< Ezekieli 42 >

1 Ndipo yule mtu akaniongoza kuelekea kaskazini mpaka kwenye ua wa nje na kunileta mpaka kwenye vyumba vinavyoelekeana na ua wa Hekalu na kuelekeana na ukuta wa nje upande wa kaskazini.
Y me llevó al patio interior en dirección al norte, y me llevó a las habitaciones que estaban frente al lugar separado y frente al edificio al norte.
2 Jengo ambalo mlango wake ulielekea kaskazini lilikuwa na urefu wa dhiraa mia moja na upana wa dhiraa hamsini.
En el lado norte tenía cien codos de largo y cincuenta codos de ancho.
3 Mbele ya zile dhiraa ishirini za ule ua wa ndani unaoelekeana na ile njia ya ua wa nje, kuliinuka vyumba virefu kimoja baada ya kingine vya ghorofa tatu.
Opuesto al espacio de veinte codos que formaba parte del patio interior, y opuesto al piso de piedra del patio exterior. Había habitaciones una frente al otra en el tercer piso.
4 Mbele ya hivi vyumba kulikuwa na njia ya ndani yenye upana wa dhiraa kumi na urefu wa dhiraa mia moja. Milango yake ilikuwa upande wa kaskazini.
Y delante de las habitaciones había un camino de diez codos de ancho y cien codos de largo; y sus puertas estaban orientadas al norte.
5 Basi vyumba vya juu vilikuwa vyembamba zaidi, kwa kuwa ujia ulichukua nafasi zaidi ndani yake kuliko katika vyumba vya sakafu ya chini na vya katikati ya jengo.
Y las habitaciones superiores eran más cortas; porque las galerías ocupaban más espacio que las habitaciones inferiores y medias.
6 Vyumba katika ghorofa ya tatu havikuwa na nguzo, kama kumbi zilivyokuwa nazo, kwa hiyo eneo la sakafu ya vyumba vya juu lilikuwa ni dogo kuliko la sakafu ya chini na ya kati.
Porque estaban en tres pisos, y no tenían pilares como los pilares del patio exterior; por lo tanto, el más alto era más estrecho que los pisos más bajos y medios desde el nivel de la tierra.
7 Kulikuwa na ukuta wa nje uliokuwa sambamba na vile vyumba na ukumbi wa nje, ulitokeza urefu wa dhiraa hamsini.
Y el muro que salía al lado de las habitaciones, en dirección al patio exterior frente a las habitaciones, tenía cincuenta codos de largo.
8 Wakati safu ya vyumba katika ua wa nje vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini, vile vyumba vilivyokuwa karibu zaidi na Hekalu vilikuwa na urefu wa dhiraa mia moja.
Porque las habitaciones en el patio exterior tenían cincuenta codos de largo: y frente al Templo había un espacio de cien codos.
9 Vyumba vya chini vilikuwa na ingilio upande wa mashariki unapoingia kutoka ukumbi wa nje.
Y debajo de estas habitaciones estaba el camino de entrada desde el lado este, a medida que uno entra en ellas desde el patio exterior.
10 Upande wa kusini kufuata urefu wa ukuta wa ukumbi wa nje, unaopakana na ukumbi wa Hekalu na kuelekeana na ukuta wa nje, kulikuwa na vyumba
Y él me llevó hacia el sur, y frente al lugar separado y frente al edificio había habitaciones.
11 vyenye ujia unayopita mbele yake. Hivi vilifanana na vile vyumba vya upande wa kaskazini, vilikuwa na urefu na upana ulio sawa, mahali pa kutokea na vipimo vyake vilikuwa sawa. Kama ilivyokuwa milango ya upande wa kaskazini,
Y había un pasillo delante de ellos así por las habitaciones en el norte; eran igualmente largos y anchos; y las salidas de ellos eran iguales en diseño y tenían el mismo tipo de puertas.
12 ndivyo ilivyokuwa milango ya vyumba vya upande wa kusini. Kulikuwa na ingilio kuanzia mwanzo wa njia ambao ulikuwa sambamba na ukuta wa pili uliokuwa upande wa mashariki, ambako ndiko kwa kuingia vyumbani.
Y debajo de las habitaciones en el sur había una puerta al comienzo del pasillo exterior en dirección al este cuando uno entra.
13 Kisha akaniambia, “Vyumba vya upande wa kaskazini na vya upande wa kusini ambavyo vinaelekeana na ukumbi wa Hekalu ni vyumba vya makuhani, mahali ambapo wale makuhani ambao humkaribia Bwana watakula zile sadaka takatifu sana. Huko ndiko watakakoweka zile sadaka takatifu sana, yaani, sadaka za nafaka, sadaka za dhambi na sadaka za hatia, kwa kuwa mahali ni patakatifu.
Y me dijo: Las habitaciones del norte y las habitaciones del sur, frente al lugar separado, son las habitaciones sagradas, donde los sacerdotes que se acercan al Señor toman las cosas más santas para su alimento; allí están las cosas santísimas, se colocan, con la ofrenda de cereal y la ofrenda por el pecado y la ofrenda por la culpa; porque el lugar es santo.
14 Mara makuhani waingiapo mahali patakatifu, hawaruhusiwi kwenda kwenye ukumbi wa nje mpaka wayaache mavazi ambayo walivaa wakiwa wanahudumu, kwa kuwa hayo mavazi ni matakatifu. Inawapasa kuvaa mavazi mengine kabla hawajakaribia eneo lililo wazi kwa ajili ya watu.”
Cuando los sacerdotes entran, no pueden salir del lugar santo a la plaza exterior, y allí deben poner las túnicas en las que hacen la obra de la casa del Señor, porque son santos; y Hay que ponerse otra ropa antes de que se acerque a lo que tiene que ver con la gente.
15 Alipomaliza kupima vile vilivyokuwa katika eneo la ndani la Hekalu, akanitoa nje kupitia lango la upande wa mashariki na kupima eneo lote linalozunguka:
Y cuando llegó al final de la medición de la casa interior, me llevó a la puerta que miraba hacia el este y tomó todas las medidas necesarias.
16 Akapima upande wa mashariki kwa ule ufito wa kupimia, nao ulikuwa dhiraa 500
Dio la vuelta y tomó la medida en el lado este con la vara de medir, quinientos, medida con la vara en todo su contorno.
17 Akapima upande wa kaskazini, nao ulikuwa dhiraa 500 kwa ufito ule wa kupimia.
Luego dio la vuelta y tomó la medida en el lado norte con la vara de medir, quinientos, medida con la vara por todas partes.
18 Tena akapima upande wa kusini, nao ulikuwa dhiraa 500 kwa ufito ule wa kupimia.
Luego, dio la vuelta y tomó la medida en el lado sur con la vara de medir, quinientos, medida con la vara por todas partes.
19 Kisha akageukia upande wa magharibi na kuupima, ulikuwa dhiraa 500 kwa ufito ule wa kupimia.
Luego dio la vuelta y tomó la medida en el lado oeste con la vara de medir, quinientos, medida con la vara por todas partes.
20 Hivyo akapima eneo katika pande zote nne. Lilikuwa na ukuta kulizunguka wenye urefu wa dhiraa 500 na upana wa dhiraa 500, uliotenganisha mahali Patakatifu na eneo la watu wote.
Tomó su medida en los cuatro lados; y tenía un muro alrededor, quinientos de largo y quinientos de ancho, que separaba lo que era santo de lo que era común.

< Ezekieli 42 >