< Ezekieli 38 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
La parole de l'Eternel me fut encore [adressée], en disant:
2 “Mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya Gogu, katika nchi ya Magogu, mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali, tabiri dhidi yake
Fils d'homme, tourne ta face vers Gog au pays de Magog, Prince des chefs de Mésec et de Tubal, et prophétise contre lui.
3 na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu, mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali.
Et dis: ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: voici, j'en veux à toi, Gog, Prince des chefs de Mésec et de Tubal;
4 Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukutia ndoana kwenye mataya yako na kukutoa nje wewe pamoja na jeshi lako lote, yaani, farasi wako, wapanda farasi wako waliojiandaa tayari kwa vita, pamoja na kundi kubwa la wajeuri wakiwa na ngao na vigao, wote wakipunga panga zao.
Et je te ferai retourner en arrière, et je mettrai des boucles dans tes mâchoires, et te ferai sortir avec toute ton armée, avec les chevaux, et les gens de cheval, tous parfaitement bien équipés, une grande multitude avec des écus et des boucliers, et tous maniant l'épée.
5 Uajemi, Kushi na Putu watakuwa pamoja nao, wote wakiwa na ngao na kofia za chuma,
Ceux de Perse, de Cus, et de Put avec eux, qui tous ont des boucliers et des casques.
6 pia Gomeri pamoja na vikosi vyake vyote, na Beth-Togarma kutoka kaskazini ya mbali pamoja na vikosi vyake vyote, mataifa mengi wakiwa pamoja nawe.
Gomer et toutes ses bandes, la maison de Togarma du fond de l'Aquilon, avec toutes ses troupes, [et] plusieurs peuples avec toi.
7 “‘Jiandae, uwe tayari, wewe na makundi yako yote ya wajeuri yaliyokusanyika pamoja nawe, nawe waamrishe.
Apprête-toi, et tiens-toi prêt, toi, et toute la multitude qui s'est assemblée vers toi, et sois-leur pour garde.
8 Baada ya siku nyingi utaitwa vitani. Katika miaka ijayo, utaivamia nchi ile ambayo imepona kutoka vita, ambayo watu wake walikusanywa kutoka mataifa mengi kuja katika milima ya Israeli, ambayo kwa muda mrefu ilikuwa imeachwa ukiwa. Wameletwa kutoka mataifa na sasa wote wanaishi katika hali ya salama.
Après plusieurs jours tu seras visité, et dans les dernières années tu viendras au pays qui aura été délivré de l'épée, et [au peuple] ramassé d'entre plusieurs peuples, aux montagnes d'Israël qui auront été continuellement en désert; [tu viendras] en ce pays-là, lorsque ce pays ayant été retiré d'entre les peuples, tous y habiteront en assurance.
9 Wewe na vikosi vyako vyote na mataifa mengi yaliyo pamoja nawe mtapanda juu, mtawazoa kama tufani na kuifunika nchi kama wingu.
Tu monteras donc comme une ruine qui éclate, et tu viendras comme une nuée pour couvrir la terre, toi, et toutes tes bandes, et plusieurs peuples avec toi.
10 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile mawazo yataingia moyoni mwako nawe utapanga mipango mibaya.
Ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: il arrivera en ces jours-là que plusieurs choses monteront en ton cœur, et que tu formeras un dessein pernicieux.
11 Utasema, “Nitapigana vita na nchi ambayo vijiji vyake havina maboma. Nitawashambulia watu wanaoishi kwa amani na wasiotarajia vita: wote wanaishi bila maboma na bila malango na makomeo.
Car tu diras: je monterai contre le pays dont les villes sont sans murailles; j'envahirai ceux qui sont en repos, qui habitent en assurance, qui demeurent tous [dans des villes] sans murailles, lesquelles n'ont ni barres ni portes;
12 Nitateka mateka na kuchukua nyara mali za wale waliorudi kuishi katika mahame na wale watu waliokusanywa kutoka kwa mataifa, ambao sasa wana mifugo na mali nyingi, wanaoishi katikati ya nchi.”
Pour enlever un grand butin et faire un grand pillage; pour remettre ta main sur les déserts qui de nouveau étaient habités et sur le peuple ramassé d'entre les nations, lequel vaque à son bétail, et à ses biens, au milieu du pays.
13 Sheba na Dedani pamoja na wafanyabiashara wa Tarshishi na vijiji vyake vyote watakuambia, “Je, umekuja kuteka mateka? Je, umekusanya makundi yako ya wajeuri ili kuchukua nyara mali, kutwaa fedha na dhahabu, kutunyangʼanya mifugo na mali na kuteka nyara nyingi zaidi?”’
