< Ezekieli 43 >

1 Kisha yule mtu akanileta kwenye lango linaloelekea upande wa mashariki,
Og han førte mig til Porten, den Port, som vender imod Østen.
2 nami nikaona utukufu wa Mungu wa Israeli ukija kutoka upande wa mashariki. Sauti yake ilikuwa kama ya ngurumo ya maji yaendayo kasi, nayo nchi ikangʼaa kwa utukufu wake.
Og se, Israels Guds Herlighed kom fra Østen af, og Lyden deraf var som vældige Vandes Lyd, og Jorden lyste af hans Herlighed.
3 Maono niliyoyaona yalikuwa kama maono yale niliyokuwa nimeyaona wakati Mungu alipokuja kuangamiza mji na kama maono niliyokuwa nimeyaona kando ya Mto wa Kebari, nami nikaanguka kifudifudi.
Og Synet, som jeg saa, var at se til som det Syn, hvilket jeg havde set, da jeg kom til Stadens Ødelæggelse, og det var Syner som det Syn, hvilket jeg havde set ved Floden Kebar; og jeg faldt paa mit Ansigt.
4 Utukufu wa Bwana ukaingia hekaluni kwa kupitia lango linaloelekea upande wa mashariki.
Og Herrens Herlighed drog ind i Huset igennem Porten, som vendte imod Østen.
5 Kisha Roho akanichukua na kunileta katika ule ua wa ndani, nao utukufu wa Bwana ulilijaza Hekalu.
Og en Aand opløftede mig og førte mig til den indre Forgaard; og se, Herrens Herlighed fyldte Huset.
6 Wakati yule mtu akiwa amesimama kando yangu, nilisikia mtu mmoja akisema nami kutoka ndani ya Hekalu.
Og jeg hørte een tale til mig fra Huset af, og der var en Mand, som stod hos mig.
7 Akasema, “Mwanadamu, hapa ni mahali pa kiti changu cha enzi na mahali pa kuweka nyayo za miguu yangu. Hapa ndipo nitakapoishi miongoni mwa Waisraeli milele. Kamwe nyumba ya Israeli hawatalinajisi tena Jina langu takatifu, yaani, wao wala wafalme wao, kwa ukahaba wao na kwa sanamu zao zisizokuwa na uhai za wafalme wao katika mahali pao pa juu pa kuabudia miungu.
Og han sagde til mig: Du Menneskesøn! dette er min Trones Sted og mine Fodsaalers Sted, hvor jeg vil bo midt iblandt Israels Børn evindelig; og Israels Hus skal ikke ydermere vanhellige mit hellige Navn, de og deres Konger, med deres Bolen og med deres Kongers Lig, med deres Høje,
8 Walipoweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu na miimo yao ya milango karibu na miimo yangu, pakiwa na ukuta tu kati yangu na wao, walilinajisi Jina langu takatifu kwa matendo yao ya machukizo. Kwa sababu hiyo niliwaangamiza kwa hasira yangu.
idet de satte deres Dørtærskel ved min Dørtærskel og deres Dørstolper ved mine Dørstolper, og der kun var en Væg imellem mig og imellem dem; og de vanhelligede mit hellige Navn med deres Vederstyggeligheder, som de bedreve, saa at jeg lod dem fortæres i min Vrede.
9 Basi sasa na waweke mbali nami ukahaba wao na sanamu za wafalme wao zisizo na uhai, nami nitakaa miongoni mwao milele.
Nu skulle de fjerne deres Bolen og deres Kongers Lig langt bort fra mig; og jeg vil bo midt iblandt dem evindelig.
10 “Mwanadamu, elezea hilo Hekalu kwa watu wa Israeli, ili wapate kuona aibu kwa ajili ya dhambi zao. Wao na wapime hicho kielelezo.
Du Menneskesøn! forkynd Israels Hus om dette Hus, at de maa skamme sig for deres Misgerninger og maale den afmaalte Bygning.
11 Wakishaona aibu kwa ajili ya yale yote waliyotenda, wafahamishe kielelezo cha hilo Hekalu, yaani mpangilio wake, maingilio yake ya kutoka na kuingia, kielelezo chake chote, na masharti yake yote na sheria zake zote. Yaandike haya mbele yao ili wapate kuwa waaminifu kwa hicho kielelezo chake na kufuata masharti yake yote.
Og dersom de skamme sig over alt det, som de have gjort, vis dem saa Husets Skikkelse og dets Indretning og dets Udgange og dets Indgange og Skikkelsen af alt det enkelte deri og alle dets Bestemmelser, ja, Skikkelsen af alt det enkelte der og alle dets Love, og skriv det for deres Øjne, at de maa bevare hele dets Skikkelse og alle dets Bestemmelser og gøre efter dem.
12 “Hii ndiyo sheria ya Hekalu: Eneo lote linalozunguka Hekalu juu ya mlima litakuwa takatifu kuliko yote. Hii ndiyo sheria ya Hekalu.
Dette er Loven om Huset: Paa Bjergets Top skal hele dets Grænse trindt omkring være højhellig; se, dette er Loven om Huset.
13 “Hivi ndivyo vipimo vya madhabahu kwa dhiraa ndefu, yaani, dhiraa moja na nyanda nne: Tako lake liwe na kina cha hiyo dhiraa moja na upana wa hiyo dhiraa moja, ikiwa na ukingo wa shibiri moja kuizunguka pembeni. Hiki kitakuwa ndicho kimo cha madhabahu:
Og dette er Alterets Maal i Alen, hver Alen til en almindelig Alen og en Haandbred: Fodens Indfatning skal være een Alen høj og een Alen bred, og Listen derom paa Randen deraf trindt omkring skal være eet Spand; og dette er Alterets Grundvold.
