< Ezekieli 40 >
1 Katika mwaka wa ishirini na tano wa uhamisho wetu, mwanzoni mwa huo mwaka, siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya kuanguka kwa mji, siku hiyo hiyo mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanipeleka huko.
V petindvajsetem letu našega ujetništva, v začetku leta, na deseti dan meseca, v štirinajstem letu, potem ko je bilo mesto udarjeno, na prav isti dan, je bila nad menoj Gospodova roka in me privedla tja.
2 Nikiwa katika maono ya Mungu alinichukua mpaka nchi ya Israeli, naye akaniweka kwenye mlima mrefu sana, ambako upande wa kusini kulikuwepo baadhi ya majengo ambayo yalionekana kama mji.
V Božjih videnjih me je privedel v deželo Izrael in me postavil na zelo visoko goro, pri kateri je bil kakor okvir mesta na jugu.
3 Akanipeleka huko, nami nikamwona mtu ambaye kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwa shaba. Alikuwa amesimama kwenye lango akiwa na kamba ya kitani na ufito wa kupimia mkononi mwake.
In privedel me je tja in glej, tam je bil mož, katerega videz je bil podoben videzu brona, z laneno vrvico v svoji roki in merilno trstiko; in stal je v velikih vratih.
4 Mtu huyo akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa macho yako na usikie kwa masikio yako nawe uzingatie kitu nitakachokuonyesha, kwa kuwa ndiyo sababu umeletwa hapa. Iambie nyumba ya Israeli kila kitu utakachoona.”
In mož mi je rekel: »Človeški sin, glej s svojimi očmi in poslušaj s svojimi ušesi in svoje srce naravnaj na vse to, kar ti bom pokazal; kajti z namenom, da ti jih lahko pokažem, si bil priveden sèm. Vse to, kar vidiš, oznani Izraelovi hiši.«
5 Nikaona ukuta uliozunguka eneo lote la Hekalu. Ule ufito wa kupimia uliokuwa mkononi mwa yule mtu ulikuwa na urefu wa dhiraa ndefu sita, yaani, dhiraa ndefu ni sawa na dhiraa na nyanda nne, akapima ule ukuta. Ukuta huo ulikuwa na unene wa dhiraa ndefu sita na kimo cha dhiraa ndefu sita.
Glej obzidje zunaj, naokoli hiše in v človeški roki merilna trstika, šest komolcev dolga, po komolec in širino roke, tako je izmeril širino zgradbe, ena trstika; in višino, ena trstika.
6 Kisha akaenda kwenye lango linaloelekea mashariki. Akapanda ngazi zake akapima kizingiti cha lango, nacho kilikuwa na kina cha huo ufito.
Potem je prišel k velikim vratom, ki gledajo proti vzhodu in odšel gor po njegovih stopnicah in izmeril prag velikih vrat, ki je bil širok eno trstiko; in drugi prag velikih vrat, ki je bil širok eno trstiko.
7 Vyumba vya kupumzikia vya walinzi vilikuwa na urefu wa huo ufito mmoja na upana wa huo ufito, kuta zilizogawa vyumba hivyo vya mapumziko zilikuwa na unene wa dhiraa tano. Nacho kizingiti cha lango lililokuwa karibu na ukumbi unaoelekea hekaluni ulikuwa na kina cha huo ufito.
In vsaka majhna soba je bila eno trstiko dolga in eno trstiko široka; in med majhnimi sobami je bilo pet komolcev; in prag velikih vrat, znotraj, pri preddverju velikih vrat, je bil eno trstiko [širok].
8 Kisha akapima baraza ya njia ya lango,
Izmeril je tudi preddverje znotraj velikih vrat, ena trstika.
9 ambayo ilikuwa na kina cha dhiraa nane na miimo yake ilikuwa na unene wa dhiraa mbili. Baraza ya lango ilielekea Hekalu.
Potem je izmeril preddverje velikih vrat, osem komolcev; in njegovi podboji, dva komolca; in preddverje velikih vrat je bilo znotraj.
10 Ndani ya lango la mashariki kulikuwepo vyumba vitatu vya kupumzikia kila upande, vyote vitatu vilikuwa na vipimo vilivyo sawa, nazo nyuso za kuta zilizotenganisha kila upande zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
In majhne sobe velikih vrat proti vzhodu so bile tri na tej strani in tri na oni strani; te tri so bile ene mere; in podboji so imeli eno mero na tej strani in na oni strani.
