< Ezekieli 39 >
1 “Mwanadamu, tabiri dhidi ya Gogu useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali.
and you(m. s.) son: child man to prophesy upon Gog and to say thus to say Lord YHWH/God look! I to(wards) you Gog leader prince Meshech and Tubal
2 Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukuburuta. Nitakuleta kutoka kaskazini ya mbali na kukupeleka wewe dhidi ya milima ya Israeli.
and to return: return you and to lead you and to ascend: attack you from flank north and to come (in): bring you upon mountain: mount Israel
3 Kisha nitaupiga upinde wako kutoka mkono wako wa kushoto na kuifanya mishale ianguke kutoka mkono wako wa kuume.
and to smite bow your from hand left your and arrow your from hand right your to fall: fall
4 Utaanguka kwenye milima ya Israeli, wewe pamoja na vikosi vyako vyote na yale mataifa yaliyo pamoja nawe. Nitakutoa uwe chakula cha ndege wa aina zote walao nyama na cha wanyama wa mwituni.
upon mountain: mount Israel to fall: kill you(m. s.) and all band your and people which with you to/for bird of prey bird all wing and living thing [the] land: country to give: give you to/for food
5 Utaanguka katika uwanja, kwa kuwa nimenena, asema Bwana Mwenyezi.
upon face: surface [the] land: country to fall: kill for I to speak: speak utterance Lord YHWH/God
6 Nitatuma moto juu ya Magogu na kwa wale wanaoishi kwa salama huko pwani, nao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana.
and to send: depart fire in/on/with Magog and in/on/with to dwell [the] coastland to/for security and to know for I LORD
7 “‘Nitalifanya Jina langu takatifu lijulikane miongoni mwa watu wangu Israeli. Sitaliacha tena Jina langu takatifu litiwe unajisi, nayo mataifa watajua kuwa Mimi Bwana ndimi Aliye Mtakatifu wa Israeli.
and [obj] name holiness my to know in/on/with midst people my Israel and not to profane/begin: profane [obj] name holiness my still and to know [the] nation for I LORD holy in/on/with Israel
8 Hili jambo linakuja! Hakika litatokea, asema Bwana Mwenyezi. Hii ndiyo siku ile niliyosema habari zake.
behold to come (in): come and to be utterance Lord YHWH/God he/she/it [the] day which to speak: speak
9 “‘Ndipo wale wanaoishi katika miji ya Israeli watakapotoka na kutumia hizo silaha kuwashia moto na kuziteketeza, yaani, kigao na ngao, pinde na mishale, rungu za vita na mikuki. Kwa miaka saba watavitumia kama kuni.
and to come out: come to dwell city Israel and to burn: burn and to kindle in/on/with weapon and shield and shield in/on/with bow and in/on/with arrow and in/on/with rod hand and in/on/with spear and to burn: burn in/on/with them fire seven year
10 Hawatahitaji kukusanya kuni kutoka mashambani wala kukata kuni kutoka kwenye misitu, kwa sababu watatumia silaha kuwa kuni. Nao watawateka mateka wale waliowateka na kuchukua nyara mali za wale waliochukua mali zao nyara, asema Bwana Mwenyezi.
and not to lift: raise tree: wood from [the] land: country and not to chop from [the] wood for in/on/with weapon to burn: burn fire and to loot [obj] to loot them and to plunder [obj] to plunder them utterance Lord YHWH/God
11 “‘Siku ile nitampa Gogu mahali pa kuzikia katika Israeli, katika bonde la wale wasafirio upande wa mashariki kuelekea baharini. Jambo hili litazuia njia ya wasafiri kwa sababu Gogu na makundi yake yote ya wajeuri watazikwa huko. Kwa hiyo litaitwa Bonde la Hamon-Gogu.
and to be in/on/with day [the] he/she/it to give: give to/for Gog place there grave in/on/with Israel Valley [the] (Valley of) the Travelers east [the] sea and to muzzle he/she/it [obj] [the] to pass and to bury there [obj] Gog and [obj] all (crowd his *Q(K)*) and to call: call to (Hamon-gog) Valley Hamon-gog (Valley) Hamon-gog (Valley)
12 “‘Kwa miezi saba nyumba ya Israeli itakuwa ikiwazika ili kuisafisha nchi.
and to bury them house: household Israel because be pure [obj] [the] land: country/planet seven month
13 Watu wote wa nchi watawazika, nayo siku nitakayotukuzwa itakuwa siku ya kumbukumbu kwa ajili yao, asema Bwana Mwenyezi.
and to bury all people [the] land: country/planet and to be to/for them to/for name day to honor: honour I utterance Lord YHWH/God
14 “‘Watu wataajiriwa mara kwa mara kuisafisha nchi. Baadhi yao watapita nchini kote na zaidi yao hao wengine, watawazika wale waliosalia juu ya uso wa nchi. Mwisho wa hiyo miezi saba wataanza upekuzi wao.
and human continually to separate to pass in/on/with land: country/planet to bury [obj] [the] to pass [obj] [the] to remain upon face: surface [the] land: country/planet to/for be pure her from end seven month to search
15 Wakati wanapopita nchini kote na mmoja wao akaona mfupa wa mwanadamu, ataweka alama kando yake mpaka wachimba kaburi wawe wameuzika katika Bonde la Hamon-Gogu.
