< Ezekieli 43 >
1 Kisha yule mtu akanileta kwenye lango linaloelekea upande wa mashariki,
Wiódł mię potem ku bramie, która brama patrzyła ku drodze na wschód słońca.
2 nami nikaona utukufu wa Mungu wa Israeli ukija kutoka upande wa mashariki. Sauti yake ilikuwa kama ya ngurumo ya maji yaendayo kasi, nayo nchi ikangʼaa kwa utukufu wake.
A oto chwała Boga Izraelskiego przychodziła drogą od wschodu, a szum jej był jako szum wód wielkich, a ziemia się lśniła od chwały jego.
3 Maono niliyoyaona yalikuwa kama maono yale niliyokuwa nimeyaona wakati Mungu alipokuja kuangamiza mji na kama maono niliyokuwa nimeyaona kando ya Mto wa Kebari, nami nikaanguka kifudifudi.
A podobne było ono widzenie, którem widział, cale onemu widzeniu, którem widział, gdym przychodził, abym psuł miasto; widzenie, mówię, podobne onemu widzeniu, którem widział u rzeki Chebar, i upadłem na twarz moję.
4 Utukufu wa Bwana ukaingia hekaluni kwa kupitia lango linaloelekea upande wa mashariki.
A gdy chwała Pańska wchodziła do domu drogą bramy, która patrzała ku drodze na wschód słońca,
5 Kisha Roho akanichukua na kunileta katika ule ua wa ndani, nao utukufu wa Bwana ulilijaza Hekalu.
Tedy mię podniósł duch, i wwiódł mię do sieni wewnętrznej, a oto dom pełen był chwały Pańskiej.
6 Wakati yule mtu akiwa amesimama kando yangu, nilisikia mtu mmoja akisema nami kutoka ndani ya Hekalu.
I usłyszałem, a oto mówiono do mnie z domu, a on mąż stał podle mnie,
7 Akasema, “Mwanadamu, hapa ni mahali pa kiti changu cha enzi na mahali pa kuweka nyayo za miguu yangu. Hapa ndipo nitakapoishi miongoni mwa Waisraeli milele. Kamwe nyumba ya Israeli hawatalinajisi tena Jina langu takatifu, yaani, wao wala wafalme wao, kwa ukahaba wao na kwa sanamu zao zisizokuwa na uhai za wafalme wao katika mahali pao pa juu pa kuabudia miungu.
I mówił do mnie: Synu człowieczy! miejsce stolicy mojej, i miejsce stóp nóg moich, na którem mieszkać będę w pośród synów Izraelskich na wieki; nie splugawi więcej dom Izraelski imienia świętobliwości mojej, ani oni, ani królowie ich w szeteczeńs twy swemi i trupami królów swych, ani wyżynami swemi.
8 Walipoweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu na miimo yao ya milango karibu na miimo yangu, pakiwa na ukuta tu kati yangu na wao, walilinajisi Jina langu takatifu kwa matendo yao ya machukizo. Kwa sababu hiyo niliwaangamiza kwa hasira yangu.
Gdy kładli próg swój podle progu mego, a podwoje swoje podle podwoi moich, a ścianę między mną i między sobą; a tak splugawiali imię świętobliwości mojej obrzydliwościami swemi, które czynili, przetożem ich zniszczył w popędliwości mojej.
9 Basi sasa na waweke mbali nami ukahaba wao na sanamu za wafalme wao zisizo na uhai, nami nitakaa miongoni mwao milele.
Ale teraz niech odrzucą wszeteczeństwo swoje, i trupy królów swoich odemnie, a będę mieszkał w pośrodku ich na wieki.
10 “Mwanadamu, elezea hilo Hekalu kwa watu wa Israeli, ili wapate kuona aibu kwa ajili ya dhambi zao. Wao na wapime hicho kielelezo.
Ty, synu człowieczy! powiedz domowi Izraelskiemu o tym domu, a niech się wstydzą za nieprawości swoje, i niech sobie rozmierzą wizerunek jego.
11 Wakishaona aibu kwa ajili ya yale yote waliyotenda, wafahamishe kielelezo cha hilo Hekalu, yaani mpangilio wake, maingilio yake ya kutoka na kuingia, kielelezo chake chote, na masharti yake yote na sheria zake zote. Yaandike haya mbele yao ili wapate kuwa waaminifu kwa hicho kielelezo chake na kufuata masharti yake yote.
A jeźliby się zawstydzili za wszystko, co czynili, tydy im oznajmij wizerunek domu tego, i wymiar jego, wyjście jego, i wejście jego, i wszystkie kształty jego, i wszystkie ustawy jego, wszystkie, mówię, kształty, i wszystkie prawa jego, a napisz przed oczyma ich, aby przestrzegali wszystkiego kształtu jego, i wszystkich ustaw jego, i czynili je.
12 “Hii ndiyo sheria ya Hekalu: Eneo lote linalozunguka Hekalu juu ya mlima litakuwa takatifu kuliko yote. Hii ndiyo sheria ya Hekalu.
A tenci jest zakon domu tego: Na wierzchu góry wszystko ogrodzenie jego wszędzie w około najświętsze jest; oto tenci jest zakon domu tego.
