< Ezekieli 46 >

1 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Lango la ukumbi wa ndani linaloelekea upande wa mashariki litakuwa linafungwa kwa siku sita za juma, ila siku ya Sabato na siku ya Mwezi Mwandamo litafunguliwa.
Le Seigneur Yahvé dit: « La porte du parvis intérieur qui donne sur l'orient sera fermée les six jours ouvrables, mais elle sera ouverte le jour du sabbat et le jour de la nouvelle lune.
2 Mkuu anayetawala ataingia kupitia baraza ya njia ya lango la ukumbi na kusimama karibu na nguzo ya lango. Makuhani watatoa sadaka za mkuu anayetawala za kuteketezwa na sadaka za amani. Mkuu anayetawala atasujudu kwenye kizingiti cha njia ya lango, kisha atatoka nje, lakini lango halitafungwa mpaka jioni.
Le prince entrera par le chemin du porche de la porte extérieure, et se tiendra sur le poteau de la porte; les prêtres prépareront son holocauste et son sacrifice d'actions de grâces, et il se prosternera sur le seuil de la porte. Il sortira ensuite, mais la porte ne sera pas fermée avant le soir.
3 Siku za Sabato na za Mwezi mwandamo watu wote wa nchi wataabudu mbele za Bwana penye lile ingilio la ile njia.
Le peuple du pays se prosternera à l'entrée de cette porte devant Yahvé, les sabbats et les nouvelles lunes.
4 Sadaka ya kuteketezwa aletazo mkuu anayetawala kwa Bwana siku ya Sabato itakuwa ni wana-kondoo sita na kondoo dume mmoja, wote wasiwe na dosari.
L'holocauste que le prince offrira à Yahvé sera, le jour du sabbat, six agneaux sans défaut et un bélier sans défaut;
5 Sadaka ya nafaka inayotolewa pamoja na huyo kondoo dume itakuwa efa moja na sadaka ya nafaka inayotolewa na hao wana-kondoo itakuwa kiasi apendacho mtu pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
l'offrande sera d'un épha pour le bélier, et l'offrande pour les agneaux, selon ce qu'il pourra donner, et un hin d'huile pour un épha.
6 Siku ya mwezi mwandamo atatoa fahali mchanga, wana-kondoo sita na kondoo dume, wote wasiwe na dosari.
Le jour de la nouvelle lune, on offrira un jeune taureau sans défaut, six agneaux et un bélier. Ils seront sans défaut.
7 Atatoa kuwa sadaka ya nafaka efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja na kondoo dume mmoja na pamoja na wana-kondoo kama atakavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
Il préparera une offrande de repas: un épha pour le taureau, un épha pour le bélier, et pour les agneaux, selon ses moyens, et un hin d'huile par épha.
8 Wakati mkuu anayetawala aingiapo, atapitia kwenye baraza ya njia ya lango, naye atatoka nje kwa njia hiyo hiyo.
Lorsque le prince entrera, il entrera par le chemin du porche de la porte, et il sortira par son chemin.
9 “‘Wakati watu wa nchi wanapokuja mbele za Bwana katika sikukuu zilizoamriwa, yeyote aingiaye kwa lango la kaskazini kuabudu atatoka nje kwa lango la kusini na yeyote aingiaye kwa lango la kusini atatoka nje kwa lango la kaskazini. Hakuna mtu yeyote atakayerudi kwa kupitia lango lile aliloingilia, lakini kila mmoja atatoka nje kwa lango linalokabili lile aliloingilia.
"''Lorsque le peuple du pays se présentera devant Yahvé aux fêtes fixées, celui qui entrera par la porte nord pour se prosterner sortira par la porte sud, et celui qui entrera par la porte sud sortira par la porte nord. Il ne reviendra pas par le chemin de la porte par laquelle il est entré, mais il sortira droit devant lui.
10 Mkuu anayetawala atakuwa miongoni mwao, akiingia nao ndani wanapoingia, naye atatoka nao nje wanapotoka.
Le prince entrera avec eux quand ils entreront. Quand ils sortiront, il sortira.
11 “‘Kwenye sikukuu na kwenye sikukuu zilizoamriwa, sadaka ya nafaka itakuwa efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja pamoja na kondoo dume mmoja, pamoja na idadi ya wana-kondoo kama mtu apendavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
"''Aux fêtes et aux jours fériés, l'offrande de repas sera d'un épha pour un taureau, d'un épha pour un bélier et pour les agneaux selon ce qu'il pourra donner, et d'un hin d'huile pour un épha.
12 Mkuu anayetawala anapotoa sadaka ya hiari kwa Bwana, ikiwa ni sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya amani, lango linaloelekea mashariki litafunguliwa kwa ajili yake. Atatoa sadaka yake ya kuteketezwa au sadaka yake ya amani kama afanyavyo katika siku ya Sabato. Kisha atatoka nje, naye akiisha kutoka nje, lango litafungwa.
Lorsque le prince préparera un sacrifice volontaire, un holocauste ou un sacrifice d'actions de grâces, comme offrande volontaire à Yahvé, on lui ouvrira la porte qui donne sur l'orient; il préparera son holocauste et son sacrifice d'actions de grâces, comme il le fait le jour du sabbat. Puis il sortira, et après sa sortie, on fermera la porte.
