa urithi.
Voici ce que dit le Seigneur: Si le prince fait sur sa part de bien un don à l'un de ses fils, celui-ci le transmettra à ses fils comme héritage.
17 Hata hivyo, kama atatoa zawadi kutoka urithi wake na kumpa mmoja wa watumishi wake, mtumishi anaweza kuiweka mpaka mwaka wa uhuru, kisha itarudishwa kwa mkuu anayetawala. Urithi wake ni wa wanawe peke yao, ni mali yao.
S'il fait un don à l'un de ses serviteurs, celui-ci ne le possèdera que jusqu'à l'année du jubilé, et alors il le rendra au prince; quant à ce qui est possédé par ses fils, c'est à eux que la possession continuera d'appartenir.
18 Mkuu anayetawala hana ruhusa kuchukua urithi wowote wa watu na kuwaondoa kwenye mali zao. Mkuu atawalaye atawapa wanawe urithi wao, kutoka kwenye mali zake mwenyewe, ili kwamba pasiwe na mtu wangu yeyote atakayetengwa na urithi wake.’”
Et le prince ne prendra rien de l'héritage du peuple: il se gardera de l'opprimer; il fera part à ses fils de ce que lui-même possède, afin que nul de mon peuple ne soit expulsé de son héritage.
19 Kisha mtu yule akanileta kwa kupitia kwenye ingilio lililokuwa kando ya lango mpaka kwenye vyumba vitakatifu vinavyoelekea kaskazini, ambavyo ni vya makuhani, naye akanionyesha mahali fulani upande wa mwisho wa magharibi.
Et l'homme me conduisit derrière la porte à la chambre des miels, consacrée aux prêtres, qui regarde l'aquilon; et là était un lieu réservé.
20 Akaniambia, “Mahali hapa ndipo makuhani watakapotokosea sadaka ya hatia na sadaka ya dhambi na kuoka sadaka ya nafaka, kuepuka kuzileta katika ukumbi wa nje na kushirikisha utakatifu kwa watu.”
Et il me dit: Voici le lieu où les prêtres feront cuire les victimes pour le péché et pour l'inadvertance; ils y feront cuire aussi tous les gâteaux de l'oblation, afin de ne les point emporter dans le parvis extérieur, quand ils purifieront le peuple.
21 Baada ya hapo akanileta kwenye ukumbi wa nje na kunizungusha kwenye pembe zake nne, nami nikaona katika kila pembe ya huo ukumbi kulikuwa na ukumbi mwingine.
Et l'homme me conduisit au parvis extérieur, et il me fit faire le tour de ses quatre côtés, et là il y avait une cour à chacun de ses côtés.
22 Katika pembe nne za huo ukumbi wa nje kulikuwa na kumbi nyingine, zenye urefu wa dhiraa arobaini na upana wake dhiraa thelathini, ambapo hizo kumbi kwenye hizo pembe nne zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
Il y avait quatre petites cours, une par côté, toutes longues, pareillement de quarante coudées, larges de trente.
23 Mzunguko wa ndani wa hizo kumbi nne ulikuwa na ukingo wa jiwe, zikiwa na sehemu zilizojengwa kwa ajili ya moto kuzunguka chini ya huo ukingo.
Et à l'entour de chacune il y avait des chambres; et au-dessous des chambres les cuisines étaient bâties alentour.
24 Akaniambia, “Hizi ndizo sehemu za kupikia ambazo wale wanaohudumu kwenye Hekalu watatokosea dhabihu za watu.”
Et il me dit: Voici les demeures des cuisiniers; c'est ici que les desservants du temple feront cuire les offrandes du peuple.

< Ezekieli 46 >