and to pass [the] to pass in/on/with land: country/planet and to see: see bone man and to build beside him signpost till to bury [obj] him [the] to bury to(wards) (Hamon-gog) Valley Hamon-gog (Valley) Hamon-gog (Valley)
16 (Pia mji uitwao Hamona utakuwa humo.) Hivyo ndivyo watakavyoisafisha nchi.’
and also name city Hamonah and be pure [the] land: country/planet
17 “Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ita kila aina ya ndege na wanyama wote wa mwituni, waambie: ‘Kusanyikeni mje pamoja kutoka pande zote kwa ajili ya dhabihu ninayowaandalia, dhabihu kuu katika milima ya Israeli. Huko mtakula nyama na kunywa damu.
and you(m. s.) son: child man thus to say Lord YHWH/God to say to/for bird all wing and to/for all living thing [the] land: country to gather and to come (in): come to gather from around upon sacrifice my which I to sacrifice to/for you sacrifice great: large upon mountain: mount Israel and to eat flesh and to drink blood
18 Mtakula nyama za watu mashujaa na kunywa damu za wakuu wa dunia kana kwamba ni za kondoo dume na kondoo wake, mbuzi na mafahali, wote walionona kutoka Bashani.
flesh mighty man to eat and blood leader [the] land: country/planet to drink ram ram and goat bullock fatling Bashan all their
19 Katika dhabihu ninayoandaa kwa ajili yenu, mtakula mafuta mpaka mkinai na kunywa damu mpaka mlewe.
and to eat fat to/for satiety and to drink blood to/for drunkenness from sacrifice my which to sacrifice to/for you
20 Kwenye meza yangu watajishibisha kwa farasi na wapanda farasi, watu mashujaa na askari wa kila aina,’ asema Bwana Mwenyezi.
and to satisfy upon table my horse and chariot mighty man and all man battle utterance Lord YHWH/God
21 “Nitauonyesha utukufu wangu miongoni mwa mataifa, nayo mataifa yote wataiona adhabu nitakayotoa na mkono wangu nitakaouweka juu yao.
and to give: put [obj] glory my in/on/with nation and to see: see all [the] nation [obj] justice: judgement my which to make: do and [obj] hand: power my which to set: put in/on/with them
22 Kuanzia siku ile na kuendelea nyumba ya Israeli itajua kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wao.
and to know house: household Israel for I LORD God their from [the] day [the] he/she/it and further
23 Na mataifa watajua kuwa nyumba ya Israeli walikwenda utumwani kwa ajili ya dhambi yao, kwa sababu hawakuwa waaminifu kwangu. Hivyo niliwaficha uso wangu na kuwatia mikononi mwa adui zao, nao wote wakaanguka kwa upanga.
and to know [the] nation for in/on/with iniquity: crime their to reveal: remove house: household Israel upon which be unfaithful in/on/with me and to hide face my from them and to give: give them in/on/with hand: power enemy their and to fall: kill in/on/with sword all their
24 Niliwatendea sawasawa na uchafu wao na makosa yao, nami nikawaficha uso wangu.
like/as uncleanness their and like/as transgression their to make: do [obj] them and to hide face my from them
25 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Sasa nitamrudisha Yakobo kutoka utumwani, nami nitawahurumia watu wote wa Israeli, nami nitakuwa na wivu kwa ajili ya Jina langu takatifu.
to/for so thus to say Lord YHWH/God now to return: rescue [obj] (captivity *Q(k)*) Jacob and to have compassion all house: household Israel and be jealous to/for name holiness my
26 Wataisahau aibu yao na jinsi walivyoonyesha kutokuwa waaminifu kwangu mimi wakati waliishi salama katika nchi yao, bila kuwa na mtu yeyote wa kuwatia hofu.
and to lift: forgive [obj] shame their and [obj] all unfaithfulness their which be unfaithful in/on/with me in/on/with to dwell they upon land: soil their to/for security and nothing to tremble
27 Nitakapokuwa nimewarudisha kutoka mataifa na kuwakusanya kutoka nchi za adui zao, mimi nitajionyesha kuwa mtakatifu kwa kupitia kwao machoni mwa mataifa mengi.
in/on/with to return: return I [obj] them from [the] people and to gather [obj] them from land: country/planet enemy their and to consecrate: holiness in/on/with them to/for eye: seeing [the] nation many
28 Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana, Mungu wao, ingawa niliwapeleka uhamishoni miongoni mwa mataifa, nitawakusanya tena katika nchi yao wenyewe, bila kumwacha yeyote nyuma.
and to know for I LORD God their in/on/with to reveal: remove I [obj] them to(wards) [the] nation and to gather them upon land: soil their and not to remain still from them there
29 Sitawaficha tena uso wangu, kwa maana nitamimina Roho wangu juu ya nyumba ya Israeli, asema Bwana Mwenyezi.”
and not to hide still face my from them which to pour: pour [obj] spirit my upon house: household Israel utterance Lord YHWH/God