< Ezekieli 38 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
And the word of the Lord came to me, saying,
2 “Mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya Gogu, katika nchi ya Magogu, mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali, tabiri dhidi yake
Son of man, let your face be turned against Gog, of the land of Magog, the ruler of Rosh, Meshech, and Tubal, and be a prophet against him,
3 na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu, mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali.
And say, This is what the Lord has said: See, I am against you, O Gog, ruler of Rosh, Meshech, and Tubal:
4 Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukutia ndoana kwenye mataya yako na kukutoa nje wewe pamoja na jeshi lako lote, yaani, farasi wako, wapanda farasi wako waliojiandaa tayari kwa vita, pamoja na kundi kubwa la wajeuri wakiwa na ngao na vigao, wote wakipunga panga zao.
And turning you round, I will put hooks in your mouth and make you come out with all your army, horses and horsemen, all of them in full war-dress, a great force with breastplate and body-cover, all of them armed with swords:
5 Uajemi, Kushi na Putu watakuwa pamoja nao, wote wakiwa na ngao na kofia za chuma,
Persia, Cush, and Put with them; all of them with body-cover and metal head-dress:
6 pia Gomeri pamoja na vikosi vyake vyote, na Beth-Togarma kutoka kaskazini ya mbali pamoja na vikosi vyake vyote, mataifa mengi wakiwa pamoja nawe.
Gomer and all her forces; the people of Togarmah in the inmost parts of the north, with all his forces: a great number of peoples with you.
7 “‘Jiandae, uwe tayari, wewe na makundi yako yote ya wajeuri yaliyokusanyika pamoja nawe, nawe waamrishe.
Be ready, make yourself ready, you and all the forces who are with you, and be ready for my orders.
8 Baada ya siku nyingi utaitwa vitani. Katika miaka ijayo, utaivamia nchi ile ambayo imepona kutoka vita, ambayo watu wake walikusanywa kutoka mataifa mengi kuja katika milima ya Israeli, ambayo kwa muda mrefu ilikuwa imeachwa ukiwa. Wameletwa kutoka mataifa na sasa wote wanaishi katika hali ya salama.
After a long time you will get your orders: in the last years you will come into the land which has been given back from the sword, which has been got together out of a great number of peoples, on the mountains of Israel which have ever been a waste: but it has been taken out from the peoples and they will be living, all of them, without fear of danger.
9 Wewe na vikosi vyako vyote na mataifa mengi yaliyo pamoja nawe mtapanda juu, mtawazoa kama tufani na kuifunika nchi kama wingu.
And you will go up, you will come like a storm, you will be like a cloud covering the land, you and all your forces, and a great number of peoples with you.
10 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile mawazo yataingia moyoni mwako nawe utapanga mipango mibaya.
This is what the Lord has said: In that day it will come about that things will come into your mind, and you will have thoughts of an evil design:
11 Utasema, “Nitapigana vita na nchi ambayo vijiji vyake havina maboma. Nitawashambulia watu wanaoishi kwa amani na wasiotarajia vita: wote wanaishi bila maboma na bila malango na makomeo.
And you will say, I will go up to the land of small unwalled towns; I will go to those who are quiet, living, all of them, without fear of danger, without walls or locks or doors:
12 Nitateka mateka na kuchukua nyara mali za wale waliorudi kuishi katika mahame na wale watu waliokusanywa kutoka kwa mataifa, ambao sasa wana mifugo na mali nyingi, wanaoishi katikati ya nchi.”
To take their property by force and go off with their goods; turning your hand against the waste places which now are peopled, and against the people who have been got together out of the nations, who have got cattle and goods for themselves, who are living in the middle of the earth.
13 Sheba na Dedani pamoja na wafanyabiashara wa Tarshishi na vijiji vyake vyote watakuambia, “Je, umekuja kuteka mateka? Je, umekusanya makundi yako ya wajeuri ili kuchukua nyara mali, kutwaa fedha na dhahabu, kutunyangʼanya mifugo na mali na kuteka nyara nyingi zaidi?”’
