< Ezekieli 45 >

1 “‘Mtakapogawa nchi kuwa urithi, mtaitoa sehemu ya nchi kwa Bwana kuwa eneo takatifu, urefu wake dhiraa 25,000, upana wake dhiraa 20,000 eneo hili lote litakuwa takatifu.
" Quand vous partagerez au sort le pays pour le posséder, vous prélèverez comme offrande à Yahweh une portion sainte du pays; sa longueur sera de vingt-cinq mille coudées, et sa largeur de dix mille; elle sera sainte dans toute son étendue, tout autour.
2 Katika hiyo, itakuwepo sehemu mraba ambayo ni mahali patakatifu kila upande dhiraa 500 ikiwa imezungukwa na eneo la wazi lenye upana wa dhiraa hamsini.
Il y en aura pour le sanctuaire, cinq cents sur cinq cents, en carré, tout autour, et cinquante coudées pour sa banlieue, tout autour.
3 Katika eneo takatifu, pima sehemu yenye urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000. Ndani ya hilo eneo kutakuwa mahali patakatifu, Patakatifu pa Patakatifu.
Sur cet espace mesuré, tu mesureras une longueur de vingt-cinq mille et une largeur de dix mille; c'est là que sera le sanctuaire, le Saint des saints.
4 Itakuwa sehemu takatifu ya nchi kwa ajili ya makuhani, wale wanaohudumu ndani ya mahali patakatifu na ambao hukaribia ili kuhudumu mbele za Bwana. Patakuwa mahali pa nyumba zao pamoja na sehemu kwa ajili ya mahali patakatifu.
Ce sera une portion sainte du pays; elle sera pour les prêtres qui font le service du sanctuaire, qui s'approchent pour servir Yahweh; ce sera pour eux une place pour leurs maisons, et un lieu saint pour le sanctuaire.
5 Eneo la urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000 litakuwa la Walawi wale wanaotumika hekaluni, kama milki yao kwa ajili ya miji ya kuishi.
Vingt-cinq mille coudées en longueur et dix mille en largeur seront pour les lévites, qui font le service de la maison; ils y posséderont des villes pour y habiter.
6 “‘Utatoa mji kama mali yao wenye upana wa dhiraa 5,000 na urefu wa dhiraa 25,000, karibu na sehemu takatifu, itakuwa mali ya nyumba yote ya Israeli.
Comme possession de la ville, vous mettrez cinq mille coudées de largeur et une longueur de vingt-cinq mille, parallèlement à la portion sainte prélevée; cela appartiendra à la maison d'Israël.
7 “‘Mkuu anayetawala atakuwa na lile eneo linalopakana na lile eneo lililowekwa wakfu upande huu na upande huu na eneo la mji. Eneo la mji litaenea upande wa magharibi kuanzia upande wa magharibi na upande wa mashariki kuanzia upande wa mashariki, likiendelea kwa urefu kutoka magharibi hadi mpaka wa mashariki sambamba na mojawapo ya sehemu za makabila.
Pour le prince, vous réserverez un espace des deux côtés de la portion sainte prélevée et de la possession de la ville, le long de la portion sainte et le long de la possession de la ville, du côté de l'occident vers l'occident, et du côté de l'orient vers l'orient, sur une longueur correspondante à l'une des parts, de la frontière occidentale à la frontière orientale.
8 Nchi hii itakuwa milki yake katika Israeli. Nao wakuu wangu hawataonea tena watu wangu bali watairuhusu nyumba ya Israeli kuimiliki nchi kulingana na makabila yao.
Ce sera son domaine, sa possession en Israël; et mes princes n'opprimeront plus mon peuple, et ils laisseront le pays à la maison d'Israël, selon ses tribus.
9 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Yatosha, enyi wakuu wa Israeli! Acheni mbali ukatili wenu na uonevu wenu mkafanye lile lililo haki na sawa. Acheni kuwatoza watu wangu isivyo haki, asema Bwana Mwenyezi.
Ainsi parle le Seigneur Yahweh: C'en est assez, princes d'Israël! Ecartez la violence et la rapine! Faites droit et justice; ôtez vos exactions de dessus mon peuple, — oracle du Seigneur Yahweh.
10 Tumieni mizani sahihi na vipimo sahihi vya efa na bathi.
Ayez des balances justes, un épha juste et un bath juste.
11 Efa na bathi viwe sawa, bathi iwe sehemu ya kumi ya homeri na efa iwe sehemu ya kumi ya homeri, homeri itakuwa ndicho kiwango cha kukubalika kwa vyote viwili.
L'épha et le bath auront une même contenance, de sorte que l'épha contienne la dixième partie du homer, et le bath le dixième du homer; leur contenance sera d'après le homer.
12 Shekeli moja itakuwa gera ishirini. Shekeli ishirini, jumlisha na shekeli ishirini na tano, jumlisha na shekeli kumi na tano zitakuwa mina moja.