13 “‘Kila siku utamtoa mwana-kondoo wa mwaka mmoja asiyekuwa na dosari kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, utaitoa kila siku asubuhi.
"''Tu prépareras chaque jour un agneau d'un an sans défaut pour l'holocauste à Yahvé. Tu le prépareras matin par matin.
14 Pia kila siku asubuhi pamoja na hiyo sadaka utatoa sadaka ya nafaka, ikiwa na sehemu ya sita ya efa pamoja na theluthi moja ya hini ya mafuta ya kuchanganya na ule unga. Utoaji wa sadaka hii ya nafaka kwa Bwana ni amri ya daima.
Tu prépareras avec lui, matin par matin, une offrande de farine, composée de la sixième partie d'un épha et du tiers d'un hin d'huile, pour mouiller la fleur de farine; c'est une offrande de farine à l'Éternel, en vertu d'une ordonnance perpétuelle.
15 Kwa hiyo mwana-kondoo na sadaka ya nafaka na mafuta vitatolewa kila siku asubuhi kwa ajili ya sadaka ya daima ya kuteketezwa.
Ils prépareront ainsi l'agneau, l'offrande et l'huile, matin par matin, pour un holocauste perpétuel. »
16 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ikiwa mkuu atawalaye atatoa zawadi kutoka kwenye urithi wake na kumpa mmoja wa wanawe, hiyo zawadi itakuwa pia kwa wazao wake, itakuwa mali yao kwa urithi.
"'Le Seigneur Yahvé dit: « Si le prince fait un don à l'un de ses fils, c'est son héritage. Il appartiendra à ses fils. C'est leur propriété par héritage.
17 Hata hivyo, kama atatoa zawadi kutoka urithi wake na kumpa mmoja wa watumishi wake, mtumishi anaweza kuiweka mpaka mwaka wa uhuru, kisha itarudishwa kwa mkuu anayetawala. Urithi wake ni wa wanawe peke yao, ni mali yao.
Mais s'il fait un don de son héritage à l'un de ses serviteurs, il lui appartiendra jusqu'à l'année de liberté; ensuite, il reviendra au prince; mais quant à son héritage, il appartiendra à ses fils.
18 Mkuu anayetawala hana ruhusa kuchukua urithi wowote wa watu na kuwaondoa kwenye mali zao. Mkuu atawalaye atawapa wanawe urithi wao, kutoka kwenye mali zake mwenyewe, ili kwamba pasiwe na mtu wangu yeyote atakayetengwa na urithi wake.’”
Le prince ne s'emparera pas de l'héritage du peuple pour l'évincer de sa propriété. Il donnera un héritage à ses fils sur sa propre propriété, afin que mon peuple ne soit pas dispersé de sa propriété. »'"
19 Kisha mtu yule akanileta kwa kupitia kwenye ingilio lililokuwa kando ya lango mpaka kwenye vyumba vitakatifu vinavyoelekea kaskazini, ambavyo ni vya makuhani, naye akanionyesha mahali fulani upande wa mwisho wa magharibi.
Puis il me fit passer par l'entrée, qui était sur le côté de la porte, dans les chambres saintes des prêtres, qui regardaient vers le nord. Voici, il y avait un endroit sur la partie arrière, vers l'ouest.
20 Akaniambia, “Mahali hapa ndipo makuhani watakapotokosea sadaka ya hatia na sadaka ya dhambi na kuoka sadaka ya nafaka, kuepuka kuzileta katika ukumbi wa nje na kushirikisha utakatifu kwa watu.”
Il me dit: « C'est ici que les prêtres feront cuire le sacrifice de culpabilité et le sacrifice pour le péché, et qu'ils feront cuire l'offrande, afin qu'ils ne les apportent pas dans le parvis extérieur, pour sanctifier le peuple. »
21 Baada ya hapo akanileta kwenye ukumbi wa nje na kunizungusha kwenye pembe zake nne, nami nikaona katika kila pembe ya huo ukumbi kulikuwa na ukumbi mwingine.
Puis il me fit sortir dans le parvis extérieur et me fit passer par les quatre coins du parvis; et voici, à chaque coin du parvis il y avait un parvis.
22 Katika pembe nne za huo ukumbi wa nje kulikuwa na kumbi nyingine, zenye urefu wa dhiraa arobaini na upana wake dhiraa thelathini, ambapo hizo kumbi kwenye hizo pembe nne zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
Aux quatre coins du parvis, il y avait des parvis fermés, longs de quarante coudées et larges de trente. Ces quatre cours aux angles étaient de même grandeur.
23 Mzunguko wa ndani wa hizo kumbi nne ulikuwa na ukingo wa jiwe, zikiwa na sehemu zilizojengwa kwa ajili ya moto kuzunguka chini ya huo ukingo.
Il y avait une muraille autour d'eux, autour des quatre, et des places bouillonnantes étaient faites sous les murs tout autour.
24 Akaniambia, “Hizi ndizo sehemu za kupikia ambazo wale wanaohudumu kwenye Hekalu watatokosea dhabihu za watu.”
Il me dit: « Ce sont les lieux d'ébullition, où les ministres de la maison feront bouillir le sacrifice du peuple. »

< Ezekieli 46 >