< Ezekieli 45 >

1 “‘Mtakapogawa nchi kuwa urithi, mtaitoa sehemu ya nchi kwa Bwana kuwa eneo takatifu, urefu wake dhiraa 25,000, upana wake dhiraa 20,000 eneo hili lote litakuwa takatifu.
«وقتی زمین میان قبایل اسرائیل تقسیم می‌شود، باید یک قسمت از آن به عنوان ملک مقدّس به خداوند وقف گردد. این ملک باید طولش دوازده کیلومتر و نیم و عرضش ده کیلومتر باشد. تمام این ملک، مقدّس خواهد بود.
2 Katika hiyo, itakuwepo sehemu mraba ambayo ni mahali patakatifu kila upande dhiraa 500 ikiwa imezungukwa na eneo la wazi lenye upana wa dhiraa hamsini.
این ملک مقدّس باید به دو قسمت مساوی تقسیم شود به طوری که طول هر قسمت دوازده کیلومتر و نیم و عرض آن پنج کیلومتر باشد. در یکی از این دو قسمت، باید خانهٔ خدا ساخته شود. مساحت خانهٔ خدا دویست و پنجاه مترمربع باشد و زمین اطراف آن به عرض بیست و پنج متر خالی بماند.
3 Katika eneo takatifu, pima sehemu yenye urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000. Ndani ya hilo eneo kutakuwa mahali patakatifu, Patakatifu pa Patakatifu.
4 Itakuwa sehemu takatifu ya nchi kwa ajili ya makuhani, wale wanaohudumu ndani ya mahali patakatifu na ambao hukaribia ili kuhudumu mbele za Bwana. Patakuwa mahali pa nyumba zao pamoja na sehemu kwa ajili ya mahali patakatifu.
این قسمت از زمین، مقدّس خواهد بود. منازل کاهنانی که در خانهٔ خدا خدمت می‌کنند، و نیز خانهٔ خدا در این قسمت از ملک مقدّس ساخته خواهد شد.
5 Eneo la urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000 litakuwa la Walawi wale wanaotumika hekaluni, kama milki yao kwa ajili ya miji ya kuishi.
قسمت دیگر ملک مقدّس، که آن هم دوازده کیلومتر و نیم طول و پنج کیلومتر عرض دارد باید برای محل سکونت لاویان که در خانهٔ خدا خدمت می‌کنند اختصاص یابد.
6 “‘Utatoa mji kama mali yao wenye upana wa dhiraa 5,000 na urefu wa dhiraa 25,000, karibu na sehemu takatifu, itakuwa mali ya nyumba yote ya Israeli.
«کنار ملک مقدّس یک قطعه زمین دیگر هم به طول دوازده کیلومتر و نیم و عرض دو کیلومتر و نیم در نظر گرفته شود. در این زمین، یک شهر برای قوم اسرائیل ساخته شود.
7 “‘Mkuu anayetawala atakuwa na lile eneo linalopakana na lile eneo lililowekwa wakfu upande huu na upande huu na eneo la mji. Eneo la mji litaenea upande wa magharibi kuanzia upande wa magharibi na upande wa mashariki kuanzia upande wa mashariki, likiendelea kwa urefu kutoka magharibi hadi mpaka wa mashariki sambamba na mojawapo ya sehemu za makabila.
«دو قطعه زمین نیز برای حاکم تعیین شود، یکی در جوار غربی ملک مقدّس و شهر، و دیگری در جوار شرقی آنها به طوری که طول هر یک از این دو قطعه زمین برابر مجموع عرض ملک مقدّس و عرض شهر باشد. این زمین از شرق به غرب به موازات یکی از زمینهای قبایل اسرائیل باشد.
8 Nchi hii itakuwa milki yake katika Israeli. Nao wakuu wangu hawataonea tena watu wangu bali watairuhusu nyumba ya Israeli kuimiliki nchi kulingana na makabila yao.
این دو قطعه زمین، سهم حاکم خواهد بود و حاکمان، دیگر بر قوم ظلم نخواهند کرد بلکه تمام زمین باقی مانده را به طور مساوی بین قبایل اسرائیل تقسیم نموده، سهم هر قبیله را به خودشان واگذار خواهند کرد.»
9 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Yatosha, enyi wakuu wa Israeli! Acheni mbali ukatili wenu na uonevu wenu mkafanye lile lililo haki na sawa. Acheni kuwatoza watu wangu isivyo haki, asema Bwana Mwenyezi.
خداوند یهوه به حاکمان اسرائیل می‌فرماید: «از غارت کردن و فریب دادن قوم من دست بکشید و ایشان را از میان ملک و خانه‌هایشان بیرون نکنید. همیشه با انصاف و درستکار باشید.
10 Tumieni mizani sahihi na vipimo sahihi vya efa na bathi.
«در معاملات خود تقلب نکنید بلکه از وزنه‌ها و میزانهای درست استفاده نمایید.
11 Efa na bathi viwe sawa, bathi iwe sehemu ya kumi ya homeri na efa iwe sehemu ya kumi ya homeri, homeri itakuwa ndicho kiwango cha kukubalika kwa vyote viwili.
ایفه و بت باید به یک اندازه یعنی هر یک، یک دهم حومر که واحد اندازه‌گیری است باشند.
12 Shekeli moja itakuwa gera ishirini. Shekeli ishirini, jumlisha na shekeli ishirini na tano, jumlisha na shekeli kumi na tano zitakuwa mina moja.
