< Ezekieli 43 >

1 Kisha yule mtu akanileta kwenye lango linaloelekea upande wa mashariki,
И веде мя ко вратом зрящым на востоки и изведе мя:
2 nami nikaona utukufu wa Mungu wa Israeli ukija kutoka upande wa mashariki. Sauti yake ilikuwa kama ya ngurumo ya maji yaendayo kasi, nayo nchi ikangʼaa kwa utukufu wake.
и се, слава Бога Израилева грядяше по пути врат зрящих на востоки, и глас полка аки глас усугубляющих многих, и земля светяшеся аки свет от славы Его окрест.
3 Maono niliyoyaona yalikuwa kama maono yale niliyokuwa nimeyaona wakati Mungu alipokuja kuangamiza mji na kama maono niliyokuwa nimeyaona kando ya Mto wa Kebari, nami nikaanguka kifudifudi.
И видение, еже видех, по видению, еже видех, егда вхождах помазати град: и видение колесницы, юже видех, подобяшеся видению, еже видех на реце Ховар. И падох на лице мое.
4 Utukufu wa Bwana ukaingia hekaluni kwa kupitia lango linaloelekea upande wa mashariki.
Слава же Господня вниде во храм по пути врат зрящих на восток.
5 Kisha Roho akanichukua na kunileta katika ule ua wa ndani, nao utukufu wa Bwana ulilijaza Hekalu.
И взя мя дух и введе мя во двор внутренний: и се, полн славы дом Господень.
6 Wakati yule mtu akiwa amesimama kando yangu, nilisikia mtu mmoja akisema nami kutoka ndani ya Hekalu.
И стах, и се, глас от храма глаголющаго ко мне, и муж стояше близ мене
7 Akasema, “Mwanadamu, hapa ni mahali pa kiti changu cha enzi na mahali pa kuweka nyayo za miguu yangu. Hapa ndipo nitakapoishi miongoni mwa Waisraeli milele. Kamwe nyumba ya Israeli hawatalinajisi tena Jina langu takatifu, yaani, wao wala wafalme wao, kwa ukahaba wao na kwa sanamu zao zisizokuwa na uhai za wafalme wao katika mahali pao pa juu pa kuabudia miungu.
и рече ко мне: сыне человечь, видел ли еси место престола Моего и место стопы ног Моих, идеже вселится имя Мое среде дому Израилева во век? И не осквернят ктому имене Моего святаго дом Израилев, тии и старейшины их во блужении своем и во убийствах старейшин своих среде себе,
8 Walipoweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu na miimo yao ya milango karibu na miimo yangu, pakiwa na ukuta tu kati yangu na wao, walilinajisi Jina langu takatifu kwa matendo yao ya machukizo. Kwa sababu hiyo niliwaangamiza kwa hasira yangu.
внегда полагаху преддверие Мое во преддвериих своих и праги Моя близ прагов своих: и даша стену Мою яко держащуюся Мене и онех, и оскверниша имя Мое святое в беззакониих своих, яже творяху: и скончах я в ярости Моей и во избиении:
9 Basi sasa na waweke mbali nami ukahaba wao na sanamu za wafalme wao zisizo na uhai, nami nitakaa miongoni mwao milele.
и ныне да отринут блужение свое и убийства старейшин своих от Мене, и вселюся среде их во век.
10 “Mwanadamu, elezea hilo Hekalu kwa watu wa Israeli, ili wapate kuona aibu kwa ajili ya dhambi zao. Wao na wapime hicho kielelezo.
Ты же, сыне человечь, покажи дому Израилеву храм, и да престанут от грехов своих: и видение его, и чиноположение его,
11 Wakishaona aibu kwa ajili ya yale yote waliyotenda, wafahamishe kielelezo cha hilo Hekalu, yaani mpangilio wake, maingilio yake ya kutoka na kuingia, kielelezo chake chote, na masharti yake yote na sheria zake zote. Yaandike haya mbele yao ili wapate kuwa waaminifu kwa hicho kielelezo chake na kufuata masharti yake yote.
и тии приимут казнь свою о всех, яже сотвориша: и распишеши храм и уготование его, и исходы его и входы его, и бытие его и вся повеления его и вся законы его возвестиши им и да впишеши пред ними, и снабдят вся оправдания Моя и вся повеления Моя и сотворят я.
12 “Hii ndiyo sheria ya Hekalu: Eneo lote linalozunguka Hekalu juu ya mlima litakuwa takatifu kuliko yote. Hii ndiyo sheria ya Hekalu.
И расписание храма на верху горы: вси пределы его окрест Святая Святых суть.
13 “Hivi ndivyo vipimo vya madhabahu kwa dhiraa ndefu, yaani, dhiraa moja na nyanda nne: Tako lake liwe na kina cha hiyo dhiraa moja na upana wa hiyo dhiraa moja, ikiwa na ukingo wa shibiri moja kuizunguka pembeni. Hiki kitakuwa ndicho kimo cha madhabahu:
Сей закон храма, и сия мера требника, в лакоть лактя и длани, недро глубины лакоть на лакоть и лакоть в широту, и ограждение устия ему окрест, пяди.
