< Ezekieli 38 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
HERRENs Ord kom til mig således:
2 “Mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya Gogu, katika nchi ya Magogu, mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali, tabiri dhidi yake
Menneskesøn, vend dit Ansigt mod Gog i Magogs Land, Fyrsten over Rosj, Mesjek og Tubal, og profeter imod ham
3 na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu, mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali.
og sig: Så siger den Herre HERREN: Se, jeg kommer over dig, Gog, Fyrste over Rosj, Mesjek og Tubal.
4 Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukutia ndoana kwenye mataya yako na kukutoa nje wewe pamoja na jeshi lako lote, yaani, farasi wako, wapanda farasi wako waliojiandaa tayari kwa vita, pamoja na kundi kubwa la wajeuri wakiwa na ngao na vigao, wote wakipunga panga zao.
Jeg vender dig og sætter Kroge i dine Kæber og trækker dig frem med hele din Hær, Heste og Ryttere, alle i smukke Klæder, en vældig Skare med store og små Skjolde, alle med Sværd i Hånd.
5 Uajemi, Kushi na Putu watakuwa pamoja nao, wote wakiwa na ngao na kofia za chuma,
Persere, Ætiopere og Putæere er med dem, alle med Skjold og Hjelm,
6 pia Gomeri pamoja na vikosi vyake vyote, na Beth-Togarma kutoka kaskazini ya mbali pamoja na vikosi vyake vyote, mataifa mengi wakiwa pamoja nawe.
Gomer med alle dets Hobe, Togarmas Hus fra det yderste Nord med alle dets Hobe, mange Folkeslag er med.
7 “‘Jiandae, uwe tayari, wewe na makundi yako yote ya wajeuri yaliyokusanyika pamoja nawe, nawe waamrishe.
Rust dig og hold dig rede med hele din Skare, som er samlet om dig, og vær mig rede til Tjeneste.
8 Baada ya siku nyingi utaitwa vitani. Katika miaka ijayo, utaivamia nchi ile ambayo imepona kutoka vita, ambayo watu wake walikusanywa kutoka mataifa mengi kuja katika milima ya Israeli, ambayo kwa muda mrefu ilikuwa imeachwa ukiwa. Wameletwa kutoka mataifa na sasa wote wanaishi katika hali ya salama.
Lang Tid herefter skal der komme Bud efter dig; ved Årenes Fjende skal du overfalde et Land, som atter er unddraget Sværdet, et Folk, som fra mange Folkeslag er sanket sammen på Israels Bjerge, der stadig lå øde hen, et Folk, som er ført bort fra Folkeslagene og nu bor trygt til Hobe.
9 Wewe na vikosi vyako vyote na mataifa mengi yaliyo pamoja nawe mtapanda juu, mtawazoa kama tufani na kuifunika nchi kama wingu.
Du skal trække op som et Uvejr og komme som en Sky og oversvømme Landet, du og alle dine Hobe og de mange Folkeslag, som følger dig.
10 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile mawazo yataingia moyoni mwako nawe utapanga mipango mibaya.
Så siger den Herre HERREN: På hin Dag skal en Tanke stige op i dit Hjerte, og du skal oplægge onde Råd
11 Utasema, “Nitapigana vita na nchi ambayo vijiji vyake havina maboma. Nitawashambulia watu wanaoishi kwa amani na wasiotarajia vita: wote wanaishi bila maboma na bila malango na makomeo.
og sige: "Jeg vil drage op imod et åbent Land og overfalde fredelige Folk, som bor trygt, som alle bor uden Mure og hverken har Portstænger eller Porte,
12 Nitateka mateka na kuchukua nyara mali za wale waliorudi kuishi katika mahame na wale watu waliokusanywa kutoka kwa mataifa, ambao sasa wana mifugo na mali nyingi, wanaoishi katikati ya nchi.”
for at gøre Bytte og røve Rov, lægge Hånd på genopbyggede ruiner og på et Folk, der er indsamlet fra Folkene og vinder sig Fæ og Gods, og som bor på Jordens Navle."
13 Sheba na Dedani pamoja na wafanyabiashara wa Tarshishi na vijiji vyake vyote watakuambia, “Je, umekuja kuteka mateka? Je, umekusanya makundi yako ya wajeuri ili kuchukua nyara mali, kutwaa fedha na dhahabu, kutunyangʼanya mifugo na mali na kuteka nyara nyingi zaidi?”’
