< Ezekieli 40 >
1 Katika mwaka wa ishirini na tano wa uhamisho wetu, mwanzoni mwa huo mwaka, siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya kuanguka kwa mji, siku hiyo hiyo mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanipeleka huko.
No vigésimo quinto ano de nosso cativeiro, no início do ano, no décimo dia do mês, no décimo quarto ano depois que a cidade foi atingida, no mesmo dia, a mão de Yahweh estava sobre mim, e ele me trouxe para lá.
2 Nikiwa katika maono ya Mungu alinichukua mpaka nchi ya Israeli, naye akaniweka kwenye mlima mrefu sana, ambako upande wa kusini kulikuwepo baadhi ya majengo ambayo yalionekana kama mji.
Nas visões de Deus, ele me trouxe para a terra de Israel, e me colocou em uma montanha muito alta, sobre a qual havia algo como a moldura de uma cidade ao sul.
3 Akanipeleka huko, nami nikamwona mtu ambaye kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwa shaba. Alikuwa amesimama kwenye lango akiwa na kamba ya kitani na ufito wa kupimia mkononi mwake.
Ele me trouxe para lá; e, eis que havia um homem cuja aparência era como a de bronze, com uma linha de linho na mão e uma palheta medidora; e ele ficou no portão.
4 Mtu huyo akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa macho yako na usikie kwa masikio yako nawe uzingatie kitu nitakachokuonyesha, kwa kuwa ndiyo sababu umeletwa hapa. Iambie nyumba ya Israeli kila kitu utakachoona.”
O homem me disse: “Filho do homem, vê com teus olhos, e ouve com teus ouvidos, e põe teu coração em tudo o que eu te mostrar; pois tu foste trazido aqui para que eu possa mostrá-los a ti”. Declarai tudo o que vedes à casa de Israel”.
5 Nikaona ukuta uliozunguka eneo lote la Hekalu. Ule ufito wa kupimia uliokuwa mkononi mwa yule mtu ulikuwa na urefu wa dhiraa ndefu sita, yaani, dhiraa ndefu ni sawa na dhiraa na nyanda nne, akapima ule ukuta. Ukuta huo ulikuwa na unene wa dhiraa ndefu sita na kimo cha dhiraa ndefu sita.
Eis que havia uma parede no exterior da casa por toda parte, e na mão do homem uma palheta medindo seis cúbitos de comprimento, de um côvado e uma largura de mão cada um. Então ele mediu a espessura do prédio, uma palheta; e a altura, uma palheta.
6 Kisha akaenda kwenye lango linaloelekea mashariki. Akapanda ngazi zake akapima kizingiti cha lango, nacho kilikuwa na kina cha huo ufito.
Então ele chegou ao portão que olha para o leste, e subiu suas escadas. Ele mediu a soleira do portão, uma palheta de largura; e a outra soleira, uma palheta de largura.
7 Vyumba vya kupumzikia vya walinzi vilikuwa na urefu wa huo ufito mmoja na upana wa huo ufito, kuta zilizogawa vyumba hivyo vya mapumziko zilikuwa na unene wa dhiraa tano. Nacho kizingiti cha lango lililokuwa karibu na ukumbi unaoelekea hekaluni ulikuwa na kina cha huo ufito.
Cada portão tinha uma palheta de comprimento e uma palheta de largura. Entre as pousadas havia cinco côvados. A soleira do portão junto ao alpendre do portão em direção à casa era uma palheta.
8 Kisha akapima baraza ya njia ya lango,
Ele mediu também a varanda do portão em direção à casa, uma palheta.
9 ambayo ilikuwa na kina cha dhiraa nane na miimo yake ilikuwa na unene wa dhiraa mbili. Baraza ya lango ilielekea Hekalu.
Então ele mediu a varanda do portão, oito côvados; e seus postes, dois côvados; e a varanda do portão estava em direção à casa.
10 Ndani ya lango la mashariki kulikuwepo vyumba vitatu vya kupumzikia kila upande, vyote vitatu vilikuwa na vipimo vilivyo sawa, nazo nyuso za kuta zilizotenganisha kila upande zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
As salas laterais do portão ao leste eram três deste lado, e três deste lado. As três eram de uma medida. Os postes tinham uma medida deste lado e outra deste lado.