Sheba, and Dedan and her traders, Tarshish with all her traders, will say to you, Have you come to take our goods? have you got your armies together to take away our property by force? to take away silver and gold, cattle and goods, to go off with great wealth?
14 “Kwa hiyo, mwanadamu, tabiri na umwambie Gogu: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile, watu wangu Israeli watakapokuwa wanaishi salama, Je, wewe mwenyewe hutalijua hilo?
For this cause, son of man, be a prophet and say to Gog, These are the words of the Lord: In that day, when my people Israel are living without fear of danger, will you not be moved against them?
15 Utakuja kutoka kwako huko kaskazini ya mbali, ukiwa pamoja na mataifa mengi, wote wakiwa wamepanda farasi, kundi kubwa, jeshi kuu.
And you will come from your place in the inmost parts of the north, you and a great number of peoples with you, all of them on horseback, a great force and a strong army:
16 Utakuja dhidi ya watu wangu Israeli kama wingu lifunikavyo nchi. Siku zijazo, ee Gogu, nitakuleta wewe dhidi ya nchi yangu, ili kwamba mataifa wapate kunijua Mimi nitakapojionyesha mtakatifu kwa kukupitia wewe mbele ya macho yao.
And you will come up against my people Israel, like a cloud covering the land; and it will come about, in the last days, that I will make you come against my land, so that the nations may have knowledge of me when I make myself holy in you, O Gog, before their eyes.
17 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, wewe si yule niliyenena juu yako katika siku za zamani kwa kupitia kwa watumishi wangu manabii wa Israeli? Wakati ule walitabiri kwa miaka mingi kwamba ningekuleta upigane nao.
This is what the Lord has said: You are he of whom I gave them word in earlier times by my servants, the prophets of Israel, who in those days went on saying, year after year, that I would make you come up against them.
18 Hili ndilo litakalotokea katika siku ile: Gogu atakaposhambulia nchi ya Israeli, hasira yangu kali itaamka, asema Bwana Mwenyezi.
And it will come about in that day, when Gog comes up against the land of Israel, says the Lord, that my wrath will come up, and my passion and my bitter feeling.
19 Katika wivu wangu na ghadhabu yangu kali ninasema kuwa wakati ule patakuwepo tetemeko kuu katika nchi ya Israeli.
For in the fire of my wrath I have said, Truly, in that day there will be a great shaking in the land of Israel;
20 Samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa kondeni, kila kiumbe kitambaacho ardhini, na watu wote walio juu ya uso wa nchi watatetemeka mbele zangu. Milima itapinduka, majabali yatapasuka na kila ukuta utaanguka chini.
So that the fish of the sea and the birds of heaven and the beasts of the field and everything moving on the earth, and all the men who are on the face of the earth, will be shaking before me, and the mountains will be overturned and the high places will come down, and every wall will come falling down to the earth.
21 Nitaita upanga vita dhidi ya Gogu juu ya milima yangu yote, asema Bwana Mwenyezi. Upanga wa kila mtu utakuwa dhidi ya ndugu yake.
And I will send to all my mountains for a sword against him, says the Lord: every man's sword will be against his brother.
22 Nitatekeleza hukumu juu yake kwa tauni na kwa umwagaji wa damu. Nitaifanya mvua ya mafuriko kunyesha, mvua ya mawe na moto wa kiberiti juu yake na juu ya vikosi vyake na juu ya mataifa mengi walio pamoja naye.
And I will take up my cause against him with disease and with blood; and I will send down on him and on his forces and on the peoples who are with him, an overflowing shower and great ice-drops, fire, and burning.
23 Nami hivyo ndivyo nitakavyoonyesha ukuu wangu na utakatifu wangu, nami nitajijulisha mbele ya macho ya mataifa mengi. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’
And I will make my name great and make myself holy, and I will make myself clear to a number of nations; and they will be certain that I am the Lord.

< Ezekieli 38 >