< Ezekieli 43 >

1 Kisha yule mtu akanileta kwenye lango linaloelekea upande wa mashariki,
And he ledde me out to the yate, that bihelde to the eest weie.
2 nami nikaona utukufu wa Mungu wa Israeli ukija kutoka upande wa mashariki. Sauti yake ilikuwa kama ya ngurumo ya maji yaendayo kasi, nayo nchi ikangʼaa kwa utukufu wake.
And lo! the glorie of God of Israel entride bi the eest weie; and a vois was to it, as the vois of many watris, and the erthe schynede of the mageste of hym.
3 Maono niliyoyaona yalikuwa kama maono yale niliyokuwa nimeyaona wakati Mungu alipokuja kuangamiza mji na kama maono niliyokuwa nimeyaona kando ya Mto wa Kebari, nami nikaanguka kifudifudi.
And Y siy a visioun, bi the licnesse whiche Y hadde seyn, whanne he cam to distrie the citee; and the licnesse was lijc the biholdyng whiche Y hadde seyn bisidis the flood Chobar.
4 Utukufu wa Bwana ukaingia hekaluni kwa kupitia lango linaloelekea upande wa mashariki.
And Y felle doun on my face, and the mageste of the Lord entride in to the temple, bi the weie of the yate that biheeld to the eest.
5 Kisha Roho akanichukua na kunileta katika ule ua wa ndani, nao utukufu wa Bwana ulilijaza Hekalu.
And the Spirit reiside me, and ledde me in to the ynnere halle; and lo! the hous was fillid of the glorie of the Lord.
6 Wakati yule mtu akiwa amesimama kando yangu, nilisikia mtu mmoja akisema nami kutoka ndani ya Hekalu.
And Y herde oon spekynge to me of the hous. And the man that stood bisidis me,
7 Akasema, “Mwanadamu, hapa ni mahali pa kiti changu cha enzi na mahali pa kuweka nyayo za miguu yangu. Hapa ndipo nitakapoishi miongoni mwa Waisraeli milele. Kamwe nyumba ya Israeli hawatalinajisi tena Jina langu takatifu, yaani, wao wala wafalme wao, kwa ukahaba wao na kwa sanamu zao zisizokuwa na uhai za wafalme wao katika mahali pao pa juu pa kuabudia miungu.
seide to me, Thou, son of man, this is the place of my seete, and the place of the steppis of my feet, where Y dwelle in the myddis of the sones of Israel withouten ende; and the hous of Israel schulen no more defoule myn hooli name, thei, and the kyngis of hem in her fornicaciouns, and in the fallyngis of her kyngis, and in hiy places.
8 Walipoweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu na miimo yao ya milango karibu na miimo yangu, pakiwa na ukuta tu kati yangu na wao, walilinajisi Jina langu takatifu kwa matendo yao ya machukizo. Kwa sababu hiyo niliwaangamiza kwa hasira yangu.
Whiche maden her threisfold bisidis my threisfold, and her postis bisidis my postis, and a wal was bitwixe me and hem; and thei defouliden myn hooli name in abhomynaciouns whiche thei diden; wherfor Y wastide hem in my wraththe.
9 Basi sasa na waweke mbali nami ukahaba wao na sanamu za wafalme wao zisizo na uhai, nami nitakaa miongoni mwao milele.
Now therfor putte thei awei fer her fornicacioun, and the fallyng of her kyngis fro me; and Y schal dwelle euere in the myddis of hem.
10 “Mwanadamu, elezea hilo Hekalu kwa watu wa Israeli, ili wapate kuona aibu kwa ajili ya dhambi zao. Wao na wapime hicho kielelezo.
But thou, sone of man, schewe the temple to the hous of Israel, and be thei schent of her wickidnessis; and mete thei the bilding,
11 Wakishaona aibu kwa ajili ya yale yote waliyotenda, wafahamishe kielelezo cha hilo Hekalu, yaani mpangilio wake, maingilio yake ya kutoka na kuingia, kielelezo chake chote, na masharti yake yote na sheria zake zote. Yaandike haya mbele yao ili wapate kuwa waaminifu kwa hicho kielelezo chake na kufuata masharti yake yote.
and be thei aschamed of alle thingis whiche thei diden. Thou schalt schewe to hem, and thou schalt write bifore the iyen of hem the figure of the hous, and of the bildyng therof; the outgoyngis, and the entryngis, and al the discryuyng therof, and alle the comaundementis therof, and al the ordre therof, `and alle the lawis therof; that thei kepe alle the discryuyngis therof, and comaundementis therof, and do tho.
12 “Hii ndiyo sheria ya Hekalu: Eneo lote linalozunguka Hekalu juu ya mlima litakuwa takatifu kuliko yote. Hii ndiyo sheria ya Hekalu.
This is the lawe of the hous, in the hiynesse of the hil; alle the coostis therof in cumpas is the hooli of hooli thingis; therfor this is the lawe of the hous.
13 “Hivi ndivyo vipimo vya madhabahu kwa dhiraa ndefu, yaani, dhiraa moja na nyanda nne: Tako lake liwe na kina cha hiyo dhiraa moja na upana wa hiyo dhiraa moja, ikiwa na ukingo wa shibiri moja kuizunguka pembeni. Hiki kitakuwa ndicho kimo cha madhabahu:
Forsothe these ben the mesuris of the auter, in a verieste cubit, that hadde a cubit and a spanne; in the bosum therof was a cubit in lengthe, and a cubit in breede; and the ende therof til to the brenke, and o spanne in cumpas; also this was the diche of the auter.
