< Ezekieli 40 >
1 Katika mwaka wa ishirini na tano wa uhamisho wetu, mwanzoni mwa huo mwaka, siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya kuanguka kwa mji, siku hiyo hiyo mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanipeleka huko.
Im fünfundzwanzigsten Jahr unserer Wegführung, im Anfang des Jahres, am zehnten Tag des Monats, im vierzehnten Jahr, nachdem die Stadt geschlagen war, an ebendemselben Tag, war über mir die Hand Jehovahs und brachte mich dahin.
2 Nikiwa katika maono ya Mungu alinichukua mpaka nchi ya Israeli, naye akaniweka kwenye mlima mrefu sana, ambako upande wa kusini kulikuwepo baadhi ya majengo ambayo yalionekana kama mji.
In Gesichten Gottes brachte Er mich hinein zum Land Israels und ließ mich nieder auf einen sehr hohen Berg, und auf ihm war wie das Gebäu einer Stadt vom Mittag her.
3 Akanipeleka huko, nami nikamwona mtu ambaye kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwa shaba. Alikuwa amesimama kwenye lango akiwa na kamba ya kitani na ufito wa kupimia mkononi mwake.
Und Er brachte mich dahin, und siehe, da war ein Mann, sein Ansehen wie das Ansehen von Erz, und eine leinene Schnur war in seiner Hand und ein Rohr zum Messen; und er stand in dem Tor.
4 Mtu huyo akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa macho yako na usikie kwa masikio yako nawe uzingatie kitu nitakachokuonyesha, kwa kuwa ndiyo sababu umeletwa hapa. Iambie nyumba ya Israeli kila kitu utakachoona.”
Und der Mann redete zu mir: Menschensohn, siehe mit deinen Augen und mit deinen Ohren höre, und richte dein Herz auf alles, was ich dich sehen lasse; denn damit ich dir es zeige, bist du hierher gebracht. Alles, was du siehst, sage an dem Hause Israel.
5 Nikaona ukuta uliozunguka eneo lote la Hekalu. Ule ufito wa kupimia uliokuwa mkononi mwa yule mtu ulikuwa na urefu wa dhiraa ndefu sita, yaani, dhiraa ndefu ni sawa na dhiraa na nyanda nne, akapima ule ukuta. Ukuta huo ulikuwa na unene wa dhiraa ndefu sita na kimo cha dhiraa ndefu sita.
Und siehe, eine Mauer war von außen am Hause, ringsum, ringsum. Und der Mann hatte in der Hand ein Rohr zum Messen von sechs Ellen, nach der Elle und eine Handbreite; und er maß die Breite des Gebäus eine Rute und die Höhe eine Rute.
6 Kisha akaenda kwenye lango linaloelekea mashariki. Akapanda ngazi zake akapima kizingiti cha lango, nacho kilikuwa na kina cha huo ufito.
Und er ging hinein zum Tor, das am Wege gegen Osten war, und stieg dessen Stufen hinauf und maß die Schwelle des Tores zu einer Rute in die Breite und die andere Schwelle eine Rute breit.
7 Vyumba vya kupumzikia vya walinzi vilikuwa na urefu wa huo ufito mmoja na upana wa huo ufito, kuta zilizogawa vyumba hivyo vya mapumziko zilikuwa na unene wa dhiraa tano. Nacho kizingiti cha lango lililokuwa karibu na ukumbi unaoelekea hekaluni ulikuwa na kina cha huo ufito.
Und die Wachtzelle eine Rute nach der Länge, eine Rute in der Breite. Und zwischen den Wachtzellen waren es fünf Ellen, und die Schwelle des Tores neben der Vorhalle des Tores von innen her eine Rute.
8 Kisha akapima baraza ya njia ya lango,
Und er maß die Vorhalle des Tores von innen zu einer Rute.
9 ambayo ilikuwa na kina cha dhiraa nane na miimo yake ilikuwa na unene wa dhiraa mbili. Baraza ya lango ilielekea Hekalu.
Und er maß die Vorhalle des Tores acht Ellen, und die Vorsprünge davon zwei Ellen; und die Vorhalle des Tores innerhalb.
10 Ndani ya lango la mashariki kulikuwepo vyumba vitatu vya kupumzikia kila upande, vyote vitatu vilikuwa na vipimo vilivyo sawa, nazo nyuso za kuta zilizotenganisha kila upande zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
Und der Wachtzellen des Tores am Wege gegen Osten waren drei hüben und drei drüben, ein Maß für deren drei, und ein Maß für die Vorsprünge hüben und drüben.
11 Kisha akapima upana wa ingilio la lango, ilikuwa dhiraa kumi na urefu wake ulikuwa dhiraa kumi na tatu.
Und er maß die Breite des Eingangs des Tores zehn Ellen, die Länge des Tores dreizehn Ellen.
