< Ezekieli 40 >

1 Katika mwaka wa ishirini na tano wa uhamisho wetu, mwanzoni mwa huo mwaka, siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya kuanguka kwa mji, siku hiyo hiyo mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanipeleka huko.
In the twenty-fifth year of our captivity, in the beginning of the year, on the tenth of the month, in the fourteenth year after that the city was smitten, on that same day the hand of Jehovah was upon me, and he brought me thither.
2 Nikiwa katika maono ya Mungu alinichukua mpaka nchi ya Israeli, naye akaniweka kwenye mlima mrefu sana, ambako upande wa kusini kulikuwepo baadhi ya majengo ambayo yalionekana kama mji.
In the visions of God brought he me into the land of Israel, and set me upon a very high mountain; and upon it was as the building of a city, on the south.
3 Akanipeleka huko, nami nikamwona mtu ambaye kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwa shaba. Alikuwa amesimama kwenye lango akiwa na kamba ya kitani na ufito wa kupimia mkononi mwake.
And he brought me thither, and behold, there was a man whose appearance was like the appearance of brass, with a flax-cord in his hand, and a measuring-reed; and he stood in the gate.
4 Mtu huyo akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa macho yako na usikie kwa masikio yako nawe uzingatie kitu nitakachokuonyesha, kwa kuwa ndiyo sababu umeletwa hapa. Iambie nyumba ya Israeli kila kitu utakachoona.”
And the man said unto me, Son of man, behold with thine eyes, and hear with thine ears, and set thy heart upon all that I shall shew thee; for in order that it might be shewn unto thee art thou brought hither. Declare to the house of Israel all that thou seest.
5 Nikaona ukuta uliozunguka eneo lote la Hekalu. Ule ufito wa kupimia uliokuwa mkononi mwa yule mtu ulikuwa na urefu wa dhiraa ndefu sita, yaani, dhiraa ndefu ni sawa na dhiraa na nyanda nne, akapima ule ukuta. Ukuta huo ulikuwa na unene wa dhiraa ndefu sita na kimo cha dhiraa ndefu sita.
And behold, there was a wall on the outside of the house round about, and in the man's hand a measuring-reed of six cubits, [each] of one cubit and a hand breadth. And he measured the breadth of the building, one reed; and the height, one reed.
6 Kisha akaenda kwenye lango linaloelekea mashariki. Akapanda ngazi zake akapima kizingiti cha lango, nacho kilikuwa na kina cha huo ufito.
And he came to the gate which looked toward the east, and went up its steps; and he measured the threshold of the gate, one reed broad; and the other threshold one reed broad.
7 Vyumba vya kupumzikia vya walinzi vilikuwa na urefu wa huo ufito mmoja na upana wa huo ufito, kuta zilizogawa vyumba hivyo vya mapumziko zilikuwa na unene wa dhiraa tano. Nacho kizingiti cha lango lililokuwa karibu na ukumbi unaoelekea hekaluni ulikuwa na kina cha huo ufito.
And [each] chamber was one reed long and one reed broad; and between the chambers were five cubits; and the threshold of the gate, beside the porch of the gate within, was one reed.
8 Kisha akapima baraza ya njia ya lango,
And he measured the porch of the gate within, one reed.
9 ambayo ilikuwa na kina cha dhiraa nane na miimo yake ilikuwa na unene wa dhiraa mbili. Baraza ya lango ilielekea Hekalu.
And he measured the porch of the gate, eight cubits; and the posts thereof, two cubits; and the porch of the gate was inward.
10 Ndani ya lango la mashariki kulikuwepo vyumba vitatu vya kupumzikia kila upande, vyote vitatu vilikuwa na vipimo vilivyo sawa, nazo nyuso za kuta zilizotenganisha kila upande zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
And the chambers of the gate which was toward the east were three on this side and three on that side: they three were of one measure; and the posts on this side and on that side had one measure.