Sabæerne og Dedaniterne, Tarsiss Købmænd og alle dets Handelsfolk skal sige til dig: "Kommer du for at gøre Bytte, har du samlet din Skare for at røve Rov, for at bortføre Sølv og Guld, rane Fæ og Gods og gøre et vældigt Bytte?"
14 “Kwa hiyo, mwanadamu, tabiri na umwambie Gogu: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile, watu wangu Israeli watakapokuwa wanaishi salama, Je, wewe mwenyewe hutalijua hilo?
Profeter derfor, Menneskesøn, og sig til Gog: Så siger den Herre HERREN: Ja, på hin Dag skal du bryde op, medens mit Folk Israel bor trygt,
15 Utakuja kutoka kwako huko kaskazini ya mbali, ukiwa pamoja na mataifa mengi, wote wakiwa wamepanda farasi, kundi kubwa, jeshi kuu.
og komme fra din Hjemstavn yderst i Nord, du og de mange Folkeslag, der følger dig, alle til Hest, en stor Skare, en vældig Hær;
16 Utakuja dhidi ya watu wangu Israeli kama wingu lifunikavyo nchi. Siku zijazo, ee Gogu, nitakuleta wewe dhidi ya nchi yangu, ili kwamba mataifa wapate kunijua Mimi nitakapojionyesha mtakatifu kwa kukupitia wewe mbele ya macho yao.
som en Sky skal du drage op mod mit Folk Israel og oversvømme Landet. I de sidste Dage skal det ske; jeg fører dig imod mit Land; og Folkene skal kende mig, når jeg for deres Øjne helliger mig på dig, Gog.
17 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, wewe si yule niliyenena juu yako katika siku za zamani kwa kupitia kwa watumishi wangu manabii wa Israeli? Wakati ule walitabiri kwa miaka mingi kwamba ningekuleta upigane nao.
Så siger den Herre HERREN: Er det dig, jeg talede om i gamle dage ved mine Tjenere, Israels Profeter, som profeterede i hine Tider, at jeg vilde bringe dig over dem?
18 Hili ndilo litakalotokea katika siku ile: Gogu atakaposhambulia nchi ya Israeli, hasira yangu kali itaamka, asema Bwana Mwenyezi.
Men på hin dag, når Gog overfalder Israels Land, lyder det fra den Herre HERREN, vil jeg give min Vrede Luft.
19 Katika wivu wangu na ghadhabu yangu kali ninasema kuwa wakati ule patakuwepo tetemeko kuu katika nchi ya Israeli.
I Nidkærhed, i glødende Vrede udtaler jeg det: Sandelig, på hin Dag skal et vældigt Jordskælv komme over Israels Land;
20 Samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa kondeni, kila kiumbe kitambaacho ardhini, na watu wote walio juu ya uso wa nchi watatetemeka mbele zangu. Milima itapinduka, majabali yatapasuka na kila ukuta utaanguka chini.
for mit Åsyn skal Havets Fisk, Himmelens Fugle, Markens vilde Dyr og alt kryb på Jorden og alle Mennesker på Jordens Flade skælve, Bjergene skal styrte, Klippevæggene falde og hver Mur synke til Jord.
21 Nitaita upanga vita dhidi ya Gogu juu ya milima yangu yote, asema Bwana Mwenyezi. Upanga wa kila mtu utakuwa dhidi ya ndugu yake.
Jeg nedkalder alle Rædsler over ham, lyder det fra den Herre HERREN; den enes Sværd skal rettes mod den anden;
22 Nitatekeleza hukumu juu yake kwa tauni na kwa umwagaji wa damu. Nitaifanya mvua ya mafuriko kunyesha, mvua ya mawe na moto wa kiberiti juu yake na juu ya vikosi vyake na juu ya mataifa mengi walio pamoja naye.
jeg går i Rette med ham med Pest og Blod, med Regnskyl og Haglsten; Ild og Svovl lader jeg regne over ham, hans Hobe og de mange Folkeslag, som følger ham.
23 Nami hivyo ndivyo nitakavyoonyesha ukuu wangu na utakatifu wangu, nami nitajijulisha mbele ya macho ya mataifa mengi. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’
Jeg viser mig stor og hellig og giver mig til Kende for de mange Folks Øjne; og de skal kende, at jeg er HERREN.

< Ezekieli 38 >