یک مثقال باید برابر بیست گِراه و یک منا برابر شصت مثقال باشد.
13 “‘Hili ndilo toleo maalum mtakalotoa: moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya ngano na moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya shayiri.
«میزان هدایایی که تقدیم می‌کنید بدین قرار است: یک شصتم از جو و گندمی که برداشت می‌کنید، یکصدم از روغنی که از درختان زیتون خود می‌گیرید، یک گوسفند از هر دویست گوسفندی که در چراگاههای اسرائیل دارید. اینها هدایای آردی و قربانیهای سوختنی و قربانیهای سلامتی هستند که قوم باید برای کفارهٔ گناهانشان تقدیم کنند. این را من که خداوند یهوه هستم می‌گویم.
14 Sehemu ya mafuta iliyoamriwa, yaliyopimwa kwa bathi, ni sehemu ya kumi ya bathi kutoka kila kori moja (ambayo ina bathi kumi au homeri moja.)
15 Pia kondoo mmoja atachukuliwa kutoka kwenye kila kundi la kondoo mia mbili kutoka kwenye malisho yaliyonyeshewa vizuri ya Israeli. Hivi vitatumika kwa ajili ya sadaka ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya watu, asema Bwana Mwenyezi.
16 Watu wote wa nchi wataungana pamoja na mkuu anayetawala Israeli ili kutoa hii sadaka maalum.
«قوم اسرائیل باید هدایای خود را به”حاکم“بدهند.
17 Huu utakuwa ndio wajibu wa mkuu anayetawala kutoa sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kwenye sikukuu, Mwezi Mwandamo na Sabato, kwenye sikukuu zote zilizoamriwa za nyumba ya Israeli. Atatoa sadaka za dhambi, sadaka za nafaka, sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ya Israeli.
وظیفهٔ حاکم این است که به هنگام عیدهای اول ماه، روزهای شَبّات و سایر اعیاد، حیوانات قربانی سوختنی، هدایای آردی و هدایای نوشیدنی را برای قوم آماده سازد. او باید قربانی گناه، هدایای آردی، قربانی سوختنی و قربانی سلامتی را برای کفارهٔ گناه قوم اسرائیل آماده سازد.»
18 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya huo mwezi utamchukua fahali mchanga asiye na dosari na kutakasa mahali patakatifu.
خداوند یهوه می‌فرماید: «در روز اول از ماه اول هر سال، برای تطهیر خانهٔ خدا یک گاو جوان بی‌عیب قربانی کن.
19 Kuhani itampasa achukue sehemu ya hiyo damu ya sadaka ya dhambi na kuipaka kwenye miimo ya Hekalu, kwenye pembe nne za juu za ukingo wa hayo madhabahu na juu ya miimo ya lango la ukumbi wa ndani.
کاهن مقداری از خون این قربانی گناه را گرفته، آن را بر چارچوب در خانهٔ خدا، بر چهار گوشهٔ مذبح و بر چهار چوب دروازهٔ حیاط داخلی بپاشد.
20 Itakupasa kufanya vivyo hivyo katika siku ya saba ya mwezi huo kwa ajili ya mtu yeyote ambaye hutenda dhambi bila kukusudia au bila kujua, hivyo utafanya upatanisho kwa ajili ya Hekalu.
در روز هفتم همان ماه، برای هر کس که سهواً یا ندانسته مرتکب گناهی شده باشد نیز همین کار را بکن. بدین ترتیب خانهٔ خدا تطهیر خواهد شد.
21 “‘Katika mwezi wa kwanza siku ya kumi na nne utaadhimisha Pasaka. Sikukuu itaendelea kwa siku saba, wakati huo wa hizo siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
«در روز چهاردهم همان ماه، عید پِسَح را به مدت هفت روز جشن بگیرید. در طی این هفت روز، فقط نان بدون خمیرمایه خورده شود.
22 Katika siku hiyo mkuu anayetawala atatoa fahali kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote wa nchi.
در روز اول عید، حاکم باید برای رفع گناه خود و گناه تمام قوم اسرائیل، یک گاو قربانی کند.
23 Kila siku wakati wa hizo siku saba za sikukuu atatoa mafahali saba na kondoo dume saba wasio na dosari kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana na beberu kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
در هر هفت روز عید، او باید قربانی سوختنی برای تقدیم به خداوند تدارک بیند. این قربانی، روزانه شامل هفت گاو و هفت قوچ بی‌عیب باشد. برای کفارهٔ گناه هم هر روز یک بز نر قربانی شود.
24 Pia atatoa sadaka ya nafaka efa moja kwa kila fahali na efa moja kwa kila kondoo dume, pamoja na hini moja ya mafuta kwa kila efa.
حاکم باید یک ایفه هدیهٔ آردی با هر گاو و یک ایفه هدیه آردی با هر قوچ تقدیم کند و نیز همراه هر ایفه آرد، یک هین روغن زیتون بدهد.
25 “‘Wakati wa hizo siku saba za sikukuu, ambayo huanza katika mwezi wa saba kwenye siku ya kumi na tano, mkuu anayetawala atatoa mahitaji yale yale kwa ajili ya sadaka za dhambi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta.
«روز پانزدهم ماه هفتم، عید سایبانها را به مدت هفت روز جشن بگیرید. در طی هفت روز این عید نیز حاکم باید قربانی گناه، قربانی سوختنی، هدیه آردی و روغن تقدیم کند.»

< Ezekieli 45 >