< Ezekieli 40 >

1 Katika mwaka wa ishirini na tano wa uhamisho wetu, mwanzoni mwa huo mwaka, siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya kuanguka kwa mji, siku hiyo hiyo mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanipeleka huko.
In the twenty-fifth year of our captivity at the beginning of the year on the tenth day of the month, in the fourteenth year after the city was captured—on that same day, the hand of Yahweh was upon me and he took me there.
2 Nikiwa katika maono ya Mungu alinichukua mpaka nchi ya Israeli, naye akaniweka kwenye mlima mrefu sana, ambako upande wa kusini kulikuwepo baadhi ya majengo ambayo yalionekana kama mji.
In visions from God he brought me to the land of Israel. He brought me to rest on a very high mountain; to the south were what appeared to be buildings of a city.
3 Akanipeleka huko, nami nikamwona mtu ambaye kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwa shaba. Alikuwa amesimama kwenye lango akiwa na kamba ya kitani na ufito wa kupimia mkononi mwake.
Then he brought me there. Behold, a man! His appearance was like the appearance of bronze. A linen cord and a measuring stick were in his hand, and he stood in the city gate.
4 Mtu huyo akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa macho yako na usikie kwa masikio yako nawe uzingatie kitu nitakachokuonyesha, kwa kuwa ndiyo sababu umeletwa hapa. Iambie nyumba ya Israeli kila kitu utakachoona.”
The man said to me, “Son of man, look with your eyes and listen with your ears, and fix your mind on all that I am revealing to you, for you were brought here so I could reveal them to you. Report everything that you will see to the house of Israel.”
5 Nikaona ukuta uliozunguka eneo lote la Hekalu. Ule ufito wa kupimia uliokuwa mkononi mwa yule mtu ulikuwa na urefu wa dhiraa ndefu sita, yaani, dhiraa ndefu ni sawa na dhiraa na nyanda nne, akapima ule ukuta. Ukuta huo ulikuwa na unene wa dhiraa ndefu sita na kimo cha dhiraa ndefu sita.
There was a wall surrounding the temple area. The length of the measuring stick in the man's hand was six long cubits. Each long cubit was a cubit and a handbreadth in length. So he measured the wall, and it was one measuring stick thick and one rod high.
6 Kisha akaenda kwenye lango linaloelekea mashariki. Akapanda ngazi zake akapima kizingiti cha lango, nacho kilikuwa na kina cha huo ufito.
Then he went to the temple gate that faced east. He went up its steps and measured the threshold of the gate—one stick in depth.
7 Vyumba vya kupumzikia vya walinzi vilikuwa na urefu wa huo ufito mmoja na upana wa huo ufito, kuta zilizogawa vyumba hivyo vya mapumziko zilikuwa na unene wa dhiraa tano. Nacho kizingiti cha lango lililokuwa karibu na ukumbi unaoelekea hekaluni ulikuwa na kina cha huo ufito.
The guard chambers were each one stick in length and one stick in width; there were five cubits between any two of the chambers, and the threshold of the temple gate by the temple portico was one stick deep.
8 Kisha akapima baraza ya njia ya lango,
He measured the portico of the gate; it was one stick in length.
9 ambayo ilikuwa na kina cha dhiraa nane na miimo yake ilikuwa na unene wa dhiraa mbili. Baraza ya lango ilielekea Hekalu.
He measured the portico of the gate. It was one stick deep. The doorposts were two cubits in width. This was the portico of the gate facing the temple.
10 Ndani ya lango la mashariki kulikuwepo vyumba vitatu vya kupumzikia kila upande, vyote vitatu vilikuwa na vipimo vilivyo sawa, nazo nyuso za kuta zilizotenganisha kila upande zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
There were three guard chambers on either side of the east gate, and each of them had the same measurement, and the walls that separated them had the same measurement.
