< Ezekieli 36 >

1 “Mwanadamu, itabirie milima ya Israeli na useme, ‘Ee milima ya Israeli, sikieni neno la Bwana.
A ty, synu człowieczy, prorokuj o górach Izraela i mów: Góry Izraela, słuchajcie słowa PANA.
2 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu adui wanasema juu yako, “Aha! Mahali palipoinuka pa zamani pamekuwa milki yetu.”’
Tak mówi Pan BÓG: Ponieważ wróg powiedział o was: Ha! Prastare wysokości stały się naszą posiadłością;
3 Kwa hiyo tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu wamewafanya ukiwa na kuwagandamiza kila upande ili mpate kuwa milki ya mataifa mengine na kuwa kitu cha kusimangwa na kudhihakiwa miongoni mwa watu,
Prorokuj i mów: Tak mówi Pan BÓG: Ponieważ zburzono was i pochłonięto zewsząd, abyście się stały dziedzictwem reszty narodów i wzięto was na język oraz na obmowę ludzi;
4 kwa hiyo, ee milima ya Israeli, sikieni neno la Bwana Mwenyezi: Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kwa milima na vilima, kwa makorongo na mabonde, kwa mahame yaliyo ukiwa, miji iliyoachwa ambayo imetekwa nyara na kudharauliwa na mataifa mengine yanayowazunguka,
Dlatego, góry Izraela, słuchajcie słowa Pana BOGA. Tak mówi Pan BÓG do gór i pagórków, do strumieni i dolin, do spustoszonych ruin i opuszczonych miast, które stały się łupem i pośmiewiskiem dla reszty okolicznych narodów.
5 hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika wivu wangu uwakao nimenena dhidi ya mataifa mengine na dhidi ya Edomu yote, kwa maana kwa furaha na hila katika mioyo yao waliifanya nchi yangu kuwa milki yao ili wapate kuteka nyara sehemu yake ya malisho.’
Dlatego tak mówi Pan BÓG: Zaprawdę, w ogniu swojej zapalczywości będę mówił przeciw reszcie tych narodów i przeciwko całemu Edomowi, którzy wzięli sobie moją ziemię w posiadanie z radością całego serca i z pogardą duszy, aby siedlisko jej wygnańców stało się łupem.
6 Kwa hiyo tabiri kuhusu nchi ya Israeli na uiambie milima na vilima, makorongo na vijito na mabonde: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninanena katika wivu wa ghadhabu yangu kwa sababu mmedharauliwa na mataifa.
Dlatego prorokuj o ziemi Izraela i mów do gór i pagórków, do strumieni i dolin: Tak mówi Pan BÓG: Oto przemówiłem w swojej zazdrości i w swojej zapalczywości, ponieważ znosiliście zniewagi narodów.
7 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninaapa kwa mkono wangu ulioinuliwa kwamba mataifa wanaowazunguka nao pia watadharauliwa.
Dlatego tak mówi Pan BÓG: Ja podniosłem swoją rękę: Zaprawdę, te narody, które są wokół was, same będą znosić swoją hańbę.
8 “‘Lakini ninyi, ee milima ya Israeli, mtatoa matawi na matunda kwa ajili ya watu wangu Israeli, kwa sababu hivi karibuni watakuja nyumbani.
A wy, góry Izraela, wypuścicie swe gałązki i wydacie swój owoc memu ludowi Izraela, bo zbliża się jego przyjście.
9 Mimi ninawajibika nanyi na nitawaangalia kwa upendeleo, mtalimwa na kupandwa mbegu,
Oto bowiem [idę] do was i powrócę do was, będziecie uprawiane i obsiane.
10 nami nitaizidisha idadi ya watu kwenu, naam, nyumba yote ya Israeli. Miji itakaliwa na watu na magofu yatajengwa upya.
I rozmnożę na was ludzi, cały dom Izraela, miasta będą zamieszkane i miejsca zburzone zostaną odbudowane.
11 Nitaongeza idadi ya watu na wanyama juu yenu, nao watazaana sana na kuwa wengi mno. Nitawakalisha watu ndani yenu kama ilivyokuwa wakati uliopita, nami nitawafanya mfanikiwe kuliko hapo kwanza. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Rozmnożę na was ludzi i bydło, będą liczni i płodni. I sprawię, że będziecie mieszkać jak za waszych dawnych czasów i będę wam czynić lepiej niż na początku. I poznacie, że ja jestem PANEM.
12 Nitawafanya watu, watu wangu Israeli, kutembea juu yenu. Watawamiliki ninyi, nanyi mtakuwa urithi wao, kamwe hamtawaondolea tena watoto wao.
