< Ezekieli 45 >

1 “‘Mtakapogawa nchi kuwa urithi, mtaitoa sehemu ya nchi kwa Bwana kuwa eneo takatifu, urefu wake dhiraa 25,000, upana wake dhiraa 20,000 eneo hili lote litakuwa takatifu.
Moreover when yee shall deuide the land for inheritance, ye shall offer an oblation vnto the Lord an holy portion of the land, fiue and twentie thousand reedes long, and ten thousand broad: this shalbe holy in all the borders thereof round about.
2 Katika hiyo, itakuwepo sehemu mraba ambayo ni mahali patakatifu kila upande dhiraa 500 ikiwa imezungukwa na eneo la wazi lenye upana wa dhiraa hamsini.
Of this there shalbe for the Sanctuarie fiue hundreth in length with fiue hundreth in breadth, all square round about, and fiftie cubites rounde about for the suburbes thereof.
3 Katika eneo takatifu, pima sehemu yenye urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000. Ndani ya hilo eneo kutakuwa mahali patakatifu, Patakatifu pa Patakatifu.
And of this measure shalt thou measure the length of fiue and twentie thousande, and the breadth of tenne thousande: and in it shalbe the Sanctuarie, and the most holy place.
4 Itakuwa sehemu takatifu ya nchi kwa ajili ya makuhani, wale wanaohudumu ndani ya mahali patakatifu na ambao hukaribia ili kuhudumu mbele za Bwana. Patakuwa mahali pa nyumba zao pamoja na sehemu kwa ajili ya mahali patakatifu.
The holy portion of the lande shalbe the Priests, which minister in the Sanctuarie, which came neere to serue the Lord: and it shalbe a place for their houses, and an holy place for the Sanctuarie.
5 Eneo la urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000 litakuwa la Walawi wale wanaotumika hekaluni, kama milki yao kwa ajili ya miji ya kuishi.
And in the fiue and twentie thousande of length, and the ten thousand of breadth shall the Leuites that minister in the house, haue their possession for twentie chambers.
6 “‘Utatoa mji kama mali yao wenye upana wa dhiraa 5,000 na urefu wa dhiraa 25,000, karibu na sehemu takatifu, itakuwa mali ya nyumba yote ya Israeli.
Also ye shall appoynt the possession of the citie, fiue thousand broad, and fiue and twentie thousand log ouer against the oblation of ye holy portion: it shalbe for the whole house of Israel.
7 “‘Mkuu anayetawala atakuwa na lile eneo linalopakana na lile eneo lililowekwa wakfu upande huu na upande huu na eneo la mji. Eneo la mji litaenea upande wa magharibi kuanzia upande wa magharibi na upande wa mashariki kuanzia upande wa mashariki, likiendelea kwa urefu kutoka magharibi hadi mpaka wa mashariki sambamba na mojawapo ya sehemu za makabila.
And a portion shalbe for the prince on ye one side, and on that side of the oblation of the holy portion, and of the possession of the citie, euen before the oblation of the holy portion, and before the possession of the citie from the West corner Westward, and from the East corner Eastward, and the length shalbe by one of the portions from the West border vnto the East border.
8 Nchi hii itakuwa milki yake katika Israeli. Nao wakuu wangu hawataonea tena watu wangu bali watairuhusu nyumba ya Israeli kuimiliki nchi kulingana na makabila yao.
In this lande shalbe his possession in Israel: and my princes shall no more oppresse my people, and the rest of the land shall they giue to ye house of Israel, according to their tribes.
9 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Yatosha, enyi wakuu wa Israeli! Acheni mbali ukatili wenu na uonevu wenu mkafanye lile lililo haki na sawa. Acheni kuwatoza watu wangu isivyo haki, asema Bwana Mwenyezi.
Thus saith the Lord God, Let it suffice you, O princes of Israel: leaue off crueltie and oppression, and execute iudgment and iustice: take away your exactions from my people, sayth the Lord God.
10 Tumieni mizani sahihi na vipimo sahihi vya efa na bathi.
Ye shall haue iust balances, and a true Ephah, and a true Bath.
11 Efa na bathi viwe sawa, bathi iwe sehemu ya kumi ya homeri na efa iwe sehemu ya kumi ya homeri, homeri itakuwa ndicho kiwango cha kukubalika kwa vyote viwili.
The Ephah and the Bath shalbe equall: a Bath shall conteyne the tenth part of an Homer, and an Ephah the tenth part of an Homer: the equalitie thereof shalbe after the Homer.
12 Shekeli moja itakuwa gera ishirini. Shekeli ishirini, jumlisha na shekeli ishirini na tano, jumlisha na shekeli kumi na tano zitakuwa mina moja.
And the shekel shalbe twentie gerahs, and twentie shekels, and fiue and twentie shekels and fifteene shekels shalbe your Maneh.
