< Ezekieli 46 >

1 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Lango la ukumbi wa ndani linaloelekea upande wa mashariki litakuwa linafungwa kwa siku sita za juma, ila siku ya Sabato na siku ya Mwezi Mwandamo litafunguliwa.
Ainsi parle le Seigneur Yahweh: " Le portique du parvis intérieur, qui regarde l'orient, restera fermé les six jours ouvriers, mais il sera ouvert le jour du sabbat; il sera aussi ouvert le jour de la nouvelle lune.
2 Mkuu anayetawala ataingia kupitia baraza ya njia ya lango la ukumbi na kusimama karibu na nguzo ya lango. Makuhani watatoa sadaka za mkuu anayetawala za kuteketezwa na sadaka za amani. Mkuu anayetawala atasujudu kwenye kizingiti cha njia ya lango, kisha atatoka nje, lakini lango halitafungwa mpaka jioni.
Le prince arrivera du dehors vers le vestibule du portique et se tiendra à côté du poteau du portique; les prêtres offriront son holocauste et ses sacrifices pacifiques. Il se prosternera sur le seuil du portique, et se retirera; et le portique ne sera pas fermé jusqu'au soir.
3 Siku za Sabato na za Mwezi mwandamo watu wote wa nchi wataabudu mbele za Bwana penye lile ingilio la ile njia.
Le peuple du pays se prosternera à l'entrée de ce portique, aux sabbats et aux nouvelles lunes, devant Yahweh.
4 Sadaka ya kuteketezwa aletazo mkuu anayetawala kwa Bwana siku ya Sabato itakuwa ni wana-kondoo sita na kondoo dume mmoja, wote wasiwe na dosari.
L'holocauste que le prince offrira à Yahweh sera, le jour du sabbat, de six agneaux sans défaut et d'un bélier sans défaut;
5 Sadaka ya nafaka inayotolewa pamoja na huyo kondoo dume itakuwa efa moja na sadaka ya nafaka inayotolewa na hao wana-kondoo itakuwa kiasi apendacho mtu pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
et, comme oblation, il offrira un épha de farine pour le bélier; et, comme oblation pour les agneaux, ce qu'il voudra donner, avec un hin d'huile par épha.
6 Siku ya mwezi mwandamo atatoa fahali mchanga, wana-kondoo sita na kondoo dume, wote wasiwe na dosari.
Le jour de la nouvelle lune, ce sera un jeune taureau, sans défaut, six agneaux et un bélier sans défaut.
7 Atatoa kuwa sadaka ya nafaka efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja na kondoo dume mmoja na pamoja na wana-kondoo kama atakavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
Et il donnera comme oblation un épha par bélier, et pour les agneaux, ce qu'il pourra donner, avec un hin d'huile par épha.
8 Wakati mkuu anayetawala aingiapo, atapitia kwenye baraza ya njia ya lango, naye atatoka nje kwa njia hiyo hiyo.
Lorsque le prince entrera, il entrera par le vestibule du portique et sortira par le même chemin.
9 “‘Wakati watu wa nchi wanapokuja mbele za Bwana katika sikukuu zilizoamriwa, yeyote aingiaye kwa lango la kaskazini kuabudu atatoka nje kwa lango la kusini na yeyote aingiaye kwa lango la kusini atatoka nje kwa lango la kaskazini. Hakuna mtu yeyote atakayerudi kwa kupitia lango lile aliloingilia, lakini kila mmoja atatoka nje kwa lango linalokabili lile aliloingilia.
Lorsque le peuple du pays entrera devant Yahweh dans les solennités, celui qui entrera par le portique du septentrion pour se prosterner, sortira par le portique du midi, et celui qui entrera par le portique du midi sortira par le portique du septentrion; on ne retournera pas par le portique par lequel on sera entré; mais on sortira par celui qui est en face de lui.
10 Mkuu anayetawala atakuwa miongoni mwao, akiingia nao ndani wanapoingia, naye atatoka nao nje wanapotoka.
Le prince aussi entrera parmi eux quand ils entreront, et sortira comme ils sortiront.
11 “‘Kwenye sikukuu na kwenye sikukuu zilizoamriwa, sadaka ya nafaka itakuwa efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja pamoja na kondoo dume mmoja, pamoja na idadi ya wana-kondoo kama mtu apendavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
Aux fêtes et aux solennités, l'oblation sera d'un épha pour le taureau et d'un épha pour le bélier, et, pour les agneaux, ce que le prince voudra donner, avec un hin d'huile par épha.
12 Mkuu anayetawala anapotoa sadaka ya hiari kwa Bwana, ikiwa ni sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya amani, lango linaloelekea mashariki litafunguliwa kwa ajili yake. Atatoa sadaka yake ya kuteketezwa au sadaka yake ya amani kama afanyavyo katika siku ya Sabato. Kisha atatoka nje, naye akiisha kutoka nje, lango litafungwa.
Quand le prince offrira une offrande volontaire, holocauste ou sacrifices pacifiques, offrande volontaire à Yahweh, on lui ouvrira le portique qui regarde l'orient. Il offrira son holocauste ou ses sacrifices pacifiques, comme il le fait le jour du sabbat, et il sortira; et l'on fermera la porte après qu'il sera sorti.
