< Ezekieli 38 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
A message from the Lord came to me, saying,
2 “Mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya Gogu, katika nchi ya Magogu, mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali, tabiri dhidi yake
“Son of man, face towards Gog of the land of Magog, the chief prince of Meshech and Tubal. Prophesy against him
3 na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu, mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali.
and declare that this is what the Lord God says: Watch out, I am condemning you, Gog, chief prince of Meshech and Tubal.
4 Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukutia ndoana kwenye mataya yako na kukutoa nje wewe pamoja na jeshi lako lote, yaani, farasi wako, wapanda farasi wako waliojiandaa tayari kwa vita, pamoja na kundi kubwa la wajeuri wakiwa na ngao na vigao, wote wakipunga panga zao.
I will send you in a different direction, put hooks in your jaws, and drag you out with your whole army, including your horses, your horsemen in uniform, and a host of men with large and small shields and bucklers, all waving their swords.
5 Uajemi, Kushi na Putu watakuwa pamoja nao, wote wakiwa na ngao na kofia za chuma,
Soldiers from Persia, Cush, and Put will join them, all equipped with shields and helmets,
6 pia Gomeri pamoja na vikosi vyake vyote, na Beth-Togarma kutoka kaskazini ya mbali pamoja na vikosi vyake vyote, mataifa mengi wakiwa pamoja nawe.
together with Gomer and all its armies, as well as Beth-togarmah from the distant places of the north with all its armies—and many other nations that join with you.
7 “‘Jiandae, uwe tayari, wewe na makundi yako yote ya wajeuri yaliyokusanyika pamoja nawe, nawe waamrishe.
Get ready! Make sure you and your whole army with you is prepared. You're the one in charge of them.
8 Baada ya siku nyingi utaitwa vitani. Katika miaka ijayo, utaivamia nchi ile ambayo imepona kutoka vita, ambayo watu wake walikusanywa kutoka mataifa mengi kuja katika milima ya Israeli, ambayo kwa muda mrefu ilikuwa imeachwa ukiwa. Wameletwa kutoka mataifa na sasa wote wanaishi katika hali ya salama.
A long time later you will be called to battle. In the final years you will invade a country that has recovered from war. Its people will have been gathered from many nations to the mountains of Israel, which had been abandoned for a long time. They had been brought back from the nations, and were all living in safety.
9 Wewe na vikosi vyako vyote na mataifa mengi yaliyo pamoja nawe mtapanda juu, mtawazoa kama tufani na kuifunika nchi kama wingu.
You and your whole army, and the armies of many nations with you, will advance like an incoming storm, like a cloud that covers the land.
10 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile mawazo yataingia moyoni mwako nawe utapanga mipango mibaya.
This is what the Lord God says: On that day you will start thinking about things in your mind, and you will come up with an evil plan.
11 Utasema, “Nitapigana vita na nchi ambayo vijiji vyake havina maboma. Nitawashambulia watu wanaoishi kwa amani na wasiotarajia vita: wote wanaishi bila maboma na bila malango na makomeo.
You tell yourself, ‘I'm going to attack a country of undefended villages, a peaceful people who don't suspect an attack. They all live in towns without defensive walls or barred gates.
12 Nitateka mateka na kuchukua nyara mali za wale waliorudi kuishi katika mahame na wale watu waliokusanywa kutoka kwa mataifa, ambao sasa wana mifugo na mali nyingi, wanaoishi katikati ya nchi.”
I'll be able to loot them—I'll rob them of their possessions. I'll attack those places that were once ruined but now are inhabited again. I'll attack a people brought back from the other nations, who now own livestock and possessions, living in the center of the country.’
13 Sheba na Dedani pamoja na wafanyabiashara wa Tarshishi na vijiji vyake vyote watakuambia, “Je, umekuja kuteka mateka? Je, umekusanya makundi yako ya wajeuri ili kuchukua nyara mali, kutwaa fedha na dhahabu, kutunyangʼanya mifugo na mali na kuteka nyara nyingi zaidi?”’