13 “‘Hili ndilo toleo maalum mtakalotoa: moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya ngano na moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya shayiri.
This is the oblation that ye shall offer, ye sixt part of an Ephah of an Homer of wheat, and ye shall giue the sixt part of an Ephah of an Homer of barley.
14 Sehemu ya mafuta iliyoamriwa, yaliyopimwa kwa bathi, ni sehemu ya kumi ya bathi kutoka kila kori moja (ambayo ina bathi kumi au homeri moja.)
Concerning ye ordinance of the oyle, euen of the Bath of oyle, ye shall offer the tenth part of a Bath out of ye Cor (ten Baths are an Homer: for ten Baths fill an Homer)
15 Pia kondoo mmoja atachukuliwa kutoka kwenye kila kundi la kondoo mia mbili kutoka kwenye malisho yaliyonyeshewa vizuri ya Israeli. Hivi vitatumika kwa ajili ya sadaka ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya watu, asema Bwana Mwenyezi.
And one lambe of two hundreth sheepe out of ye fat pastures of Israel for a meat offring, and for a burnt offring and for peace offrings, to make reconciliation for them, sayth the Lord God.
16 Watu wote wa nchi wataungana pamoja na mkuu anayetawala Israeli ili kutoa hii sadaka maalum.
All the people of the lande shall giue this oblation for the prince in Israel.
17 Huu utakuwa ndio wajibu wa mkuu anayetawala kutoa sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kwenye sikukuu, Mwezi Mwandamo na Sabato, kwenye sikukuu zote zilizoamriwa za nyumba ya Israeli. Atatoa sadaka za dhambi, sadaka za nafaka, sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ya Israeli.
And it shalbe ye princes part to giue burnt offrings, and meat offrings, and drinke offrings in the solemne feasts and in the newe moones, and in the Sabbaths, and in all the hie feasts of the house of Israel: he shall prepare the sinne offring, and the meat offring, and the burnt offring, and the peace offrings to make reconciliation for the house of Israel.
18 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya huo mwezi utamchukua fahali mchanga asiye na dosari na kutakasa mahali patakatifu.
Thus sayth the Lord God, In the first moneth, in the first day of the moneth, thou shalt take a yong bullocke without blemish and clense the Sanctuarie.
19 Kuhani itampasa achukue sehemu ya hiyo damu ya sadaka ya dhambi na kuipaka kwenye miimo ya Hekalu, kwenye pembe nne za juu za ukingo wa hayo madhabahu na juu ya miimo ya lango la ukumbi wa ndani.
And the Priest shall take of the blood of the sinne offring, and put it vpon the posts of the house, and vpon the foure corners of the frame of the altar, and vpon the postes of the gate of the inner court.
20 Itakupasa kufanya vivyo hivyo katika siku ya saba ya mwezi huo kwa ajili ya mtu yeyote ambaye hutenda dhambi bila kukusudia au bila kujua, hivyo utafanya upatanisho kwa ajili ya Hekalu.
And so shalt thou doe the seuenth day of the moneth, for euery one that hath erred and for him that is deceiued: so shall you reconcile the house.
21 “‘Katika mwezi wa kwanza siku ya kumi na nne utaadhimisha Pasaka. Sikukuu itaendelea kwa siku saba, wakati huo wa hizo siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
In the first moneth in the foureteenth day of the moneth, ye shall haue the Passeouer, a feast of seuen dayes, and ye shall eate vnleauened bread.
22 Katika siku hiyo mkuu anayetawala atatoa fahali kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote wa nchi.
And vpon that day, shall the prince prepare for him selfe, and for all the people of the lande, a bullocke for a sinne offring.
23 Kila siku wakati wa hizo siku saba za sikukuu atatoa mafahali saba na kondoo dume saba wasio na dosari kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana na beberu kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
And in the seuen dayes of the feast he shall make a burnt offring to the Lord, euen of seuen bullockes, and seuen rammes without blemish dayly for seuen dayes, and an hee goate dayly for a sinne offring.
24 Pia atatoa sadaka ya nafaka efa moja kwa kila fahali na efa moja kwa kila kondoo dume, pamoja na hini moja ya mafuta kwa kila efa.
And he shall prepare a meate offring of an Ephah for a bullocke, an Ephah for a ramme, and an Hin of oyle for an Ephah.
25 “‘Wakati wa hizo siku saba za sikukuu, ambayo huanza katika mwezi wa saba kwenye siku ya kumi na tano, mkuu anayetawala atatoa mahitaji yale yale kwa ajili ya sadaka za dhambi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta.
In the seuenth moneth, in the fifteenth day of the moneth, shall he do the like in the feast for seuen dayes, according to the sinne offring, according to the burnt offring, and according to the meate offring, and according to the oyle.

< Ezekieli 45 >