11 Kisha akapima upana wa ingilio la lango, ilikuwa dhiraa kumi na urefu wake ulikuwa dhiraa kumi na tatu.
Ele mediu a largura da abertura do portão, dez côvados; e o comprimento do portão, treze côvados;
12 Mbele ya kila chumba cha kupumzikia kulikuwepo ukuta uliokuwa na kimo cha dhiraa moja kwenda juu, navyo hivyo vyumba vilikuwa dhiraa sita mraba.
e uma borda antes das pousadas, um côvado deste lado, e uma borda, um côvado daquele lado; e as salas laterais, seis côvados deste lado, e seis côvados daquele lado.
13 Kisha akapima njia ya lango kuanzia juu ya ukuta wa nyuma wa chumba kimoja cha kupumzikia hadi juu ya ukuta wa nyuma wa chumba upande wa pili; kukawa na nafasi ya dhiraa ishirini na tano kuanzia lango la ukuta mmoja hadi lango la ukuta uliokuwa upande mwingine.
Ele mediu a porta do telhado de um lado ao telhado do outro, uma largura de vinte e cinco côvados, porta contra porta.
14 Akapima pia ukumbi, urefu wa dhiraa ishirini na lango linalofuatia hiyo nguzo kila upande wa huo ukumbi.
Ele também fez postes, sessenta côvados; e a quadra chegou até os postes, ao redor do portão.
15 Umbali kuanzia ingilio la njia ya lango hadi mwisho kabisa wa baraza yake ulikuwa dhiraa hamsini.
Da frente do portão, na entrada à frente da varanda interna do portão, havia cinqüenta côvados.
16 Kulikuwa na vidirisha kwenye hivyo vyumba vya walinzi na nguzo za hivyo vyumba zilikuwa kwenye mzunguko wa hilo lango, vivyo hivyo kulikuwa na madirisha yaliyozunguka kuelekeana na ua na juu ya kila nguzo kulikuwa na mapambo ya miti ya mitende.
There eram janelas fechadas para as salas laterais, e para seus postes dentro do portão ao redor, e também para os arcos. As janelas estavam ao redor para dentro. As palmeiras estavam em cada poste.
17 Kisha akanileta katika ukumbi wa nje. Huko nikaona vyumba vingine pamoja na njia iliyokuwa imejengwa kuzunguka ukumbi wote, kulikuwa na vyumba thelathini vimepangana kando ya hiyo njia.
Depois ele me trouxe para a corte externa. Eis que havia salas e um pavimento feito para a quadra ao redor. Trinta quartos estavam na calçada.
18 Njia hii iliyojengwa iliambaa na lango, ikiwa na urefu sawa na lango, hii ilikuwa ni njia ya chini.
O pavimento estava ao lado dos portões, correspondendo ao comprimento dos portões, até mesmo o pavimento inferior.
19 Kisha akapima umbali kutoka ndani ya lango la chini mpaka nje ya ukumbi wa ndani, nao ulikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki na dhiraa mia moja upande wa kaskazini.
Then ele mediu a largura desde a frente do portão inferior até a frente da quadra interna externa, cem côvados, tanto no leste quanto no norte.
20 Kisha akapima urefu na upana wa lango linaloelekea kaskazini, kukabili ukumbi wa nje.
Ele mediu o comprimento e a largura do portão da quadra externa que está voltada para o norte.
21 Vyumba vyake vilikuwa vitatu kila upande, kuta zilizogawanya vyumba na baraza ilikuwa na vipimo sawa na zile kuta za lango la kwanza. Zilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
As pousadas dele eram três deste lado e três deste lado. Suas colunas e seus arcos eram os mesmos que a medida do primeiro portão: seu comprimento era de cinqüenta cúbitos, e a largura de vinte e cinco cúbitos.
22 Madirisha yake, baraza yake na nakshi yake ya miti ya mitende vilikuwa na vipimo sawasawa na vile vya lango linaloelekea mashariki. Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo.
Suas janelas, seus arcos e suas palmeiras eram as mesmas que a medida do portão que está voltado para o leste. Eles subiram até ele por sete degraus. Seus arcos estavam diante deles.
23 Kulikuwa na lango kwenye ukumbi wa ndani lililoelekea lile lango la kaskazini, kama vile ilivyokuwa ule upande wa mashariki. Akapima kutoka lango moja hadi lile lililo mkabala nalo, lilikuwa dhiraa mia moja.