12 Mbele ya kila chumba cha kupumzikia kulikuwepo ukuta uliokuwa na kimo cha dhiraa moja kwenda juu, navyo hivyo vyumba vilikuwa dhiraa sita mraba.
Und die Grenzwehr vor den Wachtzellen war eine Elle, und eine Elle Grenzwehr dort. Aber die Wachtzellen waren von sechs Ellen hier und von sechs Ellen dort.
13 Kisha akapima njia ya lango kuanzia juu ya ukuta wa nyuma wa chumba kimoja cha kupumzikia hadi juu ya ukuta wa nyuma wa chumba upande wa pili; kukawa na nafasi ya dhiraa ishirini na tano kuanzia lango la ukuta mmoja hadi lango la ukuta uliokuwa upande mwingine.
Und er maß das Tor vom Dach der Wachtzelle bis zu seinem Dach, fünfundzwanzig Ellen in die Breite, Eingang gegen Eingang.
14 Akapima pia ukumbi, urefu wa dhiraa ishirini na lango linalofuatia hiyo nguzo kila upande wa huo ukumbi.
Und er machte die Erker sechzig Ellen, und vor dem Erker war der Vorhof am Tore ringsum und ringsum.
15 Umbali kuanzia ingilio la njia ya lango hadi mwisho kabisa wa baraza yake ulikuwa dhiraa hamsini.
Und vor dem Tore des Eintritts bis vor die Vorhalle am inneren Tor waren es fünfzig Ellen.
16 Kulikuwa na vidirisha kwenye hivyo vyumba vya walinzi na nguzo za hivyo vyumba zilikuwa kwenye mzunguko wa hilo lango, vivyo hivyo kulikuwa na madirisha yaliyozunguka kuelekeana na ua na juu ya kila nguzo kulikuwa na mapambo ya miti ya mitende.
Und geschlitzte Fenster waren an den Wachtzellen, und an ihren Vorsprüngen einwärts dem Tore zu, ringsum und ringsum, und so an den Vorhallen, und Fenster waren ringsum und ringsum einwärts. Und an den Vorsprüngen waren Palmen.
17 Kisha akanileta katika ukumbi wa nje. Huko nikaona vyumba vingine pamoja na njia iliyokuwa imejengwa kuzunguka ukumbi wote, kulikuwa na vyumba thelathini vimepangana kando ya hiyo njia.
Und er brachte mich zu dem äußeren Vorhof, und siehe, da waren Zellen und ein Pflaster gemacht am Vorhof ringsum, ringsum, dreißig Zellen waren auf dem Pflaster.
18 Njia hii iliyojengwa iliambaa na lango, ikiwa na urefu sawa na lango, hii ilikuwa ni njia ya chini.
Und das Pflaster war zur Seite der Tore, der Länge der Tore entlang, - das niedere Pflaster.
19 Kisha akapima umbali kutoka ndani ya lango la chini mpaka nje ya ukumbi wa ndani, nao ulikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki na dhiraa mia moja upande wa kaskazini.
Und er maß die Breite vor dem unteren Tor, vor dem inneren Vorhof, außerhalb, hundert Ellen, gegen Osten und gegen Mitternacht;
20 Kisha akapima urefu na upana wa lango linaloelekea kaskazini, kukabili ukumbi wa nje.
Und das Tor, dessen Vorderseite am Wege nach Mitternacht des äußeren Vorhofs ist, maß er nach seiner Länge und nach seiner Breite.
21 Vyumba vyake vilikuwa vitatu kila upande, kuta zilizogawanya vyumba na baraza ilikuwa na vipimo sawa na zile kuta za lango la kwanza. Zilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
Und seiner Wachtzellen waren drei hier und drei dort, und seine Vorsprünge und seine Vorhallen waren nach dem Maß des ersten Tores fünfzig Ellen in die Länge und fünfundzwanzig Ellen in die Breite.
22 Madirisha yake, baraza yake na nakshi yake ya miti ya mitende vilikuwa na vipimo sawasawa na vile vya lango linaloelekea mashariki. Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo.
Und seine Fenster und seine Vorhallen und seine Palmen waren nach dem Maß des Tores, dessen Angesicht auf dem Wege nach Morgen ist, und auf sieben Stufen stieg man dazu hinauf, und seine Vorhalle war vor denselben.
23 Kulikuwa na lango kwenye ukumbi wa ndani lililoelekea lile lango la kaskazini, kama vile ilivyokuwa ule upande wa mashariki. Akapima kutoka lango moja hadi lile lililo mkabala nalo, lilikuwa dhiraa mia moja.
