< Ezekieli 36 >

1 “Mwanadamu, itabirie milima ya Israeli na useme, ‘Ee milima ya Israeli, sikieni neno la Bwana.
“İnsanoğlu, İsrail dağlarına peygamberlik et ve de ki, ‘Ey İsrail dağları, RAB'bin sözünü dinleyin!
2 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu adui wanasema juu yako, “Aha! Mahali palipoinuka pa zamani pamekuwa milki yetu.”’
Egemen RAB şöyle diyor: Düşman sizin hakkınızda, Hah, hah! Bu eski tepeler mülkümüz oldu! dediği için
3 Kwa hiyo tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu wamewafanya ukiwa na kuwagandamiza kila upande ili mpate kuwa milki ya mataifa mengine na kuwa kitu cha kusimangwa na kudhihakiwa miongoni mwa watu,
peygamberlik et ve de ki, Egemen RAB şöyle diyor: Dağlarınızı viran ettiler, sizi her yandan sıkıştırıp çiğnediler; böylece ulusların mülkü oldunuz, dile düştünüz, alay konusu oldunuz,
4 kwa hiyo, ee milima ya Israeli, sikieni neno la Bwana Mwenyezi: Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kwa milima na vilima, kwa makorongo na mabonde, kwa mahame yaliyo ukiwa, miji iliyoachwa ambayo imetekwa nyara na kudharauliwa na mataifa mengine yanayowazunguka,
ey İsrail dağları, Egemen RAB'bin sözünü dinleyin! Egemen RAB dağlarla tepelere, vadilerle derelere, yıkıntılara, çevrenizdeki ulusların yağmasına, alayına uğramış, terk edilmiş kentlere şöyle diyor:
5 hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika wivu wangu uwakao nimenena dhidi ya mataifa mengine na dhidi ya Edomu yote, kwa maana kwa furaha na hila katika mioyo yao waliifanya nchi yangu kuwa milki yao ili wapate kuteka nyara sehemu yake ya malisho.’
Egemen RAB şöyle diyor: Yürekleri sevinç dolu, aşağılayarak otlaklarınızı yağmalamak için ülkeme sahip çıkan öteki uluslara, özellikle Edom'a karşı büyük bir kıskançlıkla konuştum.’
6 Kwa hiyo tabiri kuhusu nchi ya Israeli na uiambie milima na vilima, makorongo na vijito na mabonde: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninanena katika wivu wa ghadhabu yangu kwa sababu mmedharauliwa na mataifa.
Bu nedenle İsrail ülkesi için peygamberlik et ve dağlara, tepelere, vadilere, derelere de ki, ‘Egemen RAB şöyle diyor: Ulusların aşağılamasına hedef olduğunuz için öfkeyle, kıskançlıkla konuştum.
7 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninaapa kwa mkono wangu ulioinuliwa kwamba mataifa wanaowazunguka nao pia watadharauliwa.
Bu nedenle Egemen RAB şöyle diyor: Ant içiyorum ki, çevrenizdeki uluslar da aşağılanacaktır.
8 “‘Lakini ninyi, ee milima ya Israeli, mtatoa matawi na matunda kwa ajili ya watu wangu Israeli, kwa sababu hivi karibuni watakuja nyumbani.
“‘Ama siz, ey İsrail dağları, dal budak salacak ve halkım İsrail için ürün vereceksiniz. Çünkü halkım İsrail yakında yurduna dönecek.
9 Mimi ninawajibika nanyi na nitawaangalia kwa upendeleo, mtalimwa na kupandwa mbegu,
Sizi kayıracak, size yöneleceğim. İşlenecek, ekileceksiniz.
10 nami nitaizidisha idadi ya watu kwenu, naam, nyumba yote ya Israeli. Miji itakaliwa na watu na magofu yatajengwa upya.
Ülkenizde yaşayanların sayısını, evet, bütün İsrail halkının sayısını çoğaltacağım. Kentlerde insanlar yaşayacak, yıkıntılar onarılacak.
11 Nitaongeza idadi ya watu na wanyama juu yenu, nao watazaana sana na kuwa wengi mno. Nitawakalisha watu ndani yenu kama ilivyokuwa wakati uliopita, nami nitawafanya mfanikiwe kuliko hapo kwanza. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Ülkenizdeki insan ve hayvan sayısını çoğaltacağım. Verimli olacak, çoğalacaklar. Geçmişte olduğu gibi ülkeniz insanlarla dolup taşacak. Sizi eskisinden daha verimli kılacağım. O zaman benim RAB olduğumu anlayacaksınız.
12 Nitawafanya watu, watu wangu Israeli, kutembea juu yenu. Watawamiliki ninyi, nanyi mtakuwa urithi wao, kamwe hamtawaondolea tena watoto wao.