There era um portão para a quadra interna voltado para o outro portão, no norte e no leste. Ele media cem côvados de porta em porta.
24 Ndipo akaniongoza mpaka upande wa kusini, nami nikaona lango linaloelekea kusini. Akaipima miimo yake na baraza yake, navyo vilikuwa na vipimo sawa kama hivyo vingine.
Ele me conduziu em direção ao sul; e eis que havia um portão em direção ao sul. Ele mediu seus postes e seus arcos de acordo com estas medidas.
25 Lango na baraza yake vilikuwa na madirisha membamba pande zote, kama madirisha ya huko kwingine. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
There eram janelas nele e em seus arcos ao redor, como as outras janelas: o comprimento era de cinqüenta côvados, e a largura de vinte e cinco côvados.
26 Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo. Ilikuwa na nakshi za miti ya mitende kwenye kuta zilizogawanya vyumba kila upande.
There eram sete degraus para subir até ele, e seus arcos estavam diante deles. Tinha palmeiras, uma deste lado, e outra deste lado, em seus postes.
27 Ukumbi wa ndani pia ulikuwa na lango lililoelekea kusini. Naye akapima kutoka lango hili mpaka kwenye lango la nje upande wa kusini; ilikuwa dhiraa mia moja.
There era um portão para o pátio interno, em direção ao sul. Ele media cem côvados de porta em porta, em direção ao sul.
28 Kisha akanileta mpaka ukumbi wa ndani kwa kupitia lango la kusini, naye akapima lango la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine.
Depois ele me trouxe para a corte interna pelo portão sul. Ele mediu o portão sul de acordo com estas medidas;
29 Vyumba vyake, kuta zilizogawanya vyumba na ukumbi wake zilikuwa na vipimo sawasawa na zile nyingine. Hilo lango na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Navyo vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
com seus alojamentos, seus postes e seus arcos, de acordo com estas medidas. Havia janelas dentro dele e em seus arcos ao redor. Tinha cinqüenta côvados de comprimento e vinte e cinco côvados de largura.
30 (Baraza za malango zilizozunguka ukumbi wa ndani zilikuwa na upana wa dhiraa ishirini na tano na kina cha dhiraa tano.)
There eram arcos ao redor, com vinte e cinco cúbitos de comprimento e cinco cúbitos de largura.
31 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Its os arcos estavam em direção à quadra externa. As palmeiras estavam em seus postes. A subida até ele tinha oito degraus.
32 Kisha akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani ulioko upande wa mashariki, naye akalipima lango hilo, lilikuwa na vipimo vilivyo sawasawa na yale mengine.
Ele me trouxe para a corte interna em direção ao leste. Ele mediu o portão de acordo com estas medidas;
33 Vyumba vyake, kuta zake na baraza yake vilikuwa na vipimo vilivyo sawa na vile vingine. Lile lango pamoja na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
com seus alojamentos, seus postes e seus arcos, de acordo com estas medidas. Havia janelas dentro dele e em seus arcos ao redor. Tinha cinqüenta cúbitos de comprimento, e vinte e cinco cúbitos de largura.
34 Baraza yake ilielekea ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote. Kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Its os arcos estavam em direção à quadra externa. As palmeiras estavam em seus postes deste lado e daquele lado. A subida até ela tinha oito degraus.
35 Kisha akanileta mpaka kwenye lango la kaskazini na kulipima. Lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine,
Ele me levou ao portão norte e mediu-o de acordo com estas medidas -
36 kama vile ilivyokuwa kwa vyumba, kuta zake na baraza yake, tena kulikuwa na madirisha pande zote. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
seus alojamentos, seus postes e seus arcos. Havia janelas em toda a sua volta. O comprimento era de cinqüenta côvados e a largura de vinte e cinco côvados.
37 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Its os postes estavam em direção à quadra externa. As palmeiras estavam em seus postes deste lado e daquele lado. A subida até ela tinha oito degraus.
38 Kulikuwa na chumba na mlango karibu na baraza katika kila njia ya ndani ya lango ambamo sadaka za kuteketezwa zilioshwa.
Uma sala com sua porta estava junto aos postes nos portões. Lá eles lavaram a oferta queimada.
