< Ezekieli 45 >

1 “‘Mtakapogawa nchi kuwa urithi, mtaitoa sehemu ya nchi kwa Bwana kuwa eneo takatifu, urefu wake dhiraa 25,000, upana wake dhiraa 20,000 eneo hili lote litakuwa takatifu.
“““Além disso, ao dividir por lote a terra por herança, você oferecerá uma oferta a Iavé, uma porção sagrada da terra. O comprimento será o comprimento de vinte e cinco mil canas, e a largura será de dez mil. Ela será santa em toda a sua fronteira ao redor.
2 Katika hiyo, itakuwepo sehemu mraba ambayo ni mahali patakatifu kila upande dhiraa 500 ikiwa imezungukwa na eneo la wazi lenye upana wa dhiraa hamsini.
Dela haverá um quinhentos por quinhentos quadrados para o lugar santo, e cinqüenta côvados para suas terras de pasto ao redor.
3 Katika eneo takatifu, pima sehemu yenye urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000. Ndani ya hilo eneo kutakuwa mahali patakatifu, Patakatifu pa Patakatifu.
Desta medida, você deverá medir um comprimento de vinte e cinco mil, e uma largura de dez mil. Nele estará o santuário, que é o santíssimo.
4 Itakuwa sehemu takatifu ya nchi kwa ajili ya makuhani, wale wanaohudumu ndani ya mahali patakatifu na ambao hukaribia ili kuhudumu mbele za Bwana. Patakuwa mahali pa nyumba zao pamoja na sehemu kwa ajili ya mahali patakatifu.
É uma porção sagrada da terra; será para os sacerdotes, os ministros do santuário, que se aproximam para ministrar a Iavé. Será um lugar para suas casas e um lugar sagrado para o santuário.
5 Eneo la urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000 litakuwa la Walawi wale wanaotumika hekaluni, kama milki yao kwa ajili ya miji ya kuishi.
Vinte e cinco mil côvados de comprimento e dez mil de largura serão para os levitas, os ministros da casa, como uma posse para si mesmos, para vinte cômodos.
6 “‘Utatoa mji kama mali yao wenye upana wa dhiraa 5,000 na urefu wa dhiraa 25,000, karibu na sehemu takatifu, itakuwa mali ya nyumba yote ya Israeli.
“““Você designará a posse da cidade de cinco mil cúbitos de largura e vinte e cinco mil de comprimento, lado a lado com a oferta da porção sagrada. Será para toda a casa de Israel”.
7 “‘Mkuu anayetawala atakuwa na lile eneo linalopakana na lile eneo lililowekwa wakfu upande huu na upande huu na eneo la mji. Eneo la mji litaenea upande wa magharibi kuanzia upande wa magharibi na upande wa mashariki kuanzia upande wa mashariki, likiendelea kwa urefu kutoka magharibi hadi mpaka wa mashariki sambamba na mojawapo ya sehemu za makabila.
“““O que é para o príncipe será de um lado e do outro do loteamento santo e da posse da cidade, em frente do loteamento santo e em frente da posse da cidade, do lado oeste para oeste, e do lado leste para leste, e em comprimento correspondente a uma das porções, desde a fronteira oeste até a fronteira leste.
8 Nchi hii itakuwa milki yake katika Israeli. Nao wakuu wangu hawataonea tena watu wangu bali watairuhusu nyumba ya Israeli kuimiliki nchi kulingana na makabila yao.
Na terra será para ele uma possessão em Israel. Meus príncipes não oprimirão mais meu povo, mas darão a terra à casa de Israel de acordo com suas tribos”.
9 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Yatosha, enyi wakuu wa Israeli! Acheni mbali ukatili wenu na uonevu wenu mkafanye lile lililo haki na sawa. Acheni kuwatoza watu wangu isivyo haki, asema Bwana Mwenyezi.
“'O Senhor Javé diz: “Basta de vocês, príncipes de Israel! Removam a violência e o saque, e executem a justiça e a retidão! Parem de desapossar meu povo!” diz o Senhor Javé.
10 Tumieni mizani sahihi na vipimo sahihi vya efa na bathi.
“Vocês terão um equilíbrio justo, uma efa justa e um banho justo”.
11 Efa na bathi viwe sawa, bathi iwe sehemu ya kumi ya homeri na efa iwe sehemu ya kumi ya homeri, homeri itakuwa ndicho kiwango cha kukubalika kwa vyote viwili.
A efa e o banho serão de uma medida, que o banho pode conter um décimo de um homer, e a efa um décimo de um homer. Sua medida deve ser a mesma do homer.
12 Shekeli moja itakuwa gera ishirini. Shekeli ishirini, jumlisha na shekeli ishirini na tano, jumlisha na shekeli kumi na tano zitakuwa mina moja.
O siclo deve ser de vinte gerahs. Vinte shekels mais vinte e cinco shekels mais quinze shekels serão sua mina.