Sheba and Dedan and the traders from Tarshish with all its strong leaders will ask, ‘Are you going to loot the place? Have you gathered your armies to rob them, to carry away silver and gold, to take cattle and possessions—to grab a great deal of plunder?’
14 “Kwa hiyo, mwanadamu, tabiri na umwambie Gogu: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile, watu wangu Israeli watakapokuwa wanaishi salama, Je, wewe mwenyewe hutalijua hilo?
So prophesy, son of man, and tell Gog that this is what the Lord God says: On the day you attack aren't you going to notice that my people Israel are unsuspecting?
15 Utakuja kutoka kwako huko kaskazini ya mbali, ukiwa pamoja na mataifa mengi, wote wakiwa wamepanda farasi, kundi kubwa, jeshi kuu.
You'll advance from your place in the distant north, you and your many allies, everyone riding horses, a huge number of men, a massive army.
16 Utakuja dhidi ya watu wangu Israeli kama wingu lifunikavyo nchi. Siku zijazo, ee Gogu, nitakuleta wewe dhidi ya nchi yangu, ili kwamba mataifa wapate kunijua Mimi nitakapojionyesha mtakatifu kwa kukupitia wewe mbele ya macho yao.
You will attack my people Israel like a cloud that covers the land. Gog, in the last days I will send you to attack my land, so that the nations may acknowledge me as holy when I reveal myself to them by what I do through you.
17 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, wewe si yule niliyenena juu yako katika siku za zamani kwa kupitia kwa watumishi wangu manabii wa Israeli? Wakati ule walitabiri kwa miaka mingi kwamba ningekuleta upigane nao.
This is what the Lord God says: Aren't you the one of whom I spoke about long ago through my servants, the prophets of Israel? During that time didn't they prophesy for years that I would have you come and attack them?
18 Hili ndilo litakalotokea katika siku ile: Gogu atakaposhambulia nchi ya Israeli, hasira yangu kali itaamka, asema Bwana Mwenyezi.
Now on that day, the day when Gog comes to attack the country of Israel, I will become very angry, declares the Lord God.
19 Katika wivu wangu na ghadhabu yangu kali ninasema kuwa wakati ule patakuwepo tetemeko kuu katika nchi ya Israeli.
In my passionate, furious anger I announce that at that time a violent earthquake will hit of the country of Israel.
20 Samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa kondeni, kila kiumbe kitambaacho ardhini, na watu wote walio juu ya uso wa nchi watatetemeka mbele zangu. Milima itapinduka, majabali yatapasuka na kila ukuta utaanguka chini.
Everything that lives on the earth will tremble at my presence—the fish in the sea, the birds in the sky, the wild animals, every creature that runs upon the ground, and every human being. The mountains will be torn down, the cliffs will collapse, and every wall will be knocked to the ground.
21 Nitaita upanga vita dhidi ya Gogu juu ya milima yangu yote, asema Bwana Mwenyezi. Upanga wa kila mtu utakuwa dhidi ya ndugu yake.
I will call for an attack on Gog from all my mountains, declares the Lord God. Everyone will attack his brother with sword.
22 Nitatekeleza hukumu juu yake kwa tauni na kwa umwagaji wa damu. Nitaifanya mvua ya mafuriko kunyesha, mvua ya mawe na moto wa kiberiti juu yake na juu ya vikosi vyake na juu ya mataifa mengi walio pamoja naye.
I will punish him with disease and bloodshed. I will send rainstorms, hailstones, fire, and sulfur down on him and his army, and on the armies of his many allies.
23 Nami hivyo ndivyo nitakavyoonyesha ukuu wangu na utakatifu wangu, nami nitajijulisha mbele ya macho ya mataifa mengi. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’
I will demonstrate my true power and holiness, revealing myself to many nations. Then they will acknowledge that I am the Lord.”

< Ezekieli 38 >