11 Kisha akapima upana wa ingilio la lango, ilikuwa dhiraa kumi na urefu wake ulikuwa dhiraa kumi na tatu.
And he measured the breadth of the entry of the gate, ten cubits; [and] the length of the gate, thirteen cubits.
12 Mbele ya kila chumba cha kupumzikia kulikuwepo ukuta uliokuwa na kimo cha dhiraa moja kwenda juu, navyo hivyo vyumba vilikuwa dhiraa sita mraba.
And there was a border before the chambers of one cubit, and a border of one cubit on the other side; and the chambers were six cubits on this side, and six cubits on that side.
13 Kisha akapima njia ya lango kuanzia juu ya ukuta wa nyuma wa chumba kimoja cha kupumzikia hadi juu ya ukuta wa nyuma wa chumba upande wa pili; kukawa na nafasi ya dhiraa ishirini na tano kuanzia lango la ukuta mmoja hadi lango la ukuta uliokuwa upande mwingine.
And he measured the gate from the roof of [one] chamber to the roof [of the other], a breadth of five and twenty cubits, entry opposite entry.
14 Akapima pia ukumbi, urefu wa dhiraa ishirini na lango linalofuatia hiyo nguzo kila upande wa huo ukumbi.
And he made posts, sixty cubits, and by the post was the court of the gate round about.
15 Umbali kuanzia ingilio la njia ya lango hadi mwisho kabisa wa baraza yake ulikuwa dhiraa hamsini.
And from the front of the gate of the entrance unto the front of the porch of the inner gate were fifty cubits.
16 Kulikuwa na vidirisha kwenye hivyo vyumba vya walinzi na nguzo za hivyo vyumba zilikuwa kwenye mzunguko wa hilo lango, vivyo hivyo kulikuwa na madirisha yaliyozunguka kuelekeana na ua na juu ya kila nguzo kulikuwa na mapambo ya miti ya mitende.
And there were closed windows to the chambers, and to their posts within the gate round about, and likewise to the projections; and the windows round about were inward; and upon [each] post were palm-trees.
17 Kisha akanileta katika ukumbi wa nje. Huko nikaona vyumba vingine pamoja na njia iliyokuwa imejengwa kuzunguka ukumbi wote, kulikuwa na vyumba thelathini vimepangana kando ya hiyo njia.
And he brought me into the outer court, and behold, there were cells, and a pavement made for the court round about: thirty cells were upon the pavement.
18 Njia hii iliyojengwa iliambaa na lango, ikiwa na urefu sawa na lango, hii ilikuwa ni njia ya chini.
And the pavement was by the side of the gates, answering to the length of the gates, [namely] the lower pavement.
19 Kisha akapima umbali kutoka ndani ya lango la chini mpaka nje ya ukumbi wa ndani, nao ulikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki na dhiraa mia moja upande wa kaskazini.
And he measured the breadth from the front of the lower gate unto the front of the inner court outside, a hundred cubits eastward and northward.
20 Kisha akapima urefu na upana wa lango linaloelekea kaskazini, kukabili ukumbi wa nje.
And the gate of the outer court, that looked toward the north, he measured its length and its breadth.
21 Vyumba vyake vilikuwa vitatu kila upande, kuta zilizogawanya vyumba na baraza ilikuwa na vipimo sawa na zile kuta za lango la kwanza. Zilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
And its chambers were three on this side and three on that side; and its posts and its projections were according to the measure of the first gate: its length was fifty cubits, and breadth five and twenty cubits.
22 Madirisha yake, baraza yake na nakshi yake ya miti ya mitende vilikuwa na vipimo sawasawa na vile vya lango linaloelekea mashariki. Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo.
And its windows, and its projections, and its palm-trees were according to the measure of the gate that looked toward the east; and they went up to it by seven steps; and the projections thereof were before them.