13 “‘Kila siku utamtoa mwana-kondoo wa mwaka mmoja asiyekuwa na dosari kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, utaitoa kila siku asubuhi.
Tu offriras un agneau d'un an sans défaut comme holocauste quotidien à Yahweh; tu l'offriras chaque matin.
14 Pia kila siku asubuhi pamoja na hiyo sadaka utatoa sadaka ya nafaka, ikiwa na sehemu ya sita ya efa pamoja na theluthi moja ya hini ya mafuta ya kuchanganya na ule unga. Utoaji wa sadaka hii ya nafaka kwa Bwana ni amri ya daima.
Tu offriras avec lui chaque matin une oblation, savoir un sixième d'épha, et le tiers d'un hin d'huile pour arroser la fleur de farine, comme oblation à Yahweh; ce sont des lois permanentes, pour toujours.
15 Kwa hiyo mwana-kondoo na sadaka ya nafaka na mafuta vitatolewa kila siku asubuhi kwa ajili ya sadaka ya daima ya kuteketezwa.
On offrira chaque matin l'agneau, l'oblation avec l'huile; c'est l'holocauste perpétuel. "
16 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ikiwa mkuu atawalaye atatoa zawadi kutoka kwenye urithi wake na kumpa mmoja wa wanawe, hiyo zawadi itakuwa pia kwa wazao wake, itakuwa mali yao kwa urithi.
Ainsi parle le Seigneur Yahweh: " Si le prince fait un don à quelqu'un de ses fils, ce don sera l'héritage de ses fils; ils le posséderont comme un héritage.
17 Hata hivyo, kama atatoa zawadi kutoka urithi wake na kumpa mmoja wa watumishi wake, mtumishi anaweza kuiweka mpaka mwaka wa uhuru, kisha itarudishwa kwa mkuu anayetawala. Urithi wake ni wa wanawe peke yao, ni mali yao.
Mais s'il fait à l'un de ses serviteurs un don pris sur son héritage, ce don appartiendra au serviteur jusqu'à l'année de la libération; puis il retournera au prince; c'est à ses fils seulement que restera son héritage.
18 Mkuu anayetawala hana ruhusa kuchukua urithi wowote wa watu na kuwaondoa kwenye mali zao. Mkuu atawalaye atawapa wanawe urithi wao, kutoka kwenye mali zake mwenyewe, ili kwamba pasiwe na mtu wangu yeyote atakayetengwa na urithi wake.’”
Le prince ne prendra l'héritage de personne en l'expulsant violemment de sa propriété; c'est de sa propriété qu'il donnera un héritage à ses fils, afin que mon peuple ne soit pas chassé, chacun de sa possession. "
19 Kisha mtu yule akanileta kwa kupitia kwenye ingilio lililokuwa kando ya lango mpaka kwenye vyumba vitakatifu vinavyoelekea kaskazini, ambavyo ni vya makuhani, naye akanionyesha mahali fulani upande wa mwisho wa magharibi.
Il me conduisit, par l'entrée qui est sur le côté du portique, dans les chambres saintes destinées aux prêtres, celles qui regardent le septentrion; et voici qu'il y avait là une place dans le fond, du côté de l'occident.
20 Akaniambia, “Mahali hapa ndipo makuhani watakapotokosea sadaka ya hatia na sadaka ya dhambi na kuoka sadaka ya nafaka, kuepuka kuzileta katika ukumbi wa nje na kushirikisha utakatifu kwa watu.”
Il me dit: " C'est l'endroit où les prêtres feront bouillir les victimes offertes pour le délit et pour le péché, et feront cuire l'oblation, afin de ne pas les transporter dans le parvis extérieur pour sanctifier le peuple. "
21 Baada ya hapo akanileta kwenye ukumbi wa nje na kunizungusha kwenye pembe zake nne, nami nikaona katika kila pembe ya huo ukumbi kulikuwa na ukumbi mwingine.
Puis il me fit sortir dans le parvis extérieur et me fit passer vers les quatre angles du parvis et voici qu'à chaque angle du parvis il y avait une cour.
22 Katika pembe nne za huo ukumbi wa nje kulikuwa na kumbi nyingine, zenye urefu wa dhiraa arobaini na upana wake dhiraa thelathini, ambapo hizo kumbi kwenye hizo pembe nne zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
Aux quatre angles du parvis, il y avait des cours fermées, longues de quarante coudées et larges de trente: une même dimension pour ces quatre cours aux angles.
23 Mzunguko wa ndani wa hizo kumbi nne ulikuwa na ukingo wa jiwe, zikiwa na sehemu zilizojengwa kwa ajili ya moto kuzunguka chini ya huo ukingo.
Une enceinte les entourait toutes les quatre, et des foyers à cuire étaient établis au bas de ces enceintes, tout autour.
24 Akaniambia, “Hizi ndizo sehemu za kupikia ambazo wale wanaohudumu kwenye Hekalu watatokosea dhabihu za watu.”
Il me dit: " Ce sont ici les cuisines où les serviteurs de la maison feront bouillir la chair des sacrifices du peuple. "

< Ezekieli 46 >