< Ezekieli 39 >

1 “Mwanadamu, tabiri dhidi ya Gogu useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali.
And you, son of man, be a prophet against Gog, and say, These are the words of the Lord: See, I am against you, O Gog, ruler of Rosh, Meshech, and Tubal:
2 Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukuburuta. Nitakuleta kutoka kaskazini ya mbali na kukupeleka wewe dhidi ya milima ya Israeli.
And turning you round, I will be your guide, and make you come up from the inmost parts of the north; I will make you come on to the mountains of Israel:
3 Kisha nitaupiga upinde wako kutoka mkono wako wa kushoto na kuifanya mishale ianguke kutoka mkono wako wa kuume.
And with a blow I will send your bow out of your left hand and your arrows falling from your right hand.
4 Utaanguka kwenye milima ya Israeli, wewe pamoja na vikosi vyako vyote na yale mataifa yaliyo pamoja nawe. Nitakutoa uwe chakula cha ndege wa aina zote walao nyama na cha wanyama wa mwituni.
On the mountains of Israel you will come down, you and all your forces and the peoples who are with you: I will give you to cruel birds of every sort and to the beasts of the field to be their food.
5 Utaanguka katika uwanja, kwa kuwa nimenena, asema Bwana Mwenyezi.
You will come down in the open field: for I have said it, says the Lord.
6 Nitatuma moto juu ya Magogu na kwa wale wanaoishi kwa salama huko pwani, nao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana.
And I will send a fire on Magog, and on those who are living in the sea-lands without fear: and they will be certain that I am the Lord.
7 “‘Nitalifanya Jina langu takatifu lijulikane miongoni mwa watu wangu Israeli. Sitaliacha tena Jina langu takatifu litiwe unajisi, nayo mataifa watajua kuwa Mimi Bwana ndimi Aliye Mtakatifu wa Israeli.
And I will make clear my holy name among my people Israel; I will no longer let my holy name be made unclean: and the nations will be certain that I am the Lord, the Holy One in Israel.
8 Hili jambo linakuja! Hakika litatokea, asema Bwana Mwenyezi. Hii ndiyo siku ile niliyosema habari zake.
See, it is coming and it will be done, says the Lord; this is the day of which I have given word.
9 “‘Ndipo wale wanaoishi katika miji ya Israeli watakapotoka na kutumia hizo silaha kuwashia moto na kuziteketeza, yaani, kigao na ngao, pinde na mishale, rungu za vita na mikuki. Kwa miaka saba watavitumia kama kuni.
And those who are living in the towns of Israel will go out and make fires of the instruments of war, burning the body-covers and the breastplates, the bows and the arrows and the sticks and the spears, and for seven years they will make fires of them:
10 Hawatahitaji kukusanya kuni kutoka mashambani wala kukata kuni kutoka kwenye misitu, kwa sababu watatumia silaha kuwa kuni. Nao watawateka mateka wale waliowateka na kuchukua nyara mali za wale waliochukua mali zao nyara, asema Bwana Mwenyezi.
And they will take no wood out of the field or have any cut down in the woods; for they will make their fires of the instruments of war: and they will take by force the property of those who took their property, and go off with the goods of those who took their goods, says the Lord.
11 “‘Siku ile nitampa Gogu mahali pa kuzikia katika Israeli, katika bonde la wale wasafirio upande wa mashariki kuelekea baharini. Jambo hili litazuia njia ya wasafiri kwa sababu Gogu na makundi yake yote ya wajeuri watazikwa huko. Kwa hiyo litaitwa Bonde la Hamon-Gogu.
And it will come about in those days, that I will give to Gog a last resting-place there in Israel, in the valley of Abarim on the east of the sea: and those who go through will be stopped: and there Gog and all his people will be put to rest, and the place will be named, The valley of Hamon-gog.
12 “‘Kwa miezi saba nyumba ya Israeli itakuwa ikiwazika ili kuisafisha nchi.
And the children of Israel will be seven months putting them in the earth, so as to make the land clean.
13 Watu wote wa nchi watawazika, nayo siku nitakayotukuzwa itakuwa siku ya kumbukumbu kwa ajili yao, asema Bwana Mwenyezi.
And all the people of the land will put them in the earth; and it will be to their honour in the day when I let my glory be seen, says the Lord.
14 “‘Watu wataajiriwa mara kwa mara kuisafisha nchi. Baadhi yao watapita nchini kote na zaidi yao hao wengine, watawazika wale waliosalia juu ya uso wa nchi. Mwisho wa hiyo miezi saba wataanza upekuzi wao.
And they will put on one side men to do no other work but to go through the land and put in the earth the rest of those who are still on the face of the land, to make it clean: after seven months are ended they are to make a search.
