< Ezekieli 43 >

1 Kisha yule mtu akanileta kwenye lango linaloelekea upande wa mashariki,
Et il me mena à la porte qui regardait vers la voie de l’orient.
2 nami nikaona utukufu wa Mungu wa Israeli ukija kutoka upande wa mashariki. Sauti yake ilikuwa kama ya ngurumo ya maji yaendayo kasi, nayo nchi ikangʼaa kwa utukufu wake.
Et voilà que la gloire du Dieu d’Israël entrait par la voie de l’orient, et sa voix était comme la voix des grandes eaux, et la terre resplendissait de sa majesté.
3 Maono niliyoyaona yalikuwa kama maono yale niliyokuwa nimeyaona wakati Mungu alipokuja kuangamiza mji na kama maono niliyokuwa nimeyaona kando ya Mto wa Kebari, nami nikaanguka kifudifudi.
Et je vis une vision selon la ressemblance de celle que j’avais vue, quand il vint pour perdre la cité; et sa forme était selon la forme que j’avais vue près du fleuve de Chobar; et je tombai sur ma face.
4 Utukufu wa Bwana ukaingia hekaluni kwa kupitia lango linaloelekea upande wa mashariki.
Et la majesté du Seigneur entra dans le temple par la porte qui regardait vers l’orient.
5 Kisha Roho akanichukua na kunileta katika ule ua wa ndani, nao utukufu wa Bwana ulilijaza Hekalu.
Et un esprit m’éleva, et m’introduisit dans le parvis intérieur; et voilà que la maison était remplie de la gloire du Seigneur.
6 Wakati yule mtu akiwa amesimama kando yangu, nilisikia mtu mmoja akisema nami kutoka ndani ya Hekalu.
Et j’entendis quelqu’un me parlant du temple; et un homme, qui se tenait près de moi,
7 Akasema, “Mwanadamu, hapa ni mahali pa kiti changu cha enzi na mahali pa kuweka nyayo za miguu yangu. Hapa ndipo nitakapoishi miongoni mwa Waisraeli milele. Kamwe nyumba ya Israeli hawatalinajisi tena Jina langu takatifu, yaani, wao wala wafalme wao, kwa ukahaba wao na kwa sanamu zao zisizokuwa na uhai za wafalme wao katika mahali pao pa juu pa kuabudia miungu.
Me dit: Fils d’un homme, ici est le lieu de mon trône, et le lieu des traces de mes pieds, où j’habite au milieu des enfants d’Israël pour jamais; la maison d’Israël ne souillera plus mon nom saint, ni eux-mêmes, ni leurs rois, par leurs fornications et par les ruines de leurs rois, et par les hauts lieux.
8 Walipoweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu na miimo yao ya milango karibu na miimo yangu, pakiwa na ukuta tu kati yangu na wao, walilinajisi Jina langu takatifu kwa matendo yao ya machukizo. Kwa sababu hiyo niliwaangamiza kwa hasira yangu.
Ils ont fait leur seuil près de mon seuil, et leurs poteaux près de mes poteaux; et un mur seulement était entre moi et eux; et ils ont souillé mon nom saint par les abominations qu’ils ont faites; à cause de quoi je les ai détruits dans ma colère.
9 Basi sasa na waweke mbali nami ukahaba wao na sanamu za wafalme wao zisizo na uhai, nami nitakaa miongoni mwao milele.
Maintenant donc, qu’ils rejettent au loin leur fornication, et loin de moi les ruines de leurs rois, et j’habiterai toujours au milieu d’eux.
10 “Mwanadamu, elezea hilo Hekalu kwa watu wa Israeli, ili wapate kuona aibu kwa ajili ya dhambi zao. Wao na wapime hicho kielelezo.
Mais, toi, fils d’un homme, montre à la maison d’Israël le temple, et qu’ils soient confondus de leurs iniquités, et qu’ils mesurent eux-même sa structure;
11 Wakishaona aibu kwa ajili ya yale yote waliyotenda, wafahamishe kielelezo cha hilo Hekalu, yaani mpangilio wake, maingilio yake ya kutoka na kuingia, kielelezo chake chote, na masharti yake yote na sheria zake zote. Yaandike haya mbele yao ili wapate kuwa waaminifu kwa hicho kielelezo chake na kufuata masharti yake yote.
Et qu’ils rougissent de toutes les choses qu’ils ont faites; montre-leur la figure de la maison et de sa structure, les entrées et toute sa description, et toutes les ordonnances les concernant et tout l’ordre qu’il faut y garder, et toutes les lois faites pour elle, et tu écriras toutes ces choses devant leurs yeux, afin qu’ils gardent tout ce qui aura été décrit et les ordonnances les concernant, et qu’ils les observent.
12 “Hii ndiyo sheria ya Hekalu: Eneo lote linalozunguka Hekalu juu ya mlima litakuwa takatifu kuliko yote. Hii ndiyo sheria ya Hekalu.
Telle est la loi pour la maison sur le sommet de la montagne; toute son étendue à l’entour est très sainte; telle est donc la loi pour la maison.
13 “Hivi ndivyo vipimo vya madhabahu kwa dhiraa ndefu, yaani, dhiraa moja na nyanda nne: Tako lake liwe na kina cha hiyo dhiraa moja na upana wa hiyo dhiraa moja, ikiwa na ukingo wa shibiri moja kuizunguka pembeni. Hiki kitakuwa ndicho kimo cha madhabahu:
Or, voici les mesures de l’autel, prises avec la coudée très exacte qui avait une coudée et un palme; elle avait une coudée en profondeur et une coudée en largeur; et sa clôture jusqu’à son bord et tout à l’entour, un palme; ainsi telle était la fosse de l’autel.
