< Ezekieli 45 >

1 “‘Mtakapogawa nchi kuwa urithi, mtaitoa sehemu ya nchi kwa Bwana kuwa eneo takatifu, urefu wake dhiraa 25,000, upana wake dhiraa 20,000 eneo hili lote litakuwa takatifu.
And whanne ye schulen bigynne to departe the lond bi partis, departe ye the firste thingis to the Lord, an halewid thing of the lond, fyue and twenti thousynde of rehedis in lengthe, and ten thousynde of rehedis in breede; it schal be halewid in al the coost therof by cumpas.
2 Katika hiyo, itakuwepo sehemu mraba ambayo ni mahali patakatifu kila upande dhiraa 500 ikiwa imezungukwa na eneo la wazi lenye upana wa dhiraa hamsini.
And it schal be halewid on ech part in fyue hundrid rehedis bi fyue hundrid, in foure sidis bi cumpas, and in fifti cubitis in to the subarbis therof bi cumpas.
3 Katika eneo takatifu, pima sehemu yenye urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000. Ndani ya hilo eneo kutakuwa mahali patakatifu, Patakatifu pa Patakatifu.
And fro this mesure thou schalt mete the lengthe of fyue and twenti thousynde of rehedis, and the breede of ten thousynde; and the temple and the hooli of hooli thingis schal be in it.
4 Itakuwa sehemu takatifu ya nchi kwa ajili ya makuhani, wale wanaohudumu ndani ya mahali patakatifu na ambao hukaribia ili kuhudumu mbele za Bwana. Patakuwa mahali pa nyumba zao pamoja na sehemu kwa ajili ya mahali patakatifu.
An halewid thing of the lond schal be to prestis, the mynystris of seyntuarie, that neiyen to the seruyce of the Lord; and a place schal be to hem in to housis, and in to the seyntuarie of hoolynesse.
5 Eneo la urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000 litakuwa la Walawi wale wanaotumika hekaluni, kama milki yao kwa ajili ya miji ya kuishi.
Sotheli fyue and twenti thousynde of lengthe schulen be, and ten thousynde of breede; but the dekenes that mynystren to the hous, thei schulen haue in possessioun twenti treseries.
6 “‘Utatoa mji kama mali yao wenye upana wa dhiraa 5,000 na urefu wa dhiraa 25,000, karibu na sehemu takatifu, itakuwa mali ya nyumba yote ya Israeli.
And ye schulen yyue the possessioun of the citee, fyue thousynde rehedis of breede, and fyue and twenti thousynde of lengthe, bi the departyng of the seyntuarie, to al the hous of Israel.
7 “‘Mkuu anayetawala atakuwa na lile eneo linalopakana na lile eneo lililowekwa wakfu upande huu na upande huu na eneo la mji. Eneo la mji litaenea upande wa magharibi kuanzia upande wa magharibi na upande wa mashariki kuanzia upande wa mashariki, likiendelea kwa urefu kutoka magharibi hadi mpaka wa mashariki sambamba na mojawapo ya sehemu za makabila.
And ye schulen yyue a porcioun to the prince on this side and on that side, bisidis the departyng of the seyntuarie, and bisidis the possessioun of the citee, ayens the face of departynge of seyntuarie, and ayens the face of possessioun of the citee; fro the side of the se til to the see, and fro the side of the eest `til to the eest, schal be of the possessioun of the prince. Forsothe the lengthe bi ech of the partis, fro the west ende til to the eest ende of the lond,
8 Nchi hii itakuwa milki yake katika Israeli. Nao wakuu wangu hawataonea tena watu wangu bali watairuhusu nyumba ya Israeli kuimiliki nchi kulingana na makabila yao.
schal be possessioun to hym in Israel; and the princes schulen no more robbe my puple, but thei schulen yyue the lond to the hous of Israel, bi the lynagis of hem.
9 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Yatosha, enyi wakuu wa Israeli! Acheni mbali ukatili wenu na uonevu wenu mkafanye lile lililo haki na sawa. Acheni kuwatoza watu wangu isivyo haki, asema Bwana Mwenyezi.
The Lord God seith these thingis, O! princes of Israel, suffice it to you, leue ye wickidnesse `and raueyns, and do ye doom and riytfulnesse; departe ye youre niy coostis fro my puple, seith the Lord God.
10 Tumieni mizani sahihi na vipimo sahihi vya efa na bathi.
A iust balaunce, and a iust mesure clepid ephi, and a iust mesure clepid bathus, schulen be to you.
11 Efa na bathi viwe sawa, bathi iwe sehemu ya kumi ya homeri na efa iwe sehemu ya kumi ya homeri, homeri itakuwa ndicho kiwango cha kukubalika kwa vyote viwili.
Ephi and bathus schulen be euene, and of o mesure, that bathus take the tenthe part of the mesure clepid corus, and that ephi take the tenthe part of the mesure corus; bi the mesure of corus schal be euene weiynge of tho.
12 Shekeli moja itakuwa gera ishirini. Shekeli ishirini, jumlisha na shekeli ishirini na tano, jumlisha na shekeli kumi na tano zitakuwa mina moja.
