< Ezekieli 36 >
1 “Mwanadamu, itabirie milima ya Israeli na useme, ‘Ee milima ya Israeli, sikieni neno la Bwana.
Forsothe thou, sone of man, profesie on the hillis of Israel; and thou schalt seie, Hillis of Israel, here ye the word of the Lord.
2 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu adui wanasema juu yako, “Aha! Mahali palipoinuka pa zamani pamekuwa milki yetu.”’
The Lord God seith these thingis, For that that the enemy seide of you, Wel! euerlastyng hiynessis ben youun to vs in to eritage;
3 Kwa hiyo tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu wamewafanya ukiwa na kuwagandamiza kila upande ili mpate kuwa milki ya mataifa mengine na kuwa kitu cha kusimangwa na kudhihakiwa miongoni mwa watu,
therefore profesie thou, and seie, The Lord God seith these thingis, For that that ye ben maad desolat, and defoulid bi cumpas, and ben maad in to eritage to othere folkis, and ye stieden on the lippe of tunge, and on the schenschipe of puple;
4 kwa hiyo, ee milima ya Israeli, sikieni neno la Bwana Mwenyezi: Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kwa milima na vilima, kwa makorongo na mabonde, kwa mahame yaliyo ukiwa, miji iliyoachwa ambayo imetekwa nyara na kudharauliwa na mataifa mengine yanayowazunguka,
therfor, hillis of Israel, here ye the word of the Lord God. The Lord God seith these thingis to the mounteyns, and litle hillis, to strondis, and to valeis, and to peecis of wallis left, and to citees forsakun, that ben maad bare of puplis, and ben scorned of othere folkis bi cumpas;
5 hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika wivu wangu uwakao nimenena dhidi ya mataifa mengine na dhidi ya Edomu yote, kwa maana kwa furaha na hila katika mioyo yao waliifanya nchi yangu kuwa milki yao ili wapate kuteka nyara sehemu yake ya malisho.’
therfore the Lord God seith these thingis, For in the fier of my feruour Y spak of othere folkis, and of al Idumee, that yauen my lond in to eritage to hem silf with ioie `and al herte, and of entent, and castiden out it, to distrie it; therfor profesie thou on the erthe of Israel,
6 Kwa hiyo tabiri kuhusu nchi ya Israeli na uiambie milima na vilima, makorongo na vijito na mabonde: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninanena katika wivu wa ghadhabu yangu kwa sababu mmedharauliwa na mataifa.
and thou schalt seie to mounteyns, and litle hillis, to the hiynesse of hillis, and to valeis, The Lord God seith these thingis, For that that ye ben desolat, lo! Y spak in my feruour and in my strong veniaunce. For that that ye suffriden schenschipe of hethene men;
7 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninaapa kwa mkono wangu ulioinuliwa kwamba mataifa wanaowazunguka nao pia watadharauliwa.
therfor the Lord God seith these thingis, Lo! Y reiside myn hond ayens hethene men, that ben in youre cumpas, that thei bere her schenschipe.
8 “‘Lakini ninyi, ee milima ya Israeli, mtatoa matawi na matunda kwa ajili ya watu wangu Israeli, kwa sababu hivi karibuni watakuja nyumbani.
Forsothe, ye hillis of Israel, brynge forth youre braunchis, and bringe ye fruit to my puple Israel; for it is niy that it come.
9 Mimi ninawajibika nanyi na nitawaangalia kwa upendeleo, mtalimwa na kupandwa mbegu,
For lo! Y to you, and Y schal turne to you, and ye schulen be erid, and schulen take seed.
10 nami nitaizidisha idadi ya watu kwenu, naam, nyumba yote ya Israeli. Miji itakaliwa na watu na magofu yatajengwa upya.
And in you I schal multiplie men, and al the hous of Israel; and citees schulen be enhabitid, and ruynouse thingis schulen be reparelid.
11 Nitaongeza idadi ya watu na wanyama juu yenu, nao watazaana sana na kuwa wengi mno. Nitawakalisha watu ndani yenu kama ilivyokuwa wakati uliopita, nami nitawafanya mfanikiwe kuliko hapo kwanza. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
And Y schal fille you with men and beestis, and thei schulen be multiplied, and schulen encreesse; and Y schal make you to dwelle as at the bigynnyng, and Y schal rewarde with more goodis than ye hadden at the bigynnyng; and ye schulen wite, that Y am the Lord.
12 Nitawafanya watu, watu wangu Israeli, kutembea juu yenu. Watawamiliki ninyi, nanyi mtakuwa urithi wao, kamwe hamtawaondolea tena watoto wao.
