< Ezekieli 39 >

1 “Mwanadamu, tabiri dhidi ya Gogu useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali.
Toi donc, fils d'homme, prophétise contre Gog, et dis: ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: voici, j'en veux à toi, Gog, Prince des chefs de Mésec et de Tubal.
2 Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukuburuta. Nitakuleta kutoka kaskazini ya mbali na kukupeleka wewe dhidi ya milima ya Israeli.
Et je te ferai retourner en arrière, n'en laissant que de six l'un, après t'avoir fait monter du fond de l'Aquilon, et t'avoir fait venir sur les montagnes d'Israël.
3 Kisha nitaupiga upinde wako kutoka mkono wako wa kushoto na kuifanya mishale ianguke kutoka mkono wako wa kuume.
Car je romprai ton arc dans ta main gauche, et je ferai tomber tes flèches de ta main droite.
4 Utaanguka kwenye milima ya Israeli, wewe pamoja na vikosi vyako vyote na yale mataifa yaliyo pamoja nawe. Nitakutoa uwe chakula cha ndege wa aina zote walao nyama na cha wanyama wa mwituni.
Tu tomberas sur les montagnes d'Israël, toi et toutes tes troupes, et les peuples qui seront avec toi; je t'ai livré aux oiseaux de proie entre tous les oiseaux, et aux bêtes des champs, pour en être dévoré.
5 Utaanguka katika uwanja, kwa kuwa nimenena, asema Bwana Mwenyezi.
Tu tomberas sur le dessus des champs, parce que j'ai parlé, dit le Seigneur l'Eternel.
6 Nitatuma moto juu ya Magogu na kwa wale wanaoishi kwa salama huko pwani, nao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana.
Et je mettrai le feu en Magog, et parmi ceux qui demeurent en assurance dans les Iles; et ils sauront que je suis l'Eternel.
7 “‘Nitalifanya Jina langu takatifu lijulikane miongoni mwa watu wangu Israeli. Sitaliacha tena Jina langu takatifu litiwe unajisi, nayo mataifa watajua kuwa Mimi Bwana ndimi Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Et je ferai connaître le Nom de ma Sainteté au milieu de mon peuple d'Israël; et je ne profanerai plus le Nom de ma Sainteté; les nations sauront que je suis l'Eternel, le Saint en Israël.
8 Hili jambo linakuja! Hakika litatokea, asema Bwana Mwenyezi. Hii ndiyo siku ile niliyosema habari zake.
Voici cela est arrivé, et a été fait, dit le Seigneur l'Eternel; c'est ici la journée dont j'ai parlé.
9 “‘Ndipo wale wanaoishi katika miji ya Israeli watakapotoka na kutumia hizo silaha kuwashia moto na kuziteketeza, yaani, kigao na ngao, pinde na mishale, rungu za vita na mikuki. Kwa miaka saba watavitumia kama kuni.
Et les habitants des villes d'Israël sortiront, et allumeront le feu, et brûleront les armes, les boucliers, les écus, les arcs, les flèches, les bâtons qu'on lance de la main, et les javelots, et ils y tiendront le feu allumé sept ans durant.
10 Hawatahitaji kukusanya kuni kutoka mashambani wala kukata kuni kutoka kwenye misitu, kwa sababu watatumia silaha kuwa kuni. Nao watawateka mateka wale waliowateka na kuchukua nyara mali za wale waliochukua mali zao nyara, asema Bwana Mwenyezi.
Et on n'apportera point de bois des champs, et on n'en coupera point des forêts, parce qu'ils feront du feu de ces armes, lorsqu'ils butineront ceux qui les avaient butinés, et qu'ils pilleront ceux qui les avaient pillés, dit le Seigneur l'Eternel.
11 “‘Siku ile nitampa Gogu mahali pa kuzikia katika Israeli, katika bonde la wale wasafirio upande wa mashariki kuelekea baharini. Jambo hili litazuia njia ya wasafiri kwa sababu Gogu na makundi yake yote ya wajeuri watazikwa huko. Kwa hiyo litaitwa Bonde la Hamon-Gogu.
Et il arrivera en ce jour-là que je donnerai à Gog dans ces quartiers-là un lieu pour sépulcre en Israël, savoir la vallée des passants, qui est au devant de la mer, et d'étonnement elle réduira les passants au silence; on enterrera là Gog, et toute la multitude de son peuple, et on l'appellera, la vallée d'Hammon-Gog.
12 “‘Kwa miezi saba nyumba ya Israeli itakuwa ikiwazika ili kuisafisha nchi.
Et ceux de la maison d'Israël les enterreront pendant l'espace de sept mois pour purifier le pays.
13 Watu wote wa nchi watawazika, nayo siku nitakayotukuzwa itakuwa siku ya kumbukumbu kwa ajili yao, asema Bwana Mwenyezi.
Tout le peuple, dis-je, du pays les enterrera, et cela leur sera un nom, [savoir] le jour auquel j'aurai été glorifié, dit le Seigneur l'Eternel.
14 “‘Watu wataajiriwa mara kwa mara kuisafisha nchi. Baadhi yao watapita nchini kote na zaidi yao hao wengine, watawazika wale waliosalia juu ya uso wa nchi. Mwisho wa hiyo miezi saba wataanza upekuzi wao.
Et ils mettront à part des gens qui ne feront autre chose que parcourir le pays, lesquels avec les passants enterreront ceux qui seront demeurés de reste sur le dessus de la terre, pour la purifier, [et] ils en chercheront jusques au bout de sept mois.