23 Kulikuwa na lango kwenye ukumbi wa ndani lililoelekea lile lango la kaskazini, kama vile ilivyokuwa ule upande wa mashariki. Akapima kutoka lango moja hadi lile lililo mkabala nalo, lilikuwa dhiraa mia moja.
And the gate of the inner court was opposite to the gate toward the north, and toward the east; and he measured from gate to gate a hundred cubits.
24 Ndipo akaniongoza mpaka upande wa kusini, nami nikaona lango linaloelekea kusini. Akaipima miimo yake na baraza yake, navyo vilikuwa na vipimo sawa kama hivyo vingine.
And he brought me toward the south: and behold, there was a gate toward the south; and he measured its posts and its projections according to these measures.
25 Lango na baraza yake vilikuwa na madirisha membamba pande zote, kama madirisha ya huko kwingine. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
And there were windows to it and to its projections round about, like those windows: the length was fifty cubits, and the breadth five and twenty cubits.
26 Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo. Ilikuwa na nakshi za miti ya mitende kwenye kuta zilizogawanya vyumba kila upande.
And there were seven steps to go up to it; and its projections were before them; and it had palm-trees, one on this side and one on that side, upon its posts.
27 Ukumbi wa ndani pia ulikuwa na lango lililoelekea kusini. Naye akapima kutoka lango hili mpaka kwenye lango la nje upande wa kusini; ilikuwa dhiraa mia moja.
And there was a gate to the inner court toward the south; and he measured from gate to gate toward the south, a hundred cubits.
28 Kisha akanileta mpaka ukumbi wa ndani kwa kupitia lango la kusini, naye akapima lango la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine.
And he brought me into the inner court by the south gate; and he measured the south gate according to these measures:
29 Vyumba vyake, kuta zilizogawanya vyumba na ukumbi wake zilikuwa na vipimo sawasawa na zile nyingine. Hilo lango na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Navyo vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
and its chambers, and its posts, and its projections, according to these measures; and there were windows to it and to its projections round about: the length was fifty cubits, and the breadth twenty-five cubits.
30 (Baraza za malango zilizozunguka ukumbi wa ndani zilikuwa na upana wa dhiraa ishirini na tano na kina cha dhiraa tano.)
And there were projections round about, twenty-five cubits long, and five cubits broad.
31 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
And its projections were toward the outer court; and there were palm-trees upon its posts: and its ascent was [by] eight steps.
32 Kisha akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani ulioko upande wa mashariki, naye akalipima lango hilo, lilikuwa na vipimo vilivyo sawasawa na yale mengine.
And he brought me into the inner court toward the east; and he measured the gate according to these measures:
33 Vyumba vyake, kuta zake na baraza yake vilikuwa na vipimo vilivyo sawa na vile vingine. Lile lango pamoja na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
and its chambers, and its posts, and its projections, according to these measures; and there were windows to it and to its projections round about: the length was fifty cubits, and the breadth twenty-five cubits.
34 Baraza yake ilielekea ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote. Kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
And its projections were toward the outer court; and there were palm-trees upon its posts on this side and on that side: and its ascent was [by] eight steps.
35 Kisha akanileta mpaka kwenye lango la kaskazini na kulipima. Lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine,
And he brought me to the north gate, and he measured [it] according to these measures:
36 kama vile ilivyokuwa kwa vyumba, kuta zake na baraza yake, tena kulikuwa na madirisha pande zote. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
its chambers, its posts, and its projections; and there were windows to it round about: the length was fifty cubits, and the breadth twenty-five cubits.
37 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
And its posts were toward the outer court; and there were palm-trees upon its posts, on this side and on that side: and its ascent was [by] eight steps.
38 Kulikuwa na chumba na mlango karibu na baraza katika kila njia ya ndani ya lango ambamo sadaka za kuteketezwa zilioshwa.
And there was a cell and its entry by the posts of the gates; there they rinsed the burnt-offering.
39 Kwenye baraza ya lile lango kulikuwepo meza mbili kila upande, ambako sadaka za kuteketezwa, sadaka za dhambi na sadaka za hatia zilichinjiwa.
