< Ezekieli 38 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
And the word of the Lord came to me, saying:
2 “Mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya Gogu, katika nchi ya Magogu, mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali, tabiri dhidi yake
“Son of man, set your face against Gog, the land of Magog, the prince of the head of Meshech and Tubal, and prophesy about him.
3 na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu, mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali.
And you shall say to him: Thus says the Lord God: Behold, I am against you, O Gog, prince of the head of Meshech and Tubal.
4 Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukutia ndoana kwenye mataya yako na kukutoa nje wewe pamoja na jeshi lako lote, yaani, farasi wako, wapanda farasi wako waliojiandaa tayari kwa vita, pamoja na kundi kubwa la wajeuri wakiwa na ngao na vigao, wote wakipunga panga zao.
And I will turn you around, and I will place a bit in your jaws. And I will lead you away, with all your army, the horses and the horsemen all clothed in armor, a great multitude, equipped with spears and light shields and swords,
5 Uajemi, Kushi na Putu watakuwa pamoja nao, wote wakiwa na ngao na kofia za chuma,
the Persians, the Ethiopians, and the Libyans with them, all with heavy shields and helmets,
6 pia Gomeri pamoja na vikosi vyake vyote, na Beth-Togarma kutoka kaskazini ya mbali pamoja na vikosi vyake vyote, mataifa mengi wakiwa pamoja nawe.
Gomer, and all his companies, the house of Togarmah, the northern parts, and all his strength, and the many peoples with you.
7 “‘Jiandae, uwe tayari, wewe na makundi yako yote ya wajeuri yaliyokusanyika pamoja nawe, nawe waamrishe.
Prepare and equip yourself, with all your multitude which has been assembled to you. And you shall be like a commandment to them.
8 Baada ya siku nyingi utaitwa vitani. Katika miaka ijayo, utaivamia nchi ile ambayo imepona kutoka vita, ambayo watu wake walikusanywa kutoka mataifa mengi kuja katika milima ya Israeli, ambayo kwa muda mrefu ilikuwa imeachwa ukiwa. Wameletwa kutoka mataifa na sasa wote wanaishi katika hali ya salama.
After many days, you will be visited. At the end of the years, you will arrive at the land which was turned back by the sword, and which has been gathered from many peoples to the mountains of Israel that have been continually abandoned. These ones have been led away from the peoples, and all of them will be living confidently within it.
9 Wewe na vikosi vyako vyote na mataifa mengi yaliyo pamoja nawe mtapanda juu, mtawazoa kama tufani na kuifunika nchi kama wingu.
But you will ascend and arrive like a tempest and like a cloud, so that you may cover the land, you and all your companies, and the many peoples with you.
10 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile mawazo yataingia moyoni mwako nawe utapanga mipango mibaya.
Thus says the Lord God: In that day, words will climb into your heart, and you will invent a most wicked plan.
11 Utasema, “Nitapigana vita na nchi ambayo vijiji vyake havina maboma. Nitawashambulia watu wanaoishi kwa amani na wasiotarajia vita: wote wanaishi bila maboma na bila malango na makomeo.
And you will say: ‘I will ascend to the land without a wall. I will go to those who are resting and dwelling securely. All these live without a wall; they have no bars or gates.’
12 Nitateka mateka na kuchukua nyara mali za wale waliorudi kuishi katika mahame na wale watu waliokusanywa kutoka kwa mataifa, ambao sasa wana mifugo na mali nyingi, wanaoishi katikati ya nchi.”
Thus, you will plunder spoils, and you will take possession of prey, so that you may lay your hand upon those who had been abandoned, and afterwards were restored, and upon a people who were gathered away from the Gentiles, a people who have begun to possess, and to be the inhabitants of, the navel of the earth.
13 Sheba na Dedani pamoja na wafanyabiashara wa Tarshishi na vijiji vyake vyote watakuambia, “Je, umekuja kuteka mateka? Je, umekusanya makundi yako ya wajeuri ili kuchukua nyara mali, kutwaa fedha na dhahabu, kutunyangʼanya mifugo na mali na kuteka nyara nyingi zaidi?”’