14 Kimo cha msingi kuanzia usawa wa ardhi mpaka kwenye mfereji sehemu ya chini kimo chake ni dhiraa mbili na upana wake ni dhiraa moja na kuanzia kwenye ukingo mdogo hadi kwenye ukingo mpana kimo chake ni dhiraa nne na upana wake ni dhiraa moja.
And fro the bosum of the erthe til to the laste heiythe weren twei cubitis, and the breede of o cubit; and fro the lesse heiythe til to the grettere heiythe were foure cubitis, and the breede was of o cubit;
15 Pale pawashwapo moto madhabahuni kimo chake kitakuwa dhiraa nne, na pembe nne zinazoelekeza juu kutoka pale pawashwapo moto.
forsothe thilke ariel, that is, the hiyere part of the auter, was of foure cubitis; and fro the auter `til to aboue weren foure hornes.
16 Pale pawashwapo moto pa madhabahu ni mraba, urefu wake ni dhiraa kumi na mbili na upana wa dhiraa kumi na mbili.
And the auter of twelue cubitis in lengthe was foure cornerid with euene sidis, bi twelue cubitis of breede.
17 Pia sehemu ya juu ni mraba, urefu wake dhiraa kumi na nne na upana wa dhiraa kumi na nne, ikiwa na ukingo wa nusu dhiraa na mfereji kuizunguka madhabahu. Ngazi za kupandia madhabahuni zitaelekea upande wa mashariki.”
And the heiythe of fourtene cubitis of lengthe was bi fourtene cubitis of breede, in foure corneris therof. And a coroun of half a cubit was in the cumpas therof, and the bosum therof was of o cubit bi cumpas; forsothe the degrees therof weren turned to the eest.
18 Kisha akaniambia, “Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Haya ndiyo yatakayokuwa masharti ya kutoa dhabihu za kuteketezwa na kunyunyiza damu juu ya madhabahu itakapokuwa imejengwa.
And he seide to me, Thou, sone of man, the Lord God seith these thingis, These ben the customs of the auter, in what euer dai it is maad, that me offre on it brent sacrifice, and blood be sched out.
19 Utatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi kwa makuhani, ambao ni Walawi, wa jamaa ya Sadoki, ndio watakaonikaribia kuhudumu mbele zangu, asema Bwana Mwenyezi.
And thou schalt yyue to preestis and dekenes, that ben of the seed of Sadoch, that neiyen to me, seith the Lord God, that thei offre to me a calf of the drooue for synne.
20 Itakupasa kuchukua baadhi ya hiyo damu ya mnyama huyo na kuiweka juu ya hizo pembe nne za madhabahu na juu ya ncha zake nne za sehemu ya juu kuzunguka ukingo wote, ili kuitakasa madhabahu na kufanya upatanisho kwa ajili yake.
And thou schalt take of the blood therof, and schalt putte on foure hornes therof, and on foure corneris of heiythe, and on the coroun in cumpas; and thou schalt clense it, and make clene.
21 Itakupasa kumchukua huyo fahali mchanga kwa ajili ya sadaka ya dhambi na kumteketeza mahali palipoagizwa katika eneo la Hekalu nje ya mahali Patakatifu.
And thou schalt take the calf which is offrid for synne, and thou schalt brenne it in a departid place of the hous, with out the seyntuarie.
22 “Siku ya pili yake utamtoa beberu asiye na dosari kwa ajili ya sadaka ya dhambi, nayo madhabahu itatakaswa kama ilivyotakaswa kwa yule fahali.
And in the secounde dai thou schalt offre a buk of geet, which is with out wem, for synne; and thei schulen clense the auter, as thei clensiden in the calf.
23 Utakapokuwa umemaliza kazi ya kuitakasa, utamtoa fahali mchanga pamoja na kondoo dume toka kwenye kundi, wote wawe hawana dosari.
And whanne thou hast fillid that clensyng, thou schalt offre a calf of the drooue, which calf is without wem, and a wether with out wem of the floc.
24 Utawatoa mbele za Bwana, nao makuhani watanyunyizia chumvi juu yao na kuwatoa kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.
And thou schalt offre tho in the siyt of the Lord; and prestis schulen putte salt on tho, and schulen offre tho in to brent sacrifice to the Lord.
25 “Kwa siku saba itakupasa kutoa beberu kila siku kwa ajili ya sadaka ya dhambi, pia itakupasa kutoa fahali mchanga na kondoo dume kutoka zizini, wote wawe hawana dosari.
Bi seuene daies thou schalt make a buk of geet for synne, ech dai; and thei schulen offre a calf of the drooue, and a wether vnwemmed of scheep.
26 Kwa siku saba itawapasa kufanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuitakasa na hivyo ndivyo watakavyoiweka wakfu.
Bi seuene daies thei schulen clense the auter, and schulen make it cleene, and thei schulen fille the hond therof.
27 Mwishoni mwa hizi siku saba, kuanzia siku ya nane na kuendelea, itawapasa makuhani kutoa sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za amani juu ya madhabahu. Kisha nitawakubali ninyi, asema Bwana Mwenyezi.”
Forsothe whanne seuene daies ben fillid, in the eiythe dai and ferther prestis schulen make on the auter youre brent sacrifices, and tho thingis whiche thei offren for pees; and Y schal be plesid to you, seith the Lord God.

< Ezekieli 43 >