< Ezekieli 42 >
1 Ndipo yule mtu akaniongoza kuelekea kaskazini mpaka kwenye ua wa nje na kunileta mpaka kwenye vyumba vinavyoelekeana na ua wa Hekalu na kuelekeana na ukuta wa nje upande wa kaskazini.
I wwiódł mię do sieni zewnętrznej drogą, która idzie ku północy, i wwiódł mię do onych komórek, które były przeciwko piętru, a które były przeciwko budowaniu na północy.
2 Jengo ambalo mlango wake ulielekea kaskazini lilikuwa na urefu wa dhiraa mia moja na upana wa dhiraa hamsini.
Którego długość przy drzwiach na północy była na wejrzeniu na sto łokci, a szerokość na pięćdziesiąt łokci.
3 Mbele ya zile dhiraa ishirini za ule ua wa ndani unaoelekeana na ile njia ya ua wa nje, kuliinuka vyumba virefu kimoja baada ya kingine vya ghorofa tatu.
Przeciwko sieni wewnętrzej, która miała dwadzieścia łokci i przeciwko tłu, które było w sieni zewnętrznej z dworu, był ganek przeciwko gankowi trzema rzędami.
4 Mbele ya hivi vyumba kulikuwa na njia ya ndani yenye upana wa dhiraa kumi na urefu wa dhiraa mia moja. Milango yake ilikuwa upande wa kaskazini.
A przed komórkami był plac do przechadzki na dziesięć łokci wszerz wewnątrz, ścieszka do nich na jednym łokciu, a drzwi ich były na północy.
5 Basi vyumba vya juu vilikuwa vyembamba zaidi, kwa kuwa ujia ulichukua nafasi zaidi ndani yake kuliko katika vyumba vya sakafu ya chini na vya katikati ya jengo.
A komórki najwyższe były ciaśniejsze, przeto, że ganki były szersze niż one, niżeli spodnie i średnie budowania.
6 Vyumba katika ghorofa ya tatu havikuwa na nguzo, kama kumbi zilivyokuwa nazo, kwa hiyo eneo la sakafu ya vyumba vya juu lilikuwa ni dogo kuliko la sakafu ya chini na ya kati.
Bo było o trzech piętrach, ale nie miało słupów, jakie słupy były w sieniach; przetoż wąższe było niż spodnie i niż średnie od ziemi.
7 Kulikuwa na ukuta wa nje uliokuwa sambamba na vile vyumba na ukumbi wa nje, ulitokeza urefu wa dhiraa hamsini.
Ogrodzenia też, które było z dworu przeciwko onym komorom ku sieni zewnętrznej przed komórkami, długość była na pięćdziesiąt łokci.
8 Wakati safu ya vyumba katika ua wa nje vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini, vile vyumba vilivyokuwa karibu zaidi na Hekalu vilikuwa na urefu wa dhiraa mia moja.
Bo długość komórek, które były w sieni zewnętrzej, była na pięćdziesiąt łokci, a przed kościołem sto łokci.
9 Vyumba vya chini vilikuwa na ingilio upande wa mashariki unapoingia kutoka ukumbi wa nje.
A pod temi komórkami było wejście od wschodu słońca, przez które wchodzono do nich z onej sieni zewnętrznej.
10 Upande wa kusini kufuata urefu wa ukuta wa ukumbi wa nje, unaopakana na ukumbi wa Hekalu na kuelekeana na ukuta wa nje, kulikuwa na vyumba
Na szerokości ogrodzenia onej sieni ku wschodowi przed piętrem i przed budowaniem były komórki.
11 vyenye ujia unayopita mbele yake. Hivi vilifanana na vile vyumba vya upande wa kaskazini, vilikuwa na urefu na upana ulio sawa, mahali pa kutokea na vipimo vyake vilikuwa sawa. Kama ilivyokuwa milango ya upande wa kaskazini,
A ścieszka przed niemi była podobna ścieszce onych komórek, które były na północy; a jako była długość ich, taka też była szerokość ich, a wszystkie wyjścia ich i drzwi ich były im podobne.
12 ndivyo ilivyokuwa milango ya vyumba vya upande wa kusini. Kulikuwa na ingilio kuanzia mwanzo wa njia ambao ulikuwa sambamba na ukuta wa pili uliokuwa upande wa mashariki, ambako ndiko kwa kuingia vyumbani.
A drzwi onych komórek, które były na południe, podobne były drzwiom na początku drogi, drogi, mówię, przed ogrodzeniem prosto na wschód słońca, kędy się wchodzi do nich.
13 Kisha akaniambia, “Vyumba vya upande wa kaskazini na vya upande wa kusini ambavyo vinaelekeana na ukumbi wa Hekalu ni vyumba vya makuhani, mahali ambapo wale makuhani ambao humkaribia Bwana watakula zile sadaka takatifu sana. Huko ndiko watakakoweka zile sadaka takatifu sana, yaani, sadaka za nafaka, sadaka za dhambi na sadaka za hatia, kwa kuwa mahali ni patakatifu.
Tedy rzekł do mnie: Komórki na północy, i komórki na południe, które są przed piętrem, są komórki święte, gdzie będą jadali kapłani, którzy przystępują do Pana, przynosząc rzeczy najświętsze; tam kłaść będą rzeczy najświętsze, i ofiary śniedne, i ofiary za grzech, i za występek; bo to miejsce święte jest.
14 Mara makuhani waingiapo mahali patakatifu, hawaruhusiwi kwenda kwenye ukumbi wa nje mpaka wayaache mavazi ambayo walivaa wakiwa wanahudumu, kwa kuwa hayo mavazi ni matakatifu. Inawapasa kuvaa mavazi mengine kabla hawajakaribia eneo lililo wazi kwa ajili ya watu.”
Tam gdy wnijdą kapłani, nie wynijdą z świątnicy do sieni zewnętrznej, ale tam zostawią odzienia swoje, w których służyli (bo święte jest) a obloką się w insze szaty, gdy będą mieli przystąpić do tego, co należy ludowi.
15 Alipomaliza kupima vile vilivyokuwa katika eneo la ndani la Hekalu, akanitoa nje kupitia lango la upande wa mashariki na kupima eneo lote linalozunguka:
A gdy odprawił wymiar domu wewnętrznego, wywiódł mię drogą ku bramie, która idzie ku wschodowi, i wymierzył go wszędy w około.
16 Akapima upande wa mashariki kwa ule ufito wa kupimia, nao ulikuwa dhiraa 500
Wymierzył stronę od wschodu słońca laską pomiaru na pięćset lasek laski pomiarowej w około.
17 Akapima upande wa kaskazini, nao ulikuwa dhiraa 500 kwa ufito ule wa kupimia.
Wymierzył też stronę północną na pięćset lasek laską pomiaru w około.
18 Tena akapima upande wa kusini, nao ulikuwa dhiraa 500 kwa ufito ule wa kupimia.
Także stronę od południa wymierzył na pięćset laską pomiaru.
19 Kisha akageukia upande wa magharibi na kuupima, ulikuwa dhiraa 500 kwa ufito ule wa kupimia.
A obróciwszy się ku stronie zachodniej, wymierzył ją na pięćset lasek laską pomiaru.
20 Hivyo akapima eneo katika pande zote nne. Lilikuwa na ukuta kulizunguka wenye urefu wa dhiraa 500 na upana wa dhiraa 500, uliotenganisha mahali Patakatifu na eneo la watu wote.
Na cztery strony wymierzył to, to jest mur zewsząd w około, długość na pięćset, a szerokość także na pięćset lasek, aby się dzieliło święte miejsce od pospolitego.