Seba, et Dedan, et les marchands de Tarsis, et tous ses lionceaux, te diront: ne vas-tu pas pour faire un grand butin, et n'as-tu pas assemblé ta multitude pour faire un grand pillage, pour emporter de l'argent et de l'or, pour prendre le bétail et les biens, pour enlever un grand butin?
14 “Kwa hiyo, mwanadamu, tabiri na umwambie Gogu: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile, watu wangu Israeli watakapokuwa wanaishi salama, Je, wewe mwenyewe hutalijua hilo?
Toi donc, fils d'homme, prophétise, et dis à Gog: ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: en ce jour-là, quand mon peuple d'Israël habitera en assurance, ne le sauras-tu pas?
15 Utakuja kutoka kwako huko kaskazini ya mbali, ukiwa pamoja na mataifa mengi, wote wakiwa wamepanda farasi, kundi kubwa, jeshi kuu.
Et ne viendras-tu pas de ton lieu, du fond de l'Aquilon, toi, et plusieurs peuples avec toi, eux tous gens de cheval, une grande multitude, et une grosse armée?
16 Utakuja dhidi ya watu wangu Israeli kama wingu lifunikavyo nchi. Siku zijazo, ee Gogu, nitakuleta wewe dhidi ya nchi yangu, ili kwamba mataifa wapate kunijua Mimi nitakapojionyesha mtakatifu kwa kukupitia wewe mbele ya macho yao.
Et ne monteras-tu pas contre mon peuple d'Israël, comme une nuée pour couvrir la terre? tu seras aux derniers jours, et je te ferai venir sur ma terre, afin que les nations me connaissent, quand je serai sanctifié en toi, ô Gog! en leur présence.
17 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, wewe si yule niliyenena juu yako katika siku za zamani kwa kupitia kwa watumishi wangu manabii wa Israeli? Wakati ule walitabiri kwa miaka mingi kwamba ningekuleta upigane nao.
Ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: n'est-ce pas de toi que j'ai parlé autrefois par le ministère de mes serviteurs, les Prophètes d'Israël, qui ont prophétisé en ces jours-là pendant plusieurs années, qu'on te ferait venir contre eux?
18 Hili ndilo litakalotokea katika siku ile: Gogu atakaposhambulia nchi ya Israeli, hasira yangu kali itaamka, asema Bwana Mwenyezi.
Mais il arrivera en ce jour-là, au jour de la venue de Gog sur la terre d'Israël, dit le Seigneur l'Eternel, que ma colère éclatera.
19 Katika wivu wangu na ghadhabu yangu kali ninasema kuwa wakati ule patakuwepo tetemeko kuu katika nchi ya Israeli.
Et je parlerai en ma jalousie [et] en l'ardeur de ma fureur, si en ce jour-là il n'y a une grande agitation sur la terre d'Israël.
20 Samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa kondeni, kila kiumbe kitambaacho ardhini, na watu wote walio juu ya uso wa nchi watatetemeka mbele zangu. Milima itapinduka, majabali yatapasuka na kila ukuta utaanguka chini.
Et les poissons de la mer, et les oiseaux des cieux, et les bêtes des champs, et tout reptile qui rampe sur la terre, et tous les hommes qui sont sur le dessus de la terre seront épouvantés par ma présence; les montagnes seront renversées, les tours et les murailles seront abattues.
21 Nitaita upanga vita dhidi ya Gogu juu ya milima yangu yote, asema Bwana Mwenyezi. Upanga wa kila mtu utakuwa dhidi ya ndugu yake.
Et j'appellerai contre lui l'épée par toutes mes montagnes, dit le Seigneur l'Eternel; l'épée de chacun d'eux sera contre son frère.
22 Nitatekeleza hukumu juu yake kwa tauni na kwa umwagaji wa damu. Nitaifanya mvua ya mafuriko kunyesha, mvua ya mawe na moto wa kiberiti juu yake na juu ya vikosi vyake na juu ya mataifa mengi walio pamoja naye.
Et j'entrerai en jugement avec lui par la mortalité, et par le sang, et je ferai pleuvoir sur lui, et sur ses troupes, et sur les grands peuples qui seront avec lui, des torrents d'eau, des pierres de grêle, du feu et du soufre.
23 Nami hivyo ndivyo nitakavyoonyesha ukuu wangu na utakatifu wangu, nami nitajijulisha mbele ya macho ya mataifa mengi. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’
Je me glorifierai, je me sanctifierai, je serai connu en la présence de plusieurs nations; et elles sauront que je suis l'Eternel.

< Ezekieli 38 >