39 Kwenye baraza ya lile lango kulikuwepo meza mbili kila upande, ambako sadaka za kuteketezwa, sadaka za dhambi na sadaka za hatia zilichinjiwa.
Na varanda do portão havia duas mesas deste lado e duas mesas deste lado, nas quais se matava a oferta queimada, a oferta pelo pecado, e a oferta pela transgressão.
40 Karibu na ukuta wa nje wa baraza ya lile lango karibu na ngazi kwenye ingilio kuelekea kaskazini kulikuwa na meza mbili, nako upande mwingine wa ngazi kulikuwepo na meza mbili.
De um lado do lado de fora, ao subir para a entrada do portão em direção ao norte, havia duas mesas; e do outro lado, que pertenciam ao alpendre do portão, havia duas mesas.
41 Kwa hiyo kulikuwa na meza nne upande mmoja wa lango na nyingine nne upande mwingine, zote zilikuwa meza nane, ambapo dhabihu zilichinjiwa.
Quatro mesas estavam deste lado, e quatro mesas deste lado, ao lado do portão: oito mesas, nas quais eles matavam os sacrifícios.
42 Pia kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, kila meza ilikuwa na urefu wa dhiraa moja na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu na kimo cha dhiraa moja. Juu ya meza hizo viliwekwa vyombo vya kuchinjia sadaka za kuteketezwa na dhabihu nyingine mbalimbali.
Havia quatro mesas de pedra cortada para o holocausto, um côvado e meio de comprimento, um côvado e meio de largura, e um côvado de altura. Eles colocaram os instrumentos com os quais mataram o holocausto e o sacrifício sobre eles.
43 Kulikuwa na kulabu, urefu wake nyanda nne, zilikuwa zimeshikizwa ukutani pande zote. Meza zilikuwa kwa ajili ya nyama za sadaka.
Os ganchos, uma largura de mão longa, foram fixados em todos os lados. A carne da oferenda estava sobre as mesas.
44 Nje ya lango la ndani, kwenye ukumbi wa ndani, kulikuwa na vyumba viwili, kimoja upande wa lango la kaskazini nacho kilielekea kusini, kingine upande wa lango la kusini nacho kilielekea kaskazini.
Fora do portão interno havia salas para os cantores na quadra interna, que ficava ao lado do portão norte. Eles se dirigiam para o sul. Um ao lado do portão leste, voltado para o norte.
45 Akaniambia, “Chumba kinachoelekea upande wa kusini ni kwa ajili ya makuhani ambao wana usimamizi wa hekaluni,
Ele me disse: “Esta sala, que está voltada para o sul, é para os padres que cumprem o dever da casa”.
46 nacho chumba kinachoelekea upande wa kaskazini ni kwa ajili ya makuhani wenye usimamizi wa madhabahuni. Hawa ni wana wa Sadoki, ambao ndio Walawi pekee wanaoweza kumkaribia Bwana ili kuhudumu mbele zake.”
A sala que está voltada para o norte é para os sacerdotes que cumprem o dever do altar. Estes são os filhos de Zadok, que, dentre os filhos de Levi, se aproximam de Yahweh para ministrar a ele”.
47 Ndipo alipopima ukumbi: nao ulikuwa mraba wa dhiraa mia moja urefu na upana. Madhabahu yalikuwa mbele ya Hekalu.
Ele mediu a corte, cem côvados de comprimento e cem côvados de largura, quadrados. O altar estava diante da casa.
48 Akanileta mpaka kwenye baraza ya Hekalu naye akaipima miimo ya hiyo baraza, nayo ilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande. Upana wa ingilio ulikuwa dhiraa kumi na nne na kuta zake zilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande.
Depois ele me levou ao alpendre da casa, e mediu cada posto do alpendre, cinco côvados deste lado, e cinco côvados daquele lado. A largura do portão era de três côvados deste lado e três côvados daquele lado.
49 Baraza ilikuwa na dhiraa ishirini kwenda juu na dhiraa kumi na mbili kuanzia mbele hadi nyuma. Kulikuwa na ngazi kumi za kupandia huko, pia kulikuwa na nguzo kwa kila upande wa miimo.
O comprimento do pórtico era de vinte côvados e a largura de onze côvados, mesmo pelos degraus pelos quais eles subiam até ele. Havia pilares junto aos postes, um deste lado, e outro deste lado.