< Ezekieli 4 >

1 “Mwanadamu, sasa chukua tofali, uliweke mbele yako na uchore juu yake ramani ya mji wa Yerusalemu.
خداوند فرمود: «ای پسر انسان، آجری بزرگ بگیر و در مقابل خود بگذار و نقش شهر اورشلیم را بر آن حک کن. دور شهر، برجها، سنگر، منجنیق و اردوگاه‌های دشمن را نقش کن تا نشان دهند که شهر در محاصره است.
2 Kisha uuzingire: Simamisha askari dhidi yake kuuzunguka, uzunguke kwa majeshi, weka kambi dhidi yake pande zote pamoja na magogo ya kubomolea boma vitani.
3 Kisha chukua bamba la chuma, ukalisimamishe liwe kama ukuta wa chuma kati yako na huo mji, nawe uuelekeze uso wako. Huo mji utakuwa katika hali ya kuzingirwa, nawe utauzingira. Hii itakuwa ishara kwa nyumba ya Israeli.
یک تابهٔ آهنی نیز بردار و مثل یک دیوار، بین خودت و تصویر شهر بگذار، تا نشان دهد که سپاه دشمن چگونه اورشلیم را با عزمی آهنین، محاصره خواهد کرد. «هر یک از این جزئیاتی که به تو گفتم، معنی بخصوصی دارد، زیرا تمام اینها اخطاری است به قوم اسرائیل.
4 “Kisha ulale kwa upande wako wa kushoto na uweke dhambi za nyumba ya Israeli juu yake. Utazibeba dhambi zao kwa idadi ya siku utakazolala kwa huo upande mmoja.
«آنگاه بر پهلوی چپ خود دراز بکش و برای مدت سیصد و نود روز در همان حال بمان. من گناه اسرائیل را بر تو می‌گذارم و در طول این مدت برای گناه آنان، متحمل رنج خواهی شد. برای هر سال مجازات اسرائیل، یک روز دراز خواهی کشید.
5 Nimekupangia idadi ya siku kama miaka ya dhambi yao. Kwa hiyo kwa siku 390 utabeba dhambi za nyumba ya Israeli.
6 “Baada ya kumaliza hili, lala chini tena, wakati huu ulale chini kwa upande wa kuume, uchukue dhambi za nyumba ya Yuda. Nimekupangia siku arobaini, siku moja kwa kila mwaka mmoja.
بعد از این مدت، برگرد و چهل روز بر پهلوی راست خود بخواب و برای گناهان یهودا متحمل رنج شو. برای هر سال مجازات یهودا یک روز دراز خواهی کشید.
7 Geuza uso wako uelekeze kwenye kuzingirwa kwa Yerusalemu na mkono wako ambao haukuvikwa nguo tabiri dhidi yake.
«ضمن نمایش محاصرهٔ اورشلیم، آستینت را بالا بزن و با مشت گره کرده، کلام مرا بر ضد آن اعلام نما.
8 Nitakufunga kwa kamba ili usiweze kugeuka kutoka upande mmoja hadi upande mwingine, mpaka hapo utakapokuwa umetimiza siku za kuzingirwa kwako.
تو را با طناب می‌بندم تا نتوانی از یک پهلو به پهلوی دیگر برگردی، تا اینکه روزهای محاصره خاتمه یابد.
9 “Chukua ngano na shayiri, maharagwe na dengu, mtama na mawele, uviweke na kuvihifadhi vyote kwenye gudulia la kuhifadhia, na uvitumie kujitengenezea mkate. Utaula mkate huo kwa hizo siku 390 utakazokuwa umelala kwa upande mmoja.
«در طی آن سیصد و نود روز اول که بر پهلوی چپت می‌خوابی، خوراک تو، نانی تهیه شده از آرد گندم، جو، باقلا، عدس و ارزن باشد. آنها را در یک ظرف با هم مخلوط کن و از آن، نان بپز.
10 Pima shekeli ishirini za chakula utakachokula kwa kila siku, nawe utakula kwa wakati uliopangwa.
نان را جیره‌بندی خواهی کرد و هر روز یک وعده از آن را خواهی خورد، آن هم نه بیشتر از بیست مثقال!
11 Pia pima maji moja ya sita ya hini, nawe utakunywa kwa wakati uliopangwa.
روزی دو لیوان آب نیز بیشتر نخواهی نوشید!
12 Nawe utakula chakula kama vile ambavyo ungekula mkate wa shayiri, uoke mkate mbele ya macho ya watu, ukitumia kinyesi cha mwanadamu.”
برای پختن نان، آتش را با مدفوع خشک شدهٔ انسان درست خواهی کرد و این کار را در برابر چشمان مردم انجام خواهی داد.
13 Bwana akasema, “Hivi ndivyo watu wa Israeli watakavyokula chakula kilicho najisi miongoni mwa mataifa ninakowapeleka.”
به همین منوال قوم اسرائیل، در سرزمینهایی که تبعیدشان می‌کنم، نان نجس و حرام خواهند خورد.»
14 Ndipo nikasema, “Sivyo Bwana Mwenyezi! Kamwe mimi sijajitia unajisi. Tangu ujana wangu hadi sasa sijala kamwe kitu chochote kilichokufa au kilichoraruliwa na wanyama wa mwituni. Hakuna nyama yeyote najisi iliyoingia kinywani mwangu.”
گفتم: «آه، ای خداوند یهوه، چگونه چنین کاری بکنم؟ من در تمام عمرم هرگز نجس نشده‌ام. از جوانی تا به حال هرگز نه گوشت حرام خورده‌ام، نه گوشت حیواناتی که به‌وسیلۀ جانوران، دریده شده باشد و نه گوشت حیوانات مردار. من به هیچ وجه خوراک حرام نخورده‌ام.»
15 Akasema, “Vema sana, basi nitakuruhusu uoke mkate wako kwa kutumia kinyesi cha ngʼombe badala ya kinyesi cha mwanadamu.”
خداوند فرمود: «بسیار خوب، به جای مدفوع انسان، می‌توانی از مدفوع گاو استفاده کنی.»
16 Ndipo Mungu akaniambia, “Mwanadamu, mimi nitakatilia mbali upatikanaji wa chakula katika Yerusalemu. Watu watakula chakula cha kupimwa kwa wasiwasi pamoja na maji ya kupimiwa kwa kukata tamaa,
آنگاه خداوند فرمود: «ای پسر انسان، من نان را از اورشلیم قطع خواهم نمود! مردم با دقت زیاد نان و آب را جیره‌بندی خواهند کرد و با ترس و لرز، ذره‌ذره خواهند خورد.
17 kwa kuwa chakula na maji vitakuwa adimu. Watastajabiana kila mmoja, nao watadhoofika kwa sababu ya dhambi yao.
بله، مردم اورشلیم محتاج نان و آب خواهند شد. ایشان با ترس و لرز به یکدیگر نگاه خواهند کرد و زیر بار مجازات گناهانشان، هلاک خواهند گشت.»

< Ezekieli 4 >