And Y schal brynge men on you, my puple Israel, and bi eritage thei schulen welde thee, and thou schalt be to hem in to eritage; and thou schalt no more leie to, that thou be with out hem.
13 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu watu wanakuambia, “Unawala watu na kuliondolea taifa lako watoto wake,”
The Lord God seith these thingis, For that that thei seien of you, Thou art a deuouresse of men, and stranglist thi folk;
14 kwa hiyo hutakula tena watu wala kulifanya tena taifa lako lisiwe na watoto, asema Bwana Mwenyezi.
therfor thou schalt no more ete men, and thou schalt no more sle thi folk, seith the Lord God.
15 Sitakufanya tena usikie dhihaka za mataifa, wala kudharauliwa na kabila za watu, wala kulifanya taifa lako lianguke, asema Bwana Mwenyezi.’”
And Y schal no more make herd in thee the schenschipe of hethene men, and thou schalt no more bere the schenschipe of puplis, and thou schalt no more leese thi folk, seith the Lord God.
16 Neno la Bwana likanijia tena, kusema:
And the word of the Lord was maad to me, and he seide, Thou,
17 “Mwanadamu, nyumba ya Israeli walipokuwa wakiishi katika nchi yao wenyewe, waliinajisi kwa mwenendo wao na matendo yao. Mwenendo wao mbele zangu ulikuwa kama mwanamke aliye katika hedhi.
sone of man, the hous of Israel dwelliden in her lond, and thei defouliden it in her weies, and in her studies; bi the vnclennesse of a womman in rotun blood the weie of hem is maad bifor me.
18 Hivyo nilimwaga ghadhabu yangu juu yao kwa sababu walikuwa wamemwaga damu katika nchi na kwa sababu walikuwa wameitia nchi unajisi kwa sanamu zao.
And Y schedde out myn indignacioun on hem, for blood which thei schedden on the lond, and in her idols thei defouliden it.
19 Nikawatawanya miongoni mwa mataifa, nao wakaenda huku na huko katika nchi mbalimbali, nikawahukumu sawasawa na mwenendo wao na matendo yao.
And Y scateride hem among hethene men, and thei weren wyndewid to londis; Y demede hem bi the weies and fyndyngis of hem.
20 Tena popote walipokwenda miongoni mwa mataifa walilitia unajisi Jina langu takatifu, kwa kuwa watu walisema kuwahusu, ‘Hawa ndio watu wa Bwana, lakini imewapasa kuondoka katika nchi yake.’
And thei entriden to hethene men, to whiche thei entriden, and defouliden myn hooli name, whanne it was seid of hem, This is the puple of the Lord, and thei yeden out of the lond of hym.
21 Lakini niliwahurumia kwa ajili ya Jina langu takatifu, ambalo nyumba ya Israeli imelitia unajisi miongoni mwa mataifa huko walikokwenda.
And Y sparide myn hooli name, which the hous of Israel hadde defoulid among hethene men, to whiche thei entriden.
22 “Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Si kwa ajili yako, ee nyumba ya Israeli, kwamba ninafanya mambo haya, bali ni kwa ajili ya Jina langu takatifu, ambalo mmelitia unajisi miongoni mwa mataifa mliyoyaendea.
Therfor thou schalt seie to the hous of Israel, The Lord God seith these thingis, O! ye hous of Israel, not for you Y schal do, but for myn hooli name, which ye defouliden among hethene men, to whiche ye entriden.
23 Nitauonyesha utakatifu wa Jina langu kuu, ambalo limetiwa unajisi miongoni mwa mataifa, jina ambalo limetiwa unajisi miongoni mwao. Ndipo mataifa watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana, asema Bwana Mwenyezi, nitakapojionyesha mwenyewe kuwa mtakatifu kwa kuwapitia ninyi mbele ya macho yao.
And Y schal halewe my greet name, which is defoulid among hethene men, whiche ye defouliden in the myddis of hem; that hethene men wite, that Y am the Lord, seith the Lord of oostis, whanne Y schal be halewid in you before hem.
24 “‘Kwa kuwa nitawaondoa ninyi toka mataifa, nitawakusanya kutoka nchi zote na kuwarudisha kwenye nchi yenu wenyewe.
For Y schal take awei you fro hethene men, and Y schal gadere you fro alle londis, and Y schal brynge you in to youre lond.
25 Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi, nitawatakasa kutoka uchafu wenu wote na kutoka sanamu zenu zote.
