< Ezekieli 40 >

1 Katika mwaka wa ishirini na tano wa uhamisho wetu, mwanzoni mwa huo mwaka, siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya kuanguka kwa mji, siku hiyo hiyo mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanipeleka huko.
En la vingt-cinquième année de notre transportation, au commencement de l’année, le dixième [jour] du mois, en la quatorzième année après que la ville eut été frappée, en ce même jour, la main de l’Éternel fut sur moi, et il m’amena là.
2 Nikiwa katika maono ya Mungu alinichukua mpaka nchi ya Israeli, naye akaniweka kwenye mlima mrefu sana, ambako upande wa kusini kulikuwepo baadhi ya majengo ambayo yalionekana kama mji.
Dans les visions de Dieu, il m’amena au pays d’Israël, et me posa sur une très haute montagne; et sur elle il y avait comme une ville bâtie, du côté du midi.
3 Akanipeleka huko, nami nikamwona mtu ambaye kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwa shaba. Alikuwa amesimama kwenye lango akiwa na kamba ya kitani na ufito wa kupimia mkononi mwake.
Et il m’amena là, et voici un homme dont l’aspect était comme l’aspect de l’airain; et [il avait] dans sa main un cordeau de lin et une canne à mesurer, et il se tenait dans la porte.
4 Mtu huyo akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa macho yako na usikie kwa masikio yako nawe uzingatie kitu nitakachokuonyesha, kwa kuwa ndiyo sababu umeletwa hapa. Iambie nyumba ya Israeli kila kitu utakachoona.”
Et l’homme me dit: Fils d’homme, regarde de tes yeux, et écoute de tes oreilles, et applique ton cœur à tout ce que je te fais voir; car c’est afin de te le faire voir que tu as été amené ici. Déclare à la maison d’Israël tout ce que tu vois.
5 Nikaona ukuta uliozunguka eneo lote la Hekalu. Ule ufito wa kupimia uliokuwa mkononi mwa yule mtu ulikuwa na urefu wa dhiraa ndefu sita, yaani, dhiraa ndefu ni sawa na dhiraa na nyanda nne, akapima ule ukuta. Ukuta huo ulikuwa na unene wa dhiraa ndefu sita na kimo cha dhiraa ndefu sita.
Et voici, en dehors de la maison, un mur tout à l’entour, et, dans la main de l’homme, une canne à mesurer de six coudées, ayant [chacune] une coudée et une paume. Et il mesura la largeur de la construction, une canne, et la hauteur, une canne.
6 Kisha akaenda kwenye lango linaloelekea mashariki. Akapanda ngazi zake akapima kizingiti cha lango, nacho kilikuwa na kina cha huo ufito.
Et il vint à la porte qui regardait vers l’orient, et il monta par ses degrés; et il mesura le seuil de la porte, une canne en largeur, et l’autre seuil, une canne en largeur;
7 Vyumba vya kupumzikia vya walinzi vilikuwa na urefu wa huo ufito mmoja na upana wa huo ufito, kuta zilizogawa vyumba hivyo vya mapumziko zilikuwa na unene wa dhiraa tano. Nacho kizingiti cha lango lililokuwa karibu na ukumbi unaoelekea hekaluni ulikuwa na kina cha huo ufito.
et [chaque] chambre, une canne en longueur et une canne en largeur; et entre les chambres, cinq coudées; et le seuil de la porte, du côté du portique de la porte, en dedans, une canne.
8 Kisha akapima baraza ya njia ya lango,
Et il mesura le portique de la porte, en dedans, une canne.
9 ambayo ilikuwa na kina cha dhiraa nane na miimo yake ilikuwa na unene wa dhiraa mbili. Baraza ya lango ilielekea Hekalu.
Et il mesura le portique de la porte, huit coudées, et ses piliers, deux coudées; et le portique de la porte était vers l’intérieur.
10 Ndani ya lango la mashariki kulikuwepo vyumba vitatu vya kupumzikia kila upande, vyote vitatu vilikuwa na vipimo vilivyo sawa, nazo nyuso za kuta zilizotenganisha kila upande zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
Et les chambres de la porte qui [regardait] vers l’orient étaient trois deçà et trois delà: elles avaient, les trois, une seule mesure, et les piliers deçà et delà, une seule mesure.
