< Ezekieli 40 >

1 Katika mwaka wa ishirini na tano wa uhamisho wetu, mwanzoni mwa huo mwaka, siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya kuanguka kwa mji, siku hiyo hiyo mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanipeleka huko.
In the five and twentieth year of our captivity, in the beginning of the year, the tenth day of the month, the fourteenth year after the city was destroyed: in the selfsame day the hand of the Lord was upon me, and he brought me thither.
2 Nikiwa katika maono ya Mungu alinichukua mpaka nchi ya Israeli, naye akaniweka kwenye mlima mrefu sana, ambako upande wa kusini kulikuwepo baadhi ya majengo ambayo yalionekana kama mji.
In the visions of God he brought me into the land of Israel, and set me upon a very high mountain: upon which there was as the building of a city, bending towards the south.
3 Akanipeleka huko, nami nikamwona mtu ambaye kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwa shaba. Alikuwa amesimama kwenye lango akiwa na kamba ya kitani na ufito wa kupimia mkononi mwake.
And he brought me in thither, and behold a man, whose appearance was like the appearance of brass, with a line of flax in his hand, and a measuring reed in his hand, and he stood in the gate.
4 Mtu huyo akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa macho yako na usikie kwa masikio yako nawe uzingatie kitu nitakachokuonyesha, kwa kuwa ndiyo sababu umeletwa hapa. Iambie nyumba ya Israeli kila kitu utakachoona.”
And this man said to me: Son of man, see with thy eyes, and hear with thy ears, and set thy heart upon all that I shall shew thee: for thou art brought hither that they may be shewn to thee: declare all that thou seest, to the house of Israel.
5 Nikaona ukuta uliozunguka eneo lote la Hekalu. Ule ufito wa kupimia uliokuwa mkononi mwa yule mtu ulikuwa na urefu wa dhiraa ndefu sita, yaani, dhiraa ndefu ni sawa na dhiraa na nyanda nne, akapima ule ukuta. Ukuta huo ulikuwa na unene wa dhiraa ndefu sita na kimo cha dhiraa ndefu sita.
And behold there was a wall on the outside of the house round about, and in the man’s hand a measuring reed of six cubits and a handbreadth: and he measured the breadth of the building one reed, and the height one reed.
6 Kisha akaenda kwenye lango linaloelekea mashariki. Akapanda ngazi zake akapima kizingiti cha lango, nacho kilikuwa na kina cha huo ufito.
And he came to the gate that looked toward the east, and he went up the steps thereof: and he measured the breadth of the threshold of the gate one reed, that is, one threshold was one reed broad:
7 Vyumba vya kupumzikia vya walinzi vilikuwa na urefu wa huo ufito mmoja na upana wa huo ufito, kuta zilizogawa vyumba hivyo vya mapumziko zilikuwa na unene wa dhiraa tano. Nacho kizingiti cha lango lililokuwa karibu na ukumbi unaoelekea hekaluni ulikuwa na kina cha huo ufito.
And every little chamber was one reed long, and one reed broad: and between the little chambers were five cubits:
8 Kisha akapima baraza ya njia ya lango,
And the threshold of the gate by the porch of the gate within, was one reed.
9 ambayo ilikuwa na kina cha dhiraa nane na miimo yake ilikuwa na unene wa dhiraa mbili. Baraza ya lango ilielekea Hekalu.
And he measured the porch of the gate eight cubits, and the front thereof two cubits: and the porch of the gate was inward.
10 Ndani ya lango la mashariki kulikuwepo vyumba vitatu vya kupumzikia kila upande, vyote vitatu vilikuwa na vipimo vilivyo sawa, nazo nyuso za kuta zilizotenganisha kila upande zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
And the little chambers of the gate that looked eastward were three on this side, and three on that side: all three were of one measure, and the fronts of one measure, on both parts.
