< Ezekieli 40 >
1 Katika mwaka wa ishirini na tano wa uhamisho wetu, mwanzoni mwa huo mwaka, siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya kuanguka kwa mji, siku hiyo hiyo mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanipeleka huko.
In the five and twentieth year of our captivity, in the first month, on the tenth day of the month, in the fourteenth year after that the city was smitten, on the selfsame day the hand of Jehovah was upon me, and he brought me [[thither into the city]].
2 Nikiwa katika maono ya Mungu alinichukua mpaka nchi ya Israeli, naye akaniweka kwenye mlima mrefu sana, ambako upande wa kusini kulikuwepo baadhi ya majengo ambayo yalionekana kama mji.
In the visions of God he brought me into the land of Israel, and set me upon a very high mountain, upon which was, as it were, the frame of a city toward the south.
3 Akanipeleka huko, nami nikamwona mtu ambaye kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwa shaba. Alikuwa amesimama kwenye lango akiwa na kamba ya kitani na ufito wa kupimia mkononi mwake.
And when he had brought me thither, behold, there was a man, whose appearance was as the appearance of brass, with a line of flax in his hand, and a measuring-reed, and he stood in the gate.
4 Mtu huyo akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa macho yako na usikie kwa masikio yako nawe uzingatie kitu nitakachokuonyesha, kwa kuwa ndiyo sababu umeletwa hapa. Iambie nyumba ya Israeli kila kitu utakachoona.”
And the man said to me, Son of man, behold with thine eyes and hear with thine ears, and give heed to all which I shall show thee; for to the intent that I might show them to thee art thou brought hither; declare all which thou seest to the house of Israel!
5 Nikaona ukuta uliozunguka eneo lote la Hekalu. Ule ufito wa kupimia uliokuwa mkononi mwa yule mtu ulikuwa na urefu wa dhiraa ndefu sita, yaani, dhiraa ndefu ni sawa na dhiraa na nyanda nne, akapima ule ukuta. Ukuta huo ulikuwa na unene wa dhiraa ndefu sita na kimo cha dhiraa ndefu sita.
And behold, a wall on the outside of the house round about, and in the man's hand a measuring reed, in length six cubits of a cubit and a handbreadth; and he measured the breadth of the wall, one reed; and the height, one reed.
6 Kisha akaenda kwenye lango linaloelekea mashariki. Akapanda ngazi zake akapima kizingiti cha lango, nacho kilikuwa na kina cha huo ufito.
Then came he to the gate, which looked toward the east, and went up the steps thereof, and measured the upper threshold of the gate, one reed broad, and the other threshold of the gate one reed broad.
7 Vyumba vya kupumzikia vya walinzi vilikuwa na urefu wa huo ufito mmoja na upana wa huo ufito, kuta zilizogawa vyumba hivyo vya mapumziko zilikuwa na unene wa dhiraa tano. Nacho kizingiti cha lango lililokuwa karibu na ukumbi unaoelekea hekaluni ulikuwa na kina cha huo ufito.
And every chamber was one reed long, and one reed broad; and between the chambers were five cubits; and the threshold of the gate by the porch of the gate within was one reed.
8 Kisha akapima baraza ya njia ya lango,
He measured also the porch of the gate within, one reed.
9 ambayo ilikuwa na kina cha dhiraa nane na miimo yake ilikuwa na unene wa dhiraa mbili. Baraza ya lango ilielekea Hekalu.
Then he measured the porch of the gate, eight cubits; and the border thereof, two cubits; now the porch of the gate was inward.
10 Ndani ya lango la mashariki kulikuwepo vyumba vitatu vya kupumzikia kila upande, vyote vitatu vilikuwa na vipimo vilivyo sawa, nazo nyuso za kuta zilizotenganisha kila upande zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
And the chambers of the gate eastward were three on this side, and three on that side; they three were of one measure, and the projecting wall-pillars were of one measure on this side, and on that side.