14 Kimo cha msingi kuanzia usawa wa ardhi mpaka kwenye mfereji sehemu ya chini kimo chake ni dhiraa mbili na upana wake ni dhiraa moja na kuanzia kwenye ukingo mdogo hadi kwenye ukingo mpana kimo chake ni dhiraa nne na upana wake ni dhiraa moja.
И сия высота требника, и от глубины начала вдоления его ко очистилищу великому, еже внизу, двух лактей, широта же лакоть: а от очистилища малаго ко очистилищу великому лакти четыри, и широта лакоть.
15 Pale pawashwapo moto madhabahuni kimo chake kitakuwa dhiraa nne, na pembe nne zinazoelekeza juu kutoka pale pawashwapo moto.
И ариил четырех лактей, а от ариила и выше рогов лакоть:
16 Pale pawashwapo moto pa madhabahu ni mraba, urefu wake ni dhiraa kumi na mbili na upana wa dhiraa kumi na mbili.
ариил же дванадесять лактей в долготу и дванадесять лактей в широту, четвероуголен на четыри части своя.
17 Pia sehemu ya juu ni mraba, urefu wake dhiraa kumi na nne na upana wa dhiraa kumi na nne, ikiwa na ukingo wa nusu dhiraa na mfereji kuizunguka madhabahu. Ngazi za kupandia madhabahuni zitaelekea upande wa mashariki.”
И очистилище четыренадесять лактей в долготу и четыренадесять лактей в широту, четвероуголно на четыри части своя: и ограждение ему окрест окружающее его пол лактя, и обдержание его лакоть окрест, и степени его зрящыя на восток.
18 Kisha akaniambia, “Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Haya ndiyo yatakayokuwa masharti ya kutoa dhabihu za kuteketezwa na kunyunyiza damu juu ya madhabahu itakapokuwa imejengwa.
И рече ко мне: сыне человечь, сия глаголет Господь Бог Израилев: сия заповеди требника в день сотворения его, еже возносити на нем всесожжения и возливати нань кровь.
19 Utatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi kwa makuhani, ambao ni Walawi, wa jamaa ya Sadoki, ndio watakaonikaribia kuhudumu mbele zangu, asema Bwana Mwenyezi.
И даси жерцем и левитом, иже суть от семене Садукова, приступающым ко Мне, глаголет Господь Бог, еже служити Мне, телца от говяд за грех:
20 Itakupasa kuchukua baadhi ya hiyo damu ya mnyama huyo na kuiweka juu ya hizo pembe nne za madhabahu na juu ya ncha zake nne za sehemu ya juu kuzunguka ukingo wote, ili kuitakasa madhabahu na kufanya upatanisho kwa ajili yake.
и да возмут от крове его и да возложат на четыри роги требника и на четыри части очистилища и на основание окрест, и окропиши е, и очистят е:
21 Itakupasa kumchukua huyo fahali mchanga kwa ajili ya sadaka ya dhambi na kumteketeza mahali palipoagizwa katika eneo la Hekalu nje ya mahali Patakatifu.
и да возмут телца, иже за грех, и да сожжется во отлученнем храме вне святых.
22 “Siku ya pili yake utamtoa beberu asiye na dosari kwa ajili ya sadaka ya dhambi, nayo madhabahu itatakaswa kama ilivyotakaswa kwa yule fahali.
А во вторый день да возмут два козлища от коз непорочных за грех и да очистят требник, якоже очистиша телцем.
23 Utakapokuwa umemaliza kazi ya kuitakasa, utamtoa fahali mchanga pamoja na kondoo dume toka kwenye kundi, wote wawe hawana dosari.
И егда скончают очищение, да принесут телца от говяд непорочна и овна от овец непорочна,
24 Utawatoa mbele za Bwana, nao makuhani watanyunyizia chumvi juu yao na kuwatoa kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.
и да принесете пред Господа: и да возвергут на ня жерцы соль и да вознесут я Господеви всесожжения.
25 “Kwa siku saba itakupasa kutoa beberu kila siku kwa ajili ya sadaka ya dhambi, pia itakupasa kutoa fahali mchanga na kondoo dume kutoka zizini, wote wawe hawana dosari.
Седмь дний да сотвориши козлище за грех по вся дни, и телца от говяд и овна от овец непорочна, да сотворят седмь дний:
26 Kwa siku saba itawapasa kufanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuitakasa na hivyo ndivyo watakavyoiweka wakfu.
и да очистят требник и освятят его, и наполнят руки своя.
27 Mwishoni mwa hizi siku saba, kuanzia siku ya nane na kuendelea, itawapasa makuhani kutoa sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za amani juu ya madhabahu. Kisha nitawakubali ninyi, asema Bwana Mwenyezi.”
И скончают седмь дний, и будет от осмаго дне и потом, сотворят жерцы на жертвеннице всесожжения ваша и яже спасения вашего: и прииму вы, глаголет Господь.

< Ezekieli 43 >