< Ezekieli 40 >
1 Katika mwaka wa ishirini na tano wa uhamisho wetu, mwanzoni mwa huo mwaka, siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya kuanguka kwa mji, siku hiyo hiyo mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanipeleka huko.
Et en la vingt-cinquième année de notre captivité, le premier mois, le premier jour du mois; quatorze ans après que la ville eut été détruite, en ce jour-là la main du Seigneur fut sur moi.
2 Nikiwa katika maono ya Mungu alinichukua mpaka nchi ya Israeli, naye akaniweka kwenye mlima mrefu sana, ambako upande wa kusini kulikuwepo baadhi ya majengo ambayo yalionekana kama mji.
Et elle me conduisit en une vision de Dieu, sur la terre d'Israël, et elle me déposa au sommet d'une très haute montagne; et en face il y avait comme les constructions d'une ville.
3 Akanipeleka huko, nami nikamwona mtu ambaye kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwa shaba. Alikuwa amesimama kwenye lango akiwa na kamba ya kitani na ufito wa kupimia mkononi mwake.
Et elle me conduisit en ce lieu, et voilà qu'il y avait un homme; et son apparence était comme l'apparence de l'airain resplendissant, et il avait en sa main un cordeau de maçon et une canne pour mesure; et il se tenait près de la porte.
4 Mtu huyo akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa macho yako na usikie kwa masikio yako nawe uzingatie kitu nitakachokuonyesha, kwa kuwa ndiyo sababu umeletwa hapa. Iambie nyumba ya Israeli kila kitu utakachoona.”
Et l'homme me dit: Celui que tu vois, fils de l'homme, regarde-le bien de tes yeux, écoute-le bien de tes oreilles, et dépose en ton cœur tout ce que je vais te montrer; car tu es venu ici pour que je te le montre, et tu montreras ensuite à la maison d'Israël tout ce que tu auras vu.
5 Nikaona ukuta uliozunguka eneo lote la Hekalu. Ule ufito wa kupimia uliokuwa mkononi mwa yule mtu ulikuwa na urefu wa dhiraa ndefu sita, yaani, dhiraa ndefu ni sawa na dhiraa na nyanda nne, akapima ule ukuta. Ukuta huo ulikuwa na unene wa dhiraa ndefu sita na kimo cha dhiraa ndefu sita.
Et voilà qu'il y avait un mur tout autour du temple, et la mesure que l'homme tenait à la main était de six coudées et d'un palme; et il mesura le mur, et le mur était en largeur comme sa mesure, et comme sa mesure en hauteur.
6 Kisha akaenda kwenye lango linaloelekea mashariki. Akapanda ngazi zake akapima kizingiti cha lango, nacho kilikuwa na kina cha huo ufito.
Et il monta sept degrés, et il entra par la porte orientale; et il mesura le vestibule de la porte, qui était égal à sa mesure.
7 Vyumba vya kupumzikia vya walinzi vilikuwa na urefu wa huo ufito mmoja na upana wa huo ufito, kuta zilizogawa vyumba hivyo vya mapumziko zilikuwa na unene wa dhiraa tano. Nacho kizingiti cha lango lililokuwa karibu na ukumbi unaoelekea hekaluni ulikuwa na kina cha huo ufito.
Et la chambre était égale en longueur et en largeur à sa mesure, et le vestibule entre les chambres, de six coudées; et la seconde chambre était égale en longueur et en largeur à la mesure, et le vestibule de cinq coudées.
8 Kisha akapima baraza ya njia ya lango,
Et la troisième chambre était égale en longueur et en largeur à sa mesure, et le vestibule du porche, près du vestibule de la porte, avait huit coudées.
9 ambayo ilikuwa na kina cha dhiraa nane na miimo yake ilikuwa na unene wa dhiraa mbili. Baraza ya lango ilielekea Hekalu.
Et les frontispices étaient de deux coudées; et le vestibule de la porte intérieure,
10 Ndani ya lango la mashariki kulikuwepo vyumba vitatu vya kupumzikia kila upande, vyote vitatu vilikuwa na vipimo vilivyo sawa, nazo nyuso za kuta zilizotenganisha kila upande zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
Et les chambres de la porte, communiquant avec la chambre d'entrée, étaient au nombre de trois d'un côté, trois de l'autre; et toutes trois avaient une même mesure, comme les vestibules des deux côtés.