11 Kisha akapima upana wa ingilio la lango, ilikuwa dhiraa kumi na urefu wake ulikuwa dhiraa kumi na tatu.
In izmeril je širino vhoda velikih vrat, deset komolcev; in dolžino velikih vrat, trinajst komolcev.
12 Mbele ya kila chumba cha kupumzikia kulikuwepo ukuta uliokuwa na kimo cha dhiraa moja kwenda juu, navyo hivyo vyumba vilikuwa dhiraa sita mraba.
Tudi prostora pred majhnimi sobami je bilo en komolec na tej strani in en komolec prostora je bilo na oni strani; in majhne sobe so bile šest komolcev na tej strani in šest komolcev na oni strani.
13 Kisha akapima njia ya lango kuanzia juu ya ukuta wa nyuma wa chumba kimoja cha kupumzikia hadi juu ya ukuta wa nyuma wa chumba upande wa pili; kukawa na nafasi ya dhiraa ishirini na tano kuanzia lango la ukuta mmoja hadi lango la ukuta uliokuwa upande mwingine.
Potem je izmeril velika vrata od strehe ene majhne sobe do strehe druge: širina je bila petindvajset komolcev, vrata nasproti vratom.
14 Akapima pia ukumbi, urefu wa dhiraa ishirini na lango linalofuatia hiyo nguzo kila upande wa huo ukumbi.
Naredil je tudi podboje šestdesetih komolcev, celo podboj dvora naokoli velikih vrat.
15 Umbali kuanzia ingilio la njia ya lango hadi mwisho kabisa wa baraza yake ulikuwa dhiraa hamsini.
In od pročelja velikih vrat vhoda do pročelja preddverja notranjih velikih vrat je bilo petdeset komolcev.
16 Kulikuwa na vidirisha kwenye hivyo vyumba vya walinzi na nguzo za hivyo vyumba zilikuwa kwenye mzunguko wa hilo lango, vivyo hivyo kulikuwa na madirisha yaliyozunguka kuelekeana na ua na juu ya kila nguzo kulikuwa na mapambo ya miti ya mitende.
In tam so bila ozka okna k majhnim sobam in k njihovim podbojem znotraj, naokoli velikih vrat in podobno k obokom, in okna so bila naokoli navznoter sobe, in na vsakem podboju so bila palmova drevesa.
17 Kisha akanileta katika ukumbi wa nje. Huko nikaona vyumba vingine pamoja na njia iliyokuwa imejengwa kuzunguka ukumbi wote, kulikuwa na vyumba thelathini vimepangana kando ya hiyo njia.
Potem me je privedel na zunanji dvor in glej, tam so bile sobe in tlak, narejen za dvor naokoli. Trideset sob je bilo na tlaku.
18 Njia hii iliyojengwa iliambaa na lango, ikiwa na urefu sawa na lango, hii ilikuwa ni njia ya chini.
In tlak, ki je bil pri strani velikih vrat, nasproti dolžine velikih vrat, je bil nižji tlak.
19 Kisha akapima umbali kutoka ndani ya lango la chini mpaka nje ya ukumbi wa ndani, nao ulikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki na dhiraa mia moja upande wa kaskazini.
Potem je izmeril širino od sprednjega dela spodnjih velikih vrat do sprednjega dela notranjega dvora zunaj; sto komolcev proti vzhodu in proti severu.
20 Kisha akapima urefu na upana wa lango linaloelekea kaskazini, kukabili ukumbi wa nje.
In velika vrata zunanjega dvora, ki so gledala proti severu, izmeril je njihovo dolžino in njihovo širino.
21 Vyumba vyake vilikuwa vitatu kila upande, kuta zilizogawanya vyumba na baraza ilikuwa na vipimo sawa na zile kuta za lango la kwanza. Zilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
In njihove majhne sobe so bile tri na tej strani in tri na oni strani; in njihovi podboji in njihovi oboki so bili po meri prvih vrat. Njihova dolžina je bila petdeset komolcev in širina petindvajset komolcev.
22 Madirisha yake, baraza yake na nakshi yake ya miti ya mitende vilikuwa na vipimo sawasawa na vile vya lango linaloelekea mashariki. Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo.
In njihova okna in njihovi oboki in njihova palmova drevesa so bila po meri velikih vrat, ki gledajo proti vzhodu; in k tem so se vzpeli po sedmih stopnicah; in njihovi oboki so bili pred njimi.
23 Kulikuwa na lango kwenye ukumbi wa ndani lililoelekea lile lango la kaskazini, kama vile ilivyokuwa ule upande wa mashariki. Akapima kutoka lango moja hadi lile lililo mkabala nalo, lilikuwa dhiraa mia moja.