15 Wakati wanapopita nchini kote na mmoja wao akaona mfupa wa mwanadamu, ataweka alama kando yake mpaka wachimba kaburi wawe wameuzika katika Bonde la Hamon-Gogu.
Et ces passants-là iront par le pays, et celui qui verra l'os d'un homme, dressera auprès de lui un signal; jusqu'à ce que les enterreurs l'aient enterré dans la vallée d'Hammon-Gog.
16 (Pia mji uitwao Hamona utakuwa humo.) Hivyo ndivyo watakavyoisafisha nchi.’
Et aussi le nom de la ville sera Hamona, et on nettoiera le pays.
17 “Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ita kila aina ya ndege na wanyama wote wa mwituni, waambie: ‘Kusanyikeni mje pamoja kutoka pande zote kwa ajili ya dhabihu ninayowaandalia, dhabihu kuu katika milima ya Israeli. Huko mtakula nyama na kunywa damu.
Toi donc, fils d'homme, ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: dis aux oiseaux de toutes espèces, et à toutes les bêtes des champs: assemblez-vous et venez; amassez-vous de toutes parts vers mon sacrifice que je fais pour vous, [qui] est un grand sacrifice sur les montagnes d'Israël, vous mangerez de la chair, et vous boirez du sang.
18 Mtakula nyama za watu mashujaa na kunywa damu za wakuu wa dunia kana kwamba ni za kondoo dume na kondoo wake, mbuzi na mafahali, wote walionona kutoka Bashani.
Vous mangerez la chair des [hommes] forts, et vous boirez le sang des principaux de la terre, le sang des moutons, des agneaux, des boucs; et des veaux, tous grasses bêtes de Basan.
19 Katika dhabihu ninayoandaa kwa ajili yenu, mtakula mafuta mpaka mkinai na kunywa damu mpaka mlewe.
Vous mangerez de la graisse jusques à en être rassasiés, et vous boirez au sang jusqu'à en être ivres, [de la graisse, dis-je, et du sang] de mon sacrifice, que j'aurai sacrifié pour vous.
20 Kwenye meza yangu watajishibisha kwa farasi na wapanda farasi, watu mashujaa na askari wa kila aina,’ asema Bwana Mwenyezi.
Et vous serez rassasiés à ma table, de chevaux, et de bêtes d'attelage, d'hommes forts, et de tous hommes de guerre, dit le Seigneur l'Eternel.
21 “Nitauonyesha utukufu wangu miongoni mwa mataifa, nayo mataifa yote wataiona adhabu nitakayotoa na mkono wangu nitakaouweka juu yao.
Et je mettrai ma gloire entre les nations, et toutes les nations verront mon jugement que j'aurai exercé, et comment j'aurai mis ma main sur eux.
22 Kuanzia siku ile na kuendelea nyumba ya Israeli itajua kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wao.
Et la maison d'Israël connaîtra dès ce jour-là, et dans la suite, que je suis l'Eternel leur Dieu.
23 Na mataifa watajua kuwa nyumba ya Israeli walikwenda utumwani kwa ajili ya dhambi yao, kwa sababu hawakuwa waaminifu kwangu. Hivyo niliwaficha uso wangu na kuwatia mikononi mwa adui zao, nao wote wakaanguka kwa upanga.
Et les nations sauront que la maison d'Israël avait été transportée en captivité à cause de son iniquité, parce qu'ils avaient péché contre moi, et que je leur avais caché ma face, et les avais livrés entre les mains de leurs ennemis, tellement qu'ils étaient tous tombés par l'épée.
24 Niliwatendea sawasawa na uchafu wao na makosa yao, nami nikawaficha uso wangu.
Je leur avais fait selon leur souillure, et selon leur crime, et je leur avais caché ma face.
25 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Sasa nitamrudisha Yakobo kutoka utumwani, nami nitawahurumia watu wote wa Israeli, nami nitakuwa na wivu kwa ajili ya Jina langu takatifu.
C'est pourquoi ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: maintenant je ramènerai la captivité de Jacob, et j'aurai pitié de toute la maison d'Israël, et je serai jaloux du Nom de ma Sainteté.
26 Wataisahau aibu yao na jinsi walivyoonyesha kutokuwa waaminifu kwangu mimi wakati waliishi salama katika nchi yao, bila kuwa na mtu yeyote wa kuwatia hofu.
Après qu'ils auront porté leur ignominie, et tout leur crime, par lequel ils avaient péché contre moi, quand ils demeuraient en sûreté dans leur terre, et sans qu'il y eût personne qui les épouvantât.
27 Nitakapokuwa nimewarudisha kutoka mataifa na kuwakusanya kutoka nchi za adui zao, mimi nitajionyesha kuwa mtakatifu kwa kupitia kwao machoni mwa mataifa mengi.
Parce que je les ramènerai d'entre les peuples, que je les rassemblerai des pays de leurs ennemis, et que je serai sanctifié en eux, en la présence de plusieurs nations.
28 Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana, Mungu wao, ingawa niliwapeleka uhamishoni miongoni mwa mataifa, nitawakusanya tena katika nchi yao wenyewe, bila kumwacha yeyote nyuma.
Et ils sauront que je suis l'Eternel leur Dieu, lorsqu'après les avoir transportés entre les nations, je les aurai rassemblés en leur terre, et que je n'en aurai laissé demeurer là aucun de reste.
29 Sitawaficha tena uso wangu, kwa maana nitamimina Roho wangu juu ya nyumba ya Israeli, asema Bwana Mwenyezi.”
Et je ne leur cacherai plus ma face, depuis que j'aurai répandu mon Esprit sur la maison d'Israël, dit le Seigneur l'Eternel.

< Ezekieli 39 >