< Ezekieli 45 >
1 “‘Mtakapogawa nchi kuwa urithi, mtaitoa sehemu ya nchi kwa Bwana kuwa eneo takatifu, urefu wake dhiraa 25,000, upana wake dhiraa 20,000 eneo hili lote litakuwa takatifu.
Poleg tega, ko boste deželo z žrebom razdeljevali v dediščino, boste darovali daritev Gospodu, sveti delež dežele: dolžina bo petindvajset tisoč trstik in širina bo deset tisoč trstik. To bo sveto na vseh njihovih mejah naokoli.
2 Katika hiyo, itakuwepo sehemu mraba ambayo ni mahali patakatifu kila upande dhiraa 500 ikiwa imezungukwa na eneo la wazi lenye upana wa dhiraa hamsini.
Od tega bo tam za svetišče petsto v dolžino, s petsto v širino, kvadratno naokoli; in petdeset komolcev naokoli za njegova predmestja.
3 Katika eneo takatifu, pima sehemu yenye urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000. Ndani ya hilo eneo kutakuwa mahali patakatifu, Patakatifu pa Patakatifu.
Od te mere boš izmeril dolžino petindvajset tisoč in širino deset tisoč, in na njem bo svetišče in najsvetejši prostor.
4 Itakuwa sehemu takatifu ya nchi kwa ajili ya makuhani, wale wanaohudumu ndani ya mahali patakatifu na ambao hukaribia ili kuhudumu mbele za Bwana. Patakuwa mahali pa nyumba zao pamoja na sehemu kwa ajili ya mahali patakatifu.
Sveti delež dežele bo za duhovnike, služabnike svetišča, ki se bodo približali, da bi služili Gospodu in to bo prostor za njihove hiše in sveti prostor za svetišče.
5 Eneo la urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000 litakuwa la Walawi wale wanaotumika hekaluni, kama milki yao kwa ajili ya miji ya kuishi.
Petindvajset tisoč dolžine in deset tisoč širine bodo prav tako imeli Lévijevci, služabniki hiše, zase, za posest, za dvajset sob.
6 “‘Utatoa mji kama mali yao wenye upana wa dhiraa 5,000 na urefu wa dhiraa 25,000, karibu na sehemu takatifu, itakuwa mali ya nyumba yote ya Israeli.
Določili boste posest mesta, pet tisoč široko in petindvajset tisoč dolgo, nasproti daritve svetega deleža. Ta bo za celotno Izraelovo hišo.
7 “‘Mkuu anayetawala atakuwa na lile eneo linalopakana na lile eneo lililowekwa wakfu upande huu na upande huu na eneo la mji. Eneo la mji litaenea upande wa magharibi kuanzia upande wa magharibi na upande wa mashariki kuanzia upande wa mashariki, likiendelea kwa urefu kutoka magharibi hadi mpaka wa mashariki sambamba na mojawapo ya sehemu za makabila.
Delež bo za princa na eni strani in na drugi strani daritve svetega deleža in od mestne posesti, pred daritvijo svetega deleža in pred mestno posestjo od zahodne strani proti zahodu in od vzhodne strani proti vzhodu, in dolžina bo nasproti enemu izmed deležev od zahodne meje do vzhodne meje.
8 Nchi hii itakuwa milki yake katika Israeli. Nao wakuu wangu hawataonea tena watu wangu bali watairuhusu nyumba ya Israeli kuimiliki nchi kulingana na makabila yao.
V deželi bo njegova posest v Izraelu in moji princi ne bodo več zatirali mojega ljudstva in preostanek dežele bodo dali Izraelovi hiši, glede na njihove rodove.‹
9 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Yatosha, enyi wakuu wa Israeli! Acheni mbali ukatili wenu na uonevu wenu mkafanye lile lililo haki na sawa. Acheni kuwatoza watu wangu isivyo haki, asema Bwana Mwenyezi.
Tako govori Gospod Bog: ›Naj vam to zadostuje, oh Izraelovi princi: odstranite nasilje in rop, izvršujte sodbo in pravico, odstranite svoje razlastitve od mojega ljudstva, ‹ govori Gospod Bog.
10 Tumieni mizani sahihi na vipimo sahihi vya efa na bathi.
›Imeli boste pravične tehtnice in pravičen škaf in pravičen čeber.
11 Efa na bathi viwe sawa, bathi iwe sehemu ya kumi ya homeri na efa iwe sehemu ya kumi ya homeri, homeri itakuwa ndicho kiwango cha kukubalika kwa vyote viwili.
Škaf in čeber bosta ene mere, da bo čeber lahko vseboval deseti del tovora in škaf deseti del tovora; njegova mera bo po tovoru.
12 Shekeli moja itakuwa gera ishirini. Shekeli ishirini, jumlisha na shekeli ishirini na tano, jumlisha na shekeli kumi na tano zitakuwa mina moja.
