< Ezekieli 41 >
1 Kisha yule mtu akanileta katika sehemu ya nje ya patakatifu, naye akaipima miimo; upana wake ulikuwa dhiraa sita kila upande.
После ме заведе в храма; и като измери стълбовете, те имаха шест лакти широчина отсам и шест лакти широчина оттам, според широчината на скинията.
2 Ingilio lilikuwa la upana wa dhiraa kumi na kuta zilizojitokeza kila upande zilikuwa na upana wa dhiraa tano. Pia akapima sehemu ya nje ya patakatifu, nayo ilikuwa na urefu wa dhiraa arobaini na upana wa dhiraa ishirini.
И широчината на входа бе десет лакти; и страните на входа бяха пет лакти отсам и пет лакти оттам; и като измери дължината на храма, беше четиридесет лакти, а широчината му двадесет лакти.
3 Kisha akaingia sehemu takatifu ndani ya Hekalu na kupima miimo ya ingilio, kila mmoja ulikuwa na upana wa dhiraa mbili. Ingilio lilikuwa na upana wa dhiraa sita, na kuta zilizotokeza kila upande zilikuwa na upana wa dhiraa saba.
Тогава влезе по-навътре; и като измери всеки стълб на входа, имаха два лакътя, и входът шест лакти, и широчината на входа седем лакти.
4 Naye akapima urefu wa sehemu takatifu ndani, nao ulikuwa dhiraa ishirini, na upana wake ulikuwa dhiraa ishirini hadi mwisho wa sehemu ya nje ya sehemu takatifu. Akaniambia, “Hapa ndipo Patakatifu pa Patakatifu.”
И като измери дължината му, беше двадесет лакти, и широчината двадесет лакти, според широчината на храма. И рече ми: Това е пресветото място.
5 Kisha akapima ukuta wa Hekalu, nao ulikuwa na unene wa dhiraa sita, na kila chumba cha pembeni kuzunguka Hekalu kilikuwa na upana wa dhiraa nne.
Тогава измери стената на дома; тя имаше шест лакти; а широчината на страничните стаи, които бяха около дома на всяка страна, беше четири лакти.
6 Vyumba vya pembeni vilikuwa na ghorofa tatu, kimoja juu ya kingine, kila ghorofa ilikuwa na vyumba thelathini. Kulikuwa na boriti katika ukuta wote wa Hekalu ili kuimarisha vyumba vya pembeni, kwa hiyo boriti hizo hazikushikamanishwa kwenye ukuta wa Hekalu.
И страничните стаи бяха на три етажа, стая върху стая, и тридесет на ред; и влизаха в стената, която принадлежеше на дома за страничните стаи околовръст, за да се държат здраво, без да се държат за стената на дома.
7 Vyumba vya pembeni vilivyozunguka Hekalu vilizidi kupanuka kulingana na sakafu zilivyokwenda juu. Ujenzi uliozunguka Hekalu ulijengwa kukwea juu, kwa hiyo vyumba vilipanuka kwa kadiri ya kila kimoja kilivyokwenda juu. Ngazi za kupandia zilianzia sakafu ya chini hadi sakafu ya juu kabisa kwa kupitia sakafu ya kati.
И страничните стаи се разширяваха; и имаше вита стълба, която водеше в страничните стаи; защото витата стълба на дома водеше нагоре околовръст на дома; затова, домът ставаше по-широк нагоре; и така се изкачваха от долния етаж до най-горния през средния.
8 Nikaona pia kuwa Hekalu lilikuwa na kitako kilichoinuliwa pande zote, huu ulikuwa ndio msingi wa vile vyumba vya pembeni ambao ulikuwa na urefu wa ule ufito mmoja wa kupimia, yaani, dhiraa ndefu sita.
И видях, че домът беше висок от всяка страна; основите на страничните стаи бяха една цяла тръстика от шест големи лакти.
9 Ukuta wa nje wa vyumba vya pembeni ulikuwa na unene wa dhiraa tano. Eneo la wazi katikati ya vyumba vya pembeni vya Hekalu
Външната стена на страничните стаи беше пет лакти широка; и оставеното празно място бе за страничните стаи, които принадлежаха на дома.
10 na vyumba vya makuhani lilikuwa na upana wa dhiraa ishirini kuzunguka Hekalu pande zote.
И между стаите имаше двадесет лакти разстояние около дома на всяка страна.
11 Kulikuwa na maingilio kwenye vyumba vya pembeni kutokea eneo lililo wazi, moja upande wa kaskazini na lingine upande wa kusini, nao msingi uliounganisha lile eneo la wazi ulikuwa na upana wa dhiraa tano ukilizunguka lote.
И вратите на страничните стаи бяха към оставеното място, една врата към север и една врата към юг; и широчината на оставеното място бе пет лакти околовръст.
12 Jengo lililoelekeana na ua wa Hekalu upande wa magharibi lilikuwa na upana wa dhiraa sabini. Ukuta wa jengo hilo ulikuwa na unene wa dhiraa tano, kulizunguka lote, urefu ulikuwa wa dhiraa tisini.