11 Kisha akapima upana wa ingilio la lango, ilikuwa dhiraa kumi na urefu wake ulikuwa dhiraa kumi na tatu.
And he measured the breadth of the entry of the gate, ten cubits; and the length of the entry of the gate, thirteen cubits.
12 Mbele ya kila chumba cha kupumzikia kulikuwepo ukuta uliokuwa na kimo cha dhiraa moja kwenda juu, navyo hivyo vyumba vilikuwa dhiraa sita mraba.
There was also a space before the chambers one cubit on this side, and a space one cubit on that side; and every chamber was six cubits on this side, and six cubits on that side.
13 Kisha akapima njia ya lango kuanzia juu ya ukuta wa nyuma wa chumba kimoja cha kupumzikia hadi juu ya ukuta wa nyuma wa chumba upande wa pili; kukawa na nafasi ya dhiraa ishirini na tano kuanzia lango la ukuta mmoja hadi lango la ukuta uliokuwa upande mwingine.
Then he measured the gate from the roof of one chamber to the roof of another; the breadth was five and twenty cubits, and door was over against door.
14 Akapima pia ukumbi, urefu wa dhiraa ishirini na lango linalofuatia hiyo nguzo kila upande wa huo ukumbi.
He made also wall-pillars sixty cubits, and toward the pillars, was the court of the gate round about on every side.
15 Umbali kuanzia ingilio la njia ya lango hadi mwisho kabisa wa baraza yake ulikuwa dhiraa hamsini.
And from the front of the gate of the entrance to the front of the porch of the inner gate were fifty cubits.
16 Kulikuwa na vidirisha kwenye hivyo vyumba vya walinzi na nguzo za hivyo vyumba zilikuwa kwenye mzunguko wa hilo lango, vivyo hivyo kulikuwa na madirisha yaliyozunguka kuelekeana na ua na juu ya kila nguzo kulikuwa na mapambo ya miti ya mitende.
And there were closed windows to the chambers and to their wall-pillars inward toward the gate round about, and likewise to the cornices; there were windows round about within, and upon the wall-pillars were palm-trees.
17 Kisha akanileta katika ukumbi wa nje. Huko nikaona vyumba vingine pamoja na njia iliyokuwa imejengwa kuzunguka ukumbi wote, kulikuwa na vyumba thelathini vimepangana kando ya hiyo njia.
Then he brought me into the outer court, and behold, there were rooms, and a pavement made for the court round about; thirty rooms were upon the pavement.
18 Njia hii iliyojengwa iliambaa na lango, ikiwa na urefu sawa na lango, hii ilikuwa ni njia ya chini.
And the pavement at the sides of the gates, by the length of the gates, was the lower pavement.
19 Kisha akapima umbali kutoka ndani ya lango la chini mpaka nje ya ukumbi wa ndani, nao ulikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki na dhiraa mia moja upande wa kaskazini.
Then he measured the breadth from the front of the lower gate to the front of the inner court without, a hundred cubits toward the east and toward the north.
20 Kisha akapima urefu na upana wa lango linaloelekea kaskazini, kukabili ukumbi wa nje.
And as for the gate that looked toward the north in the outer court, he measured the length thereof, and the breadth thereof.
21 Vyumba vyake vilikuwa vitatu kila upande, kuta zilizogawanya vyumba na baraza ilikuwa na vipimo sawa na zile kuta za lango la kwanza. Zilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
And the chambers thereof were three on this side, and three on that side. And the border thereof, and the cornices thereof, were of the same measure as the former gate; the length thereof was fifty cubits, and the breadth five and twenty cubits.
22 Madirisha yake, baraza yake na nakshi yake ya miti ya mitende vilikuwa na vipimo sawasawa na vile vya lango linaloelekea mashariki. Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo.
And the windows thereof, and the cornices thereof, and the palm-trees thereof were of the same measure as the gate which looked toward the east, and they went up to it by seven steps, and the cornices thereof were before them.