13 “Hivi ndivyo vipimo vya madhabahu kwa dhiraa ndefu, yaani, dhiraa moja na nyanda nne: Tako lake liwe na kina cha hiyo dhiraa moja na upana wa hiyo dhiraa moja, ikiwa na ukingo wa shibiri moja kuizunguka pembeni. Hiki kitakuwa ndicho kimo cha madhabahu:
A teć są pomiary ołtarza według tychże łokci, a miara łokcia na łokieć i na dłoń; podstawek jego na łokieć wzwyż, a wszerz także na łokieć, a kraniec jego aż do kraju jego w około był na piędź jedną; a tać była wystawa ołtarza;
14 Kimo cha msingi kuanzia usawa wa ardhi mpaka kwenye mfereji sehemu ya chini kimo chake ni dhiraa mbili na upana wake ni dhiraa moja na kuanzia kwenye ukingo mdogo hadi kwenye ukingo mpana kimo chake ni dhiraa nne na upana wake ni dhiraa moja.
To jest od podstawku, który był przy ziemi, aż do przepasania niższego, dwa łokcie, a szerokość na jeden łokieć; a od mniejszego przepasania aż do przepasania większego cztery łokcie, a szerokość na łokieć;
15 Pale pawashwapo moto madhabahuni kimo chake kitakuwa dhiraa nne, na pembe nne zinazoelekeza juu kutoka pale pawashwapo moto.
Ale sam ołtarz niech będzie na cztery łokcie, a z ołtarza w górę cztery rogi.
16 Pale pawashwapo moto pa madhabahu ni mraba, urefu wake ni dhiraa kumi na mbili na upana wa dhiraa kumi na mbili.
A ołtarz na dwanaście łokci wdłuż, a na dwanaście wszerz czworograniasty po czterech stronach swoich;
17 Pia sehemu ya juu ni mraba, urefu wake dhiraa kumi na nne na upana wa dhiraa kumi na nne, ikiwa na ukingo wa nusu dhiraa na mfereji kuizunguka madhabahu. Ngazi za kupandia madhabahuni zitaelekea upande wa mashariki.”
A przepasanie jego na czternaście łokci wdłuż, a na czternaście wszerz, po czterech stronach jego, a kraniec około niego na pół łokcia, a podstawek jego na łokieć w około, a wschód jego na wschód słońca.
18 Kisha akaniambia, “Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Haya ndiyo yatakayokuwa masharti ya kutoa dhabihu za kuteketezwa na kunyunyiza damu juu ya madhabahu itakapokuwa imejengwa.
I rzekł do mnie: Synu człowieczy! tak mówi panujący Pan: Teć są ustawy około ołtarza w dzień, w który zbudowany będzie, aby na nim ofiarowano całopalenia, i krwią na nim kropiono.
19 Utatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi kwa makuhani, ambao ni Walawi, wa jamaa ya Sadoki, ndio watakaonikaribia kuhudumu mbele zangu, asema Bwana Mwenyezi.
A kapłanom Lewitom, którzy są z nasienia Sadokowego, a przystępują do mnie, mówi panujący Pan, aby mi służyli, dasz cielca młodego na ofiarę za grzech;
20 Itakupasa kuchukua baadhi ya hiyo damu ya mnyama huyo na kuiweka juu ya hizo pembe nne za madhabahu na juu ya ncha zake nne za sehemu ya juu kuzunguka ukingo wote, ili kuitakasa madhabahu na kufanya upatanisho kwa ajili yake.
Weźmiesz tedy ze krwi jego, a włożysz na cztery rogi jego, i na cztery węgły przepasania, i na kraniec w około; a tak go oczyścisz, i poświęcisz go.
21 Itakupasa kumchukua huyo fahali mchanga kwa ajili ya sadaka ya dhambi na kumteketeza mahali palipoagizwa katika eneo la Hekalu nje ya mahali Patakatifu.
Potem weźmiesz onego cielca za grzech, a spalisz go na miejscu postanowionem w onym domu zewnątrz przed świątnicą.
22 “Siku ya pili yake utamtoa beberu asiye na dosari kwa ajili ya sadaka ya dhambi, nayo madhabahu itatakaswa kama ilivyotakaswa kwa yule fahali.
A wtórego dnia będziesz ofiarował kozła z kóz bez wady za grzech, i oczyszczą ołtarz, tak jako go cielcem oczyścili.
23 Utakapokuwa umemaliza kazi ya kuitakasa, utamtoa fahali mchanga pamoja na kondoo dume toka kwenye kundi, wote wawe hawana dosari.
A gdy dokończysz oczyszczania, będziesz ofiarował cielca młodego bez wady, i barana z trzody bez wady.
24 Utawatoa mbele za Bwana, nao makuhani watanyunyizia chumvi juu yao na kuwatoa kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.
Które gdy ofiarować będziesz przed Panem, wrzucą kapłani na nie soli, i uczynią z nich ofiarę całopalenia Panu.
25 “Kwa siku saba itakupasa kutoa beberu kila siku kwa ajili ya sadaka ya dhambi, pia itakupasa kutoa fahali mchanga na kondoo dume kutoka zizini, wote wawe hawana dosari.
Przez siedm dni będziesz ofiarował kozła za grzech na każdy dzień, także i cielca młodego, i barana z trzody bez wady ofiarować będą,
26 Kwa siku saba itawapasa kufanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuitakasa na hivyo ndivyo watakavyoiweka wakfu.
Przez siedm dni oczyszczać będą ołtarz, i oczyszczą go, a poświęcą ręce swoje.
27 Mwishoni mwa hizi siku saba, kuanzia siku ya nane na kuendelea, itawapasa makuhani kutoa sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za amani juu ya madhabahu. Kisha nitawakubali ninyi, asema Bwana Mwenyezi.”
A wypełniwszy te dni, ósmego dnia napotem sprawować będą kapłani na ołtarzu całopalenia wasze, i spokojne ofiary wasze, i przyjmę was łaskawie, mówi panujący Pan.