Le sicle vaudra vingt guéras. La mine aura chez vous vingt sicles, vingt-cinq sicles, quinze sicles.
13 “‘Hili ndilo toleo maalum mtakalotoa: moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya ngano na moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya shayiri.
Voici l'offrande que vous prélèverez: le sixième d'un épha sur le homer de froment, et le sixième d'un épha sur le homer d'orge.
14 Sehemu ya mafuta iliyoamriwa, yaliyopimwa kwa bathi, ni sehemu ya kumi ya bathi kutoka kila kori moja (ambayo ina bathi kumi au homeri moja.)
Règle pour l'huile, pour le bath d'huile: la dixième partie d'un bath sur un cor, lequel est égal à un homer de dix baths, car un homer fait dix baths.
15 Pia kondoo mmoja atachukuliwa kutoka kwenye kila kundi la kondoo mia mbili kutoka kwenye malisho yaliyonyeshewa vizuri ya Israeli. Hivi vitatumika kwa ajili ya sadaka ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya watu, asema Bwana Mwenyezi.
Une brebis du troupeau sera donnée sur deux cents des gras pâturages d'Israël, pour l'oblation, l'holocauste et les sacrifices pacifiques, afin de faire propitiation pour eux, — oracle du Seigneur Yahweh.
16 Watu wote wa nchi wataungana pamoja na mkuu anayetawala Israeli ili kutoa hii sadaka maalum.
Tout le peuple du pays devra prélever cette offrande pour le prince d'Israël.
17 Huu utakuwa ndio wajibu wa mkuu anayetawala kutoa sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kwenye sikukuu, Mwezi Mwandamo na Sabato, kwenye sikukuu zote zilizoamriwa za nyumba ya Israeli. Atatoa sadaka za dhambi, sadaka za nafaka, sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ya Israeli.
Mais le prince sera chargé des holocaustes, des oblations et des libations, aux fêtes, aux nouvelles lunes et aux sabbats, dans toutes les solennités de la maison d'Israël; c'est lui qui pourvoira aux sacrifices pour le péché, à l'oblation, à l'holocauste et aux sacrifices d'actions de grâces, afin de faire propitiation pour la maison d'Israël. "
18 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya huo mwezi utamchukua fahali mchanga asiye na dosari na kutakasa mahali patakatifu.
Ainsi parle le Seigneur Yahweh: " Le premier mois, le premier du mois, tu prendras un jeune taureau sans défaut, et tu feras l'expiation du sanctuaire.
19 Kuhani itampasa achukue sehemu ya hiyo damu ya sadaka ya dhambi na kuipaka kwenye miimo ya Hekalu, kwenye pembe nne za juu za ukingo wa hayo madhabahu na juu ya miimo ya lango la ukumbi wa ndani.
Le prêtre prendra du sang de la victime pour le péché et en mettra sur le poteau de la maison, sur les quatre coins du cadre de l'autel et sur le poteau du portique du parvis intérieur.
20 Itakupasa kufanya vivyo hivyo katika siku ya saba ya mwezi huo kwa ajili ya mtu yeyote ambaye hutenda dhambi bila kukusudia au bila kujua, hivyo utafanya upatanisho kwa ajili ya Hekalu.
Tu feras de même le sept du mois pour celui qui pèche par erreur ou par simplicité, et vous ferez propitiation pour la maison.
21 “‘Katika mwezi wa kwanza siku ya kumi na nne utaadhimisha Pasaka. Sikukuu itaendelea kwa siku saba, wakati huo wa hizo siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
Le premier mois, le quatorzième jour du mois, vous aurez la Pâque, fête d'une semaine de jours. On mangera des pains sans levain.
22 Katika siku hiyo mkuu anayetawala atatoa fahali kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote wa nchi.
Le prince offrira ce jour-là, pour lui et pour tout le peuple du pays, un taureau en sacrifice pour le péché.
23 Kila siku wakati wa hizo siku saba za sikukuu atatoa mafahali saba na kondoo dume saba wasio na dosari kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana na beberu kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Et pendant les sept jours de la fête, il offrira un holocauste à Yahweh, sept taureaux et sept béliers sans défaut, chacun des sept jours, et un bouc en sacrifice pour le péché chaque jour.
24 Pia atatoa sadaka ya nafaka efa moja kwa kila fahali na efa moja kwa kila kondoo dume, pamoja na hini moja ya mafuta kwa kila efa.
Il fera aussi l'oblation, un épha de farine par taureau et un épha par bélier, avec un hin d'huile par épha.
25 “‘Wakati wa hizo siku saba za sikukuu, ambayo huanza katika mwezi wa saba kwenye siku ya kumi na tano, mkuu anayetawala atatoa mahitaji yale yale kwa ajili ya sadaka za dhambi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta.
Le septième mois, le quinzième jour du mois, pendant la fête, il offrira pendant sept jours les mêmes sacrifices pour le péché, les mêmes holocaustes, les mêmes oblations et la même quantité d'huile."

< Ezekieli 45 >