< Ezekieli 40 >

1 Katika mwaka wa ishirini na tano wa uhamisho wetu, mwanzoni mwa huo mwaka, siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya kuanguka kwa mji, siku hiyo hiyo mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanipeleka huko.
В двадесет и петата година от плена ни, в началото на годината, на десетия ден от месеца, в четиринадесетата година подир превземането на града, в същия ден Господната ръка биде върху мене и ме заведе там,
2 Nikiwa katika maono ya Mungu alinichukua mpaka nchi ya Israeli, naye akaniweka kwenye mlima mrefu sana, ambako upande wa kusini kulikuwepo baadhi ya majengo ambayo yalionekana kama mji.
чрез Божии видения ме заведе в Израилевата земя, та ме постави върху една твърде висока планина, на която имаше към юг нещо като здание подобно на град.
3 Akanipeleka huko, nami nikamwona mtu ambaye kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwa shaba. Alikuwa amesimama kwenye lango akiwa na kamba ya kitani na ufito wa kupimia mkononi mwake.
И като ме заведе там, ето, човек, чийто изглед бе като изглед на мед, и който държеше в ръката си ленена връв и мярка от тръстика, стоеше в портата.
4 Mtu huyo akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa macho yako na usikie kwa masikio yako nawe uzingatie kitu nitakachokuonyesha, kwa kuwa ndiyo sababu umeletwa hapa. Iambie nyumba ya Israeli kila kitu utakachoona.”
И човекът ми рече: Сине човешки, погледни с очите си, чуй с ушите си, и приложи сърцето си върху всичко, което ще ти покажа; защото ти биде въведен тука с цел да ти покажа това. Всичко, що видиш, изяви го на Израилевия дом.
5 Nikaona ukuta uliozunguka eneo lote la Hekalu. Ule ufito wa kupimia uliokuwa mkononi mwa yule mtu ulikuwa na urefu wa dhiraa ndefu sita, yaani, dhiraa ndefu ni sawa na dhiraa na nyanda nne, akapima ule ukuta. Ukuta huo ulikuwa na unene wa dhiraa ndefu sita na kimo cha dhiraa ndefu sita.
И ето извън дома една стена околовръст, и в ръката на човека мярка от тръстика дълга шест лакти, всеки лакът дълъг лакът и длан; и като измери широчината на зданието, тя беше една тръстика, и височината една тръстика.
6 Kisha akaenda kwenye lango linaloelekea mashariki. Akapanda ngazi zake akapima kizingiti cha lango, nacho kilikuwa na kina cha huo ufito.
Тогава дойде при портата, която гледаше към изток, и се изкачи по стъпалата й; и като измери прага на портата, широчината му беше една тръстика, и широчината на другия праг една тръстика.
7 Vyumba vya kupumzikia vya walinzi vilikuwa na urefu wa huo ufito mmoja na upana wa huo ufito, kuta zilizogawa vyumba hivyo vya mapumziko zilikuwa na unene wa dhiraa tano. Nacho kizingiti cha lango lililokuwa karibu na ukumbi unaoelekea hekaluni ulikuwa na kina cha huo ufito.
И всяка стражарска стая бе една тръстика дълга и една тръстика широка; и разстоянието между стаите бе пет лакти; а прагът на портата, при предверието на портата към дома, бе една тръстика.
8 Kisha akapima baraza ya njia ya lango,
Измери тоже предверието на портата към дома, една тръстика.
9 ambayo ilikuwa na kina cha dhiraa nane na miimo yake ilikuwa na unene wa dhiraa mbili. Baraza ya lango ilielekea Hekalu.
Тогава като измери предверието на портата, то беше осем лакти, а стълбовете им два лакътя; и предверието на портата беше откъм дома.
10 Ndani ya lango la mashariki kulikuwepo vyumba vitatu vya kupumzikia kila upande, vyote vitatu vilikuwa na vipimo vilivyo sawa, nazo nyuso za kuta zilizotenganisha kila upande zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
И стражарските стаи на източната порта бяха три отсам и три оттам, и трите на една мярка; и стълбовете имаха една мярка отсам и оттам.