Ülkenize insanların, halkım İsrail'in girmesini sağlayacağım. Sizi sahiplenecekler. Siz de onların mirası olacaksınız. Onları bir daha çocuklarından yoksun bırakmayacaksınız.
13 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu watu wanakuambia, “Unawala watu na kuliondolea taifa lako watoto wake,”
“‘Egemen RAB şöyle diyor: Ey ülke, insanlar sana insan yiyen, ulusunu çocuksuz bırakan ülke diyorlar.
14 kwa hiyo hutakula tena watu wala kulifanya tena taifa lako lisiwe na watoto, asema Bwana Mwenyezi.
Bundan böyle artık sen insan yemeyecek, ulusunu çocuksuz bırakmayacaksın. Egemen RAB böyle diyor.
15 Sitakufanya tena usikie dhihaka za mataifa, wala kudharauliwa na kabila za watu, wala kulifanya taifa lako lianguke, asema Bwana Mwenyezi.’”
Artık ulusların aşağılamalarını size işittirmeyeceğim. Ulusların aşağılamasına uğramayacaksınız. Halkınızın bir daha tökezlemesine izin vermeyeceksiniz.’ Egemen RAB böyle diyor.”
16 Neno la Bwana likanijia tena, kusema:
RAB bana şöyle seslendi:
17 “Mwanadamu, nyumba ya Israeli walipokuwa wakiishi katika nchi yao wenyewe, waliinajisi kwa mwenendo wao na matendo yao. Mwenendo wao mbele zangu ulikuwa kama mwanamke aliye katika hedhi.
“İnsanoğlu, İsrail halkı kendi ülkesinde yaşarken tutumu ve davranışlarıyla ülkeyi kirletti. Onların davranışı benim gözümde âdet gören bir kadının kirliliği gibiydi.
18 Hivyo nilimwaga ghadhabu yangu juu yao kwa sababu walikuwa wamemwaga damu katika nchi na kwa sababu walikuwa wameitia nchi unajisi kwa sanamu zao.
Bu yüzden öfkemi üzerlerine boşalttım. Çünkü ülkede kan döktüler, putlarıyla onu kirlettiler.
19 Nikawatawanya miongoni mwa mataifa, nao wakaenda huku na huko katika nchi mbalimbali, nikawahukumu sawasawa na mwenendo wao na matendo yao.
Onları uluslara dağıttım, ülkelere yayıldılar. Onları tutumlarına ve davranışlarına göre yargıladım.
20 Tena popote walipokwenda miongoni mwa mataifa walilitia unajisi Jina langu takatifu, kwa kuwa watu walisema kuwahusu, ‘Hawa ndio watu wa Bwana, lakini imewapasa kuondoka katika nchi yake.’
Ulusların arasında her gittikleri yerde kutsal adımı kirlettiler. Çünkü onlar için, ‘Bu RAB'bin halkı, öyleyken ülkesinden çıkmak zorunda kaldı’ dendi.
21 Lakini niliwahurumia kwa ajili ya Jina langu takatifu, ambalo nyumba ya Israeli imelitia unajisi miongoni mwa mataifa huko walikokwenda.
İsrail halkının gittiği uluslar arasında kirlettiği kutsal adımın onuru için kaygılandım.
22 “Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Si kwa ajili yako, ee nyumba ya Israeli, kwamba ninafanya mambo haya, bali ni kwa ajili ya Jina langu takatifu, ambalo mmelitia unajisi miongoni mwa mataifa mliyoyaendea.
“Bu nedenle İsrail halkına de ki, ‘Egemen RAB şöyle diyor: Ey İsrail halkı, sizin hatırınız için değil, gittiğiniz uluslar arasında kirlettiğiniz kutsal adımın hatırı için bunları yapacağım.
23 Nitauonyesha utakatifu wa Jina langu kuu, ambalo limetiwa unajisi miongoni mwa mataifa, jina ambalo limetiwa unajisi miongoni mwao. Ndipo mataifa watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana, asema Bwana Mwenyezi, nitakapojionyesha mwenyewe kuwa mtakatifu kwa kuwapitia ninyi mbele ya macho yao.
Uluslar arasında kirlenen, onlar arasında kirlettiğiniz büyük adımın kutsallığını göstereceğim. Onların gözü önünde kutsallığımı sizin aracılığınızla kanıtladığımda, uluslar benim RAB olduğumu anlayacaklar. Egemen RAB böyle diyor.
24 “‘Kwa kuwa nitawaondoa ninyi toka mataifa, nitawakusanya kutoka nchi zote na kuwarudisha kwenye nchi yenu wenyewe.
“‘Sizi uluslar arasından alacak, bütün ülkelerden toplayıp ülkenize geri getireceğim.
25 Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi, nitawatakasa kutoka uchafu wenu wote na kutoka sanamu zenu zote.
Üzerinize temiz su dökeceğim, arınacaksınız. Sizi bütün kirliliklerinizden ve putlarınızdan arındıracağım.
