< Ezekieli 42 >

1 Ndipo yule mtu akaniongoza kuelekea kaskazini mpaka kwenye ua wa nje na kunileta mpaka kwenye vyumba vinavyoelekeana na ua wa Hekalu na kuelekeana na ukuta wa nje upande wa kaskazini.
Depois disto fêz-me sair para fora, ao átrio exterior, para a banda do caminho do norte; e me levou às câmaras que estavam defronte do largo vazio, e que estavam defronte do edifício, da banda do norte.
2 Jengo ambalo mlango wake ulielekea kaskazini lilikuwa na urefu wa dhiraa mia moja na upana wa dhiraa hamsini.
Defronte do comprimento de cem côvados era a entrada do norte: e a largura era de cincoênta côvados.
3 Mbele ya zile dhiraa ishirini za ule ua wa ndani unaoelekeana na ile njia ya ua wa nje, kuliinuka vyumba virefu kimoja baada ya kingine vya ghorofa tatu.
Defronte dos vinte côvados, que tinha o átrio interior, e defronte do pavimento que tinha o átrio exterior, havia galeria contra galeria em três andares.
4 Mbele ya hivi vyumba kulikuwa na njia ya ndani yenye upana wa dhiraa kumi na urefu wa dhiraa mia moja. Milango yake ilikuwa upande wa kaskazini.
E diante das câmaras havia um passeio de dez côvados de largo, da banda de dentro, e um caminho dum côvado, e as suas entradas da banda do norte.
5 Basi vyumba vya juu vilikuwa vyembamba zaidi, kwa kuwa ujia ulichukua nafasi zaidi ndani yake kuliko katika vyumba vya sakafu ya chini na vya katikati ya jengo.
E as câmaras de cima eram mais estreitas; porquanto as galerias eram mais altas do que aquelas, a saber, as de baixo e as do meio do edifício.
6 Vyumba katika ghorofa ya tatu havikuwa na nguzo, kama kumbi zilivyokuwa nazo, kwa hiyo eneo la sakafu ya vyumba vya juu lilikuwa ni dogo kuliko la sakafu ya chini na ya kati.
Porque elas eram de três andares, porém não tinham colunas como as colunas dos átrios; por isso desde o chão se iam estreitando, mais do que as de baixo e as do meio.
7 Kulikuwa na ukuta wa nje uliokuwa sambamba na vile vyumba na ukumbi wa nje, ulitokeza urefu wa dhiraa hamsini.
E o muro que estava de fora, defronte das câmaras, no caminho do átrio exterior, por diante das câmaras, tinha cincoênta côvados de comprimento.
8 Wakati safu ya vyumba katika ua wa nje vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini, vile vyumba vilivyokuwa karibu zaidi na Hekalu vilikuwa na urefu wa dhiraa mia moja.
Porque o comprimento das câmaras, que tinha o átrio exterior, era de cincoênta côvados; e eis que defronte do templo havia cem côvados.
9 Vyumba vya chini vilikuwa na ingilio upande wa mashariki unapoingia kutoka ukumbi wa nje.
E debaixo destas câmaras estava a entrada do oriente, quando se entra nelas do átrio de fora.
10 Upande wa kusini kufuata urefu wa ukuta wa ukumbi wa nje, unaopakana na ukumbi wa Hekalu na kuelekeana na ukuta wa nje, kulikuwa na vyumba
Na largura do muro do átrio para o caminho do oriente, diante do lugar vazio, e diante do edifício, havia também câmaras.
11 vyenye ujia unayopita mbele yake. Hivi vilifanana na vile vyumba vya upande wa kaskazini, vilikuwa na urefu na upana ulio sawa, mahali pa kutokea na vipimo vyake vilikuwa sawa. Kama ilivyokuwa milango ya upande wa kaskazini,
E o caminho de diante delas era da feição das câmaras, e olhava para o caminho do norte; conforme o seu comprimento, assim era a sua largura; e todas as suas saídas eram também conforme as suas feições, e conforme as suas entradas.
12 ndivyo ilivyokuwa milango ya vyumba vya upande wa kusini. Kulikuwa na ingilio kuanzia mwanzo wa njia ambao ulikuwa sambamba na ukuta wa pili uliokuwa upande wa mashariki, ambako ndiko kwa kuingia vyumbani.
E conforme as entradas das câmaras, que olhavam para o caminho do sul, havia também uma entrada no topo do caminho, do caminho de diante do muro direito, para o caminho do oriente, quando se entra por elas.
13 Kisha akaniambia, “Vyumba vya upande wa kaskazini na vya upande wa kusini ambavyo vinaelekeana na ukumbi wa Hekalu ni vyumba vya makuhani, mahali ambapo wale makuhani ambao humkaribia Bwana watakula zile sadaka takatifu sana. Huko ndiko watakakoweka zile sadaka takatifu sana, yaani, sadaka za nafaka, sadaka za dhambi na sadaka za hatia, kwa kuwa mahali ni patakatifu.
Então me disse: As câmaras do norte, e as câmaras do sul, que estão diante do lugar vazio, elas são câmaras santas, em que os sacerdotes, que se chegam ao Senhor, comerão as coisas mais santas: ali porão as coisas mais santas, e as ofertas de comer, e a expiação pelo pecado, e a expiação pela culpa; porque o lugar é santo
14 Mara makuhani waingiapo mahali patakatifu, hawaruhusiwi kwenda kwenye ukumbi wa nje mpaka wayaache mavazi ambayo walivaa wakiwa wanahudumu, kwa kuwa hayo mavazi ni matakatifu. Inawapasa kuvaa mavazi mengine kabla hawajakaribia eneo lililo wazi kwa ajili ya watu.”
Quando os sacerdotes entrarem, não sairão do santuário para o átrio exterior, mas porão ali as suas vestiduras com que ministraram, porque elas são santidade; e vestir-se-ão de outras vestiduras, e assim se aproximarão do que toca ao povo.
15 Alipomaliza kupima vile vilivyokuwa katika eneo la ndani la Hekalu, akanitoa nje kupitia lango la upande wa mashariki na kupima eneo lote linalozunguka:
E, acabando ele de medir o templo interior, ele me fez sair pelo caminho da porta, cuja face olha para o caminho do oriente; e a mediu em redor.
16 Akapima upande wa mashariki kwa ule ufito wa kupimia, nao ulikuwa dhiraa 500
Mediu a banda oriental com a cana de medir, quinhentas canas com a cana de medir ao redor.
17 Akapima upande wa kaskazini, nao ulikuwa dhiraa 500 kwa ufito ule wa kupimia.
Mediu a banda do norte, quinhentas canas com a cana de medir ao redor.
18 Tena akapima upande wa kusini, nao ulikuwa dhiraa 500 kwa ufito ule wa kupimia.
A banda do sul também mediu, quinhentas canas com a cana de medir.
19 Kisha akageukia upande wa magharibi na kuupima, ulikuwa dhiraa 500 kwa ufito ule wa kupimia.
Deu uma volta para a banda do ocidente, e mediu quinhentas canas com a cana de medir.
20 Hivyo akapima eneo katika pande zote nne. Lilikuwa na ukuta kulizunguka wenye urefu wa dhiraa 500 na upana wa dhiraa 500, uliotenganisha mahali Patakatifu na eneo la watu wote.
Pelas quatro bandas a mediu, e tinha um muro em redor, quinhentas canas de comprimento, e quinhentas de largura, para fazer separação entre o santo e o profano.

< Ezekieli 42 >