11 Kisha akapima upana wa ingilio la lango, ilikuwa dhiraa kumi na urefu wake ulikuwa dhiraa kumi na tatu.
And he measured the breadth of the threshold of the gate ten cubits: and the length of the gate thirteen cubits:
12 Mbele ya kila chumba cha kupumzikia kulikuwepo ukuta uliokuwa na kimo cha dhiraa moja kwenda juu, navyo hivyo vyumba vilikuwa dhiraa sita mraba.
And the border before the little chambers one cubit: and one cubit was the border on both sides: and the little chambers were six cubits on this side and that side.
13 Kisha akapima njia ya lango kuanzia juu ya ukuta wa nyuma wa chumba kimoja cha kupumzikia hadi juu ya ukuta wa nyuma wa chumba upande wa pili; kukawa na nafasi ya dhiraa ishirini na tano kuanzia lango la ukuta mmoja hadi lango la ukuta uliokuwa upande mwingine.
And he measured the gate from the roof of one little chamber to the roof of another, in breadth five and twenty cubits: door against door.
14 Akapima pia ukumbi, urefu wa dhiraa ishirini na lango linalofuatia hiyo nguzo kila upande wa huo ukumbi.
He made also fronts of sixty cubits: and to the front the court of the gate on every side round about.
15 Umbali kuanzia ingilio la njia ya lango hadi mwisho kabisa wa baraza yake ulikuwa dhiraa hamsini.
And before the face of the gate which reached even to the face of the porch of the inner gate, fifty cubits.
16 Kulikuwa na vidirisha kwenye hivyo vyumba vya walinzi na nguzo za hivyo vyumba zilikuwa kwenye mzunguko wa hilo lango, vivyo hivyo kulikuwa na madirisha yaliyozunguka kuelekeana na ua na juu ya kila nguzo kulikuwa na mapambo ya miti ya mitende.
And slanting windows in the little chambers, and in their fronts, which were within the gate on every side round about: and in like, manner there wore also in the porches windows round about within, and before the fronts the representation of palm trees.
17 Kisha akanileta katika ukumbi wa nje. Huko nikaona vyumba vingine pamoja na njia iliyokuwa imejengwa kuzunguka ukumbi wote, kulikuwa na vyumba thelathini vimepangana kando ya hiyo njia.
And he brought me into the outward court, and behold there were chambers, and a pavement of stone in the court round about: thirty chambers encompassed the pavement.
18 Njia hii iliyojengwa iliambaa na lango, ikiwa na urefu sawa na lango, hii ilikuwa ni njia ya chini.
And the pavement in the front of the gates according to the length of the gates was lower.
19 Kisha akapima umbali kutoka ndani ya lango la chini mpaka nje ya ukumbi wa ndani, nao ulikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki na dhiraa mia moja upande wa kaskazini.
And he measured the breadth from the face of the lower gate to the front of the inner court without, a hundred cubits to the east, and to the north.
20 Kisha akapima urefu na upana wa lango linaloelekea kaskazini, kukabili ukumbi wa nje.
He measured also both the length and the breadth of the gate of the outward court, which looked northward.
21 Vyumba vyake vilikuwa vitatu kila upande, kuta zilizogawanya vyumba na baraza ilikuwa na vipimo sawa na zile kuta za lango la kwanza. Zilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
And the little chambers thereof three on this side, and three on that side: and the front thereof, and the porch thereof according to the measure of the former gate, fifty cubits long, and five and twenty cubits broad.
22 Madirisha yake, baraza yake na nakshi yake ya miti ya mitende vilikuwa na vipimo sawasawa na vile vya lango linaloelekea mashariki. Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo.
And the windows thereof, and the porch, and the gravings according to the measure of the gate that looked to the east, and they went up to it by seven steps, and a porch was before it.
23 Kulikuwa na lango kwenye ukumbi wa ndani lililoelekea lile lango la kaskazini, kama vile ilivyokuwa ule upande wa mashariki. Akapima kutoka lango moja hadi lile lililo mkabala nalo, lilikuwa dhiraa mia moja.