11 Kisha akapima upana wa ingilio la lango, ilikuwa dhiraa kumi na urefu wake ulikuwa dhiraa kumi na tatu.
Then the man measured the width of the gateway entrance—ten cubits; and he measured the length of the gateway entrance—thirteen cubits.
12 Mbele ya kila chumba cha kupumzikia kulikuwepo ukuta uliokuwa na kimo cha dhiraa moja kwenda juu, navyo hivyo vyumba vilikuwa dhiraa sita mraba.
He measured the wall that was bordering the front of the chambers—one cubit high. The chambers measured six cubits on each side.
13 Kisha akapima njia ya lango kuanzia juu ya ukuta wa nyuma wa chumba kimoja cha kupumzikia hadi juu ya ukuta wa nyuma wa chumba upande wa pili; kukawa na nafasi ya dhiraa ishirini na tano kuanzia lango la ukuta mmoja hadi lango la ukuta uliokuwa upande mwingine.
Then he measured the gateway from the roof of one chamber to that of the next chamber—twenty-five cubits, from the entrance of the first chamber to that of the second.
14 Akapima pia ukumbi, urefu wa dhiraa ishirini na lango linalofuatia hiyo nguzo kila upande wa huo ukumbi.
Then he measured the wall that went between the guard chambers—sixty cubits in length; he measured as far as the gate's portico.
15 Umbali kuanzia ingilio la njia ya lango hadi mwisho kabisa wa baraza yake ulikuwa dhiraa hamsini.
The entrance from the front of the gate to the other end of the gate's portico was fifty cubits.
16 Kulikuwa na vidirisha kwenye hivyo vyumba vya walinzi na nguzo za hivyo vyumba zilikuwa kwenye mzunguko wa hilo lango, vivyo hivyo kulikuwa na madirisha yaliyozunguka kuelekeana na ua na juu ya kila nguzo kulikuwa na mapambo ya miti ya mitende.
There were closed windows toward the chambers and toward their pillars within the gates all around; and likewise for the porches. The were windows all around the inside, and each jamb was decorated with palm trees.
17 Kisha akanileta katika ukumbi wa nje. Huko nikaona vyumba vingine pamoja na njia iliyokuwa imejengwa kuzunguka ukumbi wote, kulikuwa na vyumba thelathini vimepangana kando ya hiyo njia.
Then the man brought me to the outer courtyard of the temple. Behold, there were rooms, and there was pavement in the courtyard, with thirty rooms next to the pavement.
18 Njia hii iliyojengwa iliambaa na lango, ikiwa na urefu sawa na lango, hii ilikuwa ni njia ya chini.
The pavement went up to the side of the gates, and its width was the same as the gates' length. This was the lower pavement.
19 Kisha akapima umbali kutoka ndani ya lango la chini mpaka nje ya ukumbi wa ndani, nao ulikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki na dhiraa mia moja upande wa kaskazini.
Then the man measured the distance from the front of the lower gate to the front of the inner gate; it was one hundred cubits on the east side, and the same on the north side.
20 Kisha akapima urefu na upana wa lango linaloelekea kaskazini, kukabili ukumbi wa nje.
Then he measured the length and width of the gate that was at the north of the outer court.
21 Vyumba vyake vilikuwa vitatu kila upande, kuta zilizogawanya vyumba na baraza ilikuwa na vipimo sawa na zile kuta za lango la kwanza. Zilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
There were three chambers on either side of that gate, and the gate and its portico measured the same as the main gate—fifty cubits in total length and twenty-five cubits in width.
22 Madirisha yake, baraza yake na nakshi yake ya miti ya mitende vilikuwa na vipimo sawasawa na vile vya lango linaloelekea mashariki. Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo.
Its windows, portico, chambers, and its palm trees corresponded to the gate that faced east. Seven steps went up to it and to its portico.