11 Kisha akapima upana wa ingilio la lango, ilikuwa dhiraa kumi na urefu wake ulikuwa dhiraa kumi na tatu.
Et l'homme mesura la largeur de la porte du porche, et elle était de dix coudées, et la largeur du porche, de treize coudées.
12 Mbele ya kila chumba cha kupumzikia kulikuwepo ukuta uliokuwa na kimo cha dhiraa moja kwenda juu, navyo hivyo vyumba vilikuwa dhiraa sita mraba.
Et l'espace devant les chambres était réduit à une coudée sur le front de chaque chambre de chaque côté; et l'intérieur des chambres avait six coudées de long et six de large.
13 Kisha akapima njia ya lango kuanzia juu ya ukuta wa nyuma wa chumba kimoja cha kupumzikia hadi juu ya ukuta wa nyuma wa chumba upande wa pili; kukawa na nafasi ya dhiraa ishirini na tano kuanzia lango la ukuta mmoja hadi lango la ukuta uliokuwa upande mwingine.
Et l'homme mesura la porte depuis le mur d'une chambre jusqu'au mur d'une autre chambre; la largeur était de vingt-cinq coudées; et une porte était vis-à-vis une autre porte.
14 Akapima pia ukumbi, urefu wa dhiraa ishirini na lango linalofuatia hiyo nguzo kila upande wa huo ukumbi.
Et l'espace découvert du vestibule de la porte extérieure avait vingt coudées, jusqu'aux chambres qui régnaient autour de la porte.
15 Umbali kuanzia ingilio la njia ya lango hadi mwisho kabisa wa baraza yake ulikuwa dhiraa hamsini.
Et l'espace découvert de la porte extérieure avait cinquante coudées, jusqu'à l'espace découvert du vestibule de la porte intérieure.
16 Kulikuwa na vidirisha kwenye hivyo vyumba vya walinzi na nguzo za hivyo vyumba zilikuwa kwenye mzunguko wa hilo lango, vivyo hivyo kulikuwa na madirisha yaliyozunguka kuelekeana na ua na juu ya kila nguzo kulikuwa na mapambo ya miti ya mitende.
Et il y avait des fenêtres de biais aux chambres et aux vestibules de la porte du parvis tout alentour. Et de même il y avait des fenêtres aux vestibules tout alentour; à l'intérieur et sur le vestibule, il y avait des palmes des deux côtés.
17 Kisha akanileta katika ukumbi wa nje. Huko nikaona vyumba vingine pamoja na njia iliyokuwa imejengwa kuzunguka ukumbi wote, kulikuwa na vyumba thelathini vimepangana kando ya hiyo njia.
Et l'homme me conduisit au parvis le plus intérieur; et voilà qu'il y avait des chambres et un péristyle autour du parvis: trente chambres pour tout le péristyle.
18 Njia hii iliyojengwa iliambaa na lango, ikiwa na urefu sawa na lango, hii ilikuwa ni njia ya chini.
Et les portiques étaient derrière les portes, et le péristyle intérieur avait la même longueur que les portes.
19 Kisha akapima umbali kutoka ndani ya lango la chini mpaka nje ya ukumbi wa ndani, nao ulikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki na dhiraa mia moja upande wa kaskazini.
Et l'homme mesura la largeur du parvis, depuis l'espace découvert de la porte regardant le dehors; et il y avait cent coudées à partir de la porte qui regardait l'orient. Et l'homme me conduisit vers l'aquilon.
20 Kisha akapima urefu na upana wa lango linaloelekea kaskazini, kukabili ukumbi wa nje.
Et voilà qu'il y avait une porte regardant l'aquilon et appartenant au parvis extérieur; et il mesura la longueur et la largeur,
21 Vyumba vyake vilikuwa vitatu kila upande, kuta zilizogawanya vyumba na baraza ilikuwa na vipimo sawa na zile kuta za lango la kwanza. Zilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
Et ses chambres trois de chaque côté, et son frontispice, ses vestibules et ses palmes; et, comme à la porte qui regardait l'orient, sa longueur était de cinquante coudées et sa largeur de vingt-cinq.
22 Madirisha yake, baraza yake na nakshi yake ya miti ya mitende vilikuwa na vipimo sawasawa na vile vya lango linaloelekea mashariki. Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo.
Et ses fenêtres, son vestibule et ses palmes étaient comme ceux de la porte qui regardait l'orient; et l'on y montait par sept degrés, et le vestibule était intérieur.
23 Kulikuwa na lango kwenye ukumbi wa ndani lililoelekea lile lango la kaskazini, kama vile ilivyokuwa ule upande wa mashariki. Akapima kutoka lango moja hadi lile lililo mkabala nalo, lilikuwa dhiraa mia moja.
