< Ezekieli 43 >

1 Kisha yule mtu akanileta kwenye lango linaloelekea upande wa mashariki,
and to go: take me to(wards) [the] gate gate which to turn way: direction [the] east
2 nami nikaona utukufu wa Mungu wa Israeli ukija kutoka upande wa mashariki. Sauti yake ilikuwa kama ya ngurumo ya maji yaendayo kasi, nayo nchi ikangʼaa kwa utukufu wake.
and behold glory God Israel to come (in): come from way: direction [the] east and voice: sound his like/as voice: sound water many and [the] land: country/planet to light from glory his
3 Maono niliyoyaona yalikuwa kama maono yale niliyokuwa nimeyaona wakati Mungu alipokuja kuangamiza mji na kama maono niliyokuwa nimeyaona kando ya Mto wa Kebari, nami nikaanguka kifudifudi.
and like/as appearance [the] appearance which to see: see like/as appearance which to see: see in/on/with to come (in): come I to/for to ruin [obj] [the] city and vision like/as appearance which to see: see to(wards) river Chebar and to fall: fall to(wards) face my
4 Utukufu wa Bwana ukaingia hekaluni kwa kupitia lango linaloelekea upande wa mashariki.
and glory LORD to come (in): come to(wards) [the] house: home way: direction gate which face: before his way: direction [the] east
5 Kisha Roho akanichukua na kunileta katika ule ua wa ndani, nao utukufu wa Bwana ulilijaza Hekalu.
and to lift: raise me spirit and to come (in): bring me to(wards) [the] court [the] inner and behold to fill glory LORD [the] house: home
6 Wakati yule mtu akiwa amesimama kando yangu, nilisikia mtu mmoja akisema nami kutoka ndani ya Hekalu.
and to hear: hear to speak: speak to(wards) me from [the] house: home and man to be to stand: stand beside me
7 Akasema, “Mwanadamu, hapa ni mahali pa kiti changu cha enzi na mahali pa kuweka nyayo za miguu yangu. Hapa ndipo nitakapoishi miongoni mwa Waisraeli milele. Kamwe nyumba ya Israeli hawatalinajisi tena Jina langu takatifu, yaani, wao wala wafalme wao, kwa ukahaba wao na kwa sanamu zao zisizokuwa na uhai za wafalme wao katika mahali pao pa juu pa kuabudia miungu.
and to say to(wards) me son: child man [obj] place throne my and [obj] place palm: sole foot my which to dwell there in/on/with midst son: descendant/people Israel to/for forever: enduring and not to defile still house: household Israel name holiness my they(masc.) and king their in/on/with fornication their and in/on/with corpse king their high place their
8 Walipoweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu na miimo yao ya milango karibu na miimo yangu, pakiwa na ukuta tu kati yangu na wao, walilinajisi Jina langu takatifu kwa matendo yao ya machukizo. Kwa sababu hiyo niliwaangamiza kwa hasira yangu.
in/on/with to give: put they threshold their with threshold my and doorpost their beside doorpost my and [the] wall between me and between them and to defile [obj] name holiness my in/on/with abomination their which to make and to end: destroy [obj] them in/on/with face: anger my
9 Basi sasa na waweke mbali nami ukahaba wao na sanamu za wafalme wao zisizo na uhai, nami nitakaa miongoni mwao milele.
now to remove [obj] fornication their and corpse king their from me and to dwell in/on/with midst their to/for forever: enduring
10 “Mwanadamu, elezea hilo Hekalu kwa watu wa Israeli, ili wapate kuona aibu kwa ajili ya dhambi zao. Wao na wapime hicho kielelezo.
you(m. s.) son: child man to tell [obj] house: household Israel [obj] [the] house: home and be humiliated from iniquity: crime their and to measure [obj] proportion
11 Wakishaona aibu kwa ajili ya yale yote waliyotenda, wafahamishe kielelezo cha hilo Hekalu, yaani mpangilio wake, maingilio yake ya kutoka na kuingia, kielelezo chake chote, na masharti yake yote na sheria zake zote. Yaandike haya mbele yao ili wapate kuwa waaminifu kwa hicho kielelezo chake na kufuata masharti yake yote.
and if be humiliated from all which to make: do design [the] house: home and fitting his and exit his and entrance his and all (design his *Q(K)*) and [obj] all statute his and all (design his *Q(K)*) and all (instruction his *Q(K)*) to know [obj] them and to write to/for eye: seeing their and to keep: obey [obj] all design his and [obj] all statute his and to make: do [obj] them
12 “Hii ndiyo sheria ya Hekalu: Eneo lote linalozunguka Hekalu juu ya mlima litakuwa takatifu kuliko yote. Hii ndiyo sheria ya Hekalu.
this instruction [the] house: home upon head: top [the] mountain: mount all border: area his around around holiness holiness behold this instruction [the] house: home
13 “Hivi ndivyo vipimo vya madhabahu kwa dhiraa ndefu, yaani, dhiraa moja na nyanda nne: Tako lake liwe na kina cha hiyo dhiraa moja na upana wa hiyo dhiraa moja, ikiwa na ukingo wa shibiri moja kuizunguka pembeni. Hiki kitakuwa ndicho kimo cha madhabahu:
and these measure [the] altar in/on/with cubit cubit cubit and handbreadth and bosom: lap [the] cubit and cubit width and border: boundary her to(wards) lip: edge her around span [the] one and this back/rim/brow [the] altar
14 Kimo cha msingi kuanzia usawa wa ardhi mpaka kwenye mfereji sehemu ya chini kimo chake ni dhiraa mbili na upana wake ni dhiraa moja na kuanzia kwenye ukingo mdogo hadi kwenye ukingo mpana kimo chake ni dhiraa nne na upana wake ni dhiraa moja.
