< Ezekieli 39 >

1 “Mwanadamu, tabiri dhidi ya Gogu useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali.
Ty synu člověčí, prorokuj ještě proti Gogovi a rci: Takto praví Panovník Hospodin: Aj, já povstanu proti tobě, ó Gogu, kníže a hlavo v Mešech a Tubal.
2 Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukuburuta. Nitakuleta kutoka kaskazini ya mbali na kukupeleka wewe dhidi ya milima ya Israeli.
A odvedu tě zpět, navštívě tě šesti ranami, když tě vzbudím, abys přitáhl od stran půlnočních, a přivedu tě na hory Izraelské.
3 Kisha nitaupiga upinde wako kutoka mkono wako wa kushoto na kuifanya mishale ianguke kutoka mkono wako wa kuume.
Nebo vyrazím lučiště tvé z ruky tvé levé, a střely z ruky tvé pravé vyvrhu.
4 Utaanguka kwenye milima ya Israeli, wewe pamoja na vikosi vyako vyote na yale mataifa yaliyo pamoja nawe. Nitakutoa uwe chakula cha ndege wa aina zote walao nyama na cha wanyama wa mwituni.
Na horách Izraelských padneš ty i všickni houfové tvoji i národové, kteříž budou s tebou; ptákům a všemu ptactvu křídla majícímu i zvěři polní dám tě k sežrání.
5 Utaanguka katika uwanja, kwa kuwa nimenena, asema Bwana Mwenyezi.
Na svrchku pole padneš; neboť jsem já mluvil, praví Panovník Hospodin.
6 Nitatuma moto juu ya Magogu na kwa wale wanaoishi kwa salama huko pwani, nao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana.
Vypustím také oheň na Magoga i na ty, kteříž přebývají na ostrovích bezpečně, i zvědíť, že já jsem Hospodin.
7 “‘Nitalifanya Jina langu takatifu lijulikane miongoni mwa watu wangu Israeli. Sitaliacha tena Jina langu takatifu litiwe unajisi, nayo mataifa watajua kuwa Mimi Bwana ndimi Aliye Mtakatifu wa Israeli.
A jméno svatosti své uvedu v známost u prostřed lidu svého Izraelského. Nedopustím, pravím, více poškvrňovati jména svatosti své, i zvědíť národové, že já jsem Hospodin Svatý v Izraeli.
8 Hili jambo linakuja! Hakika litatokea, asema Bwana Mwenyezi. Hii ndiyo siku ile niliyosema habari zake.
Aj, přijdeť a stane se to, praví Panovník Hospodin, téhož dne, o kterémž jsem mluvil.
9 “‘Ndipo wale wanaoishi katika miji ya Israeli watakapotoka na kutumia hizo silaha kuwashia moto na kuziteketeza, yaani, kigao na ngao, pinde na mishale, rungu za vita na mikuki. Kwa miaka saba watavitumia kama kuni.
Tehdy vyjdou obyvatelé měst Izraelských, a zapálíce, popálí zbroj a štíty i pavézy, lučiště i střely, dřevce i kopí, a budou je páliti ohněm sedm let.
10 Hawatahitaji kukusanya kuni kutoka mashambani wala kukata kuni kutoka kwenye misitu, kwa sababu watatumia silaha kuwa kuni. Nao watawateka mateka wale waliowateka na kuchukua nyara mali za wale waliochukua mali zao nyara, asema Bwana Mwenyezi.
Aniž nositi budou dříví s pole, ani sekati v lesích, proto že zbrojí zaněcovati budou oheň, když zloupí ty, kteříž je loupívali, a mocí poberou těm, kteříž jim mocí brávali, praví Panovník Hospodin.
11 “‘Siku ile nitampa Gogu mahali pa kuzikia katika Israeli, katika bonde la wale wasafirio upande wa mashariki kuelekea baharini. Jambo hili litazuia njia ya wasafiri kwa sababu Gogu na makundi yake yote ya wajeuri watazikwa huko. Kwa hiyo litaitwa Bonde la Hamon-Gogu.
I stane se v ten den, že dám Gogovi místo ku pohřbu tam v Izraeli, údolí, kudyž se jde k východní straně k moři, kteréžto zacpá ústa tudy jdoucích. I pohřbí tam Goga i všecko množství jeho, a nazovou je údolí množství Gogova.
12 “‘Kwa miezi saba nyumba ya Israeli itakuwa ikiwazika ili kuisafisha nchi.
Nebo pochovávati je budou dům Izraelský za sem měsíců proto, aby vyčistili zemi.
13 Watu wote wa nchi watawazika, nayo siku nitakayotukuzwa itakuwa siku ya kumbukumbu kwa ajili yao, asema Bwana Mwenyezi.
A tak pohřbí je všecken lid té země, a bude jim to ku poctivosti v den, v kterýž oslaven budu, praví Panovník Hospodin.
14 “‘Watu wataajiriwa mara kwa mara kuisafisha nchi. Baadhi yao watapita nchini kote na zaidi yao hao wengine, watawazika wale waliosalia juu ya uso wa nchi. Mwisho wa hiyo miezi saba wataanza upekuzi wao.
Oddělíť pak muže statečné, kteříž by procházeli tu zemi, proto aby pochovávali ty, kteříž by pozůstali na svrchku země, aby ji vyčistili. Po vyjití sedmi měsíců přehledávati začnou.