Et il y avait une porte au parvis intérieur regardant la porte de l'aquilon, semblable à la porte qui regardait l'orient; et l'homme mesura le parvis d'une porte à l'autre, et il y avait cent coudées.
24 Ndipo akaniongoza mpaka upande wa kusini, nami nikaona lango linaloelekea kusini. Akaipima miimo yake na baraza yake, navyo vilikuwa na vipimo sawa kama hivyo vingine.
Et il me conduisit au côté méridional, et voilà qu'il y avait une porte regardant le midi, et il la mesura, ainsi que les chambres, les frontispices et les vestibules; et il y avait les mêmes dimensions.
25 Lango na baraza yake vilikuwa na madirisha membamba pande zote, kama madirisha ya huko kwingine. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
Les fenêtres et les vestibules environnants étaient comme les fenêtres du vestibule; le tout avait cinquante coudées de long et vingt-cinq de large.
26 Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo. Ilikuwa na nakshi za miti ya mitende kwenye kuta zilizogawanya vyumba kila upande.
Et l'on y montait par sept degrés, et le vestibule était extérieur, et il y avait des palmes des deux côtés du frontispice.
27 Ukumbi wa ndani pia ulikuwa na lango lililoelekea kusini. Naye akapima kutoka lango hili mpaka kwenye lango la nje upande wa kusini; ilikuwa dhiraa mia moja.
Et il y avait une porte en face de la porte du parvis intérieur du côté méridional; et il mesura le parvis d'une porte à l'autre; et la largeur du côté du midi était de cinquante coudées.
28 Kisha akanileta mpaka ukumbi wa ndani kwa kupitia lango la kusini, naye akapima lango la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine.
Et il me conduisit au parvis intérieur en entrant par la porte du midi, et il mesura la porte, et elle avait les mêmes dimensions;
29 Vyumba vyake, kuta zilizogawanya vyumba na ukumbi wake zilikuwa na vipimo sawasawa na zile nyingine. Hilo lango na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Navyo vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
Les chambres, les frontispices et les vestibules avaient aussi les mêmes dimensions; et il y avait des fenêtres au parvis et au vestibule environnants; et le parvis était long de cinquante coudées et large de vingt-cinq,
30 (Baraza za malango zilizozunguka ukumbi wa ndani zilikuwa na upana wa dhiraa ishirini na tano na kina cha dhiraa tano.)
À partir du vestibule du parvis extérieur; et il y avait des palmes au frontispice, et on y montait par huit degrés.
31 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
À partir du vestibule du parvis extérieur; et il y avait des palmes au frontispice, et on y montait par huit degrés.
32 Kisha akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani ulioko upande wa mashariki, naye akalipima lango hilo, lilikuwa na vipimo vilivyo sawasawa na yale mengine.
Et l'homme me conduisit à la porte qui regardait l'orient, et il la mesura, et elle avait les mêmes dimensions;
33 Vyumba vyake, kuta zake na baraza yake vilikuwa na vipimo vilivyo sawa na vile vingine. Lile lango pamoja na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
Les chambres, les frontispices et les vestibules avaient aussi les mêmes dimensions; et il y avait des fenêtres au parvis et au vestibule environnants; et le parvis était long de cinquante coudées et large de vingt-cinq.
34 Baraza yake ilielekea ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote. Kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Et il y avait des vestibules ouvrant sur le parvis intérieur, et des palmes des deux côtés du frontispice; et on y montait par huit degrés.
35 Kisha akanileta mpaka kwenye lango la kaskazini na kulipima. Lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine,
Et l'homme me conduisit à la porte de l'aquilon, et il la mesura, et elle avait les mêmes dimensions.
36 kama vile ilivyokuwa kwa vyumba, kuta zake na baraza yake, tena kulikuwa na madirisha pande zote. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
Et les chambres, et les frontispices et les vestibules et le parvis avaient des fenêtres tout alentour avec des vestibules; et il avait cinquante coudées de long et vingt-cinq de large.
37 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Et les vestibules ouvraient sur le parvis extérieur, et il y avait des palmes des deux côtés du frontispice, et on y montait par huit degrés.
38 Kulikuwa na chumba na mlango karibu na baraza katika kila njia ya ndani ya lango ambamo sadaka za kuteketezwa zilioshwa.
