< Ezekieli 41 >
1 Kisha yule mtu akanileta katika sehemu ya nje ya patakatifu, naye akaipima miimo; upana wake ulikuwa dhiraa sita kila upande.
Bundan sonra adam beni tapınağın ana bölümüne götürüp kapı sövelerini ölçtü. Sövelerin genişliği her yandan altı arşındı.
2 Ingilio lilikuwa la upana wa dhiraa kumi na kuta zilizojitokeza kila upande zilikuwa na upana wa dhiraa tano. Pia akapima sehemu ya nje ya patakatifu, nayo ilikuwa na urefu wa dhiraa arobaini na upana wa dhiraa ishirini.
Girişinin genişliği on arşın, her yandan buna bağlı duvarların genişliği beşer arşındı. Ana bölümü de ölçtü. Uzunluğu kırk arşın, genişliği yirmi arşındı.
3 Kisha akaingia sehemu takatifu ndani ya Hekalu na kupima miimo ya ingilio, kila mmoja ulikuwa na upana wa dhiraa mbili. Ingilio lilikuwa na upana wa dhiraa sita, na kuta zilizotokeza kila upande zilikuwa na upana wa dhiraa saba.
Sonra iç odaya gidip girişin sövelerini ölçtü. Her biri iki arşın genişliğindeydi. Girişin genişliği altı arşın, her yandan buna bağlı duvarların genişliği yedi arşındı.
4 Naye akapima urefu wa sehemu takatifu ndani, nao ulikuwa dhiraa ishirini, na upana wake ulikuwa dhiraa ishirini hadi mwisho wa sehemu ya nje ya sehemu takatifu. Akaniambia, “Hapa ndipo Patakatifu pa Patakatifu.”
Ana bölümün ötesindeki iç odayı ölçtü. Uzunluğu ve genişliği yirmişer arşındı. Adam, “Bu En Kutsal Yer'dir” dedi.
5 Kisha akapima ukuta wa Hekalu, nao ulikuwa na unene wa dhiraa sita, na kila chumba cha pembeni kuzunguka Hekalu kilikuwa na upana wa dhiraa nne.
Tapınağın duvarını ölçtü, kalınlığı altı arşındı. Tapınağın çevresindeki her yan odanın genişliği dört arşındı.
6 Vyumba vya pembeni vilikuwa na ghorofa tatu, kimoja juu ya kingine, kila ghorofa ilikuwa na vyumba thelathini. Kulikuwa na boriti katika ukuta wote wa Hekalu ili kuimarisha vyumba vya pembeni, kwa hiyo boriti hizo hazikushikamanishwa kwenye ukuta wa Hekalu.
Bu yan odalar üç kattı, her katta otuz oda vardı. Tapınağın duvarları boyunca yan odalara destek görevi yapan çıkıntılar vardı. Öyle ki, destekler tapınak duvarlarına girmesin.
7 Vyumba vya pembeni vilivyozunguka Hekalu vilizidi kupanuka kulingana na sakafu zilivyokwenda juu. Ujenzi uliozunguka Hekalu ulijengwa kukwea juu, kwa hiyo vyumba vilipanuka kwa kadiri ya kila kimoja kilivyokwenda juu. Ngazi za kupandia zilianzia sakafu ya chini hadi sakafu ya juu kabisa kwa kupitia sakafu ya kati.
Tapınağın çevresindeki yan odalar yukarı kata doğru çıktıkça genişliyordu. Tapınağın çevresindeki yapının yukarıya çıkan bir merdiveni vardı. Yukarıya doğru çıkıldıkça yan odalar genişliyordu. Merdivenle alt kattan orta kata, oradan da üst kata çıkılıyordu.
8 Nikaona pia kuwa Hekalu lilikuwa na kitako kilichoinuliwa pande zote, huu ulikuwa ndio msingi wa vile vyumba vya pembeni ambao ulikuwa na urefu wa ule ufito mmoja wa kupimia, yaani, dhiraa ndefu sita.
Tapınağın çevresinde yan odaların temelini oluşturan yüksek bir kaldırım gördüm. Uzunluğu bir değnek kadar, yani altı arşındı.
9 Ukuta wa nje wa vyumba vya pembeni ulikuwa na unene wa dhiraa tano. Eneo la wazi katikati ya vyumba vya pembeni vya Hekalu
Yan odaların dış duvarının kalınlığı beş arşındı. Tapınağın yan odaları ile kâhin odaları arasındaki açık alanın genişliği tapınak çevresi boyunca yirmi arşındı.
10 na vyumba vya makuhani lilikuwa na upana wa dhiraa ishirini kuzunguka Hekalu pande zote.
11 Kulikuwa na maingilio kwenye vyumba vya pembeni kutokea eneo lililo wazi, moja upande wa kaskazini na lingine upande wa kusini, nao msingi uliounganisha lile eneo la wazi ulikuwa na upana wa dhiraa tano ukilizunguka lote.
Yan odaların girişi açık alana bakıyordu; biri kuzeyde, öbürü güneydeydi. Açık alana bitişik temelin genişliği her yandan beş arşındı.
12 Jengo lililoelekeana na ua wa Hekalu upande wa magharibi lilikuwa na upana wa dhiraa sabini. Ukuta wa jengo hilo ulikuwa na unene wa dhiraa tano, kulizunguka lote, urefu ulikuwa wa dhiraa tisini.