11 Kisha akapima upana wa ingilio la lango, ilikuwa dhiraa kumi na urefu wake ulikuwa dhiraa kumi na tatu.
И като измери широчината на входа на портата, тя беше десет лакти, а дължината на портата тринадесет лакти.
12 Mbele ya kila chumba cha kupumzikia kulikuwepo ukuta uliokuwa na kimo cha dhiraa moja kwenda juu, navyo hivyo vyumba vilikuwa dhiraa sita mraba.
А пред стаите имаше един лакът разстояние отсам и един лакът разстояние оттам; и стаите бяха шест лакти отсам и шест лакти оттам.
13 Kisha akapima njia ya lango kuanzia juu ya ukuta wa nyuma wa chumba kimoja cha kupumzikia hadi juu ya ukuta wa nyuma wa chumba upande wa pili; kukawa na nafasi ya dhiraa ishirini na tano kuanzia lango la ukuta mmoja hadi lango la ukuta uliokuwa upande mwingine.
После измери портата от покрива на едната стражарска стая до покрива на другата, и широчината бе двадесет и пет лакти, врата срещу врата.
14 Akapima pia ukumbi, urefu wa dhiraa ishirini na lango linalofuatia hiyo nguzo kila upande wa huo ukumbi.
И намери стълбовете шестдесет лакти; и предверието стигаше до стълбовете околовръст портата.
15 Umbali kuanzia ingilio la njia ya lango hadi mwisho kabisa wa baraza yake ulikuwa dhiraa hamsini.
И от лицето на портата, при входа, до лицето на предверието на вътрешната порта, имаше петдесет лакти.
16 Kulikuwa na vidirisha kwenye hivyo vyumba vya walinzi na nguzo za hivyo vyumba zilikuwa kwenye mzunguko wa hilo lango, vivyo hivyo kulikuwa na madirisha yaliyozunguka kuelekeana na ua na juu ya kila nguzo kulikuwa na mapambo ya miti ya mitende.
И на стражарските стаи имаше затворени прозорци, също и на стълбовете им извътре портата околовръст, така и на сводовете; а имаше прозорци извътре околовръст; а върху всеки стълб имаше палми.
17 Kisha akanileta katika ukumbi wa nje. Huko nikaona vyumba vingine pamoja na njia iliyokuwa imejengwa kuzunguka ukumbi wote, kulikuwa na vyumba thelathini vimepangana kando ya hiyo njia.
Тогава ме заведе във външния двор; и ето стаи и под направени около двора; имаше тридесет стаи върху пода.
18 Njia hii iliyojengwa iliambaa na lango, ikiwa na urefu sawa na lango, hii ilikuwa ni njia ya chini.
И подът, който бе от страните на портата, съответстващ на дължината на портите, беше долният под.
19 Kisha akapima umbali kutoka ndani ya lango la chini mpaka nje ya ukumbi wa ndani, nao ulikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki na dhiraa mia moja upande wa kaskazini.
Тогава измери широчината от лицето на долната порта до лицето на вътрешния двор извън, и тя беше сто лакти и откъм изток и откъм север.
20 Kisha akapima urefu na upana wa lango linaloelekea kaskazini, kukabili ukumbi wa nje.
И измери дължината и широчината на портата на външния двор, която гледаше към север.
21 Vyumba vyake vilikuwa vitatu kila upande, kuta zilizogawanya vyumba na baraza ilikuwa na vipimo sawa na zile kuta za lango la kwanza. Zilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
И стражарските стаи бяха три отсам и три оттам; а стълбовете й и сводовете й бяха според мярката на първата порта; дължината й беше петдесет лакти, и широчината й двадесет и пет лакти.
22 Madirisha yake, baraza yake na nakshi yake ya miti ya mitende vilikuwa na vipimo sawasawa na vile vya lango linaloelekea mashariki. Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo.
И прозорците й, и сводовете й, и палмите й бяха според мярката на портата, която гледа към изток; и изкачваха се към нея по седем стъпала; и сводовете й бяха пред нея.
23 Kulikuwa na lango kwenye ukumbi wa ndani lililoelekea lile lango la kaskazini, kama vile ilivyokuwa ule upande wa mashariki. Akapima kutoka lango moja hadi lile lililo mkabala nalo, lilikuwa dhiraa mia moja.