Bo przyprowadzę na was ludzi, swój lud Izraela. Posiądą cię i będziesz dla nich dziedzictwem, i nigdy więcej nie pozbawisz ich potomstwa.
13 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu watu wanakuambia, “Unawala watu na kuliondolea taifa lako watoto wake,”
Tak mówi Pan BÓG: Ponieważ mówią do was: Ty jesteś tą [ziemią], która pożera ludzi i pozbawia narody potomstwa;
14 kwa hiyo hutakula tena watu wala kulifanya tena taifa lako lisiwe na watoto, asema Bwana Mwenyezi.
Już nie będziesz pożerać ludzi ani pozbawiać potomstwa swoje narody, mówi Pan BÓG.
15 Sitakufanya tena usikie dhihaka za mataifa, wala kudharauliwa na kabila za watu, wala kulifanya taifa lako lianguke, asema Bwana Mwenyezi.’”
I już nie dopuszczę, aby w tobie były słyszane obelgi narodów, nie będziesz już znosić zniewag ludzi i nie będziesz już doprowadzać swoich narodów do upadku, mówi Pan BÓG.
16 Neno la Bwana likanijia tena, kusema:
I doszło do mnie słowo PANA mówiące:
17 “Mwanadamu, nyumba ya Israeli walipokuwa wakiishi katika nchi yao wenyewe, waliinajisi kwa mwenendo wao na matendo yao. Mwenendo wao mbele zangu ulikuwa kama mwanamke aliye katika hedhi.
Synu człowieczy, gdy dom Izraela mieszkał w swej ziemi, plugawił ją swymi drogami i czynami. Jego droga wobec mnie była jak nieczystość odłączonej [kobiety].
18 Hivyo nilimwaga ghadhabu yangu juu yao kwa sababu walikuwa wamemwaga damu katika nchi na kwa sababu walikuwa wameitia nchi unajisi kwa sanamu zao.
Dlatego wylałem na nich swój gniew z powodu krwi, którą wylali na ziemię, i z powodu ich bożków, którymi ją splugawili.
19 Nikawatawanya miongoni mwa mataifa, nao wakaenda huku na huko katika nchi mbalimbali, nikawahukumu sawasawa na mwenendo wao na matendo yao.
I rozproszyłem ich między narodami, i zostali rozrzuceni po ziemiach. Osądziłem ich według ich dróg i według ich czynów.
20 Tena popote walipokwenda miongoni mwa mataifa walilitia unajisi Jina langu takatifu, kwa kuwa watu walisema kuwahusu, ‘Hawa ndio watu wa Bwana, lakini imewapasa kuondoka katika nchi yake.’
A [gdy] weszli do narodów, do których przybyli, zbezcześcili [tam] moje święte imię, gdy o nich mówiono: To jest lud PANA, a z jego ziemi wyszli.
21 Lakini niliwahurumia kwa ajili ya Jina langu takatifu, ambalo nyumba ya Israeli imelitia unajisi miongoni mwa mataifa huko walikokwenda.
Ale żal mi się zrobiło mojego świętego imienia, które zbezcześcił dom Izraela wśród narodów, do których przybył.
22 “Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Si kwa ajili yako, ee nyumba ya Israeli, kwamba ninafanya mambo haya, bali ni kwa ajili ya Jina langu takatifu, ambalo mmelitia unajisi miongoni mwa mataifa mliyoyaendea.
Dlatego mów do domu Izraela: Tak mówi Pan BÓG: Nie dla was ja [to] czynię, domu Izraela, ale przez wzgląd na moje święte imię, które zbezcześciliście wśród narodów, do których przybyliście.
23 Nitauonyesha utakatifu wa Jina langu kuu, ambalo limetiwa unajisi miongoni mwa mataifa, jina ambalo limetiwa unajisi miongoni mwao. Ndipo mataifa watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana, asema Bwana Mwenyezi, nitakapojionyesha mwenyewe kuwa mtakatifu kwa kuwapitia ninyi mbele ya macho yao.
I uświęcę moje wielkie imię, które było zbezczeszczone wśród narodów, które wy zbezcześciliście pośród nich. I poznają narody, że ja jestem PANEM, mówi Pan BÓG, gdy będę uświęcony w was na ich oczach.
24 “‘Kwa kuwa nitawaondoa ninyi toka mataifa, nitawakusanya kutoka nchi zote na kuwarudisha kwenye nchi yenu wenyewe.
Zabiorę was bowiem spośród narodów, zgromadzę was ze wszystkich ziem i przyprowadzę was do waszej ziemi.
25 Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi, nitawatakasa kutoka uchafu wenu wote na kutoka sanamu zenu zote.
I pokropię was czystą wodą, i będziecie czyści. Oczyszczę was ze wszystkich waszych nieczystości i ze wszystkich waszych bożków.
