< Ezekieli 38 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
La parole de Yahvé me fut adressée en ces termes:
2 “Mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya Gogu, katika nchi ya Magogu, mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali, tabiri dhidi yake
Fils d'homme, tourne ta face vers Gog, du pays de Magog, prince de Rosh, de Meshech et de Tubal, et prophétise contre lui.
3 na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu, mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali.
Tu diras: « Le Seigneur Yahvé dit: Voici, j'en veux à toi, Gog, prince de Rosh, de Meshech et de Tubal.
4 Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukutia ndoana kwenye mataya yako na kukutoa nje wewe pamoja na jeshi lako lote, yaani, farasi wako, wapanda farasi wako waliojiandaa tayari kwa vita, pamoja na kundi kubwa la wajeuri wakiwa na ngao na vigao, wote wakipunga panga zao.
Je te tournerai, je mettrai des crochets dans tes mâchoires, et je te ferai sortir avec toute ton armée, chevaux et cavaliers, tous revêtus d'une armure complète, une grande troupe, avec bouclier et cuirasse, tous maniant l'épée;
5 Uajemi, Kushi na Putu watakuwa pamoja nao, wote wakiwa na ngao na kofia za chuma,
la Perse, Cush, et Put avec eux, tous avec bouclier et casque;
6 pia Gomeri pamoja na vikosi vyake vyote, na Beth-Togarma kutoka kaskazini ya mbali pamoja na vikosi vyake vyote, mataifa mengi wakiwa pamoja nawe.
Gomer et toutes ses hordes, la maison de Togarma, à l'extrémité du nord, et toutes ses hordes, beaucoup de peuples avec toi.
7 “‘Jiandae, uwe tayari, wewe na makundi yako yote ya wajeuri yaliyokusanyika pamoja nawe, nawe waamrishe.
"''Prépare-toi, oui, prépare-toi, toi et toutes tes troupes qui sont rassemblées auprès de toi, et sois un gardien pour elles.
8 Baada ya siku nyingi utaitwa vitani. Katika miaka ijayo, utaivamia nchi ile ambayo imepona kutoka vita, ambayo watu wake walikusanywa kutoka mataifa mengi kuja katika milima ya Israeli, ambayo kwa muda mrefu ilikuwa imeachwa ukiwa. Wameletwa kutoka mataifa na sasa wote wanaishi katika hali ya salama.
Après bien des jours, vous serez visités. Dans la suite des temps, tu entreras dans le pays qu'on ramène de l'épée, qu'on recueille d'un grand nombre de peuples, sur les montagnes d'Israël, qui ont été un désert continuel; mais on le retire des peuples et ils habiteront en sécurité, tous.
9 Wewe na vikosi vyako vyote na mataifa mengi yaliyo pamoja nawe mtapanda juu, mtawazoa kama tufani na kuifunika nchi kama wingu.
Tu monteras. Tu viendras comme une tempête. Tu seras comme une nuée pour couvrir le pays, toi et toutes tes hordes, et de nombreux peuples avec toi. »
10 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile mawazo yataingia moyoni mwako nawe utapanga mipango mibaya.
"'Le Seigneur Yahvé dit: « En ce jour-là, des choses te viendront à l'esprit et tu concevras un plan diabolique.
11 Utasema, “Nitapigana vita na nchi ambayo vijiji vyake havina maboma. Nitawashambulia watu wanaoishi kwa amani na wasiotarajia vita: wote wanaishi bila maboma na bila malango na makomeo.
Tu diras: « Je monterai dans le pays des villages sans murs. J'irai vers ceux qui sont au repos, qui habitent en sécurité, tous sans murs, sans barres ni portes,
12 Nitateka mateka na kuchukua nyara mali za wale waliorudi kuishi katika mahame na wale watu waliokusanywa kutoka kwa mataifa, ambao sasa wana mifugo na mali nyingi, wanaoishi katikati ya nchi.”
pour prendre le pillage et le butin; pour tourner ta main contre les ruines habitées, et contre le peuple rassemblé des nations, qui a du bétail et des biens, qui habite au milieu de la terre.''
13 Sheba na Dedani pamoja na wafanyabiashara wa Tarshishi na vijiji vyake vyote watakuambia, “Je, umekuja kuteka mateka? Je, umekusanya makundi yako ya wajeuri ili kuchukua nyara mali, kutwaa fedha na dhahabu, kutunyangʼanya mifugo na mali na kuteka nyara nyingi zaidi?”’