Forsothe a sicle schal haue twenti halpens; certis twenti siclis, and fyue and twenti siclis, and fiftene siclis maken a besaunt.
13 “‘Hili ndilo toleo maalum mtakalotoa: moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya ngano na moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya shayiri.
And these ben the firste fruytis whiche ye schulen take awei; the sixte part of ephi of a corus of wheete, and the sixte part of ephi of a corus of barli.
14 Sehemu ya mafuta iliyoamriwa, yaliyopimwa kwa bathi, ni sehemu ya kumi ya bathi kutoka kila kori moja (ambayo ina bathi kumi au homeri moja.)
Also the mesure of oile; a bathus of oile is the tenthe part of corus, and ten bathus maken o corus; for ten bathus fillen o corus.
15 Pia kondoo mmoja atachukuliwa kutoka kwenye kila kundi la kondoo mia mbili kutoka kwenye malisho yaliyonyeshewa vizuri ya Israeli. Hivi vitatumika kwa ajili ya sadaka ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya watu, asema Bwana Mwenyezi.
And `a ram of the floc of twei hundrid, of these whiche the men of Israel nurschen, in to sacrifice, and in to brent sacrifice, and in to pesible sacrifices, to clense for hem, seith the Lord God.
16 Watu wote wa nchi wataungana pamoja na mkuu anayetawala Israeli ili kutoa hii sadaka maalum.
Al the puple of the lond schal be boundun in these firste fruytis to the prince of Israel.
17 Huu utakuwa ndio wajibu wa mkuu anayetawala kutoa sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kwenye sikukuu, Mwezi Mwandamo na Sabato, kwenye sikukuu zote zilizoamriwa za nyumba ya Israeli. Atatoa sadaka za dhambi, sadaka za nafaka, sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ya Israeli.
And on the prince schulen be brent sacrifices, and sacrifice, and moiste sacrifices, in solempnytees, and in kalendis, ether bigynnyngis of monethis, and in sabatis, and in alle the solempnytees of the hous of Israel; he schal make sacrifice, for synne, and brent sacrifice, and pesible sacrifices, to clense for the hous of Israel.
18 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya huo mwezi utamchukua fahali mchanga asiye na dosari na kutakasa mahali patakatifu.
The Lord God seith these thingis, In the firste moneth, in the firste dai of the monethe, thou schalt take a calf with out wem of the drooue, and thou schalt clense the seyntuarie.
19 Kuhani itampasa achukue sehemu ya hiyo damu ya sadaka ya dhambi na kuipaka kwenye miimo ya Hekalu, kwenye pembe nne za juu za ukingo wa hayo madhabahu na juu ya miimo ya lango la ukumbi wa ndani.
And the preest schal take of the blood of the beeste, that schal be for synne; and he schal putte in the postis of the hous, and in foure corneris of the heiythe of the auter, and in the postis of the yate of the ynnere halle.
20 Itakupasa kufanya vivyo hivyo katika siku ya saba ya mwezi huo kwa ajili ya mtu yeyote ambaye hutenda dhambi bila kukusudia au bila kujua, hivyo utafanya upatanisho kwa ajili ya Hekalu.
And thus thou schalt do in the seuenthe dai of the monethe, for ech that knew not, and was disseyued bi errour, and thou schalt clense for the hous.
21 “‘Katika mwezi wa kwanza siku ya kumi na nne utaadhimisha Pasaka. Sikukuu itaendelea kwa siku saba, wakati huo wa hizo siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
In the firste monethe, in the fourtenthe dai of the monethe, the solempnytee of pask schal be to you; therf looues schulen be etun bi seuene daies.
22 Katika siku hiyo mkuu anayetawala atatoa fahali kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote wa nchi.
And the prince schal make a calf for synne in that dai, for hym silf and for al the puple of the lond.
23 Kila siku wakati wa hizo siku saba za sikukuu atatoa mafahali saba na kondoo dume saba wasio na dosari kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana na beberu kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
And in the solempnytee of seuene daies he schal make brent sacrifice to the Lord; he schal offre seuene caluys and seuene wetheris with out wem ech dai, bi seuene daies, and ech dai a buc of geet, for synne.
24 Pia atatoa sadaka ya nafaka efa moja kwa kila fahali na efa moja kwa kila kondoo dume, pamoja na hini moja ya mafuta kwa kila efa.
And he schal make the sacrifice of ephi by a calf, and of ephi by a wether, and of oile the mesure hyn, bi ech ephi.
25 “‘Wakati wa hizo siku saba za sikukuu, ambayo huanza katika mwezi wa saba kwenye siku ya kumi na tano, mkuu anayetawala atatoa mahitaji yale yale kwa ajili ya sadaka za dhambi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta.
In the seuenthe monethe, in the fiftenthe dai of the monethe, in the solempnytee, he schal make as tho ben biforseid, bi seuene daies, as wel for synne as for brent sacrifice, and in sacrifice, and in oile.

< Ezekieli 45 >