In velika vrata notranjega dvora so bila nasproti velikih vrat proti severu in proti vzhodu; in od velikih vrat do velikih vrat je izmeril sto komolcev.
24 Ndipo akaniongoza mpaka upande wa kusini, nami nikaona lango linaloelekea kusini. Akaipima miimo yake na baraza yake, navyo vilikuwa na vipimo sawa kama hivyo vingine.
Po tem me je privedel proti jugu in glej, velika vrata proti jugu. Izmeril je njihove podboje in njihove oboke, glede na te mere.
25 Lango na baraza yake vilikuwa na madirisha membamba pande zote, kama madirisha ya huko kwingine. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
In tam so bila okna in njihovi oboki naokoli, podobni tistim oknom. Dolžina je bila petdeset komolcev in širina petindvajset komolcev.
26 Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo. Ilikuwa na nakshi za miti ya mitende kwenye kuta zilizogawanya vyumba kila upande.
In tam je bilo sedem stopnic, da se gre gor do njih in njihovi oboki so bili pred njimi. Ta so imela palmovi drevesi, eno na tej strani in drugo na oni strani, na njihovih podbojih.
27 Ukumbi wa ndani pia ulikuwa na lango lililoelekea kusini. Naye akapima kutoka lango hili mpaka kwenye lango la nje upande wa kusini; ilikuwa dhiraa mia moja.
In na notranjem dvoru, proti jugu, so bila velika vrata, in od velikih vrat do velikih vrat je proti jugu izmeril sto komolcev.
28 Kisha akanileta mpaka ukumbi wa ndani kwa kupitia lango la kusini, naye akapima lango la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine.
In privedel me je na notranji dvor pri južnih velikih vratih: in južna velika vrata je izmeril glede na te mere;
29 Vyumba vyake, kuta zilizogawanya vyumba na ukumbi wake zilikuwa na vipimo sawasawa na zile nyingine. Hilo lango na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Navyo vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
in njihove majhne sobe in njihovi podboji in njihovi oboki, glede na te mere: in tam so bila okna v njej in njihovi oboki naokoli: in ta so bila petdeset komolcev dolga in petindvajset komolcev široka.
30 (Baraza za malango zilizozunguka ukumbi wa ndani zilikuwa na upana wa dhiraa ishirini na tano na kina cha dhiraa tano.)
Oboki naokoli so bili petindvajset komolcev dolgi in pet komolcev široki.
31 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Njihovi oboki so bili proti skrajnemu dvoru; palmova drevesa so bila na njihovih podbojih. Gor do njih je vodilo osem stopnic.
32 Kisha akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani ulioko upande wa mashariki, naye akalipima lango hilo, lilikuwa na vipimo vilivyo sawasawa na yale mengine.
Privedel me je na notranji dvor proti vzhodu in izmeril velika vrata glede na te mere.
33 Vyumba vyake, kuta zake na baraza yake vilikuwa na vipimo vilivyo sawa na vile vingine. Lile lango pamoja na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
Njihove majhne sobe, njihovi podboji in njihovi oboki so bili glede na te mere. Tam so bila okna v njihovih obokih naokoli. To je bilo petdeset komolcev dolgo in petindvajset komolcev široko.
34 Baraza yake ilielekea ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote. Kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Njihovi oboki so bili proti zunanjemu dvoru; in palmova drevesa so bila na njihovih podbojih, na tej strani in na oni strani in gor do njih je vodilo osem stopnic.
35 Kisha akanileta mpaka kwenye lango la kaskazini na kulipima. Lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine,
Privedel me je k severnim velikim vratom in jih izmeril glede na te mere;
36 kama vile ilivyokuwa kwa vyumba, kuta zake na baraza yake, tena kulikuwa na madirisha pande zote. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
njihove majhne sobe, njihove podboje in njihove oboke in okna k tem naokoli; dolžina je bila petdeset komolcev in širina petindvajset komolcev.
37 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Njihovi podboji so bili proti skrajnemu dvoru; in palmova drevesa so bila na njihovih podbojih, na tej strani in na oni strani in gor do njih je vodilo osem stopnic.
38 Kulikuwa na chumba na mlango karibu na baraza katika kila njia ya ndani ya lango ambamo sadaka za kuteketezwa zilioshwa.
Sobe in njihovi vhodi so bili ob podbojih velikih vrat, kjer so prali žgalno daritev.