11 Kisha akapima upana wa ingilio la lango, ilikuwa dhiraa kumi na urefu wake ulikuwa dhiraa kumi na tatu.
Et il mesura la largeur de l’entrée de la porte, dix coudées, [et] la longueur de la porte, 13 coudées.
12 Mbele ya kila chumba cha kupumzikia kulikuwepo ukuta uliokuwa na kimo cha dhiraa moja kwenda juu, navyo hivyo vyumba vilikuwa dhiraa sita mraba.
Et il y avait devant les chambres une banquette d’une coudée, et une banquette d’une coudée de [l’autre] côté; et [chaque] chambre avait six coudées deçà et six coudées delà.
13 Kisha akapima njia ya lango kuanzia juu ya ukuta wa nyuma wa chumba kimoja cha kupumzikia hadi juu ya ukuta wa nyuma wa chumba upande wa pili; kukawa na nafasi ya dhiraa ishirini na tano kuanzia lango la ukuta mmoja hadi lango la ukuta uliokuwa upande mwingine.
Et il mesura la porte depuis le toit d’une chambre jusqu’au toit [de l’autre chambre], une largeur de 25 coudées, entrée vis-à-vis d’entrée.
14 Akapima pia ukumbi, urefu wa dhiraa ishirini na lango linalofuatia hiyo nguzo kila upande wa huo ukumbi.
Et il fit des piliers, 60 coudées; et à côté du pilier était le parvis, tout autour de la porte.
15 Umbali kuanzia ingilio la njia ya lango hadi mwisho kabisa wa baraza yake ulikuwa dhiraa hamsini.
Et depuis le devant de la porte d’entrée jusqu’au-devant du portique de la porte intérieure, 50 coudées.
16 Kulikuwa na vidirisha kwenye hivyo vyumba vya walinzi na nguzo za hivyo vyumba zilikuwa kwenye mzunguko wa hilo lango, vivyo hivyo kulikuwa na madirisha yaliyozunguka kuelekeana na ua na juu ya kila nguzo kulikuwa na mapambo ya miti ya mitende.
Et il y avait aux chambres des fenêtres fermées, ainsi qu’à leurs piliers, en dedans de la porte, tout autour, et de même aux avancées; et les fenêtres tout autour [donnaient] vers l’intérieur; et sur les piliers il y avait des palmiers.
17 Kisha akanileta katika ukumbi wa nje. Huko nikaona vyumba vingine pamoja na njia iliyokuwa imejengwa kuzunguka ukumbi wote, kulikuwa na vyumba thelathini vimepangana kando ya hiyo njia.
Et il m’amena dans le parvis extérieur; et voici, des cellules, et un pavement garnissant le parvis, tout autour; il y avait 30 cellules sur le pavement.
18 Njia hii iliyojengwa iliambaa na lango, ikiwa na urefu sawa na lango, hii ilikuwa ni njia ya chini.
Et le pavement était à côté des portes, répondant à la longueur des portes, [savoir] le pavement inférieur.
19 Kisha akapima umbali kutoka ndani ya lango la chini mpaka nje ya ukumbi wa ndani, nao ulikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki na dhiraa mia moja upande wa kaskazini.
Et il mesura la largeur depuis le devant de la porte inférieure jusqu’au-devant du parvis intérieur, en dehors, 100 coudées à l’orient et au nord.
20 Kisha akapima urefu na upana wa lango linaloelekea kaskazini, kukabili ukumbi wa nje.
Et il mesura la longueur et la largeur de la porte du parvis extérieur, qui regardait vers le nord;
21 Vyumba vyake vilikuwa vitatu kila upande, kuta zilizogawanya vyumba na baraza ilikuwa na vipimo sawa na zile kuta za lango la kwanza. Zilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
et ses chambres, trois deçà et trois delà, et ses piliers, et ses avancées: elle était selon la mesure de la première porte, sa longueur, 50 coudées, et sa largeur, 25 coudées.
22 Madirisha yake, baraza yake na nakshi yake ya miti ya mitende vilikuwa na vipimo sawasawa na vile vya lango linaloelekea mashariki. Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo.
Et ses fenêtres, et ses avancées, et ses palmiers, étaient selon la mesure de la porte qui regardait vers l’orient; et on y montait par sept degrés, et ses avancées étaient devant eux.
23 Kulikuwa na lango kwenye ukumbi wa ndani lililoelekea lile lango la kaskazini, kama vile ilivyokuwa ule upande wa mashariki. Akapima kutoka lango moja hadi lile lililo mkabala nalo, lilikuwa dhiraa mia moja.
