< Ezekieli 43 >

1 Kisha yule mtu akanileta kwenye lango linaloelekea upande wa mashariki,
Then he brought me to the gate, even to the gate that looketh toward the east.
2 nami nikaona utukufu wa Mungu wa Israeli ukija kutoka upande wa mashariki. Sauti yake ilikuwa kama ya ngurumo ya maji yaendayo kasi, nayo nchi ikangʼaa kwa utukufu wake.
And behold, the glory of the God of Israel came from the east; and the sound thereof was as the sound of great waters, and the earth shone with his glory.
3 Maono niliyoyaona yalikuwa kama maono yale niliyokuwa nimeyaona wakati Mungu alipokuja kuangamiza mji na kama maono niliyokuwa nimeyaona kando ya Mto wa Kebari, nami nikaanguka kifudifudi.
And the appearance was like the vision which I saw, like the vision which I saw when I came to destroy the city; it was a vision like the vision which I saw at the river Chebar. And I fell upon my face.
4 Utukufu wa Bwana ukaingia hekaluni kwa kupitia lango linaloelekea upande wa mashariki.
And the glory of Jehovah came into the house by way of the gate, whose prospect was toward the east.
5 Kisha Roho akanichukua na kunileta katika ule ua wa ndani, nao utukufu wa Bwana ulilijaza Hekalu.
Then the spirit took me up and brought me into the inner court; and behold, the glory of Jehovah filled the house.
6 Wakati yule mtu akiwa amesimama kando yangu, nilisikia mtu mmoja akisema nami kutoka ndani ya Hekalu.
And I heard one speaking to me out of the house, and a man was standing by me.
7 Akasema, “Mwanadamu, hapa ni mahali pa kiti changu cha enzi na mahali pa kuweka nyayo za miguu yangu. Hapa ndipo nitakapoishi miongoni mwa Waisraeli milele. Kamwe nyumba ya Israeli hawatalinajisi tena Jina langu takatifu, yaani, wao wala wafalme wao, kwa ukahaba wao na kwa sanamu zao zisizokuwa na uhai za wafalme wao katika mahali pao pa juu pa kuabudia miungu.
And he said to me: Son of man, this is the place of my throne, and the place of the soles of my feet, where I will dwell in the midst of the sons of Israel forever; and the house of Israel shall no more pollute my holy name, neither they nor their kings, by their fornication, and by the dead bodies of their kings in their sepulchres;
8 Walipoweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu na miimo yao ya milango karibu na miimo yangu, pakiwa na ukuta tu kati yangu na wao, walilinajisi Jina langu takatifu kwa matendo yao ya machukizo. Kwa sababu hiyo niliwaangamiza kwa hasira yangu.
in that they set their threshold by my threshold, and their post near my post, so that there was only a wall between me and them, and defiled my holy name by the abominations which they committed; wherefore I have consumed them in my anger.
9 Basi sasa na waweke mbali nami ukahaba wao na sanamu za wafalme wao zisizo na uhai, nami nitakaa miongoni mwao milele.
Now let them remove far away from me their fornication, and the carcasses of their kings; and I will dwell in the midst of them forever.
10 “Mwanadamu, elezea hilo Hekalu kwa watu wa Israeli, ili wapate kuona aibu kwa ajili ya dhambi zao. Wao na wapime hicho kielelezo.
And thou, son of man, show this house to the house of Israel, that they may be ashamed of their iniquities, and that they may measure the pattern.
11 Wakishaona aibu kwa ajili ya yale yote waliyotenda, wafahamishe kielelezo cha hilo Hekalu, yaani mpangilio wake, maingilio yake ya kutoka na kuingia, kielelezo chake chote, na masharti yake yote na sheria zake zote. Yaandike haya mbele yao ili wapate kuwa waaminifu kwa hicho kielelezo chake na kufuata masharti yake yote.
And if they be ashamed of all which they have done, let them know the form of the house and the fashion thereof, and the passages for going out and coming in, and all the forms thereof, and all the statutes thereof, and all the laws thereof, and write it in their sight, that they may keep the whole form thereof, and all the statutes thereof, and do them.
12 “Hii ndiyo sheria ya Hekalu: Eneo lote linalozunguka Hekalu juu ya mlima litakuwa takatifu kuliko yote. Hii ndiyo sheria ya Hekalu.
This is the law of the house. Upon the top of the mountain, all within its limits shall be most holy. Behold, this is the law of the house.
13 “Hivi ndivyo vipimo vya madhabahu kwa dhiraa ndefu, yaani, dhiraa moja na nyanda nne: Tako lake liwe na kina cha hiyo dhiraa moja na upana wa hiyo dhiraa moja, ikiwa na ukingo wa shibiri moja kuizunguka pembeni. Hiki kitakuwa ndicho kimo cha madhabahu:
And these are the measures of the altar by cubits; each cubit being a cubit and a hand-breadth. The bottom shall be a cubit high and a cubit broad; and the border thereof, by the edge thereof round about, shall be a span; and this shall be the outer part of the altar.