26 Nitawapa moyo mpya na kuweka roho mpya ndani yenu, nitaondoa ndani yenu moyo wenu wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama.
Size yeni bir yürek verecek, içinize yeni bir ruh koyacağım. İçinizdeki taştan yüreği çıkaracak, size etten bir yürek vereceğim.
27 Nami nitaweka Roho yangu ndani yenu na kuwafanya ninyi mfuate amri zangu na kuwafanya kuwa waangalifu kuzishika sheria zangu.
Ruhumu içinize koyacağım; kurallarımı izlemenizi, buyruklarıma uyup onları uygulamanızı sağlayacağım.
28 Mtaishi katika nchi niliyowapa baba zenu, ninyi mtakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wenu.
Atalarınıza verdiğim ülkede yaşayacak, benim halkım olacaksınız, ben de sizin Tanrınız olacağım.
29 Nitawaokoa ninyi kutoka unajisi wenu wote. Nitaiita nafaka na kuiongeza iwe nyingi sana nami sitaleta njaa juu yenu.
Sizi bütün kirliliklerinizden kurtaracağım. Buğdaya seslenecek ve onu çoğaltacağım. Artık size kıtlık göndermeyeceğim.
30 Nitaongeza matunda ya miti na mazao ya mashamba, ili kwamba msipate tena aibu miongoni mwa mataifa kwa ajili ya njaa.
Ulusların arasında bir daha kıtlık utancı çekmemeniz için ağaçların meyvesini, tarlaların ürününü çoğaltacağım.
31 Ndipo mtakapozikumbuka njia zenu za uovu na matendo yenu maovu, nanyi mtajichukia wenyewe kwa ajili ya dhambi zote na matendo yenu ya kuchukiza.
O zaman kötü yollarınızı, kötü işlerinizi anımsayacaksınız. Günahlarınız, iğrenç uygulamalarınız yüzünden kendinizden tiksineceksiniz.
32 Ninataka ninyi mjue kwamba sifanyi hili kwa ajili yenu, asema Bwana Mwenyezi. Oneni aibu na mkatahayari kwa ajili ya mwenendo wenu, ee nyumba ya Israeli!
Bunu sizin hatırınız için yapmadığımı iyi bilin. Egemen RAB böyle diyor. Davranışlarınızdan utanın, yüzünüz kızarsın, ey İsrail halkı!
33 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Siku ile nitakapowasafisha kutoka dhambi zenu zote, nitarudisha watu waishi katika miji yenu na magofu yatajengwa upya.
“‘Egemen RAB şöyle diyor: Sizi bütün günahlarınızdan arıttığım gün, kentlerinizde yaşamanızı sağlayacağım; yıkıntılar onarılacak.
34 Nchi iliyokuwa ukiwa italimwa badala ya kukaa ukiwa machoni mwa wale wote wanaopita ndani yake.
Gelip geçenlerin gözünde viran olan ülkenin toprakları işlenecek.
35 Watasema, “Hii nchi iliyokuwa imeachwa ukiwa sasa imekuwa kama bustani ya Edeni, miji ile iliyokuwa magofu, ukiwa na kuangamizwa, sasa imejengewa ngome na kukaliwa na watu.”
Şöyle diyecekler: Viran olan bu ülke Aden bahçesi gibi oldu; yıkılıp yerle bir olmuş, kimsesiz kalmış kentler yeniden güçlendiriliyor, içinde oturuluyor.
36 Ndipo mataifa yanayowazunguka yaliyobakia watakapojua kuwa Mimi Bwana nimejenga tena kile kilichoharibiwa na nimepanda tena kile kilichokuwa ukiwa. Mimi Bwana nimenena, nami nitalifanya.’
O zaman çevrenizde kalan uluslar yıkılanı yeniden yapanın, çıplak yerleri yeniden dikenin ben RAB olduğumu anlayacaklar. Bunu ben RAB söylüyorum ve dediğimi yapacağım.’
37 “Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mara nyingine tena nitasikia maombi ya nyumba ya Israeli na kuwatendea jambo hili: Nitawafanya watu wake kuwa wengi kama kondoo,
“Egemen RAB şöyle diyor: İsrail halkının benden yine yardım dilemesini sağlayacak ve onlar için şunu yapacağım: Onları bir koyun sürüsü gibi çoğaltacağım.
38 kuwa wengi kama kundi la kondoo kwa ajili ya dhabihu huko Yerusalemu wakati wa sikukuu zao za wakati ulioamriwa. Hivyo ndivyo miji iliyokuwa magofu itajazwa na makundi ya watu. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
Bayramlarda Yeruşalim nasıl kurbanlık hayvanlarla doluyorsa, viran olmuş kentler de insan topluluklarıyla öyle dolup taşacak. O zaman benim RAB olduğumu anlayacaklar.”

< Ezekieli 36 >