15 Wakati wanapopita nchini kote na mmoja wao akaona mfupa wa mwanadamu, ataweka alama kando yake mpaka wachimba kaburi wawe wameuzika katika Bonde la Hamon-Gogu.
A ti procházejíce, choditi budou po zemi, a když uzří kosti člověčí, vzdělají při nich znamení pamětné, aby je pohřbili hrobaři v údolí množství Gogova.
16 (Pia mji uitwao Hamona utakuwa humo.) Hivyo ndivyo watakavyoisafisha nchi.’
Nýbrž to množství jeho bude k slávě i městu, když vyčistí tu zemi.
17 “Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ita kila aina ya ndege na wanyama wote wa mwituni, waambie: ‘Kusanyikeni mje pamoja kutoka pande zote kwa ajili ya dhabihu ninayowaandalia, dhabihu kuu katika milima ya Israeli. Huko mtakula nyama na kunywa damu.
Ty pak synu člověčí, takto praví Panovník Hospodin: Rci ke všelijakým ptákům křídla majícím i ke všelijaké zvěři polní: Shromažďte se a přiďte, zbeřte se odevšad k obětem mým, kterýchž já nabiji vám, obětí velikých na horách Izraelských, a budete jísti maso a píti krev.
18 Mtakula nyama za watu mashujaa na kunywa damu za wakuu wa dunia kana kwamba ni za kondoo dume na kondoo wake, mbuzi na mafahali, wote walionona kutoka Bashani.
Maso silných reků jísti budete, a krev knížat zemských píti, skopců, beranů a kozlů, volků, všecko tučných Bázanských.
19 Katika dhabihu ninayoandaa kwa ajili yenu, mtakula mafuta mpaka mkinai na kunywa damu mpaka mlewe.
A budete jísti tuk do sytosti, a píti krev do opití z obětí mých, kterýchž vám nabiji.
20 Kwenye meza yangu watajishibisha kwa farasi na wapanda farasi, watu mashujaa na askari wa kila aina,’ asema Bwana Mwenyezi.
A nasytíte se z stolu mého koňmi i jezdci, silnými reky i všemi muži válečnými, dí Panovník Hospodin.
21 “Nitauonyesha utukufu wangu miongoni mwa mataifa, nayo mataifa yote wataiona adhabu nitakayotoa na mkono wangu nitakaouweka juu yao.
A tak zjevím slávu svou mezi národy, aby viděli všickni národové soud můj, kterýž jsem vykonal, i ruku mou, kterouž jsem doložil na ně.
22 Kuanzia siku ile na kuendelea nyumba ya Israeli itajua kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wao.
I zvíť dům Izraelský, že já jsem Hospodin Bůh jejich, od tohoto dne i potom.
23 Na mataifa watajua kuwa nyumba ya Israeli walikwenda utumwani kwa ajili ya dhambi yao, kwa sababu hawakuwa waaminifu kwangu. Hivyo niliwaficha uso wangu na kuwatia mikononi mwa adui zao, nao wote wakaanguka kwa upanga.
Zvědí také i národové, že pro svou nepravost zajat jest dům Izraelský, proto že se dopouštěli přestoupení proti mně; pročež jsem skryl tvář svou před nimi, a vydal jsem je v ruku protivníků jejich, aby padli mečem všickni napořád.
24 Niliwatendea sawasawa na uchafu wao na makosa yao, nami nikawaficha uso wangu.
Podlé nečistoty jejich a podlé zpronevěření se jejich učinil jsem jim, a skryl jsem tvář svou před nimi.
25 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Sasa nitamrudisha Yakobo kutoka utumwani, nami nitawahurumia watu wote wa Israeli, nami nitakuwa na wivu kwa ajili ya Jina langu takatifu.
Z té příčiny takto praví Panovník Hospodin: Jižť zase přivedu zajaté Jákobovy, a smiluji se nade vším domem Izraelským a horliti budu příčinou jména svatosti své,
26 Wataisahau aibu yao na jinsi walivyoonyesha kutokuwa waaminifu kwangu mimi wakati waliishi salama katika nchi yao, bila kuwa na mtu yeyote wa kuwatia hofu.
Ač ponesou potupu svou a všecko přestoupení své, kteréhož se dopustili proti mně, když bydlili v zemi své bezpečně, aniž byl, kdo by je přestrašil.
27 Nitakapokuwa nimewarudisha kutoka mataifa na kuwakusanya kutoka nchi za adui zao, mimi nitajionyesha kuwa mtakatifu kwa kupitia kwao machoni mwa mataifa mengi.
A však je zase přivedu z národů, a shromáždím je z zemí nepřátel jejich, a posvěcen budu v nich před očima národů mnohých.
28 Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana, Mungu wao, ingawa niliwapeleka uhamishoni miongoni mwa mataifa, nitawakusanya tena katika nchi yao wenyewe, bila kumwacha yeyote nyuma.
A tak poznají, že já jsem Hospodin Bůh jejich, když zaveda je do národů, shromáždím je do země jejich, a nepozůstavím tam žádného z nich.
29 Sitawaficha tena uso wangu, kwa maana nitamimina Roho wangu juu ya nyumba ya Israeli, asema Bwana Mwenyezi.”
Aniž skryji více tváři své před nimi, když vyleji Ducha svého na dům Izraelský, praví Panovník Hospodin.

< Ezekieli 39 >