И портата на вътрешния двор бе срещу портата, която бе към север и към изток; и като измери от порта до порта, намери сто лакти.
24 Ndipo akaniongoza mpaka upande wa kusini, nami nikaona lango linaloelekea kusini. Akaipima miimo yake na baraza yake, navyo vilikuwa na vipimo sawa kama hivyo vingine.
И заведе ме към юг, и ето порта, която гледаше към юг; и като измери стълбовете й и сводовете й, те имаха същите мерки.
25 Lango na baraza yake vilikuwa na madirisha membamba pande zote, kama madirisha ya huko kwingine. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
И имаше прозорци на нея и на сводовете й околовръст, подобни на ония прозорци; дължината им беше петдесет лакти, и широчината двадесет и пет лакти.
26 Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo. Ilikuwa na nakshi za miti ya mitende kwenye kuta zilizogawanya vyumba kila upande.
И изкачваха се към нея по седем стъпала; и сводовете й бяха пред нея; и на стълбовете й имаше палми, една отсам и една оттам.
27 Ukumbi wa ndani pia ulikuwa na lango lililoelekea kusini. Naye akapima kutoka lango hili mpaka kwenye lango la nje upande wa kusini; ilikuwa dhiraa mia moja.
И във вътрешния двор имаше порта към юг; и като измери от порта до порта към юг, намери сто лакти.
28 Kisha akanileta mpaka ukumbi wa ndani kwa kupitia lango la kusini, naye akapima lango la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine.
Тогава ме заведе във вътрешния двор през южната порта; и като измери южната порта, тя имаше същите мерки,
29 Vyumba vyake, kuta zilizogawanya vyumba na ukumbi wake zilikuwa na vipimo sawasawa na zile nyingine. Hilo lango na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Navyo vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
и стражарските й стаи, и стълбовете й, и сводовете й имаха същите мерки; и на нея и на сводовете й имаше прозорци околовръст; дължината й беше петдесет лакти, а широчината й двадесет и пет лакти.
30 (Baraza za malango zilizozunguka ukumbi wa ndani zilikuwa na upana wa dhiraa ishirini na tano na kina cha dhiraa tano.)
И сводовете околовръст бяха двадесет и пет лакти дълги, и пет лакти широки.
31 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
И сводовете й бяха към външния двор; и имаше палми по стълбовете й; и изкачваха се към нея по осем стъпала.
32 Kisha akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani ulioko upande wa mashariki, naye akalipima lango hilo, lilikuwa na vipimo vilivyo sawasawa na yale mengine.
И заведе ме във вътрешния двор към изток; и като измери портата тя имаше същите мерки;
33 Vyumba vyake, kuta zake na baraza yake vilikuwa na vipimo vilivyo sawa na vile vingine. Lile lango pamoja na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
и стражарските й стаи, стълбовете й, и сводовете й имаха същите мерки; и на нея и на сводовете й имаше прозорци околовръст; а тя беше петдесет лакти дълга и двадесет и пет лакти широка.
34 Baraza yake ilielekea ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote. Kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
И сводовете й бяха към външния двор; и по стълбовете й имаше палми отсам и оттам; и изкачваха се към нея по осем стъпала.
35 Kisha akanileta mpaka kwenye lango la kaskazini na kulipima. Lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine,
И заведе ме при северната порта; и като я измери, тя имаше същите мерки,
36 kama vile ilivyokuwa kwa vyumba, kuta zake na baraza yake, tena kulikuwa na madirisha pande zote. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
както и стражарските й стаи, стълбовете й, и сводовете й; и на нея имаше прозорци околовръст; а тя беше петдесет лакти дълга и двадесет и пет лакти широка.
37 Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
И стълбовете й бяха към външния двор; и по стълбовете й имаше палми отсам и оттам; и изкачваха се към нея по осем стъпала.
38 Kulikuwa na chumba na mlango karibu na baraza katika kila njia ya ndani ya lango ambamo sadaka za kuteketezwa zilioshwa.
И имаше една стая, чиято врата беше при стълбовете на портата, гдето миеха всеизгарянето.
