< Ezekieli 39 >
1 “Mwanadamu, tabiri dhidi ya Gogu useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali.
Toi donc, fils de l'homme, prophétise contre Gog et dis: Ainsi parle le Seigneur, l'Éternel: J'en veux à toi, Gog, prince de Rosch, Mésech et Thubal!
2 Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukuburuta. Nitakuleta kutoka kaskazini ya mbali na kukupeleka wewe dhidi ya milima ya Israeli.
Je te détournerai et t'entraînerai, et te tirerai du fond du nord, et t'amènerai sur les montagnes d'Israël.
3 Kisha nitaupiga upinde wako kutoka mkono wako wa kushoto na kuifanya mishale ianguke kutoka mkono wako wa kuume.
Et j'arracherai ton arc de ta main gauche, et ferai tomber tes flèches de ta main droite;
4 Utaanguka kwenye milima ya Israeli, wewe pamoja na vikosi vyako vyote na yale mataifa yaliyo pamoja nawe. Nitakutoa uwe chakula cha ndege wa aina zote walao nyama na cha wanyama wa mwituni.
sur les montagnes d'Israël tu succomberas, toi et tous tes bataillons, et les peuples qui sont avec toi; des vautours, de tous les oiseaux et des bêtes des champs je te ferai la pâture;
5 Utaanguka katika uwanja, kwa kuwa nimenena, asema Bwana Mwenyezi.
sur la face de la terre tu tomberas, car j'ai parlé, dit le Seigneur, l'Éternel.
6 Nitatuma moto juu ya Magogu na kwa wale wanaoishi kwa salama huko pwani, nao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana.
Et je darderai un feu en Magog et sur ceux qui habitent les îles en sécurité, afin qu'ils sachent que je suis l'Éternel.
7 “‘Nitalifanya Jina langu takatifu lijulikane miongoni mwa watu wangu Israeli. Sitaliacha tena Jina langu takatifu litiwe unajisi, nayo mataifa watajua kuwa Mimi Bwana ndimi Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Et je manifesterai mon saint nom au milieu de mon peuple d'Israël, et n'exposerai plus mon saint nom au déshonneur; mais les nations reconnaîtront que je suis l'Éternel, le Saint d'Israël.
8 Hili jambo linakuja! Hakika litatokea, asema Bwana Mwenyezi. Hii ndiyo siku ile niliyosema habari zake.
Voici, il vient, il arrive, dit le Seigneur, l'Éternel, ce jour que j'ai dit.
9 “‘Ndipo wale wanaoishi katika miji ya Israeli watakapotoka na kutumia hizo silaha kuwashia moto na kuziteketeza, yaani, kigao na ngao, pinde na mishale, rungu za vita na mikuki. Kwa miaka saba watavitumia kama kuni.
Alors les habitants des villes d'Israël sortiront et allumeront et brûleront les armes et les boucliers et les pavois, les arcs et les flèches, les épieux et les lances, et s'en feront du feu pendant sept années.
10 Hawatahitaji kukusanya kuni kutoka mashambani wala kukata kuni kutoka kwenye misitu, kwa sababu watatumia silaha kuwa kuni. Nao watawateka mateka wale waliowateka na kuchukua nyara mali za wale waliochukua mali zao nyara, asema Bwana Mwenyezi.
Ils n'iront point chercher du bois dans la campagne, ni en couper dans les forêts, car c'est avec les armes qu'ils nourriront leur feu: et ils dépouilleront ceux qui les auront dépouillés, et pilleront ceux qui les auront pillés, dit le Seigneur, l'Éternel.
11 “‘Siku ile nitampa Gogu mahali pa kuzikia katika Israeli, katika bonde la wale wasafirio upande wa mashariki kuelekea baharini. Jambo hili litazuia njia ya wasafiri kwa sababu Gogu na makundi yake yote ya wajeuri watazikwa huko. Kwa hiyo litaitwa Bonde la Hamon-Gogu.
Et dans ce même jour je donnerai là à Gog un lieu pour son tombeau en Israël, la vallée des voyageurs, à l'orient de la mer; et cela fermera le passage aux voyageurs; c'est là qu'on enterrera Gog et toute sa multitude, et on la nommera Vallée de la multitude de Gog.
12 “‘Kwa miezi saba nyumba ya Israeli itakuwa ikiwazika ili kuisafisha nchi.
Et la maison d'Israël les enterrera, afin de purifier le pays, durant sept mois;
13 Watu wote wa nchi watawazika, nayo siku nitakayotukuzwa itakuwa siku ya kumbukumbu kwa ajili yao, asema Bwana Mwenyezi.
et tout le peuple du pays enterrera; et cela lui donnera un nom au jour où je me glorifierai, dit le Seigneur, l'Éternel.
14 “‘Watu wataajiriwa mara kwa mara kuisafisha nchi. Baadhi yao watapita nchini kote na zaidi yao hao wengine, watawazika wale waliosalia juu ya uso wa nchi. Mwisho wa hiyo miezi saba wataanza upekuzi wao.
Et ils choisiront des hommes en permanence dont les uns parcourront le pays, et les autres à leur suite enterreront les corps restés sur la face du pays, afin de le purifier; pendant sept mois entiers ils feront cette recherche.
15 Wakati wanapopita nchini kote na mmoja wao akaona mfupa wa mwanadamu, ataweka alama kando yake mpaka wachimba kaburi wawe wameuzika katika Bonde la Hamon-Gogu.
