< Ezekieli 42 >
1 Ndipo yule mtu akaniongoza kuelekea kaskazini mpaka kwenye ua wa nje na kunileta mpaka kwenye vyumba vinavyoelekeana na ua wa Hekalu na kuelekeana na ukuta wa nje upande wa kaskazini.
Potem me je odvedel naprej na skrajni dvor, ob poti proti severu in me privedel v sobo, ki je bila nasproti ločenemu kraju in ki je bila pred zgradbo proti severu.
2 Jengo ambalo mlango wake ulielekea kaskazini lilikuwa na urefu wa dhiraa mia moja na upana wa dhiraa hamsini.
Pred dolžino stotih komolcev so bila severna vrata in širina je bila petdeset komolcev.
3 Mbele ya zile dhiraa ishirini za ule ua wa ndani unaoelekeana na ile njia ya ua wa nje, kuliinuka vyumba virefu kimoja baada ya kingine vya ghorofa tatu.
Nasproti dvajsetim komolcem, ki so bili za notranji dvor in nasproti tlaku, ki je bil za skrajni dvor, je bila galerija nasproti galeriji, v treh nadstropjih.
4 Mbele ya hivi vyumba kulikuwa na njia ya ndani yenye upana wa dhiraa kumi na urefu wa dhiraa mia moja. Milango yake ilikuwa upande wa kaskazini.
Pred sobami je bil hodnik desetih komolcev širine znotraj, pot enega komolca; in njihova vrata proti severu.
5 Basi vyumba vya juu vilikuwa vyembamba zaidi, kwa kuwa ujia ulichukua nafasi zaidi ndani yake kuliko katika vyumba vya sakafu ya chini na vya katikati ya jengo.
Torej zgornje sobe so bile krajše, kajti galerije so bile višje kakor te, kakor spodnje in kakor tiste, ki so bile v sredini zgradbe.
6 Vyumba katika ghorofa ya tatu havikuwa na nguzo, kama kumbi zilivyokuwa nazo, kwa hiyo eneo la sakafu ya vyumba vya juu lilikuwa ni dogo kuliko la sakafu ya chini na ya kati.
Kajti bile so v treh nadstropjih, toda niso imele stebrov kakor stebri dvora, zato je bila zgradba ožja, bolj kakor nižje in srednje od tal.
7 Kulikuwa na ukuta wa nje uliokuwa sambamba na vile vyumba na ukumbi wa nje, ulitokeza urefu wa dhiraa hamsini.
Zid, ki je bil zunaj, nasproti sobam, proti skrajnemu dvoru, na sprednjem delu sob, njegova dolžina je bila petdeset komolcev.
8 Wakati safu ya vyumba katika ua wa nje vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini, vile vyumba vilivyokuwa karibu zaidi na Hekalu vilikuwa na urefu wa dhiraa mia moja.
Kajti dolžina sob, ki so bile na skrajnem dvoru, je bila petdeset komolcev, in glej, pred templjem je bilo sto komolcev.
9 Vyumba vya chini vilikuwa na ingilio upande wa mashariki unapoingia kutoka ukumbi wa nje.
Izpod teh sob je bil vhod na vzhodni strani, kakor gre nekdo vanje od skrajnega dvora.
10 Upande wa kusini kufuata urefu wa ukuta wa ukumbi wa nje, unaopakana na ukumbi wa Hekalu na kuelekeana na ukuta wa nje, kulikuwa na vyumba
Sobe so bile v debelini zidu dvora proti vzhodu, nasproti ločenemu kraju in nasproti zgradbi.
11 vyenye ujia unayopita mbele yake. Hivi vilifanana na vile vyumba vya upande wa kaskazini, vilikuwa na urefu na upana ulio sawa, mahali pa kutokea na vipimo vyake vilikuwa sawa. Kama ilivyokuwa milango ya upande wa kaskazini,
Pot pred njimi je bila podobna videzu sob, ki so bile proti severu, tako dolga kakor one in tako široka kakor one, in vsi njihovi izhodi so bili tako glede na njihove oblike kakor glede na njihova vrata.
12 ndivyo ilivyokuwa milango ya vyumba vya upande wa kusini. Kulikuwa na ingilio kuanzia mwanzo wa njia ambao ulikuwa sambamba na ukuta wa pili uliokuwa upande wa mashariki, ambako ndiko kwa kuingia vyumbani.
Glede na vrata sob, ki so bila proti jugu, so bila vrata na začetku poti, celó na poti neposredno pred zidom proti vzhodu, kakor nekdo vstopa vanje.
13 Kisha akaniambia, “Vyumba vya upande wa kaskazini na vya upande wa kusini ambavyo vinaelekeana na ukumbi wa Hekalu ni vyumba vya makuhani, mahali ambapo wale makuhani ambao humkaribia Bwana watakula zile sadaka takatifu sana. Huko ndiko watakakoweka zile sadaka takatifu sana, yaani, sadaka za nafaka, sadaka za dhambi na sadaka za hatia, kwa kuwa mahali ni patakatifu.
Potem mi je rekel: »Severne sobe in južne sobe, ki so pred ločenim krajem, te so svete sobe, kjer bodo duhovniki, ki pristopajo h Gospodu, jedli najsvetejše stvari. Tam bodo polagali najsvetejše stvari in jedilno daritev in daritev za greh in daritev za prestopke; kajti kraj je svet.
14 Mara makuhani waingiapo mahali patakatifu, hawaruhusiwi kwenda kwenye ukumbi wa nje mpaka wayaache mavazi ambayo walivaa wakiwa wanahudumu, kwa kuwa hayo mavazi ni matakatifu. Inawapasa kuvaa mavazi mengine kabla hawajakaribia eneo lililo wazi kwa ajili ya watu.”
Ko duhovniki vstopijo vanj, potem ne bodo šli ven iz svetega kraja na skrajni dvor, temveč bodo tam odložili oblačila, v katerih so služili, kajti ta so sveta in nadeli si bodo druga oblačila in pristopili bodo k tistim stvarem, ki so za ljudstvo.«
15 Alipomaliza kupima vile vilivyokuwa katika eneo la ndani la Hekalu, akanitoa nje kupitia lango la upande wa mashariki na kupima eneo lote linalozunguka:
Torej ko je končal merjenje notranje hiše, me je privedel naprej proti velikim vratom, katerih pročelje je proti vzhodu in ga izmeril naokrog.
16 Akapima upande wa mashariki kwa ule ufito wa kupimia, nao ulikuwa dhiraa 500
Izmeril je vzhodno stran z merilno trstiko, petsto trstik, z merilno trstiko naokrog.
17 Akapima upande wa kaskazini, nao ulikuwa dhiraa 500 kwa ufito ule wa kupimia.
Izmeril je severno stran, petsto trstik, z merilno trstiko naokrog.
18 Tena akapima upande wa kusini, nao ulikuwa dhiraa 500 kwa ufito ule wa kupimia.
Izmeril je južno stran, petsto trstik, z merilno trstiko.
19 Kisha akageukia upande wa magharibi na kuupima, ulikuwa dhiraa 500 kwa ufito ule wa kupimia.
Obrnil se je k zahodni strani in izmeril petsto trstik z merilno trstiko.
20 Hivyo akapima eneo katika pande zote nne. Lilikuwa na ukuta kulizunguka wenye urefu wa dhiraa 500 na upana wa dhiraa 500, uliotenganisha mahali Patakatifu na eneo la watu wote.
Izmeril jo je ob štirih straneh. Naokrog je imela obzidje, petsto trstik dolgo in petsto široko, da bi naredil oddvojitev med svetiščem in oskrunjenim krajem.