Šekel bo dvajset ger. Dvajset šeklov, petindvajset šeklov, petnajst šeklov bo vaša mina.
13 “‘Hili ndilo toleo maalum mtakalotoa: moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya ngano na moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya shayiri.
To je daritev, ki jo boste darovali: šesti del škafa od tovora pšenice in dali boste šesti del škafa od tovora ječmena.
14 Sehemu ya mafuta iliyoamriwa, yaliyopimwa kwa bathi, ni sehemu ya kumi ya bathi kutoka kila kori moja (ambayo ina bathi kumi au homeri moja.)
Glede odredbe olja, čeber olja; darovali boste deseti del čebra iz kadi, kar je tovor desetih čebrov, kajti deset čebrov je tovor.
15 Pia kondoo mmoja atachukuliwa kutoka kwenye kila kundi la kondoo mia mbili kutoka kwenye malisho yaliyonyeshewa vizuri ya Israeli. Hivi vitatumika kwa ajili ya sadaka ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya watu, asema Bwana Mwenyezi.
Eno jagnje iz tropa, izmed dvesto, iz obilnih Izraelovih pašnikov; za jedilno daritev in za žgalno daritev in za mirovne daritve, da zanje opravijo pobotanje, ‹ govori Gospod Bog.
16 Watu wote wa nchi wataungana pamoja na mkuu anayetawala Israeli ili kutoa hii sadaka maalum.
›Vse ljudstvo dežele bo dalo to daritev za princa v Izraelu.
17 Huu utakuwa ndio wajibu wa mkuu anayetawala kutoa sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kwenye sikukuu, Mwezi Mwandamo na Sabato, kwenye sikukuu zote zilizoamriwa za nyumba ya Israeli. Atatoa sadaka za dhambi, sadaka za nafaka, sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ya Israeli.
To bo delež princa, da da žgalne daritve in jedilne daritve in pitne daritve ob praznikih, ob mlajih, ob šabatih, ob vseh slovesnostih Izraelove hiše. Pripravil bo daritev za greh, jedilno daritev, žgalno daritev in mirovne daritve, da opravi pobotanje za Izraelovo hišo.‹
18 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya huo mwezi utamchukua fahali mchanga asiye na dosari na kutakasa mahali patakatifu.
Tako govori Gospod Bog: ›V prvem mesecu, na prvi dan meseca, boš vzel mladega bikca brez pomanjkljivosti in očistil svetišče.
19 Kuhani itampasa achukue sehemu ya hiyo damu ya sadaka ya dhambi na kuipaka kwenye miimo ya Hekalu, kwenye pembe nne za juu za ukingo wa hayo madhabahu na juu ya miimo ya lango la ukumbi wa ndani.
Duhovnik bo vzel od krvi daritve za greh in jo pomazal na podboje hiše in na štiri vogale oltarnega podzidka in na podboje velikih vrat notranjega dvora.
20 Itakupasa kufanya vivyo hivyo katika siku ya saba ya mwezi huo kwa ajili ya mtu yeyote ambaye hutenda dhambi bila kukusudia au bila kujua, hivyo utafanya upatanisho kwa ajili ya Hekalu.
Tako boš delal sedmi dan meseca, za vsakega, ki se moti in za tistega, ki je preprost. Tako boš pobotal hišo.
21 “‘Katika mwezi wa kwanza siku ya kumi na nne utaadhimisha Pasaka. Sikukuu itaendelea kwa siku saba, wakati huo wa hizo siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
V prvem mesecu, na štirinajsti dan meseca, boste imeli pasho, sedemdnevni praznik; jedel se bo nekvašeni kruh.
22 Katika siku hiyo mkuu anayetawala atatoa fahali kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote wa nchi.
Na tisti dan bo princ zase in za vse ljudstvo dežele pripravil bikca za daritev za greh.
23 Kila siku wakati wa hizo siku saba za sikukuu atatoa mafahali saba na kondoo dume saba wasio na dosari kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana na beberu kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Sedem dni praznika bo pripravljal žgalno daritev Gospodu, sedem bikcev in sedem ovnov brez pomanjkljivosti, vsak dan, sedem dni; in vsak dan kozlička od koz za daritev za greh.
24 Pia atatoa sadaka ya nafaka efa moja kwa kila fahali na efa moja kwa kila kondoo dume, pamoja na hini moja ya mafuta kwa kila efa.
Pripravil bo jedilno daritev: škaf za bikca, škaf za ovna in vrč olja za škaf.
25 “‘Wakati wa hizo siku saba za sikukuu, ambayo huanza katika mwezi wa saba kwenye siku ya kumi na tano, mkuu anayetawala atatoa mahitaji yale yale kwa ajili ya sadaka za dhambi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta.
V sedmem mesecu, na petnajsti dan meseca, bo podobno storil ob prazniku sedmih dni, glede na daritev za greh, glede na žgalno daritev in glede na jedilno daritev in glede na olje.‹