And Y schal schede out clene watir on you, and ye schulen be clensid fro alle youre filthis; and Y schal clense you fro alle youre idols.
26 Nitawapa moyo mpya na kuweka roho mpya ndani yenu, nitaondoa ndani yenu moyo wenu wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama.
And Y schal yyue to you a newe herte, and Y schal sette a newe spirit in the myddis of you; and Y schal do awei an herte of stoon fro youre fleisch, and Y schal yyue to you an herte of fleisch,
27 Nami nitaweka Roho yangu ndani yenu na kuwafanya ninyi mfuate amri zangu na kuwafanya kuwa waangalifu kuzishika sheria zangu.
and Y schal sette my spirit in the myddis of you. And Y schal make that ye go in my comaundementis, and kepe and worche my domes.
28 Mtaishi katika nchi niliyowapa baba zenu, ninyi mtakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wenu.
And ye schulen dwelle in the lond, whiche Y yaf to youre fadris; and ye schulen be in to a puple to me, and Y schal be in to a God to you.
29 Nitawaokoa ninyi kutoka unajisi wenu wote. Nitaiita nafaka na kuiongeza iwe nyingi sana nami sitaleta njaa juu yenu.
And Y schal saue you fro alle youre filthis; and Y schal clepe wheete, and Y schal multiplie it, and Y schal not put hungur on you.
30 Nitaongeza matunda ya miti na mazao ya mashamba, ili kwamba msipate tena aibu miongoni mwa mataifa kwa ajili ya njaa.
And Y schal multiplie the fruyt of tree, and the seedis of the feeld, that ye bere no more the schenschipe of hungur among hethene men.
31 Ndipo mtakapozikumbuka njia zenu za uovu na matendo yenu maovu, nanyi mtajichukia wenyewe kwa ajili ya dhambi zote na matendo yenu ya kuchukiza.
And ye schulen haue mynde on youre worste weies, and on studies not goode; and youre wickidnessis, and youre grete trespassis schulen displese you.
32 Ninataka ninyi mjue kwamba sifanyi hili kwa ajili yenu, asema Bwana Mwenyezi. Oneni aibu na mkatahayari kwa ajili ya mwenendo wenu, ee nyumba ya Israeli!
Not for you Y schal do, seith the Lord God, be it knowun to you; O! the hous of Israel, be ye schent, and be ye aschamed on youre weies.
33 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Siku ile nitakapowasafisha kutoka dhambi zenu zote, nitarudisha watu waishi katika miji yenu na magofu yatajengwa upya.
The Lord God seith these thingis, In the dai in which Y schal clense you fro alle youre wickidnessis, and Y schal make citees to be enhabitid, and Y schal reparele ruynouse thingis,
34 Nchi iliyokuwa ukiwa italimwa badala ya kukaa ukiwa machoni mwa wale wote wanaopita ndani yake.
and the desert lond schal be tilid, that was sum tyme desolat, bifor the iyen of ech weiegoere,
35 Watasema, “Hii nchi iliyokuwa imeachwa ukiwa sasa imekuwa kama bustani ya Edeni, miji ile iliyokuwa magofu, ukiwa na kuangamizwa, sasa imejengewa ngome na kukaliwa na watu.”
thei schulen seie, Thilke lond vntilid is maad as a gardyn of likyng, and citees forsakun and destitute and vndur myned saten maad strong; and hethene men,
36 Ndipo mataifa yanayowazunguka yaliyobakia watakapojua kuwa Mimi Bwana nimejenga tena kile kilichoharibiwa na nimepanda tena kile kilichokuwa ukiwa. Mimi Bwana nimenena, nami nitalifanya.’
whiche euer ben left in youre cumpas, schulen wite, that Y the Lord haue bildid distried thingis, and Y haue plauntid vntilid thingis; Y the Lord spak, and Y dide.
37 “Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mara nyingine tena nitasikia maombi ya nyumba ya Israeli na kuwatendea jambo hili: Nitawafanya watu wake kuwa wengi kama kondoo,
The Lord God seith these thingis, Yit in this thing the hous of Israel schulen fynde me, that Y do to hem; Y schal multiplie hem as the floc of men, as an hooli floc,
38 kuwa wengi kama kundi la kondoo kwa ajili ya dhabihu huko Yerusalemu wakati wa sikukuu zao za wakati ulioamriwa. Hivyo ndivyo miji iliyokuwa magofu itajazwa na makundi ya watu. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
as the floc of Jerusalem in the solempnytees therof, so the citees that ben forsakun, schulen be fulle of the flockis of men; and thei schulen wite, that Y am the Lord.