23 Kulikuwa na lango kwenye ukumbi wa ndani lililoelekea lile lango la kaskazini, kama vile ilivyokuwa ule upande wa mashariki. Akapima kutoka lango moja hadi lile lililo mkabala nalo, lilikuwa dhiraa mia moja.
And the gate of the inner court was over against the gate toward the north and east. And he measured from gate to gate a hundred cubits.
24 Ndipo akaniongoza mpaka upande wa kusini, nami nikaona lango linaloelekea kusini. Akaipima miimo yake na baraza yake, navyo vilikuwa na vipimo sawa kama hivyo vingine.
Then he led me toward the south; and behold, there was a gate toward the south; and he measured the border thereof and the cornices thereof according to those measures.
25 Lango na baraza yake vilikuwa na madirisha membamba pande zote, kama madirisha ya huko kwingine. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
And there were windows in it, and within the cornices thereof round about, like those windows; the length was fifty cubits, and the breadth five and twenty cubits.
26 Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo. Ilikuwa na nakshi za miti ya mitende kwenye kuta zilizogawanya vyumba kila upande.
And there were seven steps to go up to it, and the cornices thereof were before them; and it had palm-trees, one on this side and another on that side, upon the wall-pillars thereof.
27 Ukumbi wa ndani pia ulikuwa na lango lililoelekea kusini. Naye akapima kutoka lango hili mpaka kwenye lango la nje upande wa kusini; ilikuwa dhiraa mia moja.
And there was a gate in the inner court toward the south; and he measured from gate to gate toward the south a hundred cubits.
28 Kisha akanileta mpaka ukumbi wa ndani kwa kupitia lango la kusini, naye akapima lango la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine.
And he brought me to the inner court through the south gate; and he measured the south gate according to the same measures.
29 Vyumba vyake, kuta zilizogawanya vyumba na ukumbi wake zilikuwa na vipimo sawasawa na zile nyingine. Hilo lango na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Navyo vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
And the chambers thereof, and the border thereof, and the cornices thereof were according to those measures. And there were windows in it, and within the cornices thereof, round about; it was fifty cubits long, and five and twenty cubits broad.
30 (Baraza za malango zilizozunguka ukumbi wa ndani zilikuwa na upana wa dhiraa ishirini na tano na kina cha dhiraa tano.)
And the cornices round about were five and twenty cubits long, and five cubits broad.
31 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
And the cornices thereof were toward the outer court; and palm-trees were upon the wall-pillars thereof; and in going up to it there were eight steps.
32 Kisha akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani ulioko upande wa mashariki, naye akalipima lango hilo, lilikuwa na vipimo vilivyo sawasawa na yale mengine.
And he brought me to the inner court toward the east; and he measured the gate according to those measures.
33 Vyumba vyake, kuta zake na baraza yake vilikuwa na vipimo vilivyo sawa na vile vingine. Lile lango pamoja na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
And the chambers thereof, and the border thereof, and the cornices thereof, were according to those measures; and there were windows in it, and in the cornices thereof, round about; the length was fifty cubits, and the breadth five and twenty cubits.
34 Baraza yake ilielekea ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote. Kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
And the cornices thereof were toward the outer court; and palm-trees were upon the wall-pillars thereof, on this side and on that side; and in going up to it there were eight steps.
35 Kisha akanileta mpaka kwenye lango la kaskazini na kulipima. Lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine,
And he brought me to the north gate, and measured it according to those measures;
36 kama vile ilivyokuwa kwa vyumba, kuta zake na baraza yake, tena kulikuwa na madirisha pande zote. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
the chambers thereof, and the border thereof, and the cornices thereof; and there were windows to it, round about; the length was fifty cubits, and the breadth five and twenty cubits.
37 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
And the cornices thereof were toward the outer court; and palm-trees were upon the wall-pillars thereof, on this side and on that side; and in going up to it there were eight steps.
38 Kulikuwa na chumba na mlango karibu na baraza katika kila njia ya ndani ya lango ambamo sadaka za kuteketezwa zilioshwa.
And a room with its doors was by the borders of the gates, where they washed the burnt-offering.