26 Nitawapa moyo mpya na kuweka roho mpya ndani yenu, nitaondoa ndani yenu moyo wenu wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama.
I dam wam nowe serce, i włożę nowego ducha do waszego wnętrza. Wyjmę serce kamienne z waszego ciała, a dam wam serce mięsiste.
27 Nami nitaweka Roho yangu ndani yenu na kuwafanya ninyi mfuate amri zangu na kuwafanya kuwa waangalifu kuzishika sheria zangu.
Włożę mego Ducha do waszego wnętrza i sprawię, że będziecie chodzić według moich ustaw [i będziecie] przestrzegać moich sądów, i wykonywać je.
28 Mtaishi katika nchi niliyowapa baba zenu, ninyi mtakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wenu.
Zamieszkacie w ziemi, którą dałem waszym ojcom, będziecie moim ludem, a ja będę waszym Bogiem.
29 Nitawaokoa ninyi kutoka unajisi wenu wote. Nitaiita nafaka na kuiongeza iwe nyingi sana nami sitaleta njaa juu yenu.
I wyzwolę was od wszystkich waszych nieczystości. Przywołam zboża i rozmnożę je, a nie dopuszczę do was głodu.
30 Nitaongeza matunda ya miti na mazao ya mashamba, ili kwamba msipate tena aibu miongoni mwa mataifa kwa ajili ya njaa.
Rozmnożę też owoc drzew i plony pól, abyście już nie znosili hańby głodu wśród narodów.
31 Ndipo mtakapozikumbuka njia zenu za uovu na matendo yenu maovu, nanyi mtajichukia wenyewe kwa ajili ya dhambi zote na matendo yenu ya kuchukiza.
Wtedy przypomnicie sobie wasze złe drogi i wasze czyny, które nie [były] dobre, i samych siebie będziecie się brzydzić z powodu waszych nieprawości i obrzydliwości.
32 Ninataka ninyi mjue kwamba sifanyi hili kwa ajili yenu, asema Bwana Mwenyezi. Oneni aibu na mkatahayari kwa ajili ya mwenendo wenu, ee nyumba ya Israeli!
Nie ze względu na was [to] czynię, mówi Pan BÓG, niech wam to będzie wiadome. Wstydźcie się i rumieńcie się z powodu waszych dróg, domu Izraela.
33 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Siku ile nitakapowasafisha kutoka dhambi zenu zote, nitarudisha watu waishi katika miji yenu na magofu yatajengwa upya.
Tak mówi Pan BÓG: W dniu, w którym was oczyszczę ze wszystkich waszych nieprawości, zaludnię miasta i miejsca zburzone zostaną odbudowane.
34 Nchi iliyokuwa ukiwa italimwa badala ya kukaa ukiwa machoni mwa wale wote wanaopita ndani yake.
A spustoszała ziemia będzie uprawiana, zamiast być spustoszeniem na oczach wszystkich przechodniów.
35 Watasema, “Hii nchi iliyokuwa imeachwa ukiwa sasa imekuwa kama bustani ya Edeni, miji ile iliyokuwa magofu, ukiwa na kuangamizwa, sasa imejengewa ngome na kukaliwa na watu.”
I powiedzą: Ta spustoszona ziemia stała się jak ogród Eden; miasta puste, opuszczone i zniszczone, [są] teraz obwarowane i zamieszkałe.
36 Ndipo mataifa yanayowazunguka yaliyobakia watakapojua kuwa Mimi Bwana nimejenga tena kile kilichoharibiwa na nimepanda tena kile kilichokuwa ukiwa. Mimi Bwana nimenena, nami nitalifanya.’
I narody, które wokół was pozostaną, poznają, że ja, PAN, odbudowałem to, co zburzone, i zasadziłem to, co spustoszone. Ja, PAN, to powiedziałem i uczynię.
37 “Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mara nyingine tena nitasikia maombi ya nyumba ya Israeli na kuwatendea jambo hili: Nitawafanya watu wake kuwa wengi kama kondoo,
Tak mówi Pan BÓG: Jeszcze w tym [jednym] dam się uprosić domowi Izraela, aby im [to] uczynić: Pomnożę [liczbę] ich ludzi jak trzodę.
38 kuwa wengi kama kundi la kondoo kwa ajili ya dhabihu huko Yerusalemu wakati wa sikukuu zao za wakati ulioamriwa. Hivyo ndivyo miji iliyokuwa magofu itajazwa na makundi ya watu. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
Jak trzodę na ofiary, jak trzodę Jerozolimy w czasie jej uroczystych świąt, tak spustoszone miasta będą wypełnione trzodami ludzi. I poznają, że ja jestem PANEM.

< Ezekieli 36 >