And in the porch of the gate were two tables on this side, and two tables on that side, to slay thereon the burnt-offering and the sin-offering and the trespass-offering.
40 Karibu na ukuta wa nje wa baraza ya lile lango karibu na ngazi kwenye ingilio kuelekea kaskazini kulikuwa na meza mbili, nako upande mwingine wa ngazi kulikuwepo na meza mbili.
And at the side without, at the ascent to the entry of the north gate, were two tables; and on the other side, which was at the porch of the gate, were two tables:
41 Kwa hiyo kulikuwa na meza nne upande mmoja wa lango na nyingine nne upande mwingine, zote zilikuwa meza nane, ambapo dhabihu zilichinjiwa.
four tables on this side, and four tables on that side, by the side of the gate, — eight tables, whereon they slew [the sacrifice],
42 Pia kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, kila meza ilikuwa na urefu wa dhiraa moja na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu na kimo cha dhiraa moja. Juu ya meza hizo viliwekwa vyombo vya kuchinjia sadaka za kuteketezwa na dhabihu nyingine mbalimbali.
— and at the ascent, four tables of hewn stone, of a cubit and a half long, and a cubit and a half broad, and one cubit high; whereon also they laid the instruments with which they slew the burnt-offering and the sacrifice.
43 Kulikuwa na kulabu, urefu wake nyanda nne, zilikuwa zimeshikizwa ukutani pande zote. Meza zilikuwa kwa ajili ya nyama za sadaka.
And the double hooks of a hand breadth were fastened round about within; and upon the tables [they put] the flesh of the offering.
44 Nje ya lango la ndani, kwenye ukumbi wa ndani, kulikuwa na vyumba viwili, kimoja upande wa lango la kaskazini nacho kilielekea kusini, kingine upande wa lango la kusini nacho kilielekea kaskazini.
And outside the inner gate were two cells in the inner court, one at the side of the north gate, and its front towards the south; the other was at the side of the south gate, the front towards the north.
45 Akaniambia, “Chumba kinachoelekea upande wa kusini ni kwa ajili ya makuhani ambao wana usimamizi wa hekaluni,
And he said unto me, This cell whose front is towards the south is for the priests, the keepers of the charge of the house.
46 nacho chumba kinachoelekea upande wa kaskazini ni kwa ajili ya makuhani wenye usimamizi wa madhabahuni. Hawa ni wana wa Sadoki, ambao ndio Walawi pekee wanaoweza kumkaribia Bwana ili kuhudumu mbele zake.”
And the cell whose front is toward the north is for the priests, the keepers of the charge of the altar. These are the sons of Zadok, those who, from among the sons of Levi, approach unto Jehovah to minister unto him.
47 Ndipo alipopima ukumbi: nao ulikuwa mraba wa dhiraa mia moja urefu na upana. Madhabahu yalikuwa mbele ya Hekalu.
And he measured the court, the length a hundred cubits, and the breadth a hundred cubits, four square: and the altar was before the house.
48 Akanileta mpaka kwenye baraza ya Hekalu naye akaipima miimo ya hiyo baraza, nayo ilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande. Upana wa ingilio ulikuwa dhiraa kumi na nne na kuta zake zilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande.
And he brought me to the porch of the house; and he measured the post of the porch, five cubits on this side, and five cubits on that side; and the breadth of the gate, three cubits on this side, and three cubits on that side.
49 Baraza ilikuwa na dhiraa ishirini kwenda juu na dhiraa kumi na mbili kuanzia mbele hadi nyuma. Kulikuwa na ngazi kumi za kupandia huko, pia kulikuwa na nguzo kwa kila upande wa miimo.
The length of the porch was twenty cubits, and the breadth eleven cubits, even by the steps whereby they went up to it; and there were pillars by the posts, one on this side, and one on that side.

< Ezekieli 40 >