And the gate of the inner court was over against the gate of the north, and that of the ease: and he measured from gate to gate a hundred cubits.
24 Ndipo akaniongoza mpaka upande wa kusini, nami nikaona lango linaloelekea kusini. Akaipima miimo yake na baraza yake, navyo vilikuwa na vipimo sawa kama hivyo vingine.
And he brought me out to the way of the south, and behold the gate that looked to the south: and he measured the front thereof, and the porch thereof according to the former measures.
25 Lango na baraza yake vilikuwa na madirisha membamba pande zote, kama madirisha ya huko kwingine. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
And the windows thereof, and the porches round about, as the other windows: the length was fifty cubits, and the breadth five and twenty cubits.
26 Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo. Ilikuwa na nakshi za miti ya mitende kwenye kuta zilizogawanya vyumba kila upande.
And there were seven steps to go up to it: and a porch before the doors thereof: and there were graven palm trees, one on this side, and another on that side in the front thereof.
27 Ukumbi wa ndani pia ulikuwa na lango lililoelekea kusini. Naye akapima kutoka lango hili mpaka kwenye lango la nje upande wa kusini; ilikuwa dhiraa mia moja.
And there was a gate of the inner court towards the south: and he measured from gate to gate towards the south, a hundred cubits.
28 Kisha akanileta mpaka ukumbi wa ndani kwa kupitia lango la kusini, naye akapima lango la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine.
And he brought me into the inner court at the south gate: and he measured the gate according to the former measures.
29 Vyumba vyake, kuta zilizogawanya vyumba na ukumbi wake zilikuwa na vipimo sawasawa na zile nyingine. Hilo lango na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Navyo vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
The little chamber thereof, and the front thereof, and the porch thereof with the same measures: and the windows thereof, and the porch thereof round about it was fifty cubits in length, and five and twenty cubits in breadth.
30 (Baraza za malango zilizozunguka ukumbi wa ndani zilikuwa na upana wa dhiraa ishirini na tano na kina cha dhiraa tano.)
And the porch round about was five and twenty cubits long, and five cubits broad.
31 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
And the porch thereof to the outward court, and the palm trees thereof in the front: and there were eight steps to go up to It.
32 Kisha akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani ulioko upande wa mashariki, naye akalipima lango hilo, lilikuwa na vipimo vilivyo sawasawa na yale mengine.
And he brought me into the inner court by the way of the east: and he measured the gate according to the former measures.
33 Vyumba vyake, kuta zake na baraza yake vilikuwa na vipimo vilivyo sawa na vile vingine. Lile lango pamoja na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
The little chamber thereof, and the front thereof, and the porch thereof as before: and the windows thereof, and the porches thereof round about it was fifty cubits long, and five and twenty cubits broad.
34 Baraza yake ilielekea ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote. Kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
And the porch thereof, that is, of the outward court: and the graven palm trees in the front thereof on this side and on that side: and the going up thereof was by eight steps.
35 Kisha akanileta mpaka kwenye lango la kaskazini na kulipima. Lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine,
And he brought me into the gate that looked to the north: and he measured according to the former measures.
36 kama vile ilivyokuwa kwa vyumba, kuta zake na baraza yake, tena kulikuwa na madirisha pande zote. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
The little chamber thereof, and the front thereof, and the porch thereof, and the windows thereof round about it was fifty cubits long, and five and twenty cubits broad.
37 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
And the porch thereof looked to the outward court: and the graving of palm trees in the front thereof was on this side and on that side: and the going up to it was by eight steps.
38 Kulikuwa na chumba na mlango karibu na baraza katika kila njia ya ndani ya lango ambamo sadaka za kuteketezwa zilioshwa.
And at every chamber was a door in the forefronts of the gates: there they washed the holocaust.
39 Kwenye baraza ya lile lango kulikuwepo meza mbili kila upande, ambako sadaka za kuteketezwa, sadaka za dhambi na sadaka za hatia zilichinjiwa.