15 Wakati wanapopita nchini kote na mmoja wao akaona mfupa wa mwanadamu, ataweka alama kando yake mpaka wachimba kaburi wawe wameuzika katika Bonde la Hamon-Gogu.
And while they go through the land, if anyone sees a man's bone, he is to put up a sign by the place till those who are doing the work have put it in the earth in the valley of Hamon-gog.
16 (Pia mji uitwao Hamona utakuwa humo.) Hivyo ndivyo watakavyoisafisha nchi.’
And there they will put all the army of Gog in the earth. So they will make the land clean.
17 “Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ita kila aina ya ndege na wanyama wote wa mwituni, waambie: ‘Kusanyikeni mje pamoja kutoka pande zote kwa ajili ya dhabihu ninayowaandalia, dhabihu kuu katika milima ya Israeli. Huko mtakula nyama na kunywa damu.
And you, son of man, this is what the Lord has said: Say to the birds of every sort and to all the beasts of the field, Get together and come; come together on every side to the offering which I am putting to death for you, a great offering on the mountains of Israel, so that you may have flesh for your food and blood for your drink.
18 Mtakula nyama za watu mashujaa na kunywa damu za wakuu wa dunia kana kwamba ni za kondoo dume na kondoo wake, mbuzi na mafahali, wote walionona kutoka Bashani.
The flesh of the men of war will be your food, and your drink the blood of the princes of the earth, of sheep and lambs, of he-goats, of oxen, all of them fat beasts of Bashan.
19 Katika dhabihu ninayoandaa kwa ajili yenu, mtakula mafuta mpaka mkinai na kunywa damu mpaka mlewe.
You will go on feasting on the fat till you are full, and drinking the blood till you are overcome with it, of my offering which I have put to death for you.
20 Kwenye meza yangu watajishibisha kwa farasi na wapanda farasi, watu mashujaa na askari wa kila aina,’ asema Bwana Mwenyezi.
At my table you will have food in full measure, horses and war-carriages, great men and all the men of war, says the Lord.
21 “Nitauonyesha utukufu wangu miongoni mwa mataifa, nayo mataifa yote wataiona adhabu nitakayotoa na mkono wangu nitakaouweka juu yao.
And I will put my glory among the nations, and all the nations will see my punishments which I have put into effect, and my hand which I have put on them.
22 Kuanzia siku ile na kuendelea nyumba ya Israeli itajua kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wao.
So the children of Israel will be certain that I am the Lord their God, from that day and for the future.
23 Na mataifa watajua kuwa nyumba ya Israeli walikwenda utumwani kwa ajili ya dhambi yao, kwa sababu hawakuwa waaminifu kwangu. Hivyo niliwaficha uso wangu na kuwatia mikononi mwa adui zao, nao wote wakaanguka kwa upanga.
And it will be clear to the nations that the children of Israel were taken away prisoners for their evil-doing; because they did wrong against me, and my face was covered from them: so I gave them up into the hands of their attackers, and they all came to their end by the sword.
24 Niliwatendea sawasawa na uchafu wao na makosa yao, nami nikawaficha uso wangu.
In the measure of their unclean ways and their sins, so I did to them; and I kept my face covered from them.
25 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Sasa nitamrudisha Yakobo kutoka utumwani, nami nitawahurumia watu wote wa Israeli, nami nitakuwa na wivu kwa ajili ya Jina langu takatifu.
For this cause the Lord has said, Now I will let the fate of Jacob be changed, and I will have mercy on all the children of Israel, and will take care of the honour of my holy name.
26 Wataisahau aibu yao na jinsi walivyoonyesha kutokuwa waaminifu kwangu mimi wakati waliishi salama katika nchi yao, bila kuwa na mtu yeyote wa kuwatia hofu.
And they will be conscious of their shame and of all the wrong which they have done against me, when they are living in their land with no sense of danger and with no one to be a cause of fear to them;
27 Nitakapokuwa nimewarudisha kutoka mataifa na kuwakusanya kutoka nchi za adui zao, mimi nitajionyesha kuwa mtakatifu kwa kupitia kwao machoni mwa mataifa mengi.
When I have taken them back from among the peoples and got them together out of the lands of their haters, and have made myself holy in them before the eyes of a great number of nations.
28 Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana, Mungu wao, ingawa niliwapeleka uhamishoni miongoni mwa mataifa, nitawakusanya tena katika nchi yao wenyewe, bila kumwacha yeyote nyuma.
And they will be certain that I am the Lord their God, because I sent them away as prisoners among the nations, and have taken them together back to their land; and I have not let one of them be there any longer.
29 Sitawaficha tena uso wangu, kwa maana nitamimina Roho wangu juu ya nyumba ya Israeli, asema Bwana Mwenyezi.”
And my face will no longer be covered from them: for I have sent the out-flowing of my spirit on the children of Israel, says the Lord.

< Ezekieli 39 >