14 Kimo cha msingi kuanzia usawa wa ardhi mpaka kwenye mfereji sehemu ya chini kimo chake ni dhiraa mbili na upana wake ni dhiraa moja na kuanzia kwenye ukingo mdogo hadi kwenye ukingo mpana kimo chake ni dhiraa nne na upana wake ni dhiraa moja.
And from the bottom upon the ground to the lower ledge shall be two cubits, and the breadth one cubit; and from the lesser ledge to the greater ledge shall be four cubits, and the breadth a cubit.
15 Pale pawashwapo moto madhabahuni kimo chake kitakuwa dhiraa nne, na pembe nne zinazoelekeza juu kutoka pale pawashwapo moto.
And the altar shall be four cubits; and from the altar upward shall be four horns.
16 Pale pawashwapo moto pa madhabahu ni mraba, urefu wake ni dhiraa kumi na mbili na upana wa dhiraa kumi na mbili.
And the altar shall be twelve cubits long by twelve broad; square on the four sides thereof.
17 Pia sehemu ya juu ni mraba, urefu wake dhiraa kumi na nne na upana wa dhiraa kumi na nne, ikiwa na ukingo wa nusu dhiraa na mfereji kuizunguka madhabahu. Ngazi za kupandia madhabahuni zitaelekea upande wa mashariki.”
And the ledge shall be fourteen cubits long by fourteen broad on the four sides thereof; and the border about it shall be half a cubit; and the bottom thereof shall be a cubit round about; and its steps shall look toward the east.
18 Kisha akaniambia, “Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Haya ndiyo yatakayokuwa masharti ya kutoa dhabihu za kuteketezwa na kunyunyiza damu juu ya madhabahu itakapokuwa imejengwa.
And he said to me, Son of man, thus saith the Lord Jehovah: These are the statutes of the altar, in the day when it is made, to offer burnt-offerings thereon, and to sprinkle blood thereon.
19 Utatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi kwa makuhani, ambao ni Walawi, wa jamaa ya Sadoki, ndio watakaonikaribia kuhudumu mbele zangu, asema Bwana Mwenyezi.
To the priests, the sons of Levi, of the race of Zadok, that come near to me, saith the Lord Jehovah, to minister to me, thou shalt give a young bullock for a sin-offering.
20 Itakupasa kuchukua baadhi ya hiyo damu ya mnyama huyo na kuiweka juu ya hizo pembe nne za madhabahu na juu ya ncha zake nne za sehemu ya juu kuzunguka ukingo wote, ili kuitakasa madhabahu na kufanya upatanisho kwa ajili yake.
And thou shalt take of the blood thereof, and put it on its four horns, and on the four corners of the ledge, and on the border round about, and thus cleanse and purge it.
21 Itakupasa kumchukua huyo fahali mchanga kwa ajili ya sadaka ya dhambi na kumteketeza mahali palipoagizwa katika eneo la Hekalu nje ya mahali Patakatifu.
And thou shalt take the bullock of the sin-offering, and it shall be burned in the appointed place of the house, without the sanctuary.
22 “Siku ya pili yake utamtoa beberu asiye na dosari kwa ajili ya sadaka ya dhambi, nayo madhabahu itatakaswa kama ilivyotakaswa kwa yule fahali.
And on the second day thou shalt offer a he-goat without blemish for a sin-offering; and they shall cleanse the altar, as they cleansed it with the bullock.
23 Utakapokuwa umemaliza kazi ya kuitakasa, utamtoa fahali mchanga pamoja na kondoo dume toka kwenye kundi, wote wawe hawana dosari.
And when thou hast made an end of cleansing it, thou shalt offer a young bullock without blemish, and a ram out of the flock without blemish.
24 Utawatoa mbele za Bwana, nao makuhani watanyunyizia chumvi juu yao na kuwatoa kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.
And thou shalt offer them before Jehovah, and the priests shall cast salt upon them, and offer them up for a burnt-offering to Jehovah.
25 “Kwa siku saba itakupasa kutoa beberu kila siku kwa ajili ya sadaka ya dhambi, pia itakupasa kutoa fahali mchanga na kondoo dume kutoka zizini, wote wawe hawana dosari.
Seven days shalt thou sacrifice daily a goat for a sin-offering; they shall also sacrifice a young bullock, and a ram out of the flock without blemish.
26 Kwa siku saba itawapasa kufanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuitakasa na hivyo ndivyo watakavyoiweka wakfu.
Seven days shall they purge the altar, and purify it, and consecrate themselves.
27 Mwishoni mwa hizi siku saba, kuanzia siku ya nane na kuendelea, itawapasa makuhani kutoa sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za amani juu ya madhabahu. Kisha nitawakubali ninyi, asema Bwana Mwenyezi.”
And when they have finished these days, it shall be that on the eighth day and forward the priests shall present your burnt-offerings and your thank-offerings upon the altar, and I will accept you, saith the Lord Jehovah.

< Ezekieli 43 >