Et la porte du parvis intérieur était vis-à-vis de la porte du nord et de l’orient; et il mesura, de porte à porte, 100 coudées.
24 Ndipo akaniongoza mpaka upande wa kusini, nami nikaona lango linaloelekea kusini. Akaipima miimo yake na baraza yake, navyo vilikuwa na vipimo sawa kama hivyo vingine.
Et il me conduisit vers le midi; et voici, une porte vers le midi; et il mesura ses piliers et ses avancées selon ces [mêmes] mesures;
25 Lango na baraza yake vilikuwa na madirisha membamba pande zote, kama madirisha ya huko kwingine. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
et il y avait des fenêtres à la [porte] et à ses avancées, tout autour, comme ces fenêtres-là: la longueur, 50 coudées, et la largeur, 25 coudées.
26 Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo. Ilikuwa na nakshi za miti ya mitende kwenye kuta zilizogawanya vyumba kila upande.
Et il y avait sept degrés pour y monter, et ses avancées devant eux; et la porte avait des palmiers, un deçà et un delà, sur ses piliers.
27 Ukumbi wa ndani pia ulikuwa na lango lililoelekea kusini. Naye akapima kutoka lango hili mpaka kwenye lango la nje upande wa kusini; ilikuwa dhiraa mia moja.
Et il y avait une porte au parvis intérieur vers le midi; et il mesura de porte à porte, vers le midi, 100 coudées.
28 Kisha akanileta mpaka ukumbi wa ndani kwa kupitia lango la kusini, naye akapima lango la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine.
Et il m’amena dans le parvis intérieur, par la porte du midi; et il mesura la porte du midi selon ces [mêmes] mesures;
29 Vyumba vyake, kuta zilizogawanya vyumba na ukumbi wake zilikuwa na vipimo sawasawa na zile nyingine. Hilo lango na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Navyo vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
et ses chambres, et ses piliers, et ses avancées, selon ces mesures-là; et il y avait des fenêtres à la [porte] et à ses avancées, tout autour: la longueur, 50 coudées, et la largeur, 25 coudées.
30 (Baraza za malango zilizozunguka ukumbi wa ndani zilikuwa na upana wa dhiraa ishirini na tano na kina cha dhiraa tano.)
Et il y avait des avancées tout autour; la longueur, 25 coudées, et la largeur, cinq coudées.
31 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Et ses avancées étaient vers le parvis extérieur; et il y avait des palmiers sur ses piliers; et son escalier avait huit degrés.
32 Kisha akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani ulioko upande wa mashariki, naye akalipima lango hilo, lilikuwa na vipimo vilivyo sawasawa na yale mengine.
Et il m’amena dans le parvis intérieur, vers l’orient; et il mesura la porte selon ces [mêmes] mesures;
33 Vyumba vyake, kuta zake na baraza yake vilikuwa na vipimo vilivyo sawa na vile vingine. Lile lango pamoja na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
et ses chambres, et ses piliers, et ses avancées, selon ces mesures-là; et il y avait des fenêtres à la [porte] et à ses avancées, tout autour: la longueur, 50 coudées, et la largeur, 25 coudées.
34 Baraza yake ilielekea ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote. Kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Et ses avancées étaient vers le parvis extérieur; et il y avait des palmiers sur ses piliers, deçà et delà; et son escalier avait huit degrés.
35 Kisha akanileta mpaka kwenye lango la kaskazini na kulipima. Lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine,
Et il m’amena à la porte du nord, et il mesura selon ces mesures-là
36 kama vile ilivyokuwa kwa vyumba, kuta zake na baraza yake, tena kulikuwa na madirisha pande zote. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
ses chambres, ses piliers, et ses avancées; et elle avait des fenêtres tout autour: la longueur, 50 coudées, et la largeur, 25 coudées.
37 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Et ses piliers étaient vers le parvis extérieur; et il y avait des palmiers sur ses piliers, deçà et delà; et son escalier avait huit degrés.
38 Kulikuwa na chumba na mlango karibu na baraza katika kila njia ya ndani ya lango ambamo sadaka za kuteketezwa zilioshwa.
Et il y avait une cellule et son entrée auprès des piliers des portes: là on lavait l’holocauste.