Et les premiers parcourront le pays; et si l'un d'eux aperçoit les ossements d'un homme, il élèvera à côté un cippe, en attendant que les fossoyeurs l'enterrent dans la vallée de la multitude de Gog.
16 (Pia mji uitwao Hamona utakuwa humo.) Hivyo ndivyo watakavyoisafisha nchi.’
Hamona sera aussi le nom d'une ville. Et c'est ainsi qu'ils purifieront le pays.
17 “Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ita kila aina ya ndege na wanyama wote wa mwituni, waambie: ‘Kusanyikeni mje pamoja kutoka pande zote kwa ajili ya dhabihu ninayowaandalia, dhabihu kuu katika milima ya Israeli. Huko mtakula nyama na kunywa damu.
Or, fils de l'homme, ainsi parle le Seigneur, l'Éternel: Dis aux oiseaux, à tous les volatiles et à toutes les bêtes des champs: Rassemblez-vous et venez, réunissez-vous de toutes parts pour le sacrifice où je vais égorger des victimes pour vous, grand sacrifice sur les montagnes d'Israël, et repaissez-vous de chair et abreuvez-vous de sang!
18 Mtakula nyama za watu mashujaa na kunywa damu za wakuu wa dunia kana kwamba ni za kondoo dume na kondoo wake, mbuzi na mafahali, wote walionona kutoka Bashani.
C'est de la chair des héros que vous y serez nourris, et du sang des princes de la terre que vous boirez; ce sont tout autant de béliers, d'agneaux et de boucs, de taureaux engraissés en Basan.
19 Katika dhabihu ninayoandaa kwa ajili yenu, mtakula mafuta mpaka mkinai na kunywa damu mpaka mlewe.
Et vous mangerez de la graisse, à vous rassasier, et vous boirez du sang, à vous enivrer, au sacrifice où pour vous j'égorgerai des victimes;
20 Kwenye meza yangu watajishibisha kwa farasi na wapanda farasi, watu mashujaa na askari wa kila aina,’ asema Bwana Mwenyezi.
et à ma table vous vous rassasierez de chevaux et de cavaliers, de héros et de toutes sortes d'hommes de guerre, dit le Seigneur, l'Éternel.
21 “Nitauonyesha utukufu wangu miongoni mwa mataifa, nayo mataifa yote wataiona adhabu nitakayotoa na mkono wangu nitakaouweka juu yao.
Et je manifesterai ma gloire parmi les nations, et toutes les nations seront témoins du jugement que j'exercerai, et des coups dont les frappera ma main;
22 Kuanzia siku ile na kuendelea nyumba ya Israeli itajua kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wao.
et toute la maison d'Israël comprendra que moi, l'Éternel, je suis son Dieu, dès ce jour-là et à l'avenir;
23 Na mataifa watajua kuwa nyumba ya Israeli walikwenda utumwani kwa ajili ya dhambi yao, kwa sababu hawakuwa waaminifu kwangu. Hivyo niliwaficha uso wangu na kuwatia mikononi mwa adui zao, nao wote wakaanguka kwa upanga.
et les nations comprendront que c'est par suite de son crime que la maison d'Israël a été déportée, parce qu'ils furent coupables envers moi, et que je leur cachai ma face, et que je les livrai à la main de leurs ennemis, afin que par l'épée ils périssent tous.
24 Niliwatendea sawasawa na uchafu wao na makosa yao, nami nikawaficha uso wangu.
Je les ai traités selon leur souillure et leur désobéissance, et je leur ai caché ma face.
25 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Sasa nitamrudisha Yakobo kutoka utumwani, nami nitawahurumia watu wote wa Israeli, nami nitakuwa na wivu kwa ajili ya Jina langu takatifu.
Aussi, ainsi parle le Seigneur, l'Éternel: Maintenant je veux ramener les captifs de Jacob, et prendre pitié de toute la maison d'Israël, et être jaloux de mon saint nom.
26 Wataisahau aibu yao na jinsi walivyoonyesha kutokuwa waaminifu kwangu mimi wakati waliishi salama katika nchi yao, bila kuwa na mtu yeyote wa kuwatia hofu.
Alors ils comprendront quel fut leur opprobre et tout le crime qu'ils ont commis contre moi, lorsqu'ils habiteront leur pays en sécurité, sans terreur aucune,
27 Nitakapokuwa nimewarudisha kutoka mataifa na kuwakusanya kutoka nchi za adui zao, mimi nitajionyesha kuwa mtakatifu kwa kupitia kwao machoni mwa mataifa mengi.
lorsque je les ramènerai du milieu des peuples, et les recueillerai des pays de leurs ennemis, et que je manifesterai ma sainteté sur eux au milieu de peuples nombreux.
28 Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana, Mungu wao, ingawa niliwapeleka uhamishoni miongoni mwa mataifa, nitawakusanya tena katika nchi yao wenyewe, bila kumwacha yeyote nyuma.
Alors ils reconnaîtront que moi, l'Éternel, je suis leur Dieu, quand, après les avoir envoyés captifs aux nations, je les réunirai dans leur pays, sans laisser aucun d'eux là au milieu d'elles;
29 Sitawaficha tena uso wangu, kwa maana nitamimina Roho wangu juu ya nyumba ya Israeli, asema Bwana Mwenyezi.”
et je ne leur cacherai plus ma face, parce que j'aurai répandu mon Esprit sur la maison d'Israël, dit le Seigneur, l'Éternel.