39 Kwenye baraza ya lile lango kulikuwepo meza mbili kila upande, ambako sadaka za kuteketezwa, sadaka za dhambi na sadaka za hatia zilichinjiwa.
V preddverju velikih vrat sta bili dve mizi na tej strani in dve mizi na oni strani, da na njih zakoljejo žgalno daritev in daritev za greh in daritev za prestopek.
40 Karibu na ukuta wa nje wa baraza ya lile lango karibu na ngazi kwenye ingilio kuelekea kaskazini kulikuwa na meza mbili, nako upande mwingine wa ngazi kulikuwepo na meza mbili.
Zunaj ob strani, kakor gre kdo gor k vhodu severnih velikih vrat, sta bili dve mizi; in na drugi strani, ki je bila pri preddverju velikih vrat, sta bili dve mizi.
41 Kwa hiyo kulikuwa na meza nne upande mmoja wa lango na nyingine nne upande mwingine, zote zilikuwa meza nane, ambapo dhabihu zilichinjiwa.
Štiri mize so bile na tej strani in štiri mize na oni strani, pri straneh velikih vrat; osem miz, na katerih so klali svoje daritve.
42 Pia kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, kila meza ilikuwa na urefu wa dhiraa moja na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu na kimo cha dhiraa moja. Juu ya meza hizo viliwekwa vyombo vya kuchinjia sadaka za kuteketezwa na dhabihu nyingine mbalimbali.
Štiri mize so bile iz klesanega kamna za žgalno daritev, komolec in pol dolge in komolec in pol široke in en komolec visoke, na katere so prav tako položili orodje, s katerim so zaklali žgalno daritev in klavno daritev.
43 Kulikuwa na kulabu, urefu wake nyanda nne, zilikuwa zimeshikizwa ukutani pande zote. Meza zilikuwa kwa ajili ya nyama za sadaka.
Znotraj so bili kavlji, dlan široki, pritrjeni naokoli in na mizah je bilo meso daritve.
44 Nje ya lango la ndani, kwenye ukumbi wa ndani, kulikuwa na vyumba viwili, kimoja upande wa lango la kaskazini nacho kilielekea kusini, kingine upande wa lango la kusini nacho kilielekea kaskazini.
Zunaj notranjih velikih vrat so bile sobe pevcev notranjega dvora, ki je bil ob strani severnih velikih vrat in njihova pročelja so bila proti jugu. Ena je bila ob strani vzhodnih velikih vrat in imela pročelje proti severu.
45 Akaniambia, “Chumba kinachoelekea upande wa kusini ni kwa ajili ya makuhani ambao wana usimamizi wa hekaluni,
In rekel mi je: »Ta soba, katere pročelje je proti jugu, je za duhovnike, čuvaje oskrbe hiše.
46 nacho chumba kinachoelekea upande wa kaskazini ni kwa ajili ya makuhani wenye usimamizi wa madhabahuni. Hawa ni wana wa Sadoki, ambao ndio Walawi pekee wanaoweza kumkaribia Bwana ili kuhudumu mbele zake.”
Soba, katere pročelje je proti severu, je za duhovnike, čuvaje oskrbe oltarja: to so Cadókovi sinovi med Lévijevimi sinovi, ki so prišli blizu h Gospodu, da mu služijo.
47 Ndipo alipopima ukumbi: nao ulikuwa mraba wa dhiraa mia moja urefu na upana. Madhabahu yalikuwa mbele ya Hekalu.
Tako je izmeril dvor, sto komolcev dolg in sto komolcev širok, štirioglat; in oltar, ki je bil pred hišo.
48 Akanileta mpaka kwenye baraza ya Hekalu naye akaipima miimo ya hiyo baraza, nayo ilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande. Upana wa ingilio ulikuwa dhiraa kumi na nne na kuta zake zilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande.
Privedel me je k preddverju hiše in izmeril vsak podboj preddverja, pet komolcev na tej strani in pet komolcev na oni strani in širina velikih vrat je bila tri komolce na tej strani in tri komolce na oni strani.
49 Baraza ilikuwa na dhiraa ishirini kwenda juu na dhiraa kumi na mbili kuanzia mbele hadi nyuma. Kulikuwa na ngazi kumi za kupandia huko, pia kulikuwa na nguzo kwa kila upande wa miimo.
Dolžina preddverja je bila dvajset komolcev in širina enajst komolcev; in privedel me je poleg stopnic, po katerih so se dvignili do njega. Tam so bili stebri ob podbojih, eden na tej strani, drugi pa na oni strani.