39 Kwenye baraza ya lile lango kulikuwepo meza mbili kila upande, ambako sadaka za kuteketezwa, sadaka za dhambi na sadaka za hatia zilichinjiwa.
Et, dans le portique de la porte, il y avait deux tables deçà et deux tables delà, pour égorger sur elles l’holocauste et le sacrifice pour le péché et le sacrifice pour le délit.
40 Karibu na ukuta wa nje wa baraza ya lile lango karibu na ngazi kwenye ingilio kuelekea kaskazini kulikuwa na meza mbili, nako upande mwingine wa ngazi kulikuwepo na meza mbili.
Et sur le côté, en dehors, à la montée, à l’entrée de la porte du nord, il y avait deux tables; et de l’autre côté, près du portique de la porte, deux tables:
41 Kwa hiyo kulikuwa na meza nne upande mmoja wa lango na nyingine nne upande mwingine, zote zilikuwa meza nane, ambapo dhabihu zilichinjiwa.
quatre tables deçà et quatre tables delà, à côté de la porte, – huit tables, sur lesquelles on égorgeait;
42 Pia kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, kila meza ilikuwa na urefu wa dhiraa moja na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu na kimo cha dhiraa moja. Juu ya meza hizo viliwekwa vyombo vya kuchinjia sadaka za kuteketezwa na dhabihu nyingine mbalimbali.
et, auprès de l’escalier, quatre tables en pierre de taille, longues d’une coudée et demie, et larges d’une coudée et demie, et hautes d’une coudée; on y posait les instruments avec lesquels on égorgeait l’holocauste et les [autres] sacrifices.
43 Kulikuwa na kulabu, urefu wake nyanda nne, zilikuwa zimeshikizwa ukutani pande zote. Meza zilikuwa kwa ajili ya nyama za sadaka.
Et les doubles crochets, d’une paume, étaient fixés à la maison, tout autour; et, sur les tables, [on mettait] la chair des offrandes.
44 Nje ya lango la ndani, kwenye ukumbi wa ndani, kulikuwa na vyumba viwili, kimoja upande wa lango la kaskazini nacho kilielekea kusini, kingine upande wa lango la kusini nacho kilielekea kaskazini.
Et en dehors de la porte intérieure il y avait dans le parvis intérieur deux cellules, l’une sur le côté de la porte du nord et qui regardait vers le midi, l’autre sur le côté de la porte du midi, qui regardait vers le nord.
45 Akaniambia, “Chumba kinachoelekea upande wa kusini ni kwa ajili ya makuhani ambao wana usimamizi wa hekaluni,
Et il me dit: Cette cellule qui regarde vers le midi est pour les sacrificateurs qui font l’acquit de la charge de la maison;
46 nacho chumba kinachoelekea upande wa kaskazini ni kwa ajili ya makuhani wenye usimamizi wa madhabahuni. Hawa ni wana wa Sadoki, ambao ndio Walawi pekee wanaoweza kumkaribia Bwana ili kuhudumu mbele zake.”
et la cellule qui regarde vers le nord est pour les sacrificateurs qui font l’acquit de la charge concernant l’autel. Ce sont les fils de Tsadok, qui, d’entre les fils de Lévi, s’approchent de l’Éternel pour faire son service.
47 Ndipo alipopima ukumbi: nao ulikuwa mraba wa dhiraa mia moja urefu na upana. Madhabahu yalikuwa mbele ya Hekalu.
Et il mesura le parvis: la longueur, 100 coudées, et la largeur, 100 coudées, un carré; et l’autel était devant la maison.
48 Akanileta mpaka kwenye baraza ya Hekalu naye akaipima miimo ya hiyo baraza, nayo ilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande. Upana wa ingilio ulikuwa dhiraa kumi na nne na kuta zake zilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande.
Et il m’amena au portique de la maison; et il mesura le pilier du portique, cinq coudées deçà, et cinq coudées delà; et la largeur de la porte était de trois coudées deçà, et de trois coudées delà.
49 Baraza ilikuwa na dhiraa ishirini kwenda juu na dhiraa kumi na mbili kuanzia mbele hadi nyuma. Kulikuwa na ngazi kumi za kupandia huko, pia kulikuwa na nguzo kwa kila upande wa miimo.
La longueur du portique était de 20 coudées, et la largeur, de onze coudées, et [cela] aux degrés par lesquels on y montait; et il y avait des colonnes près des piliers, une deçà et une delà.

< Ezekieli 40 >