Und das Tor zum inneren Vorhof war gegenüber dem Tore nach Mitternacht und nach Osten, und er maß hundert Ellen von Tor zu Tor.
24 Ndipo akaniongoza mpaka upande wa kusini, nami nikaona lango linaloelekea kusini. Akaipima miimo yake na baraza yake, navyo vilikuwa na vipimo sawa kama hivyo vingine.
Und er ließ mich den Weg gen Mittag gehen, und siehe, ein Tor am Weg nach Mittag, und er maß seine Pfeiler und seine Vorhallen nach denselben Maßen.
25 Lango na baraza yake vilikuwa na madirisha membamba pande zote, kama madirisha ya huko kwingine. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
Und Fenster hatte es, und seine Vorhallen ringsum und ringsum, wie die selbigen Fenster fünfzig Ellen die Länge und die Breite fünfundzwanzig Ellen.
26 Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo. Ilikuwa na nakshi za miti ya mitende kwenye kuta zilizogawanya vyumba kila upande.
Und sieben Stufen hatten seine Treppen und seine Vorhalle davor, und hatte Palmen, eine hüben und eine drüben an seinen Pfeilern.
27 Ukumbi wa ndani pia ulikuwa na lango lililoelekea kusini. Naye akapima kutoka lango hili mpaka kwenye lango la nje upande wa kusini; ilikuwa dhiraa mia moja.
Und ein Tor zum inneren Vorhof war am Wege nach Mittag, und er maß von Tor zu Tor am Wege nach Mittag hundert Ellen.
28 Kisha akanileta mpaka ukumbi wa ndani kwa kupitia lango la kusini, naye akapima lango la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine.
Und er brachte mich hinein in den inneren Vorhof durch das Tor nach Mittag, und maß das Tor nach Mittag, nach denselben Maßen.
29 Vyumba vyake, kuta zilizogawanya vyumba na ukumbi wake zilikuwa na vipimo sawasawa na zile nyingine. Hilo lango na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Navyo vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
Und seine Wachtzellen und seine Pfeiler und seine Vorhallen waren nach diesen Maßen, und waren Fenster daran und an seinen Vorhallen ringsum und ringsum: fünfzig Ellen in die Länge und fünfundzwanzig in die Breite.
30 (Baraza za malango zilizozunguka ukumbi wa ndani zilikuwa na upana wa dhiraa ishirini na tano na kina cha dhiraa tano.)
Und ringsum und ringsum waren Vorhallen, fünfundzwanzig Ellen in der Länge und fünf Ellen in der Breite.
31 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Und seine Vorhallen waren dem äußeren Vorhof zu, und Palmen waren an seinen Pfeilern, und acht Stufen stieg man zu ihm hinauf.
32 Kisha akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani ulioko upande wa mashariki, naye akalipima lango hilo, lilikuwa na vipimo vilivyo sawasawa na yale mengine.
Und er brachte mich hinein nach dem inneren Vorhof am Wege nach Osten, und maß das Tor nach denselben Maßen.
33 Vyumba vyake, kuta zake na baraza yake vilikuwa na vipimo vilivyo sawa na vile vingine. Lile lango pamoja na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
Und seine Wachtzellen und seine Pfeiler und seine Vorhallen waren nach denselben Maßen, und Fenster hatte es und seine Vorhallen ringsum, ringsum, in die Länge fünfzig Ellen, fünfundzwanzig Ellen in die Breite.
34 Baraza yake ilielekea ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote. Kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Und seine Vorhalle war nach dem äußeren Vorhof, und Palmen waren an seinen Pfeilern hüben und drüben, und acht Stufen stieg man zu ihm hinauf.
35 Kisha akanileta mpaka kwenye lango la kaskazini na kulipima. Lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine,
Und er brachte mich hinein zum Tor nach Mitternacht, und maß nach denselben Maßen,
36 kama vile ilivyokuwa kwa vyumba, kuta zake na baraza yake, tena kulikuwa na madirisha pande zote. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
Seine Wachtzellen, seine Pfeiler und seine Vorhallen, und seine Fenster waren ringsum, ringsum, fünfzig Ellen in die Länge und fünfundzwanzig Ellen in die Breite.
37 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Und seine Pfeiler waren dem äußeren Vorhof zu, und Palmen waren an seinen Pfeilern hier und dort, und acht Stufen stieg man zu ihm hinauf.
38 Kulikuwa na chumba na mlango karibu na baraza katika kila njia ya ndani ya lango ambamo sadaka za kuteketezwa zilioshwa.
Und da war eine Zelle, und ihr Eingang war an den Pfeilern der Tore. Da wuschen sie das Brandopfer ab.
