< Ezekieli 43 >

1 Kisha yule mtu akanileta kwenye lango linaloelekea upande wa mashariki,
Adam beni doğuya bakan kapıya götürdü.
2 nami nikaona utukufu wa Mungu wa Israeli ukija kutoka upande wa mashariki. Sauti yake ilikuwa kama ya ngurumo ya maji yaendayo kasi, nayo nchi ikangʼaa kwa utukufu wake.
İsrail Tanrısı'nın görkeminin doğudan geldiğini gördüm. Sesi gürül gürül akan suların sesi gibiydi. Görkeminden yeryüzü aydınlıkla doldu.
3 Maono niliyoyaona yalikuwa kama maono yale niliyokuwa nimeyaona wakati Mungu alipokuja kuangamiza mji na kama maono niliyokuwa nimeyaona kando ya Mto wa Kebari, nami nikaanguka kifudifudi.
Gördüğüm görüm, Tanrı kenti yok etmeye geldiğinde ve Kevar Irmağı kıyısında gördüğüm görümlere benziyordu. Yüzüstü yere düştüm.
4 Utukufu wa Bwana ukaingia hekaluni kwa kupitia lango linaloelekea upande wa mashariki.
RAB'bin görkemi doğuya bakan kapıdan tapınağa girdi.
5 Kisha Roho akanichukua na kunileta katika ule ua wa ndani, nao utukufu wa Bwana ulilijaza Hekalu.
Ruh beni ayağa kaldırıp iç avluya götürdü. RAB'bin görkemi tapınağı doldurdu.
6 Wakati yule mtu akiwa amesimama kando yangu, nilisikia mtu mmoja akisema nami kutoka ndani ya Hekalu.
Adam orada yanımda dururken, tapınaktan birinin bana seslendiğini duydum.
7 Akasema, “Mwanadamu, hapa ni mahali pa kiti changu cha enzi na mahali pa kuweka nyayo za miguu yangu. Hapa ndipo nitakapoishi miongoni mwa Waisraeli milele. Kamwe nyumba ya Israeli hawatalinajisi tena Jina langu takatifu, yaani, wao wala wafalme wao, kwa ukahaba wao na kwa sanamu zao zisizokuwa na uhai za wafalme wao katika mahali pao pa juu pa kuabudia miungu.
Bana şöyle dedi: “İnsanoğlu, tahtımın yeri, ayaklarımın basacağı, İsrail halkıyla sonsuza dek yaşayacağım yer burasıdır. Bundan böyle İsrail halkı da kralları da fahişelikleriyle ve krallarının cesetleriyle bir daha kutsal adımı kirletmeyecek.
8 Walipoweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu na miimo yao ya milango karibu na miimo yangu, pakiwa na ukuta tu kati yangu na wao, walilinajisi Jina langu takatifu kwa matendo yao ya machukizo. Kwa sababu hiyo niliwaangamiza kwa hasira yangu.
Onlar kapı eşiklerini kapı eşiğimin, sövelerini sövelerimin bitişiğine yerleştirdiler. Benimle aralarında yalnızca bir duvar vardı. İğrenç uygulamalarıyla kutsal adımı kirlettiler. Bu yüzden öfkemle onları yok ettim.
9 Basi sasa na waweke mbali nami ukahaba wao na sanamu za wafalme wao zisizo na uhai, nami nitakaa miongoni mwao milele.
Şimdi fahişeliklerini, krallarının cesetlerini benden uzaklaştırsınlar; ben de sonsuza dek aralarında yaşayayım.
10 “Mwanadamu, elezea hilo Hekalu kwa watu wa Israeli, ili wapate kuona aibu kwa ajili ya dhambi zao. Wao na wapime hicho kielelezo.
“İnsanoğlu, günahlarından utanmaları için bu tapınağı İsrail halkına tanıt. Tapınağın tasarısını incelesinler.
11 Wakishaona aibu kwa ajili ya yale yote waliyotenda, wafahamishe kielelezo cha hilo Hekalu, yaani mpangilio wake, maingilio yake ya kutoka na kuingia, kielelezo chake chote, na masharti yake yote na sheria zake zote. Yaandike haya mbele yao ili wapate kuwa waaminifu kwa hicho kielelezo chake na kufuata masharti yake yote.
Eğer bütün yaptıklarından utanıyorlarsa, tapınağın tasarını –düzenlemesini, girişlerini, çıkışlarını– kurallarını, yasalarını onlara bildir. Tasarı onların gözü önünde yaz ki, bütün düzenine, kurallarına bağlılıkla uyabilsinler.
12 “Hii ndiyo sheria ya Hekalu: Eneo lote linalozunguka Hekalu juu ya mlima litakuwa takatifu kuliko yote. Hii ndiyo sheria ya Hekalu.
Tapınakla ilgili yasa şudur: Dağın tepesinde tapınağı çevreleyen bütün alan çok kutsal olacak. İşte tapınakla ilgili yasa böyle.
13 “Hivi ndivyo vipimo vya madhabahu kwa dhiraa ndefu, yaani, dhiraa moja na nyanda nne: Tako lake liwe na kina cha hiyo dhiraa moja na upana wa hiyo dhiraa moja, ikiwa na ukingo wa shibiri moja kuizunguka pembeni. Hiki kitakuwa ndicho kimo cha madhabahu:
“Arşın ölçüsüyle sunağın ölçüleri şunlardır: –Bu arşın, bir arşına ek olarak bir elin eni kadardır.– Sunağı çevreleyen hendeğin derinliği bir arşın, genişliği bir arşın, çevresindeki kenarlık bir karış. Sunağın yüksekliğiyse şöyle:
14 Kimo cha msingi kuanzia usawa wa ardhi mpaka kwenye mfereji sehemu ya chini kimo chake ni dhiraa mbili na upana wake ni dhiraa moja na kuanzia kwenye ukingo mdogo hadi kwenye ukingo mpana kimo chake ni dhiraa nne na upana wake ni dhiraa moja.