Saba, Dedan et les marchands de Tarsis, avec tous ses jeunes lions, te demanderont: « Es-tu venu pour prendre le butin? As-tu rassemblé ta troupe pour prendre le butin, pour emporter de l'argent et de l'or, pour emporter du bétail et des biens, pour faire un grand pillage? »
14 “Kwa hiyo, mwanadamu, tabiri na umwambie Gogu: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile, watu wangu Israeli watakapokuwa wanaishi salama, Je, wewe mwenyewe hutalijua hilo?
« C'est pourquoi, fils d'homme, prophétise et dis à Gog: « Le Seigneur Yahvé dit: « En ce jour où mon peuple Israël habitera en sécurité, ne le sauras-tu pas?
15 Utakuja kutoka kwako huko kaskazini ya mbali, ukiwa pamoja na mataifa mengi, wote wakiwa wamepanda farasi, kundi kubwa, jeshi kuu.
Tu viendras de ton lieu de résidence, des extrémités du nord, toi et beaucoup de peuples avec toi, tous montés sur des chevaux, une grande troupe et une armée puissante.
16 Utakuja dhidi ya watu wangu Israeli kama wingu lifunikavyo nchi. Siku zijazo, ee Gogu, nitakuleta wewe dhidi ya nchi yangu, ili kwamba mataifa wapate kunijua Mimi nitakapojionyesha mtakatifu kwa kukupitia wewe mbele ya macho yao.
Tu monteras contre mon peuple d'Israël comme une nuée qui couvre le pays. C'est dans la suite des temps que je te ferai venir contre mon pays, afin que les nations me connaissent, quand je serai sanctifié en toi, Gog, sous leurs yeux. »
17 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, wewe si yule niliyenena juu yako katika siku za zamani kwa kupitia kwa watumishi wangu manabii wa Israeli? Wakati ule walitabiri kwa miaka mingi kwamba ningekuleta upigane nao.
"'Le Seigneur Yahvé dit: « Es-tu celui dont j'ai parlé autrefois par mes serviteurs les prophètes d'Israël, qui ont prophétisé en ces jours-là pendant des années que je te ferais venir contre eux?
18 Hili ndilo litakalotokea katika siku ile: Gogu atakaposhambulia nchi ya Israeli, hasira yangu kali itaamka, asema Bwana Mwenyezi.
En ce jour-là, quand Gog viendra contre le pays d'Israël, dit le Seigneur Yahvé, ma colère montera dans mes narines.
19 Katika wivu wangu na ghadhabu yangu kali ninasema kuwa wakati ule patakuwepo tetemeko kuu katika nchi ya Israeli.
Car j'ai parlé dans ma jalousie et dans le feu de ma colère. En ce jour-là, il y aura une grande secousse dans le pays d'Israël,
20 Samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa kondeni, kila kiumbe kitambaacho ardhini, na watu wote walio juu ya uso wa nchi watatetemeka mbele zangu. Milima itapinduka, majabali yatapasuka na kila ukuta utaanguka chini.
en sorte que les poissons de la mer, les oiseaux du ciel, les animaux des champs, tous les reptiles qui rampent sur la terre et tous les hommes qui sont à la surface de la terre trembleront en ma présence. Alors les montagnes seront renversées, les lieux escarpés s'écrouleront, et toutes les murailles tomberont à terre.
21 Nitaita upanga vita dhidi ya Gogu juu ya milima yangu yote, asema Bwana Mwenyezi. Upanga wa kila mtu utakuwa dhidi ya ndugu yake.
J'appellerai l'épée contre lui sur toutes mes montagnes, dit le Seigneur Yahvé. « L'épée de chacun sera contre son frère.
22 Nitatekeleza hukumu juu yake kwa tauni na kwa umwagaji wa damu. Nitaifanya mvua ya mafuriko kunyesha, mvua ya mawe na moto wa kiberiti juu yake na juu ya vikosi vyake na juu ya mataifa mengi walio pamoja naye.
J'entrerai en jugement avec lui par la peste et par le sang. Je ferai pleuvoir sur lui, sur ses hordes et sur les nombreux peuples qui sont avec lui, des pluies torrentielles avec de grosses grêles, du feu et du soufre.
23 Nami hivyo ndivyo nitakavyoonyesha ukuu wangu na utakatifu wangu, nami nitajijulisha mbele ya macho ya mataifa mengi. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’
Je me glorifierai et me sanctifierai, et je me ferai connaître aux yeux de nombreuses nations. Alors ils sauront que je suis Yahvé. »''

< Ezekieli 38 >