39 Kwenye baraza ya lile lango kulikuwepo meza mbili kila upande, ambako sadaka za kuteketezwa, sadaka za dhambi na sadaka za hatia zilichinjiwa.
Und in der Vorhalle des Tores waren zwei Tische hüben und zwei Tische drüben, das Brandopfer und das Sündopfer und das Schuldopfer darauf zu schlachten.
40 Karibu na ukuta wa nje wa baraza ya lile lango karibu na ngazi kwenye ingilio kuelekea kaskazini kulikuwa na meza mbili, nako upande mwingine wa ngazi kulikuwepo na meza mbili.
Und auf der Seite nach außen, da man zum Eingang des Tores nach Mitternacht aufsteigt, waren zwei Tische, und auf der anderen Seite der Vorhalle des Tores waren zwei Tische.
41 Kwa hiyo kulikuwa na meza nne upande mmoja wa lango na nyingine nne upande mwingine, zote zilikuwa meza nane, ambapo dhabihu zilichinjiwa.
Vier Tische hüben und vier Tische drüben zur Seite des Tores: acht Tische, auf denen sie schlachteten.
42 Pia kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, kila meza ilikuwa na urefu wa dhiraa moja na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu na kimo cha dhiraa moja. Juu ya meza hizo viliwekwa vyombo vya kuchinjia sadaka za kuteketezwa na dhabihu nyingine mbalimbali.
Und die vier Tische für das Brandopfer waren von behauenen Steinen, anderthalb Ellen die Länge und anderthalb Ellen die Breite, und eine Elle die Höhe, auf dieselben legten sie die Geräte nieder, mit denen sie das Brandopfer und das Schlachtopfer schlachteten.
43 Kulikuwa na kulabu, urefu wake nyanda nne, zilikuwa zimeshikizwa ukutani pande zote. Meza zilikuwa kwa ajili ya nyama za sadaka.
Und Herdsteine von einer Handbreite waren einwärts zugerichtet ringsum, ringsum, und auf den Tischen das Fleisch der Opfergabe.
44 Nje ya lango la ndani, kwenye ukumbi wa ndani, kulikuwa na vyumba viwili, kimoja upande wa lango la kaskazini nacho kilielekea kusini, kingine upande wa lango la kusini nacho kilielekea kaskazini.
Und außerhalb des inneren Tores waren Zellen der Sänger in dem inneren Hofe zur Seite des Tores gen Mitternacht, und ihre Vorderseiten waren des Weges gen Mittag; eine war an der Seite des Tores gen Osten, mit der Vorderseite des Weges gen Mitternacht.
45 Akaniambia, “Chumba kinachoelekea upande wa kusini ni kwa ajili ya makuhani ambao wana usimamizi wa hekaluni,
Und er redete zu mir: Diese Zelle, deren Vorderseite des Weges gen Mittag ist, ist für die Priester, die der Hut des Hauses hüten.
46 nacho chumba kinachoelekea upande wa kaskazini ni kwa ajili ya makuhani wenye usimamizi wa madhabahuni. Hawa ni wana wa Sadoki, ambao ndio Walawi pekee wanaoweza kumkaribia Bwana ili kuhudumu mbele zake.”
Die Zelle aber, deren Vorderseite des Weges gen Mitternacht ist, ist für die Priester, welche die Hut des Altares hüten. Dies sind die Söhne Zadoks, die von den Söhnen Levis dem Jehovah nahen, Ihm Dienst zu tun.
47 Ndipo alipopima ukumbi: nao ulikuwa mraba wa dhiraa mia moja urefu na upana. Madhabahu yalikuwa mbele ya Hekalu.
Und er maß den Hof, zu einer Länge von hundert Ellen, und hundert Ellen Breite in das Gevierte. Und der Altar war vor dem Haus.
48 Akanileta mpaka kwenye baraza ya Hekalu naye akaipima miimo ya hiyo baraza, nayo ilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande. Upana wa ingilio ulikuwa dhiraa kumi na nne na kuta zake zilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande.
Und er brachte mich hinein zur Vorhalle des Hauses, und maß den Pfeiler der Vorhalle zu fünf Ellen hüben und fünf Ellen drüben, und die Breite des Tores war drei Ellen hüben und drei Ellen drüben.
49 Baraza ilikuwa na dhiraa ishirini kwenda juu na dhiraa kumi na mbili kuanzia mbele hadi nyuma. Kulikuwa na ngazi kumi za kupandia huko, pia kulikuwa na nguzo kwa kila upande wa miimo.
Die Länge der Halle zwanzig Ellen, und die Breite elf Ellen, und samt den Stufen, auf denen sie hinangingen zu derselben, und Säulen waren bei den Pfeilern, eine hüben und eine drüben.