and from bosom: lap [the] land: soil till [the] enclosure [the] lower two cubit and width cubit one and from [the] enclosure [the] small till [the] enclosure [the] great: large four cubit and width [the] cubit
15 Pale pawashwapo moto madhabahuni kimo chake kitakuwa dhiraa nne, na pembe nne zinazoelekeza juu kutoka pale pawashwapo moto.
and [the] altar four cubit (and from [the] altar *Q(K)*) and to/for above [to] [the] horn four
16 Pale pawashwapo moto pa madhabahu ni mraba, urefu wake ni dhiraa kumi na mbili na upana wa dhiraa kumi na mbili.
(and [the] altar *Q(K)*) two ten length in/on/with two ten width to square to(wards) four fourth his
17 Pia sehemu ya juu ni mraba, urefu wake dhiraa kumi na nne na upana wa dhiraa kumi na nne, ikiwa na ukingo wa nusu dhiraa na mfereji kuizunguka madhabahu. Ngazi za kupandia madhabahuni zitaelekea upande wa mashariki.”
and [the] enclosure four ten length in/on/with four ten width to(wards) four fourth her and [the] border: boundary around [obj] her half [the] cubit and [the] bosom: lap to/for her cubit around and step his to turn east
18 Kisha akaniambia, “Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Haya ndiyo yatakayokuwa masharti ya kutoa dhabihu za kuteketezwa na kunyunyiza damu juu ya madhabahu itakapokuwa imejengwa.
and to say to(wards) me son: child man thus to say Lord YHWH/God these statute [the] altar in/on/with day to make he to/for to ascend: offer up upon him burnt offering and to/for to scatter upon him blood
19 Utatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi kwa makuhani, ambao ni Walawi, wa jamaa ya Sadoki, ndio watakaonikaribia kuhudumu mbele zangu, asema Bwana Mwenyezi.
and to give: give to(wards) [the] priest [the] Levi which they(masc.) from seed: children Zadok [the] near to(wards) me utterance Lord YHWH/God to/for to minister me bullock son: young animal cattle to/for sin: sin offering
20 Itakupasa kuchukua baadhi ya hiyo damu ya mnyama huyo na kuiweka juu ya hizo pembe nne za madhabahu na juu ya ncha zake nne za sehemu ya juu kuzunguka ukingo wote, ili kuitakasa madhabahu na kufanya upatanisho kwa ajili yake.
and to take: take from blood his and to give: put upon four horn his and to(wards) four corner [the] enclosure and to(wards) [the] border: boundary around and to sin [obj] him and to atone him
21 Itakupasa kumchukua huyo fahali mchanga kwa ajili ya sadaka ya dhambi na kumteketeza mahali palipoagizwa katika eneo la Hekalu nje ya mahali Patakatifu.
and to take: take [obj] [the] bullock [the] sin: sin offering and to burn him in/on/with appointment [the] house: home from outside to/for sanctuary
22 “Siku ya pili yake utamtoa beberu asiye na dosari kwa ajili ya sadaka ya dhambi, nayo madhabahu itatakaswa kama ilivyotakaswa kwa yule fahali.
and in/on/with day [the] second to present: bring he-goat goat unblemished to/for sin: sin offering and to sin [obj] [the] altar like/as as which to sin in/on/with bullock
23 Utakapokuwa umemaliza kazi ya kuitakasa, utamtoa fahali mchanga pamoja na kondoo dume toka kwenye kundi, wote wawe hawana dosari.
in/on/with to end: finish you from to sin to present: bring bullock son: young animal cattle unblemished and ram from [the] flock unblemished
24 Utawatoa mbele za Bwana, nao makuhani watanyunyizia chumvi juu yao na kuwatoa kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.
and to present: bring them to/for face: before LORD and to throw [the] priest upon them salt and to ascend: offer up [obj] them burnt offering to/for LORD
25 “Kwa siku saba itakupasa kutoa beberu kila siku kwa ajili ya sadaka ya dhambi, pia itakupasa kutoa fahali mchanga na kondoo dume kutoka zizini, wote wawe hawana dosari.
seven day to make: offer he-goat sin: sin offering to/for day: daily and bullock son: young animal cattle and ram from [the] flock unblemished to make: offer
26 Kwa siku saba itawapasa kufanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuitakasa na hivyo ndivyo watakavyoiweka wakfu.
seven day to atone [obj] [the] altar and be pure [obj] him and to fill (hand: donate his *Q(K)*)
27 Mwishoni mwa hizi siku saba, kuanzia siku ya nane na kuendelea, itawapasa makuhani kutoa sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za amani juu ya madhabahu. Kisha nitawakubali ninyi, asema Bwana Mwenyezi.”
and to end: finish [obj] [the] day and to be in/on/with day [the] eighth and further to make: offer [the] priest upon [the] altar [obj] burnt offering your and [obj] peace offering your and to accept [obj] you utterance Lord YHWH/God

< Ezekieli 43 >