Tapınağın batısında açık alana bakan bir yapı vardı. Genişliği yetmiş arşındı; duvarının kalınlığı her yandan beş arşın, uzunluğu doksan arşındı.
13 Kisha akapima Hekalu, lilikuwa na urefu wa dhiraa mia moja na ua wa Hekalu na jengo pamoja na kuta zake vilikuwa na urefu wa dhiraa mia moja pia.
Bundan sonra adam tapınağı ölçtü. Uzunluğu yüz arşındı. Tapınağın açık alanı, yapı ve duvarları yüz arşın uzunluktaydı.
14 Upana wa ua wa Hekalu upande wa mashariki, pamoja na upande wa mbele wa Hekalu ulikuwa dhiraa mia moja.
Doğuda tapınağın açık alanının tapınağın önüyle birlikte genişliği yüz arşındı.
15 Kisha akapima urefu wa jengo linaloelekeana na ua upande wa nyuma wa Hekalu, pamoja na vyumba vyake kila upande, ilikuwa dhiraa mia moja. Sehemu takatifu ya nje, sehemu takatifu ya ndani, pamoja na baraza inayoelekeana na ukumbi,
Adam tapınağın arkasındaki açık alana bakan yapının iki yanındaki koridorların uzunluğunu ölçtü; yüz arşındı. Ana bölüm, iç oda, avluya bakan eyvan,
16 pamoja na vizingiti, madirisha membamba na vyumba vyote vitatu, kila kimoja pamoja na kizingiti vilifunikwa kwa mbao. Sakafu, ukuta mpaka kwenye madirisha na madirisha yenyewe vilifunikwa kwa mbao.
kapı eşikleri, kafesli pencereler, eşiğin karşısındaki üç katı çevreleyen koridorlar tabandan pencerelere dek ağaç kaplıydı. Pencereler açılıp kapanabiliyordu.
17 Katika nafasi iliyokuwa juu ya upande wa nje wa ingilio la sehemu takatifu ya ndani, na katika kuta zilizozunguka sehemu takatifu ya ndani na sehemu takatifu ya nje, kwa nafasi zilizo sawa,
Girişin üstü, iç oda, dışarısı ve bütün iç ve dış duvarlar düzenli aralıklarla
18 kulinakshiwa makerubi na miti ya mitende. Miti ya mitende ilikuwa kati ya kerubi na kerubi. Kila kerubi alikuwa na nyuso mbili:
Keruv ve hurma ağacı motifleriyle kaplıydı. İki Keruv arasında bir hurma ağacı vardı. Her Keruv'un iki yüzü vardı:
19 upande mmoja uso wa mwanadamu kuelekea mti wa mtende na upande mwingine uso wa simba ukielekea mti mwingine wa mtende. Ilinakshiwa kuzunguka Hekalu lote.
Bir yanda hurma ağacına bakan insan yüzü, öbür yanda hurma ağacına bakan genç aslan yüzü. Tapınak çepeçevre Keruv ve hurma ağacı oymalarıyla bezenmişti.
20 Kuanzia sakafu mpaka eneo lililo juu ya ingilio, palinakshiwa makerubi na miti ya mitende pamoja na kwenye ukuta wa nje wa patakatifu.
Tabandan girişin üstündeki bölüme dek ana bölümün duvarları Keruv ve hurma ağacı oymalarıyla kaplıydı.
21 Mahali patakatifu pa nje palikuwa na miimo ya mlango uliokuwa mraba na ule uliokuwa katika Patakatifu Pa Patakatifu ulikuwa unafanana na huo mwingine.
Ana bölümün kapı söveleri kare şeklindeydi, En Kutsal Yer'in önündeki kapı söveleri bunlara benziyordu.
22 Kulikuwa na madhabahu ya mbao kimo chake dhiraa tatu na ilikuwa dhiraa mbili mraba pande zote, tako lake na pande zake zilikuwa za mbao. Yule mtu akaniambia, “Hii ni meza ambayo iko mbele za Bwana.”
Üç arşın yüksekliğinde, iki arşın uzunluğunda ağaçtan yapılmış bir sunak vardı. Köşeleri, ayakları, yanları ağaçtandı. Adam bana, “RAB'bin önündeki masa budur” dedi.
23 Mahali patakatifu pa nje na Patakatifu Pa Patakatifu zilikuwa na milango miwili.
Ana bölümün ve En Kutsal Yer'in çift kanatlı birer kapısı vardı.
24 Kila mlango ulikuwa na vipande viwili, vipande viwili vilivyoshikwa na bawaba vyenye kufunguka kwa kila mlango.
Her kapının iki menteşeli kanadı vardı.
25 Juu ya hiyo milango ya Patakatifu palinakshiwa makerubi na miti ya mitende kama yale yaliyonakshiwa kwenye kuta, na kulikuwa na ubao ulioningʼinia mbele ya baraza kwa nje.
Duvarlara olduğu gibi, ana bölümün kapılarına da Keruv ve hurma ağacı oymaları yapılmıştı. Dışarda, eyvanın önünde ağaçtan bir asma tavan vardı.
26 Katika kuta za pembeni za ukumbi kulikuwa na madirisha membamba yaliyonakshiwa miti ya mitende kila upande. Vyumba vya pembeni vya Hekalu pia vilikuwa vimefunikwa kwa mbao.
Eyvanın yan duvarlarındaki kafesli pencerelerin iki yanı hurma ağacı oymalarıyla kaplıydı. Tapınağın yan odalarıyla asma tavanları böyleydi.