23 Kulikuwa na lango kwenye ukumbi wa ndani lililoelekea lile lango la kaskazini, kama vile ilivyokuwa ule upande wa mashariki. Akapima kutoka lango moja hadi lile lililo mkabala nalo, lilikuwa dhiraa mia moja.
There was a gate to the inner courtyard in front of the gate facing north, just as also there was a gate to the east; the man measured from one gate to the other gate—one hundred cubits in distance.
24 Ndipo akaniongoza mpaka upande wa kusini, nami nikaona lango linaloelekea kusini. Akaipima miimo yake na baraza yake, navyo vilikuwa na vipimo sawa kama hivyo vingine.
Next the man brought me to the gate of the southern entrance, and its walls and portico measured the same as the other outer gates.
25 Lango na baraza yake vilikuwa na madirisha membamba pande zote, kama madirisha ya huko kwingine. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
There were closed windows in the gateway and its portico just as at that gate. The south gate and its portico measured fifty cubits in length and twenty-five cubits in width.
26 Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo. Ilikuwa na nakshi za miti ya mitende kwenye kuta zilizogawanya vyumba kila upande.
There were seven steps up to the gate and its portico, and there were carvings of palm trees on the walls on either side.
27 Ukumbi wa ndani pia ulikuwa na lango lililoelekea kusini. Naye akapima kutoka lango hili mpaka kwenye lango la nje upande wa kusini; ilikuwa dhiraa mia moja.
There was a gate to the inner courtyard on the southern side, and the man measured from that gate to the gate of the south entrance—one hundred cubits in distance.
28 Kisha akanileta mpaka ukumbi wa ndani kwa kupitia lango la kusini, naye akapima lango la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine.
Then the man brought me to the inner courtyard by way of its southern gate, which had the same measurements as the other gates.
29 Vyumba vyake, kuta zilizogawanya vyumba na ukumbi wake zilikuwa na vipimo sawasawa na zile nyingine. Hilo lango na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Navyo vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
Its chambers, walls, and porticos measured the same as the other gates; there were windows all around in the portico. The inner gate and its portico measured fifty cubits in length and twenty-five cubits in width.
30 (Baraza za malango zilizozunguka ukumbi wa ndani zilikuwa na upana wa dhiraa ishirini na tano na kina cha dhiraa tano.)
There were also porticos all around the inner wall; these were twenty-five cubits in length and five cubits in width.
31 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
This portico faced the outer courtyard with carved palm trees on its walls and eight steps going up to it.
32 Kisha akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani ulioko upande wa mashariki, naye akalipima lango hilo, lilikuwa na vipimo vilivyo sawasawa na yale mengine.
Then the man brought me to the inner courtyard by the eastern way and measured the gate, which had the same measurements as the other gates.
33 Vyumba vyake, kuta zake na baraza yake vilikuwa na vipimo vilivyo sawa na vile vingine. Lile lango pamoja na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
Its chambers, walls, and portico measured the same as the other gates, and there were windows all around. The inner gate and its portico measured fifty cubits in length and twenty-five cubits in width.
34 Baraza yake ilielekea ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote. Kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Its portico faced the outer courtyard; it had palm trees on either side of it and eight steps going up it.
35 Kisha akanileta mpaka kwenye lango la kaskazini na kulipima. Lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine,
Next the man brought me to the northern gate and measured it; it measured the same as the other gates.
36 kama vile ilivyokuwa kwa vyumba, kuta zake na baraza yake, tena kulikuwa na madirisha pande zote. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
Its chambers, walls, and portico measured the same as the other gates, and there were windows all around. The gateway and its portico measured fifty cubits in length and twenty-five cubits in width.
37 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
Its portico faced the outer courtyard; it had palm trees on either side of it and eight steps going up it.
38 Kulikuwa na chumba na mlango karibu na baraza katika kila njia ya ndani ya lango ambamo sadaka za kuteketezwa zilioshwa.
There was a room with a door by each of the inner gateways. This was where they rinsed the burnt offerings.