14 Kimo cha msingi kuanzia usawa wa ardhi mpaka kwenye mfereji sehemu ya chini kimo chake ni dhiraa mbili na upana wake ni dhiraa moja na kuanzia kwenye ukingo mdogo hadi kwenye ukingo mpana kimo chake ni dhiraa nne na upana wake ni dhiraa moja.
Du bas de la terre jusqu’au rebord inférieur il y avait deux coudées de hauteur, et la largeur de ce rebord était d’une coudée; et de ce rebord qui était le plus petit, jusqu’au rebord le plus grand, il y avait quatre coudées, et la largeur de ce rebord était d’une coudée.
15 Pale pawashwapo moto madhabahuni kimo chake kitakuwa dhiraa nne, na pembe nne zinazoelekeza juu kutoka pale pawashwapo moto.
Mais Ariel lui-même avait quatre coudées; d’Ariel jusqu’en haut s’élevaient quatre cornes.
16 Pale pawashwapo moto pa madhabahu ni mraba, urefu wake ni dhiraa kumi na mbili na upana wa dhiraa kumi na mbili.
Et Ariel était de douze coudées en longueur sur douze coudées de largeur; quadrangulaire à côtés égaux.
17 Pia sehemu ya juu ni mraba, urefu wake dhiraa kumi na nne na upana wa dhiraa kumi na nne, ikiwa na ukingo wa nusu dhiraa na mfereji kuizunguka madhabahu. Ngazi za kupandia madhabahuni zitaelekea upande wa mashariki.”
Et son rebord était de quatorze coudées de longueur, sur quatorze coudées de largeur, à ses quatre coins; et la couronne autour d’elle était d’une demi-coudée, et son enfoncement d’une coudée tout autour; or ses degrés étaient tournés vers l’orient.
18 Kisha akaniambia, “Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Haya ndiyo yatakayokuwa masharti ya kutoa dhabihu za kuteketezwa na kunyunyiza damu juu ya madhabahu itakapokuwa imejengwa.
Et il me dit: Fils d’un homme, voici ce que dit le Seigneur Dieu: Voici les rites pour l’autel au jour quelconque où il aura été construit, afin qu’un holocauste y soit offert dessus, que du sang y soit répandu.
19 Utatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi kwa makuhani, ambao ni Walawi, wa jamaa ya Sadoki, ndio watakaonikaribia kuhudumu mbele zangu, asema Bwana Mwenyezi.
Et tu les donneras aux prêtres et aux Lévites qui sont de la race de Sadoc, qui s’approchent de moi, dit le Seigneur Dieu, afin qu’ils m’offrent un veau du troupeau pour le péché.
20 Itakupasa kuchukua baadhi ya hiyo damu ya mnyama huyo na kuiweka juu ya hizo pembe nne za madhabahu na juu ya ncha zake nne za sehemu ya juu kuzunguka ukingo wote, ili kuitakasa madhabahu na kufanya upatanisho kwa ajili yake.
Et prenant de son sang, tu en mettras sur les quatre cornes de l’autel, et sur les quatre coins de son rebord, et sur la couronne tout autour; et tu le purifieras et le sanctifieras.
21 Itakupasa kumchukua huyo fahali mchanga kwa ajili ya sadaka ya dhambi na kumteketeza mahali palipoagizwa katika eneo la Hekalu nje ya mahali Patakatifu.
Et tu emporteras le veau qui aura été offert pour le péché, et tu le brûleras dans un lieu de la maison séparé, hors du sanctuaire.
22 “Siku ya pili yake utamtoa beberu asiye na dosari kwa ajili ya sadaka ya dhambi, nayo madhabahu itatakaswa kama ilivyotakaswa kwa yule fahali.
Et le second jour, tu offriras un bouc de chèvres sans tache pour le péché; et l’on sanctifiera l’autel, comme on l’a sanctifié avec le veau.
23 Utakapokuwa umemaliza kazi ya kuitakasa, utamtoa fahali mchanga pamoja na kondoo dume toka kwenye kundi, wote wawe hawana dosari.
Et lorsque tu auras achevé de le sanctifier, tu offriras un veau sans tache, pris d’un troupeau, et un bélier sans tache, pris d’un troupeau.
24 Utawatoa mbele za Bwana, nao makuhani watanyunyizia chumvi juu yao na kuwatoa kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.
Et tu les offriras en présence du Seigneur, et les prêtres répandront du sel sur eux, et les offriront en holocauste au Seigneur.
25 “Kwa siku saba itakupasa kutoa beberu kila siku kwa ajili ya sadaka ya dhambi, pia itakupasa kutoa fahali mchanga na kondoo dume kutoka zizini, wote wawe hawana dosari.
Durant sept jours, tu sacrifieras chaque jour un bouc pour le péché; et l’on offrira un veau pris d’un troupeau, tous deux sans tache.
26 Kwa siku saba itawapasa kufanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuitakasa na hivyo ndivyo watakavyoiweka wakfu.
Durant sept jours, les prêtres sanctifieront l’autel, et le purifieront, et le consacreront.
27 Mwishoni mwa hizi siku saba, kuanzia siku ya nane na kuendelea, itawapasa makuhani kutoa sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za amani juu ya madhabahu. Kisha nitawakubali ninyi, asema Bwana Mwenyezi.”
Et les sept jours accomplis, les prêtres offriront, le huitième jour et dans la suite, vos holocaustes sur l’autel, et les hosties qu’ils offrent pour la paix, et je m’attendrirai sur vous, dit le Seigneur Dieu.

< Ezekieli 43 >