39 Kwenye baraza ya lile lango kulikuwepo meza mbili kila upande, ambako sadaka za kuteketezwa, sadaka za dhambi na sadaka za hatia zilichinjiwa.
И в предверието на портата имаше две, трапези отсам и две трапези оттам, на които да колят всеизгарянето, приноса за грях, и приноса за престъпление.
40 Karibu na ukuta wa nje wa baraza ya lile lango karibu na ngazi kwenye ingilio kuelekea kaskazini kulikuwa na meza mbili, nako upande mwingine wa ngazi kulikuwepo na meza mbili.
И на външната страна, при стъпалата към входа на северната порта, имаше две трапези; и на другата страна, която принадлежеше към предверието на портата, имаше две трапези.
41 Kwa hiyo kulikuwa na meza nne upande mmoja wa lango na nyingine nne upande mwingine, zote zilikuwa meza nane, ambapo dhabihu zilichinjiwa.
Четири трапези имаше отсам и четири трапези оттам при страните на портата; всичко осем трапези, на които колеха жертвите.
42 Pia kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, kila meza ilikuwa na urefu wa dhiraa moja na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu na kimo cha dhiraa moja. Juu ya meza hizo viliwekwa vyombo vya kuchinjia sadaka za kuteketezwa na dhabihu nyingine mbalimbali.
И четирите трапези за всеизгарянето бяха от дялан камък, един лакът и половина дълги, един лакът и половина широки, и един лакът високи; и на тях туряха оръдията, с които колеха всеизгарянето и жертвата.
43 Kulikuwa na kulabu, urefu wake nyanda nne, zilikuwa zimeshikizwa ukutani pande zote. Meza zilikuwa kwa ajili ya nyama za sadaka.
И извътре имаше полица, една длан широка, прикована околовръст; а на трапезите туряха месото на приносите.
44 Nje ya lango la ndani, kwenye ukumbi wa ndani, kulikuwa na vyumba viwili, kimoja upande wa lango la kaskazini nacho kilielekea kusini, kingine upande wa lango la kusini nacho kilielekea kaskazini.
И извън вътрешната порта бяха стаите на певците, във вътрешния двор, който бе на страните на северната порта; и лицата им бяха към юг; а една от тях, на страната на източната порта, гледаше към север.
45 Akaniambia, “Chumba kinachoelekea upande wa kusini ni kwa ajili ya makuhani ambao wana usimamizi wa hekaluni,
И рече ми: Тая стая, която гледа към юг, е за свещениците, които се грижат за дома;
46 nacho chumba kinachoelekea upande wa kaskazini ni kwa ajili ya makuhani wenye usimamizi wa madhabahuni. Hawa ni wana wa Sadoki, ambao ndio Walawi pekee wanaoweza kumkaribia Bwana ili kuhudumu mbele zake.”
а стаята, която гледа към север, е за свещениците, които прислужват около олтара; те са потомци на Садока, които измежду Левиевите потомци се приближават при Господа да Му служат.
47 Ndipo alipopima ukumbi: nao ulikuwa mraba wa dhiraa mia moja urefu na upana. Madhabahu yalikuwa mbele ya Hekalu.
И като измери двора, дължината му беше сто лакти, и широчината му сто лакти; беше квадратен, и олтарът беше пред дома.
48 Akanileta mpaka kwenye baraza ya Hekalu naye akaipima miimo ya hiyo baraza, nayo ilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande. Upana wa ingilio ulikuwa dhiraa kumi na nne na kuta zake zilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande.
Тогава ме заведе в предхрамието на дома; и като измери всеки стълб на предхрамието, те бяха пет лакти отсам и пет лакти оттам; а широчината на портата беше три лакти отсам и три лакти оттам.
49 Baraza ilikuwa na dhiraa ishirini kwenda juu na dhiraa kumi na mbili kuanzia mbele hadi nyuma. Kulikuwa na ngazi kumi za kupandia huko, pia kulikuwa na nguzo kwa kila upande wa miimo.
Дължината на предхрамието бе двадесет лакти, и широчината му единадесет лакти; и изкачваха се към него по десет стъпала; и при стълбовете имаше други стълбове, един отсам и един оттам.

< Ezekieli 40 >