39 Kwenye baraza ya lile lango kulikuwepo meza mbili kila upande, ambako sadaka za kuteketezwa, sadaka za dhambi na sadaka za hatia zilichinjiwa.
There were two tables on each side of each portico, on which the burnt offering was slaughtered, and also the sin offering and the guilt offering.
40 Karibu na ukuta wa nje wa baraza ya lile lango karibu na ngazi kwenye ingilio kuelekea kaskazini kulikuwa na meza mbili, nako upande mwingine wa ngazi kulikuwepo na meza mbili.
By the wall of the courtyard, going up to the gate to the north, there were two tables. Also on the other side there were two tables at the gate's portico.
41 Kwa hiyo kulikuwa na meza nne upande mmoja wa lango na nyingine nne upande mwingine, zote zilikuwa meza nane, ambapo dhabihu zilichinjiwa.
There were four tables on either side by the gate; they slaughtered animals on the eight tables.
42 Pia kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, kila meza ilikuwa na urefu wa dhiraa moja na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu na kimo cha dhiraa moja. Juu ya meza hizo viliwekwa vyombo vya kuchinjia sadaka za kuteketezwa na dhabihu nyingine mbalimbali.
There were four tables of cut stone for the burnt offerings, one and a half cubits in length, one and a half cubits in width, and one cubit tall. On them they laid the tools with which they slaughtered the burnt offerings for the sacrifices.
43 Kulikuwa na kulabu, urefu wake nyanda nne, zilikuwa zimeshikizwa ukutani pande zote. Meza zilikuwa kwa ajili ya nyama za sadaka.
Two-pronged hooks a handbreadth in length were fastened in the portico all around, and the flesh of the offerings would be put on the tables.
44 Nje ya lango la ndani, kwenye ukumbi wa ndani, kulikuwa na vyumba viwili, kimoja upande wa lango la kaskazini nacho kilielekea kusini, kingine upande wa lango la kusini nacho kilielekea kaskazini.
On the outside of the inner gate, within the inner courtyard, were singers' chambers, one on the north side facing south, and the other on the south side facing north.
45 Akaniambia, “Chumba kinachoelekea upande wa kusini ni kwa ajili ya makuhani ambao wana usimamizi wa hekaluni,
Then the man said to me, “This room facing south is for the priests who are on duty in the temple.
46 nacho chumba kinachoelekea upande wa kaskazini ni kwa ajili ya makuhani wenye usimamizi wa madhabahuni. Hawa ni wana wa Sadoki, ambao ndio Walawi pekee wanaoweza kumkaribia Bwana ili kuhudumu mbele zake.”
The room facing north is for the priests on duty at the altar. These are the sons of Zadok who come near to Yahweh to serve him; they are among the sons of Levi.”
47 Ndipo alipopima ukumbi: nao ulikuwa mraba wa dhiraa mia moja urefu na upana. Madhabahu yalikuwa mbele ya Hekalu.
Next he measured the courtyard—one hundred cubits in length and one hundred cubits in width in a square, with the altar in front of the house.
48 Akanileta mpaka kwenye baraza ya Hekalu naye akaipima miimo ya hiyo baraza, nayo ilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande. Upana wa ingilio ulikuwa dhiraa kumi na nne na kuta zake zilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande.
Then the man brought me to the portico of the house and measured its doorposts—they were five cubits thick on either side. The entryway itself was fourteen cubits in width, and the walls on each side of it were three cubits in width.
49 Baraza ilikuwa na dhiraa ishirini kwenda juu na dhiraa kumi na mbili kuanzia mbele hadi nyuma. Kulikuwa na ngazi kumi za kupandia huko, pia kulikuwa na nguzo kwa kila upande wa miimo.
The length of the portico was twenty cubits, and its depth was eleven cubits. There were steps that went up to it and columns that stood on either side of it.

< Ezekieli 40 >