А зданието, което бе пред отделеното място към западната страна, бе седемдесет лакти широко; и стената на зданието бе пет лакти дебела околовръст, а дължината му деветдесет лакти.
13 Kisha akapima Hekalu, lilikuwa na urefu wa dhiraa mia moja na ua wa Hekalu na jengo pamoja na kuta zake vilikuwa na urefu wa dhiraa mia moja pia.
И тъй, като измери дома, беше сто лакти дълъг; и отделеното място, зданието, и стените му сто лакти дълги.
14 Upana wa ua wa Hekalu upande wa mashariki, pamoja na upande wa mbele wa Hekalu ulikuwa dhiraa mia moja.
Тоже и широчината на лицето на дома и на отделеното място към изток беше сто лакти.
15 Kisha akapima urefu wa jengo linaloelekeana na ua upande wa nyuma wa Hekalu, pamoja na vyumba vyake kila upande, ilikuwa dhiraa mia moja. Sehemu takatifu ya nje, sehemu takatifu ya ndani, pamoja na baraza inayoelekeana na ukumbi,
И като измери дължината на зданието, което беше в лицето на отделеното място зад него, и галериите му отсам и оттам, те имаха сто лакти; измери и вътрешния храм, предверията на двора,
16 pamoja na vizingiti, madirisha membamba na vyumba vyote vitatu, kila kimoja pamoja na kizingiti vilifunikwa kwa mbao. Sakafu, ukuta mpaka kwenye madirisha na madirisha yenyewe vilifunikwa kwa mbao.
праговете, затворените прозорци, и галериите наоколо в трите им етажа, срещу прага, облечени с дърво околовръст от земята до прозорците, (а прозорците бяха покрити),
17 Katika nafasi iliyokuwa juu ya upande wa nje wa ingilio la sehemu takatifu ya ndani, na katika kuta zilizozunguka sehemu takatifu ya ndani na sehemu takatifu ya nje, kwa nafasi zilizo sawa,
до над вратата, до вътрешния дом, и извън, и през цялата стена околовръст извътре и извън; всичко бе според мерките.
18 kulinakshiwa makerubi na miti ya mitende. Miti ya mitende ilikuwa kati ya kerubi na kerubi. Kila kerubi alikuwa na nyuso mbili:
И то бе изработено с херувими и с палми, така щото имаше палма между херувим и херувим. Всеки херувим имаше две лица,
19 upande mmoja uso wa mwanadamu kuelekea mti wa mtende na upande mwingine uso wa simba ukielekea mti mwingine wa mtende. Ilinakshiwa kuzunguka Hekalu lote.
тъй щото имаше човешко лице към палмата отсам, а лице на млад лъв към палмата оттам; така бе изработено по целия дом околовръст.
20 Kuanzia sakafu mpaka eneo lililo juu ya ingilio, palinakshiwa makerubi na miti ya mitende pamoja na kwenye ukuta wa nje wa patakatifu.
От пода до над вратата бяха изработени херувими и палми; такава беше стената на храма.
21 Mahali patakatifu pa nje palikuwa na miimo ya mlango uliokuwa mraba na ule uliokuwa katika Patakatifu Pa Patakatifu ulikuwa unafanana na huo mwingine.
Колкото за храма, стълбовете му бяха квадратни, а колкото за лицето на светилището, изгледът му беше като изгледа на храма.
22 Kulikuwa na madhabahu ya mbao kimo chake dhiraa tatu na ilikuwa dhiraa mbili mraba pande zote, tako lake na pande zake zilikuwa za mbao. Yule mtu akaniambia, “Hii ni meza ambayo iko mbele za Bwana.”
Олтарът бе дървен, три лакти висок, и два лакътя дълъг; и ъглите му, подножието му, и страните му бяха дървени. И той ми рече: Това е трапезата, която стои пред Господа.
23 Mahali patakatifu pa nje na Patakatifu Pa Patakatifu zilikuwa na milango miwili.
А храмът и светилището имаха две врати.
24 Kila mlango ulikuwa na vipande viwili, vipande viwili vilivyoshikwa na bawaba vyenye kufunguka kwa kila mlango.
И вратите имаха по две крила, две движещи се крила, две крила за едната врата, и две крила за другата.
25 Juu ya hiyo milango ya Patakatifu palinakshiwa makerubi na miti ya mitende kama yale yaliyonakshiwa kwenye kuta, na kulikuwa na ubao ulioningʼinia mbele ya baraza kwa nje.
И по тях, по вратите на храма, бяха изработени херувими и палми, както бяха работени по стените; и имаше дебели дъски по лицето на предверието извън.
26 Katika kuta za pembeni za ukumbi kulikuwa na madirisha membamba yaliyonakshiwa miti ya mitende kila upande. Vyumba vya pembeni vya Hekalu pia vilikuwa vimefunikwa kwa mbao.
И имаше затворени прозорци и палми отсам и оттам от страните на предверието, и по страничните стаи на дома, и по дебелите дъски.