Sheba, and Dedan, and the merchants of Tarshish, and all its lions will say to you: ‘Could you have arrived in order to purchase from the spoils? Behold, you have gathered your multitude in order to plunder a prey, so that you may take silver and gold, and carry away equipment and substance, and plunder immeasurable wealth.’
14 “Kwa hiyo, mwanadamu, tabiri na umwambie Gogu: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile, watu wangu Israeli watakapokuwa wanaishi salama, Je, wewe mwenyewe hutalijua hilo?
Because of this, son of man, prophesy, and you shall say to Gog: Thus says the Lord God: How is it that you do not know of that day, when my people, Israel, will be living in confidence?
15 Utakuja kutoka kwako huko kaskazini ya mbali, ukiwa pamoja na mataifa mengi, wote wakiwa wamepanda farasi, kundi kubwa, jeshi kuu.
And you will advance from your place, from the parts of the north, you and the many peoples with you, all of them riding on horses, a great assembly and an immense army.
16 Utakuja dhidi ya watu wangu Israeli kama wingu lifunikavyo nchi. Siku zijazo, ee Gogu, nitakuleta wewe dhidi ya nchi yangu, ili kwamba mataifa wapate kunijua Mimi nitakapojionyesha mtakatifu kwa kukupitia wewe mbele ya macho yao.
And you will rise up over my people, Israel, like a cloud, so that you may cover the earth. In the latter days, you will be. And I will lead you over my own land, so that the Gentiles may know me, when I will have been sanctified in you, O Gog, before their eyes.
17 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, wewe si yule niliyenena juu yako katika siku za zamani kwa kupitia kwa watumishi wangu manabii wa Israeli? Wakati ule walitabiri kwa miaka mingi kwamba ningekuleta upigane nao.
Thus says the Lord God: Therefore, you are the one, about whom I spoke in the days of antiquity, by the hand of my servants the prophets of Israel, who prophesied in the days of those times that I would lead you over them.
18 Hili ndilo litakalotokea katika siku ile: Gogu atakaposhambulia nchi ya Israeli, hasira yangu kali itaamka, asema Bwana Mwenyezi.
And this shall be in that day, in the day of the advent of Gog over the land of Israel, says the Lord God: my indignation will rise up in my fury.
19 Katika wivu wangu na ghadhabu yangu kali ninasema kuwa wakati ule patakuwepo tetemeko kuu katika nchi ya Israeli.
And I have spoken, in my zeal and in the fire of my wrath, that there shall be a great commotion over the land of Israel, in that day.
20 Samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa kondeni, kila kiumbe kitambaacho ardhini, na watu wote walio juu ya uso wa nchi watatetemeka mbele zangu. Milima itapinduka, majabali yatapasuka na kila ukuta utaanguka chini.
And before my face there shall be stirred up: the fish of the sea, and the flying things of the air, and the beasts of the field, and every crawling thing that moves across the soil, and all the men who are upon the face of the earth. And the mountains will be overturned, and the hedges will fall, and every wall will fall in ruin to the ground.
21 Nitaita upanga vita dhidi ya Gogu juu ya milima yangu yote, asema Bwana Mwenyezi. Upanga wa kila mtu utakuwa dhidi ya ndugu yake.
And I will call for the sword against him on all my mountains, says the Lord God. Each one’s sword will be directed toward his brother.
22 Nitatekeleza hukumu juu yake kwa tauni na kwa umwagaji wa damu. Nitaifanya mvua ya mafuriko kunyesha, mvua ya mawe na moto wa kiberiti juu yake na juu ya vikosi vyake na juu ya mataifa mengi walio pamoja naye.
And I will judge him by pestilence, and blood, and violent rainstorms, and immense hailstones. I will rain fire and brimstone upon him, and upon his army, and upon the many peoples who are with him.
23 Nami hivyo ndivyo nitakavyoonyesha ukuu wangu na utakatifu wangu, nami nitajijulisha mbele ya macho ya mataifa mengi. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’
And I will be magnified and sanctified. And I will be known in the eyes of the many nations. And they shall know that I am the Lord.”

< Ezekieli 38 >