13 “‘Hili ndilo toleo maalum mtakalotoa: moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya ngano na moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya shayiri.
“““Esta é a oferta que você deve oferecer: a sexta parte de uma efa de um homer de trigo, e você dará a sexta parte de uma efa de um homer de cevada,
14 Sehemu ya mafuta iliyoamriwa, yaliyopimwa kwa bathi, ni sehemu ya kumi ya bathi kutoka kila kori moja (ambayo ina bathi kumi au homeri moja.)
e a porção de óleo, de um banho de óleo, um décimo de um banho fora do cor, que é dez banhos, até mesmo um homer (para dez banhos é um homer),
15 Pia kondoo mmoja atachukuliwa kutoka kwenye kila kundi la kondoo mia mbili kutoka kwenye malisho yaliyonyeshewa vizuri ya Israeli. Hivi vitatumika kwa ajili ya sadaka ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya watu, asema Bwana Mwenyezi.
e um cordeiro do rebanho em duzentos, dos pastos bem irrigados de Israel para uma oferta de refeição, para um holocausto e para ofertas de paz, para fazer expiação por eles”, diz o Senhor Yahweh.
16 Watu wote wa nchi wataungana pamoja na mkuu anayetawala Israeli ili kutoa hii sadaka maalum.
“Todo o povo da terra dará a esta oferta pelo príncipe em Israel.
17 Huu utakuwa ndio wajibu wa mkuu anayetawala kutoa sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kwenye sikukuu, Mwezi Mwandamo na Sabato, kwenye sikukuu zote zilizoamriwa za nyumba ya Israeli. Atatoa sadaka za dhambi, sadaka za nafaka, sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ya Israeli.
Será da parte do príncipe dar os holocaustos, as ofertas de refeições e as ofertas de bebidas, nas festas, nas luas novas e nos sábados, em todas as festas designadas da casa de Israel. Ele preparará a oferta pelo pecado, a oferta de refeição, o holocausto e as ofertas de paz, para fazer expiação pela casa de Israel”.
18 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya huo mwezi utamchukua fahali mchanga asiye na dosari na kutakasa mahali patakatifu.
“'O Senhor Javé diz: “No primeiro mês, no primeiro dia do mês, você tomará um touro jovem sem defeito, e limpará o santuário.
19 Kuhani itampasa achukue sehemu ya hiyo damu ya sadaka ya dhambi na kuipaka kwenye miimo ya Hekalu, kwenye pembe nne za juu za ukingo wa hayo madhabahu na juu ya miimo ya lango la ukumbi wa ndani.
O sacerdote tomará do sangue da oferta pelo pecado e o colocará nos umbrais da porta da casa, e nos quatro cantos do parapeito do altar, e nos umbrais do portão do pátio interno.
20 Itakupasa kufanya vivyo hivyo katika siku ya saba ya mwezi huo kwa ajili ya mtu yeyote ambaye hutenda dhambi bila kukusudia au bila kujua, hivyo utafanya upatanisho kwa ajili ya Hekalu.
Assim fará no sétimo dia do mês para todo aquele que erra, e para aquele que é simples. Assim fará a expiação pela casa.
21 “‘Katika mwezi wa kwanza siku ya kumi na nne utaadhimisha Pasaka. Sikukuu itaendelea kwa siku saba, wakati huo wa hizo siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
“““No primeiro mês, no décimo quarto dia do mês, você terá a Páscoa, uma festa de sete dias; pão ázimo será comido.
22 Katika siku hiyo mkuu anayetawala atatoa fahali kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote wa nchi.
Nesse dia, o príncipe preparará para si mesmo e para todo o povo da terra um touro para uma oferta pelo pecado.
23 Kila siku wakati wa hizo siku saba za sikukuu atatoa mafahali saba na kondoo dume saba wasio na dosari kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana na beberu kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Os sete dias da festa ele preparará um holocausto para Iavé, sete touros e sete carneiros sem defeito diariamente os sete dias; e um bode macho diariamente para uma oferta pelo pecado.
24 Pia atatoa sadaka ya nafaka efa moja kwa kila fahali na efa moja kwa kila kondoo dume, pamoja na hini moja ya mafuta kwa kila efa.
Ele preparará uma oferta de refeição, um efa para um touro, um efa para um carneiro, e um hin de óleo para um efa.
25 “‘Wakati wa hizo siku saba za sikukuu, ambayo huanza katika mwezi wa saba kwenye siku ya kumi na tano, mkuu anayetawala atatoa mahitaji yale yale kwa ajili ya sadaka za dhambi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta.
“““No sétimo mês, no décimo quinto dia do mês, durante a festa, ele fará assim durante sete dias. Ele fará a mesma provisão para a oferta pelo pecado, a oferta queimada, a oferta de refeição e o óleo”.

< Ezekieli 45 >