And in the porch of the gate were two tables on this side, and two tables on that side: that the holocaust, and the sin offering, and the trespass offering might be slain thereon.
40 Karibu na ukuta wa nje wa baraza ya lile lango karibu na ngazi kwenye ingilio kuelekea kaskazini kulikuwa na meza mbili, nako upande mwingine wa ngazi kulikuwepo na meza mbili.
And on the outward side, which goeth up to the entry of the gate that looketh toward the north, were two tables. and at the other side before the porch of the gate were two tables.
41 Kwa hiyo kulikuwa na meza nne upande mmoja wa lango na nyingine nne upande mwingine, zote zilikuwa meza nane, ambapo dhabihu zilichinjiwa.
Four tables were on this side, and four tables on that side: at the sides of the gate were eight tables, upon which they slew the victims.
42 Pia kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, kila meza ilikuwa na urefu wa dhiraa moja na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu na kimo cha dhiraa moja. Juu ya meza hizo viliwekwa vyombo vya kuchinjia sadaka za kuteketezwa na dhabihu nyingine mbalimbali.
And the four tables for the holocausts were made of square stones: one cubit and a half long, and one cubit and a half broad, and one cubit high: to lay the vessels upon, in which the holocaust and the victim is slain.
43 Kulikuwa na kulabu, urefu wake nyanda nne, zilikuwa zimeshikizwa ukutani pande zote. Meza zilikuwa kwa ajili ya nyama za sadaka.
And the borders of them were of one handbreadth, turned inwards round about: and upon the tables was the flesh of the offering.
44 Nje ya lango la ndani, kwenye ukumbi wa ndani, kulikuwa na vyumba viwili, kimoja upande wa lango la kaskazini nacho kilielekea kusini, kingine upande wa lango la kusini nacho kilielekea kaskazini.
And without the inner gate were the chambers of the singing men in the inner court, which was on the side of the gate that looketh to the north: and their prospect was towards the south, one at the side of the east gate, which looketh toward the north.
45 Akaniambia, “Chumba kinachoelekea upande wa kusini ni kwa ajili ya makuhani ambao wana usimamizi wa hekaluni,
And he said to me: This chamber, which looketh toward the south shall be for the priests that watch in the wards of the temple.
46 nacho chumba kinachoelekea upande wa kaskazini ni kwa ajili ya makuhani wenye usimamizi wa madhabahuni. Hawa ni wana wa Sadoki, ambao ndio Walawi pekee wanaoweza kumkaribia Bwana ili kuhudumu mbele zake.”
But the chamber that looketh towards the north shall be for the priests that watch over the ministry of the altar. These are the sons of Sadoc, who among the sons of Levi, come near to the Lord, to minister to him.
47 Ndipo alipopima ukumbi: nao ulikuwa mraba wa dhiraa mia moja urefu na upana. Madhabahu yalikuwa mbele ya Hekalu.
And he measured the court a hundred cubits long, and a hundred cubits broad foursquare: and the altar that was before the face of the temple.
48 Akanileta mpaka kwenye baraza ya Hekalu naye akaipima miimo ya hiyo baraza, nayo ilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande. Upana wa ingilio ulikuwa dhiraa kumi na nne na kuta zake zilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande.
And he brought me into the porch of the temple: and he measured the porch five cubits on this side, and five cubits on that side: and the breadth of the gate three cubits on this side, and three cubits on that side.
49 Baraza ilikuwa na dhiraa ishirini kwenda juu na dhiraa kumi na mbili kuanzia mbele hadi nyuma. Kulikuwa na ngazi kumi za kupandia huko, pia kulikuwa na nguzo kwa kila upande wa miimo.
And the length of the porch was twenty cubits, and the breadth eleven cubits, and there were eight, steps to go up to it. And there were pillars in the fronts: one on this side, and another on that side.

< Ezekieli 40 >