39 Kwenye baraza ya lile lango kulikuwepo meza mbili kila upande, ambako sadaka za kuteketezwa, sadaka za dhambi na sadaka za hatia zilichinjiwa.
And in the porch of the gate were two tables on this side, and two tables on that side, to slay thereon the burnt-offering, and the sin-offering, and the trespass-offering.
40 Karibu na ukuta wa nje wa baraza ya lile lango karibu na ngazi kwenye ingilio kuelekea kaskazini kulikuwa na meza mbili, nako upande mwingine wa ngazi kulikuwepo na meza mbili.
And at the side without, as one goeth up to the entrance of the north gate, were two tables; and on the other side, which was at the porch of the gate, were two tables;
41 Kwa hiyo kulikuwa na meza nne upande mmoja wa lango na nyingine nne upande mwingine, zote zilikuwa meza nane, ambapo dhabihu zilichinjiwa.
four tables were on this side, and four tables on that side; on the other side of the gate eight tables, whereon they slew their sacrifices.
42 Pia kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, kila meza ilikuwa na urefu wa dhiraa moja na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu na kimo cha dhiraa moja. Juu ya meza hizo viliwekwa vyombo vya kuchinjia sadaka za kuteketezwa na dhabihu nyingine mbalimbali.
And the four tables for the burnt-offering were of hewn stone; their length was a cubit and a half, and their breadth a cubit and a half, and their height a cubit. Thereon they laid the instruments with which they slew the burnt-offering and the sacrifice.
43 Kulikuwa na kulabu, urefu wake nyanda nne, zilikuwa zimeshikizwa ukutani pande zote. Meza zilikuwa kwa ajili ya nyama za sadaka.
And there were edging-boards of a handbreadth, prepared within round about; and upon the tables was the flesh of the offering.
44 Nje ya lango la ndani, kwenye ukumbi wa ndani, kulikuwa na vyumba viwili, kimoja upande wa lango la kaskazini nacho kilielekea kusini, kingine upande wa lango la kusini nacho kilielekea kaskazini.
And without the inner gate were rooms for the singers in the inner court; they were at the side of the north gate, and their prospect was toward the south; one at the side of the east gate having the prospect toward the north.
45 Akaniambia, “Chumba kinachoelekea upande wa kusini ni kwa ajili ya makuhani ambao wana usimamizi wa hekaluni,
And he said to me, This room, whose prospect is toward the south, is for the priests that keep the charge of the house.
46 nacho chumba kinachoelekea upande wa kaskazini ni kwa ajili ya makuhani wenye usimamizi wa madhabahuni. Hawa ni wana wa Sadoki, ambao ndio Walawi pekee wanaoweza kumkaribia Bwana ili kuhudumu mbele zake.”
And the room whose prospect is toward the north is for the priests that keep the charge of the altar. These are the sons of Zadok, who, among the sons of Levi, come near to Jehovah to minister to him.
47 Ndipo alipopima ukumbi: nao ulikuwa mraba wa dhiraa mia moja urefu na upana. Madhabahu yalikuwa mbele ya Hekalu.
Then he measured the court; its length was a hundred cubits, and its breadth a hundred cubits, being square. And the altar stood before the house.
48 Akanileta mpaka kwenye baraza ya Hekalu naye akaipima miimo ya hiyo baraza, nayo ilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande. Upana wa ingilio ulikuwa dhiraa kumi na nne na kuta zake zilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande.
Then he brought me to the porch of the temple, and he measured the door-border of the porch, five cubits on this side, and five cubits on that side. And the breadth of the gate was three cubits on this side, and three cubits on that side.
49 Baraza ilikuwa na dhiraa ishirini kwenda juu na dhiraa kumi na mbili kuanzia mbele hadi nyuma. Kulikuwa na ngazi kumi za kupandia huko, pia kulikuwa na nguzo kwa kila upande wa miimo.
The length of the porch was twenty cubits, and the breadth eleven cubits; and they went up to it by steps. And there were columns by the door-border, one on this side, and another on that side.