Et ses chambres, ses portes, et ses vestibules, situés vers la porte,
39 Kwenye baraza ya lile lango kulikuwepo meza mbili kila upande, ambako sadaka za kuteketezwa, sadaka za dhambi na sadaka za hatia zilichinjiwa.
Seconde servaient d'écoulement, afin qu'en ce parvis on immolât les victimes pour le péché et pour les fautes d'inadvertance.
40 Karibu na ukuta wa nje wa baraza ya lile lango karibu na ngazi kwenye ingilio kuelekea kaskazini kulikuwa na meza mbili, nako upande mwingine wa ngazi kulikuwepo na meza mbili.
Et derrière la rigole des holocaustes il y avait deux tables à l'orient, vers la porte qui regarde l'aquilon; derrière la seconde porte, et derrière le vestibule de la porte, deux tables à l'orient.
41 Kwa hiyo kulikuwa na meza nne upande mmoja wa lango na nyingine nne upande mwingine, zote zilikuwa meza nane, ambapo dhabihu zilichinjiwa.
C'étaient donc quatre tables d'un côté et quatre de l'autre côté, derrière la porte; et sur ces tables on sacrifiait les victimes. Devant ces huit tables destinées aux victimes
42 Pia kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, kila meza ilikuwa na urefu wa dhiraa moja na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu na kimo cha dhiraa moja. Juu ya meza hizo viliwekwa vyombo vya kuchinjia sadaka za kuteketezwa na dhabihu nyingine mbalimbali.
Il y avait de plus, pour les holocaustes, quatre tables en pierre de taille, larges d'une demi-coudée, longues de deux coudées et demie, épaisses d'une coudée. Sur ces tables on posait les instruments avec lesquels on y égorgeait les holocaustes et les autres victimes.
43 Kulikuwa na kulabu, urefu wake nyanda nne, zilikuwa zimeshikizwa ukutani pande zote. Meza zilikuwa kwa ajili ya nyama za sadaka.
Et ces tables avaient en dedans, tout alentour, une gouttière creusée au ciseau, profonde d'un palme, et au-dessus d'elles un toit pour les préserver de la pluie et de la sécheresse.
44 Nje ya lango la ndani, kwenye ukumbi wa ndani, kulikuwa na vyumba viwili, kimoja upande wa lango la kaskazini nacho kilielekea kusini, kingine upande wa lango la kusini nacho kilielekea kaskazini.
Et l'homme me conduisit au parvis intérieur; et voilà, qu'il y avait deux chambres dans le parvis intérieur, l'une derrière la porte septentrionale, se prolongeant au midi, l'autre derrière la porte méridionale et se prolongeant à l'aquilon.
45 Akaniambia, “Chumba kinachoelekea upande wa kusini ni kwa ajili ya makuhani ambao wana usimamizi wa hekaluni,
Et il me dit: Cette chambre, située au midi, est pour les prêtres qui gardent le temple;
46 nacho chumba kinachoelekea upande wa kaskazini ni kwa ajili ya makuhani wenye usimamizi wa madhabahuni. Hawa ni wana wa Sadoki, ambao ndio Walawi pekee wanaoweza kumkaribia Bwana ili kuhudumu mbele zake.”
Et la salle située à l'aquilon est pour les prêtres qui gardent l'autel. Ce sont les fils de Sadduc, de la tribu de Lévi, qui s'approchent du Seigneur pour le servir.
47 Ndipo alipopima ukumbi: nao ulikuwa mraba wa dhiraa mia moja urefu na upana. Madhabahu yalikuwa mbele ya Hekalu.
Et il mesura le parvis qui était long de cent coudées dans tous les sens, et l'autel devant le temple.
48 Akanileta mpaka kwenye baraza ya Hekalu naye akaipima miimo ya hiyo baraza, nayo ilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande. Upana wa ingilio ulikuwa dhiraa kumi na nne na kuta zake zilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande.
Et il me conduisit dans le vestibule du temple, et il mesura les deux poteaux du vestibule, ayant chacun cinq coudées de large, et les portes larges de treize coudées, et les montants et chambranles de la porte du vestibule, qui avaient trois coudées de chaque côté;
49 Baraza ilikuwa na dhiraa ishirini kwenda juu na dhiraa kumi na mbili kuanzia mbele hadi nyuma. Kulikuwa na ngazi kumi za kupandia huko, pia kulikuwa na nguzo kwa kila upande wa miimo.
Et la longueur du vestibule était de vingt coudées, et sa largeur de douze. Et l'on y montait par douze degrés, et près du vestibule il y avait des colonnes, une d'un côté, une de l'autre.