Sunağın yerdeki hendekten alt çıkıntıya kadarki bölümünün yüksekliği iki arşın, genişliği bir arşın, küçük çıkıntıdan büyük çıkıntıya kadarki bölümün yüksekliği dört arşın, genişliği bir arşın.
15 Pale pawashwapo moto madhabahuni kimo chake kitakuwa dhiraa nne, na pembe nne zinazoelekeza juu kutoka pale pawashwapo moto.
Sunağın kurban yakılan üst bölümünün yüksekliği dört arşın; üst bölümden yukarı doğru dört boynuz uzanacak.
16 Pale pawashwapo moto pa madhabahu ni mraba, urefu wake ni dhiraa kumi na mbili na upana wa dhiraa kumi na mbili.
Sunağın üst bölümü kare şeklinde olacak. Uzunluğu on iki arşın, genişliği on iki arşın.
17 Pia sehemu ya juu ni mraba, urefu wake dhiraa kumi na nne na upana wa dhiraa kumi na nne, ikiwa na ukingo wa nusu dhiraa na mfereji kuizunguka madhabahu. Ngazi za kupandia madhabahuni zitaelekea upande wa mashariki.”
Üst çıkıntının dört yandan uzunluğu ve genişliği de on dörder arşın. Çevresindeki kenarlık yarım arşın, hendeğin çevresi bir arşın. Sunağın basamakları doğuya bakacak.”
18 Kisha akaniambia, “Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Haya ndiyo yatakayokuwa masharti ya kutoa dhabihu za kuteketezwa na kunyunyiza damu juu ya madhabahu itakapokuwa imejengwa.
Adam konuşmasını şöyle sürdürdü: “İnsanoğlu, Egemen RAB şöyle diyor: ‘Sunak yapılacağı gün, üzerinde yakmalık sunular sunmak ve kan dökmek için kurallar şunlardır:
19 Utatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi kwa makuhani, ambao ni Walawi, wa jamaa ya Sadoki, ndio watakaonikaribia kuhudumu mbele zangu, asema Bwana Mwenyezi.
Bana hizmet etmek üzere önüme gelen Sadok soyundan Levili kâhinlere günah sunusu olarak bir boğa vereceksin. Egemen RAB böyle diyor.
20 Itakupasa kuchukua baadhi ya hiyo damu ya mnyama huyo na kuiweka juu ya hizo pembe nne za madhabahu na juu ya ncha zake nne za sehemu ya juu kuzunguka ukingo wote, ili kuitakasa madhabahu na kufanya upatanisho kwa ajili yake.
Boğanın kanından biraz alıp sunağın dört boynuzuna, çıkıntının dört köşesine ve çevresindeki kenarlığın üzerine süreceksin. Böylece sunağı pak kılıp arındıracaksın.
21 Itakupasa kumchukua huyo fahali mchanga kwa ajili ya sadaka ya dhambi na kumteketeza mahali palipoagizwa katika eneo la Hekalu nje ya mahali Patakatifu.
Boğayı günah sunusu olarak alacak, tapınağın dışında, tapınak alanında belirlenen yerde yakacaksın.
22 “Siku ya pili yake utamtoa beberu asiye na dosari kwa ajili ya sadaka ya dhambi, nayo madhabahu itatakaswa kama ilivyotakaswa kwa yule fahali.
“‘İkinci gün günah sunusu olarak kusursuz bir teke sunacaksın. Sunağı boğanın kanıyla arındırdığın gibi tekenin kanıyla da arındır.
23 Utakapokuwa umemaliza kazi ya kuitakasa, utamtoa fahali mchanga pamoja na kondoo dume toka kwenye kundi, wote wawe hawana dosari.
Arındırma işlemini bitirince, sürüden kusursuz bir boğayla bir koç sunacaksın.
24 Utawatoa mbele za Bwana, nao makuhani watanyunyizia chumvi juu yao na kuwatoa kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.
Bunları RAB'bin önüne getireceksin. Kâhinler üzerlerine tuz serpip yakmalık sunu olarak RAB'be sunacaklar.
25 “Kwa siku saba itakupasa kutoa beberu kila siku kwa ajili ya sadaka ya dhambi, pia itakupasa kutoa fahali mchanga na kondoo dume kutoka zizini, wote wawe hawana dosari.
“‘Yedi gün boyunca günah sunusu olarak her gün bir teke sağlayacaksın; kusursuz bir boğayla sürüden bir koç da sağlayacaksın.
26 Kwa siku saba itawapasa kufanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuitakasa na hivyo ndivyo watakavyoiweka wakfu.
Yedi gün sunağı arındırıp pak kılacaklar. Böylece sunak adanmış olacak.
27 Mwishoni mwa hizi siku saba, kuanzia siku ya nane na kuendelea, itawapasa makuhani kutoa sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za amani juu ya madhabahu. Kisha nitawakubali ninyi, asema Bwana Mwenyezi.”
Yedi gün bitince, kâhinler sekizinci gün ve daha sonra yakmalık ve esenlik sunularınızı sunağın üzerinde sunacak. O zaman sizi kabul edeceğim. Egemen RAB böyle diyor.’”

< Ezekieli 43 >