< Ezekieli 42 >

1 Ndipo yule mtu akaniongoza kuelekea kaskazini mpaka kwenye ua wa nje na kunileta mpaka kwenye vyumba vinavyoelekeana na ua wa Hekalu na kuelekeana na ukuta wa nje upande wa kaskazini.
Derpå førte han mig ud i den indre forgård i nordlig retning, og han førte mig til Kamrene, som lå ud imod den afspærrede Plads og Bagbygningen, nogle på den ene Side, andre på den anden.
2 Jengo ambalo mlango wake ulielekea kaskazini lilikuwa na urefu wa dhiraa mia moja na upana wa dhiraa hamsini.
Længden var hundrede Alen og Bredden halvtredsindstyve.
3 Mbele ya zile dhiraa ishirini za ule ua wa ndani unaoelekeana na ile njia ya ua wa nje, kuliinuka vyumba virefu kimoja baada ya kingine vya ghorofa tatu.
Over for Portene, som hørte til den indre Forgård, og over for Stenbroen, som hørte til den ydre Forgård, var der Gang over for Gang i tre Stokværk.
4 Mbele ya hivi vyumba kulikuwa na njia ya ndani yenye upana wa dhiraa kumi na urefu wa dhiraa mia moja. Milango yake ilikuwa upande wa kaskazini.
Foran Kamrene var der en Forgang, ti Alen bred og hundrede Alen lang, og deres Døre vendte mod Nord.
5 Basi vyumba vya juu vilikuwa vyembamba zaidi, kwa kuwa ujia ulichukua nafasi zaidi ndani yake kuliko katika vyumba vya sakafu ya chini na vya katikati ya jengo.
De øvre Kamre var de snævreste, thi Gangen tog noget af deres Plads, så at de var mindre end de nederste og mellemste.
6 Vyumba katika ghorofa ya tatu havikuwa na nguzo, kama kumbi zilivyokuwa nazo, kwa hiyo eneo la sakafu ya vyumba vya juu lilikuwa ni dogo kuliko la sakafu ya chini na ya kati.
Thi de havde tre Stokværk og ingen Søjler svarende til den ydre Forgårds; derfor var de øverste snævrere end de nederste og mellemste.
7 Kulikuwa na ukuta wa nje uliokuwa sambamba na vile vyumba na ukumbi wa nje, ulitokeza urefu wa dhiraa hamsini.
Der løb en Mur udenfor langs Kamrene i Retning af den ydre Forgård; foran Kamrene var dens Længde halvtredsindstyve Alen;
8 Wakati safu ya vyumba katika ua wa nje vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini, vile vyumba vilivyokuwa karibu zaidi na Hekalu vilikuwa na urefu wa dhiraa mia moja.
thi Kamrene, som lå ved den ydre Forgård, havde en samlet Længde af halvtredsindstyve Alen, og de lå over for hine, i alt hundrede Alen.
9 Vyumba vya chini vilikuwa na ingilio upande wa mashariki unapoingia kutoka ukumbi wa nje.
Neden for disse Kamre var indgangen på Østsiden, når man gik ind i dem fra den ydre Forgård,
10 Upande wa kusini kufuata urefu wa ukuta wa ukumbi wa nje, unaopakana na ukumbi wa Hekalu na kuelekeana na ukuta wa nje, kulikuwa na vyumba
ved Begyndelsen af den ydre Mur. Derpå førte han mig mod Syd; og der var også Kamre ud imod den afspærrede Plads og Bagbygningen
11 vyenye ujia unayopita mbele yake. Hivi vilifanana na vile vyumba vya upande wa kaskazini, vilikuwa na urefu na upana ulio sawa, mahali pa kutokea na vipimo vyake vilikuwa sawa. Kama ilivyokuwa milango ya upande wa kaskazini,
med en Gang foran; de så ud som Kamrene mod Nord; havde samme Længde og Bredde, og alle Udgange var her som hist, ligesom de var indrettet på samme Måde.
12 ndivyo ilivyokuwa milango ya vyumba vya upande wa kusini. Kulikuwa na ingilio kuanzia mwanzo wa njia ambao ulikuwa sambamba na ukuta wa pili uliokuwa upande wa mashariki, ambako ndiko kwa kuingia vyumbani.
Men deres Døre vendte mod Syd..."
13 Kisha akaniambia, “Vyumba vya upande wa kaskazini na vya upande wa kusini ambavyo vinaelekeana na ukumbi wa Hekalu ni vyumba vya makuhani, mahali ambapo wale makuhani ambao humkaribia Bwana watakula zile sadaka takatifu sana. Huko ndiko watakakoweka zile sadaka takatifu sana, yaani, sadaka za nafaka, sadaka za dhambi na sadaka za hatia, kwa kuwa mahali ni patakatifu.
Og han sagde til mig: "Kamrene mod Nord og Syd, som ligger ud mod den afspærrede Plads, er de hellige Kamre, hvor Præsterne, der nærmer sig HERREN, skal spise det højhellige; der skal de gemme det højhellige, Afgrødeofrene, Syndofrene og Skyldofrene, thi Stedet er helligt;
14 Mara makuhani waingiapo mahali patakatifu, hawaruhusiwi kwenda kwenye ukumbi wa nje mpaka wayaache mavazi ambayo walivaa wakiwa wanahudumu, kwa kuwa hayo mavazi ni matakatifu. Inawapasa kuvaa mavazi mengine kabla hawajakaribia eneo lililo wazi kwa ajili ya watu.”
og når Præsterne træder ind - de må ikke fra Helligdommen træde ud i den ydre Forgård - skal de der nedlægge deres Klæder, som de gør Tjeneste i, da de er hellige, og iføre sig andre Klæder; da først må de nærme sig det, der hører Folket til."
15 Alipomaliza kupima vile vilivyokuwa katika eneo la ndani la Hekalu, akanitoa nje kupitia lango la upande wa mashariki na kupima eneo lote linalozunguka:
Da han var til Ende med at udmåle Templets Indre, førte han mig hen til den Port, hvis Forside vendte mod Øst, og målte til alle Sider;
16 Akapima upande wa mashariki kwa ule ufito wa kupimia, nao ulikuwa dhiraa 500
han målte med Målestangen Østsiden; den var efter Målestangen 500 Alen; så vendte han sig og
17 Akapima upande wa kaskazini, nao ulikuwa dhiraa 500 kwa ufito ule wa kupimia.
målte med Målestangen Nordsiden til 500 Alen;
18 Tena akapima upande wa kusini, nao ulikuwa dhiraa 500 kwa ufito ule wa kupimia.
så vendte han sig og målte med Målestangen Sydsiden til 500 Alen;
19 Kisha akageukia upande wa magharibi na kuupima, ulikuwa dhiraa 500 kwa ufito ule wa kupimia.
og han vendte sig og målte med Målestangen Vestsiden til 500 Alen.
20 Hivyo akapima eneo katika pande zote nne. Lilikuwa na ukuta kulizunguka wenye urefu wa dhiraa 500 na upana wa dhiraa 500, uliotenganisha mahali Patakatifu na eneo la watu wote.
Til alle fire Sider målte han Pladsen; og der var en Mur rundt om, 500 Alen lang og 500 Alen bred, til at sætte Skel mellem det, som er helligt, og det, som ikke er helligt.

< Ezekieli 42 >