14 Kimo cha msingi kuanzia usawa wa ardhi mpaka kwenye mfereji sehemu ya chini kimo chake ni dhiraa mbili na upana wake ni dhiraa moja na kuanzia kwenye ukingo mdogo hadi kwenye ukingo mpana kimo chake ni dhiraa nne na upana wake ni dhiraa moja.
Og fra Indfatningen af Foden paa Jorden indtil den nederste Afsætning skal der være to Alen og i Bredden een Alen; men fra den lille Afsætning indtil den store Afsætning skal der være fire Alen og i Bredden een Alen.
15 Pale pawashwapo moto madhabahuni kimo chake kitakuwa dhiraa nne, na pembe nne zinazoelekeza juu kutoka pale pawashwapo moto.
Og Harel skal være fire Alen, og fra Ariel og opad skal der være de fire Horn.
16 Pale pawashwapo moto pa madhabahu ni mraba, urefu wake ni dhiraa kumi na mbili na upana wa dhiraa kumi na mbili.
Og Ariel skal være tolv Alen lang og tolv Alen bred, i Firkant, efter sine fire Sider.
17 Pia sehemu ya juu ni mraba, urefu wake dhiraa kumi na nne na upana wa dhiraa kumi na nne, ikiwa na ukingo wa nusu dhiraa na mfereji kuizunguka madhabahu. Ngazi za kupandia madhabahuni zitaelekea upande wa mashariki.”
Og Afsætningen skal være fjorten Alen i Længden, med, fjorten Alen i Bredden, efter sine fire Sider, og Listen trindt omkring den en halv Alen, og Indfatningen af Foden dertil en Alen trindt omkring, og Trappen derop vende imod Østen.
18 Kisha akaniambia, “Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Haya ndiyo yatakayokuwa masharti ya kutoa dhabihu za kuteketezwa na kunyunyiza damu juu ya madhabahu itakapokuwa imejengwa.
Og han sagde til mig: Du Menneskesøn! saa siger den Herre, Herre: Dette er Bestemmelserne om Alteret, paa den Dag det bliver gjort for at ofre Brændoffer derpaa og for at stænke Blod derpaa.
19 Utatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi kwa makuhani, ambao ni Walawi, wa jamaa ya Sadoki, ndio watakaonikaribia kuhudumu mbele zangu, asema Bwana Mwenyezi.
Og du skal give Præsterne af Levi Stamme, som ere af Zadoks Sæd, og som ere mig nær for at tjene mig, siger den Herre, Herre, en ung Okse til Syndoffer.
20 Itakupasa kuchukua baadhi ya hiyo damu ya mnyama huyo na kuiweka juu ya hizo pembe nne za madhabahu na juu ya ncha zake nne za sehemu ya juu kuzunguka ukingo wote, ili kuitakasa madhabahu na kufanya upatanisho kwa ajili yake.
Og du skal tage af dens Blod og stryge paa dets fire Horn og paa de fire Hjørner af Afsætningen og paa Listen trindt omkring; og du skal rense det for Synd og udsone det.
21 Itakupasa kumchukua huyo fahali mchanga kwa ajili ya sadaka ya dhambi na kumteketeza mahali palipoagizwa katika eneo la Hekalu nje ya mahali Patakatifu.
Og du skal tage Syndofferets Okse, og man skal opbrænde den paa den bestemte Plads i Huset, liden for Helligdommen.
22 “Siku ya pili yake utamtoa beberu asiye na dosari kwa ajili ya sadaka ya dhambi, nayo madhabahu itatakaswa kama ilivyotakaswa kwa yule fahali.
Men den anden Dag skal du ofre en Gedebuk, som er lydefri, til Syndoffer; og de skulle rense Alteret for Synd, ligesom de rensede det for Synd med Oksen.
23 Utakapokuwa umemaliza kazi ya kuitakasa, utamtoa fahali mchanga pamoja na kondoo dume toka kwenye kundi, wote wawe hawana dosari.
Naar du er færdig med at rense det for Synd, skal du ofre en ung Okse, lydefri, og en lydefri Væder af Hjorden.
24 Utawatoa mbele za Bwana, nao makuhani watanyunyizia chumvi juu yao na kuwatoa kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.
Og du skal føre dem frem for Herrens Ansigt; og Præsterne skulle kaste Salt paa dem og ofre dem til et Brændoffer for Herren.
25 “Kwa siku saba itakupasa kutoa beberu kila siku kwa ajili ya sadaka ya dhambi, pia itakupasa kutoa fahali mchanga na kondoo dume kutoka zizini, wote wawe hawana dosari.
Syv Dage skal du tilberede en Buk til Syndoffer hver Dag; og en ung Okse og en Væder af Hjorden, som ere lydefri, skulle de tilberede.
26 Kwa siku saba itawapasa kufanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuitakasa na hivyo ndivyo watakavyoiweka wakfu.
I syv Dage skulle de udsone Alteret og rense det og fylde dets Haand.
27 Mwishoni mwa hizi siku saba, kuanzia siku ya nane na kuendelea, itawapasa makuhani kutoa sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za amani juu ya madhabahu. Kisha nitawakubali ninyi, asema Bwana Mwenyezi.”
Og naar de have fuldendt de Dage, da skal det ske paa den ottende Dag og fremdeles, at Præsterne skulle tilberede eders Brændofre og eders Takofre paa Alteret, og jeg vil have Behag i eder, siger den Herre, Herre.

< Ezekieli 43 >